Wednesday, November 27, 2019

Bagonza "Waliopiga Kura Hawana Furaha na Walioshinda Pia Hawana Furaha"


"Waliopiga kura hawana furaha na waliosusa au kususwa hawana furaha, waliopita bila kupingwa nao hawana furaha, waliosimamia kura hawana furaha, walioshinda hawana furaha na hata walioshindwa hawana pia furaha na uchaguzi huo."- Askofu wa KKKT, Dayosisi ya Karagwe, Benson Bagonza

Tuesday, November 26, 2019

Agizo la Rais Magufuli Latekelezwa Ndani ya Saa 24.....Taasisi 4 Zatoa Gawio la Bilioni 2.75

Na. Immaculate Makilika- MAELEZO
Saa chache baada ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli kutoa siku 60 kwa Taasisi, Kampuni ambazo Serikali ina hisa chache na Mashirika ya Umma 187 ambayo hayajatoa gawio au mchango kwa Serikali tayari Taasisi nne zimetekeleza agizo hilo leo.

Akizungumza leo, jijini Dodoma, wakati akipokea gawio na michango kutoka Shirika la Posta, Shirika la Reli (TRC), Self Microfinance Fund, na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), ambapo jumla ya fedha zilizowasilishwa ni shilingi bilioni 2.75, Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango alisema kuwa baada ya agizo la Rais alilolitoa jana, hakutakuwa na mzaha kwa Taasisi, Kampuni na Mashirika ambayo hayatekeleza agizo hilo ndani ya siku 59 zilizobaki.

"Nitasimamia kikamilifu agizo hili la Mheshimiwa Rais, itakapofika siku ya 60 nitatembeza panga bila uoga wala kupepesa macho kwa Taasisi, Kampuni na Mashirika ambayo hayatakuwa yametekeleza agizo hili, hatutanii katika hili" alisema Waziri Mipango.

Aidha, Waziri Mpango alizishukuru Taasisi hizo kwa kutekeleza agizo la Rais na kuongeza kuwa angependa kuona Mashirika yaliyobaki yakitekeleza agizo hilo kwa wakati, kwa kuwa fedha hizi si zake wala za Rais bali ni kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo kwa faida ya watanzania wote.

Naye, Msajili wa Hazina, Athumani Mbutuka alisema kuwa alitekeleza agizo la Rais Magufuli la kumtaka kuzijulisha Taasisi, Kampuni na Mashirika 187 ambayo hayakuwa yametoa gawio na michango kufanya hivyo ndani ya siku 60, ambapo Taasisi za TRC, TIC, Shirika la Posta na Self Microfinance Fund  wamekuwa wa kwanza kutekeleza agizo hilo.

Rais Dkt. John Pombe Magufuli jana alipokea gawio na michango kutoka kwa Taasisi, Kampuni na Mashirika 79 ambayo yalitoa jumla ya shilingi trilioni 1.05, ambapo Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA), Mamlaka ya Hifadhi ya Bonde la Ngorongoro, Wakala wa Huduma za Misitu na Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) yalikabidhiwa cheti kwa kufanya vizuri. Aidha, TPA iliyotoa gawio la shilingi bilioni 169 na TPC iliyotoa shilingi bilioni 14 yalipewa tuzo kwa  kutoa gawio kubwa zaidi.


Tuesday, November 19, 2019

I Love My Boyfriend But I Enjoy Having S3x With Strangers


I know my romantic boyfriend is planning some Valentine's treat but whatever it is, it won't thrill me as much as having séx with strangers.

I'm 24 and he's 25. We met in school and we both work in tourism. He's a really nice guy and we've been together five years. We've been happy for most of that time but lately I've realised I'm totally bored with my life.

He worked late one night and I went to the bar with a friend. I was up at the bar when this really cool guy started flírting with me. When I sat down he kept turning to look and then giving a smile. It made me feel séxy and hot.

My friend had a cold and soon phoned for a cab. I said I'd walk home as it wasn't that far. That guy was still there at the bar and I wanted to see what would happen.

What happened was that we flirtéd some more and then we went back to his car and had séx. It was great and I felt like a wild child or something who lives for the moment and isn't afraid to have fun.

That was the first time I did it but last month it happened again, this time with a guy I met on a training course. I'd never seen him before and I've no wish to see him again but the thrill was imménse.

Last night I had séx with a stranger I met in a club. I know that it's wrong but it's thrilling and risky and fun. I don't like telling lies but if I told my boyfriend the truth it would destroy him.

Monday, November 18, 2019

Boeing Waanza Kuunda NDEGE Zenye Kasi zaidi Mara Tano ya Ndege Zilizopo Sasa

Kampuni ya #Boeing imeanza kushughulikia muundo wa ndege mpya
ya abiria yenye uwezo wa kwenda kasi mara tano ya sauti #Hypersonic.

Tangu kustaafishwa kwa ndege za abiria aina #Concord (supersonic transport) ambazo zilikuwa na uwezo wa kufanya safari zake kwa nusu ya muda unaochukua ndege za sasa, kampuni nyingi zinazo jishughulisha na uundaji wa vyombo vya usafiri wa anga vinajaribu kubuni ndege tofauti tofauti zenye uwezo wa kwenda kasi zaidi ya Concord huku zikitoa udhaifu ulikuwepo wa kelele, uchafuzi mazingira na ulaji mdogo wa mafuta.

Kitendo cha kuunda umbile na injini zitakazoweza kufanya kazi katika kasi inayozidi mara tano ya sauti (zaidi ya 5500km/h) imekuwa ni suala gumu kwani linahitaji fedha nyingi na muda katika uwekezaji na utafiti.

Chombo chochote cha usafiri wa anga kinachotaka kufika mwendokasi huo inahitajika malighafi tofauti katika uundaji wake kama #Titanium ili kukabiliana na joto kali linalosababishwa na msuguano wa chombo husika na hewa.

Kampuni Boeing imekuja na mchoro wa ubunifu wa ngamizi kuonesha ndege hiyo ambayo inategemea kufika mwendokasi zaidi ya 6000km/saa huku ikitumia injini ya #TurboRamjet ambayo ni 'modification' ya ile ambayo awali ilitumika kwenye ndege ya kijasusi aina ya #SR71 "Blackbird" ambayo itakuwa inafanya kazi kama injini ya kawaida ikiwa #Supersonic chini ya mwendokasi wa 4000km/saa na baadae kufanya kazi kama #Ramjet ikifika kasi mara tano ya sauti 'Hypersonic speed' (kuanzia 5000km/saa) kwa kufunga vidirisha upande wa feni za injini hiyo kwakuwa haziwezi tena kufanya kazi katika mwendokasi huo na kuruhusu hewa yenye kasi kuingia moja kwa moja kwenye injini na kuchomwa pasipo kuhitaji mkamizo 'compression' ya injini za kawaida.

Wanasema ndege hiyo itakuwa inaenda usawa wa futi 95,000 kutoka usawa wa bahari na kasi ya 6000km/saa.

Ndege za kisasa kama #Boeing787 #Dreamliner na #Airbus350 #XWB zina uwezo wa kwenda hadi futi 43,000 kutoka usawa wa bahari na kasi ya 930-950km/saa

Mkutano wa Taasisi za fedha nchini wahamishiwa Dar


Mkutano wa 19 wa taasisi za fedha nchini uliokuwa ufanyike jijini Arusha tarehe 21 na 22 Novemba 2019 sasa utafanyika Dar es Salaam kwa tarehe hizo hizo.

Mkutano huo ambao umeandaliwa na Benki Kuu ya Tanzania kwa kushirikiana na Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA) utawakutanisha washiriki wapatao 300 ili kujadili namna ya kuharakisha maendeleo ya ya sekta ya fedha nchini. Watakaohudhuria mkutano huo ni pamoja an mawaziri wakiongozwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, wakuu wa taasisi za fedha, wachumi wabobezi, wanataaluma na washirika mbalimbali wa maendeleo.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Mkutano huo na Mkurugenzi wa Utumishi na Uendeshaji wa Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Kened Nyoni, alisema mkutano huo utafanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam.

Mada katika mkutano huo zitahusu 'Matumizi ya teknolojia katika kukuza sekta ya fedha ili kuleta mapinduzi ya viwanda'; 'Maeneo yenye fursa za uwekezaji katika sekta ya fedha', 'Vigezo vinavyochangia kujenga tabia za ukopaji', 'Jinsi ya kukinga vihatarishi katika sekta ya fedha'; 'Namna ya kuoanisha sekta ya fedha na maendeleo ya viwanda'; na 'Tathmini ya mchango wa sekta ya benki katika huduma jumuishi za kifedha nchini'.

Benki Kuu ya Tanzania imekuwa ikiandaa mikutano ya taasisi za fedha kila baada ya miaka miwili tangu miaka ya 1980. Katika mikutano hii, viongozi wakuu wa taasisi za fedha, yakiwemo mabenki, mashirika ya bima, mifuko ya hifadhi za jamii na taasisi zingine za fedha wamekuwa wakikutana na kujadili masuala mbalimbali kwa ajili ya maendeleo ya sekta ya fedha na uchumi wa nchi kwa ujumla. Mkutano wa 18 wa taasisi za fedha ulifanyika mwaka 2016 jijini Arusha na mada kuu katika mkutano huo ilikuwa ni 'Jinsi sekta ya fedha inavyoweza kuifanya Tanzania inufaike kiuchumi kutokana na uwepo wake kijiografia' (Harnessing Tanzania's Geographical Advantage: The role of financial sector).


Sunday, November 17, 2019

KAMPENI YA ELIMU KWA MLIPAKODI YAWAFIKIA WAFANYABIASHARA ZAIDI YA 700 MOROGORO


Na Veronica Kazimoto
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewafikia na kuwaelimisha wafanyabiashara zaidi ya 700 kupitia kampeni ya Huduma na Elimu kwa Mlipakodi iliyofanyika mkoani Morogoro.

Lengo la kampeni hiyo ilikuwa ni kutoa elimu kuhusu masuala mbalimbali ya kodi pamoja na kusikiliza malalamiko, changamoto na maoni kutoka kwa wafanyabiashara hao.

Akizungumza mara baada ya kukamilika kwa kampeni hiyo mwishoni mwa wiki, Afisa Msimamizi wa Kodi Mkuu wa TRA, Julius Mjenga amesema kuwa, mamlaka hiyo ililenga kuwafikia wafanyabiasha 500 lakini kutokana na mwitikio mkubwa, TRA imefanikiwa kuvuka lengo hilo na kuwafikia zaidi ya 700.

"Wiki hii moja ya elimu kwa mlipakodi, tuliwalenga wafanyabiashara wa wilayani ambapo kumekuwa na changamoto ya kutokupata elimu ya kodi kwa wakati. Nashukuru tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa kwa sababu tumeweza kuwaelimisha wafanyabiashara 774 katika kampeni hii", alisema Mjenga.

Mjenga ameongeza kuwa "Tumefika karibu wilaya zote za mkoa huu wa Morogoro ambazo ni Malinyi, Ulanga, Kilosa, Mvomero, Kilombero na Gairo na kila mahali tulipopita tumepata mwitikio mkubwa kutoka kwa wafanyabiashara na wananchi mbalimbali."

Kwa upande wa wafanyabiashara waliotembelewa na TRA, wameishukuru mamlaka hiyo kwa kuwaelimisha masuala mbalimbali yanayohusu kodi na kuomba elimu hiyo iwe endelevu.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya wafanyabiashara hao wamesema kuwa, TRA ya sasa sio ile ya zamani kwa sababu sasa hivi maafisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania wamekuwa karibu na walipakodi na siku hizi hawana tabia ya kufunga biashara zao.

"Zamani mtu alikuwa akisikia watu wa TRA wanakuja, anafunga duka anaondoka lakini siku hizi, TRA wamekuwa marafiki, wanatuelimisha na wala hawafungi biashara zetu, kwakweli tunashukuru sana," alisema Eleonora Kisimba, mfanyabiashara wa duka la nguo wa wilayani Mvomero.

Naye Stanphord Mjumbe ambaye ni mfanyabiashara wa duka la vifaa vya ujenzi wilayani Gairo mkoani hapa alisema kuwa, kampeni ya elimu kwa mlipakodi ifanyike mara kwa mara kwa sababu wafanyabiashara walio wengi hususani wadogo hawajasoma hivyo wanahitaji kuelimishwa zaidi juu ya haki na wajibu wao katika ulipaji kodi.

"Sisi wafanyabiashara wadogo, tulio wengi hatujasoma hivyo tunahitaji elimu hii angalau kwa mwaka mara tatu ili tuweze kuelewa kwa kina haya mambo ya ulipaji kodi maana wakati mwingine tunakuwa hatujui haki zetu," alisisitiza Mjumbe.

Aidha, wafanyabiashara hao wameiomba Mamlaka ya Mapato Tanzania kurejesha Kodi ya Zuio kwa wamiliki wa majengo kwa kuwa baadhi yao hawataki wapangaji kuzuia asimilia kumi na kuiwasilisha TRA.

Vilevile, wameomba kuelimishwa jinsi ya kulipa kodi ya mapato kwa awamu mara tu wanapokadiriwa kodi hususani kwa wafanyabiashara wapya kwani wengi wao wanapitiliza tarehe za kulipa kodi hiyo kwa kukosa uelewa.

Kampeni ya huduma na elimu kwa mlipakodi imemalizika tarehe 17 Novemba, 2019 na ilifanyika katika Mikoa ya Morogoro na Pwani ambapo wafanyabiashara wamepata fursa ya kutembelewa katika maduka yao na wengine walihudhuria semina kwa ajili ya kuelimishwa masuala mbalimbali yanayohusu kodi.


Mwisho.


Waandamanaji 40 wakamatwa Iran

Watu 40 wamekamatwa katika mji wa Yazd nchini Iran baada ya kupambana na polisi wakati wa maandamano ya kupinga ongezeko la bei ya petroli.

Taarifa hii ni kulingana na shirika la habari nchini humo la ISNA hii leo. Shirika hilo lilimnukuu mwendesha mashitaka wa serikali Mohammad Hadadzadeh akisema wale wanaoshikiliwa ni waliosababisha vurugu akiwatuhumu kwa matukio ya uharibifu na wengi miongoni mwao si wakaazi wa eneo hilo.

ISNA hata hivyo, haikuweka wazi ni wakati gani watu hao walikamatwa. Iran ilikabiliwa na maandamano makubwa siku ya Ijumaa masaa kadhaa baada ya tangazo la bei la petroli kupandishwa kwa asilimia 50 katika lita 60 za mwanzo na asilimia 300 kwa kiasi chochote kitakachozidi kila mwezi.

Saturday, November 16, 2019

Maneno ambayo husaidia kuamsha hisia za kimapenzi



Kuna mwanafalsafa fulani aliwahi kuandika katika maandiko yake akisema ya kwamba, maneno ya upendo yana nguvu sana katika mahusiano. Mtu unamwambia maneno mazuri na matamu katika mahusiano hujenga hisia mpya za kimapenzi.

Hivyo kila wakati unatakiwa kujifunza kumwambia maneno yafuatayo mpenzi wako ili kujenga hisia za kimapenzi :

1. Umenifanya niwe mtu bora

2. Umenifanya nijisikie Kupendwa

3. I love you so much.

4. Kila niwapo na wewe najisikia vizuri.

5. Sitasubiri kukuona tena.

6. Napenda kutumia muda mwingi na wewe.

7. Napenda niwe wako.

8. Hakuna mtu anaweza kunipa amani nipatayo kwako.

9. Napenda uso wako.

10. Nashukuru kukuona

11. You're so beautiful/handsome

12. Unanijali vizuri

13. Unanifundisha vitu vipya kila siku

14.I love how funny you are

15. Unanitaka niwe mwenza bora, naweza kuwa hivyo kwa ajili yako

16. Asante kwa kuwa nyuma yangu kila mara.

17. Napenda uwepo wako

18. You're amazing

19. Wewe ni mtu wangu pekee katika sayari hii

20. Kuwa na wewe napata furaha

21. Unaufanya moyo wangu utulie

22. I feel so loved by you

23. Napenda jinsi ulivyo mtu wa fikra

24. Mara zote unanipa ushauri mzuri

25. Maisha ni mazuri nikiwa upande wako/ukiwa upande wangu

26. You're the best

27. Kamwe sitaki kuwa na mwingine lakini wewe.

28. Wewe ni familia ambayo nilitaka niwepo.

29. Kila wakati unajua kitu kizuri cha kusema

30. Napenda maisha tuliyonayo pamoja

31. Siamini jinsi nilivyo na bahati ya kuwepo na wewe.

32. Sijawahi kusikia hali hii niliyo nayo kuhusu wewe

33. Unanifanya niwe mwanamke bora/mwanaume bora kwa sababu niko na wewe.

34. Napenda jinsi ulivyo na akili

35. Wewe ni mwenza mzuri

36. Nafurahia ninapokuwa na wewe

37. You're incredible

38.Una akili sana

39. Unaufanya moyo wangu ushibe

40. Kila niwapo na wewe  nina furaha

41. Nakutamani

42. Umeniletea furaha

43. Sihitaji mtu mwingine ni wewe

44. Tukue sote pamoja

45. Nashukuru kukupata

46. Najisikia vizuri ninapokuwa karibu yako

47. Najisikia kupata msaada mkubwa kwako

48. Maisha ni mazuri sana nikiwa na wewe

49. Sitaboreka nikiwepo na wewe

50. You make me so happy.

Wednesday, November 13, 2019

Zari Confirms She is Still Dating King Bae


Just a few days ago Zari went on to claim that her new man King bae was dead and none existent in her life.

The lady revealed this while responding to one of her concerned fans who wanted to know where King bae had disappeared to.

Well, according to Zari's response it was evident to see that the two might have been having issues or had gone their separate ways since Zari claimed that King bae was dead.

Back like he never left
Anyway, seems that Zari has been forced to bow down to the pressure she's been receiving from fans who want to know where King bae is.



Through her Snapchat account, Zari once again went on to share a new photo with her man and went on to caption saying;

For everyone asking about him, the less he is in the public the less the pressure. Am at peace

Monday, November 11, 2019

Yanga yamtangaza rasmi Katibu Mkuu wa klabu hiyo


Uongozi wa Klabu ya Yanga umemtangaza rasmi David Ruhago kuwa Katibu Mkuu wa klabu hiyo kuanzia leo tarehe 11/11/2019. 

Taarifa iliyotolewa leo na Afisa Habari wa Yanga, imesema uteuzi huo umefanywa na kamati yake ya utendaji chini ya Mwenyekiti Dkt. Mshindo Msolla.


Mkuti Marketing yaipa kichapo Yanga

Klabu ya Yanga imechezea kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Mkuti Marketing katika mchezo wa kirafiki uliochezwa kwenye Uwanja wa Boma, wilayani Masasi, Mtwara.

Bao pekee la Mkuti limefungwa na Hassan Mtepeto dakika ya 28.

FT: Mkuti Marketing 1-0 Yanga SC.

Ebitoke amvamia Mlela na Mpenzi Wake kwa fujo mbele ya Waandishi wa Habari

Mchekeshaji Ebitoke ameuvamia mkutano wa Mwigizaji Yusuph Mlela na Waandishi wa Habari Dar es salaam na kutaka kupigana na Mlela na Mpenzi wake mpya ambae alikua ameongozana nae kwenye mkutano huo na Waandishi wa Habari ikiwa ni siku chache tu toka Mlela adaiwe kuachana na Ebitoke..

Ebitoke amesikika akisema; "Mwacheni nimwonyeshe", huku akitukana matusi ya nguoni licha ya kudhibitwa na mabaunsa.

Kaka wa Ebitoke naye amesikika akimwambia Mlela, "Umemuharibia maisha mdogo wangu" huku waandishi wa habari na wasanii wenzake waliokuwepo wakibaki wameduwaa.


Barua nzito, Aliyejinyonga Tarime “Msiwaamini Waganga fanyeni kazi halali”

Mkazi wa Kijiji cha Kowak, Wilayani Rorya mkoani Mara, Juma Olemo, amekutwa amejinyonga hadi kufa katika Nyumba ya kulala wageni ya Silent Inn iliyopo mjini Tarime na kuacha ujumbe wa barua yanye kurasa mbili, akiwataka rafiki zake kuachana na waganga wa kienyeji wapotoshaji.

Akisoma ujumbe ulioandikwa katika barua hiyo kwa waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Tarime – Rorya, Henry Mwaibambe, amesema Olemo aliomba msamaha kwa uamuzi aliouchukua na kuwaasha vijana wenzake kuachana na waganga wa kienyeji ambao wanawaaminisha kubadili maisha yao kwa imani za kishirikina.

Kamanda Mwaibambe amesema katika barua hiyo Olemo aliwataka marafiki na vijana wenzake, siku ya mazishi yake wacheze mpira wa miguu ili kumuaga.

" Novemba 7, mwaka huu, wahudumu wa nyumba ya kulala wageni ya Silent Inn iliyopo mjini Tarime, baada ya kuamka asubuhi na kutaka kufanya usafi vymbani, walijaribu kugonga mlango wa chumba alimokuwa amelala Olemo lakini haukufunguliwa na kuwalazimu kuita askari polisi ili kushirikiana nao kufungua mlango huo" Amesema Kamanda Mwaibambe.

"Walifanikiwa kuvunja na walipoingia ndani walikuta mwili wa Olemo ukining'inia juu ya dari na pembeni yake walikuta barua hiyo iliyokuwa na ujumbe mrefu wa kurasa mbili" alieleza.

Na kuongeza kuwa " Jamaa wa marehemu walifika na kubaini kuwa mwandiko uliomo kwenye barua hiyo ni wake marehemu ambapo katika ujumbe huo alimtaja mke wake na kuomba msamaha kwa uamuzi aliochukua na kumuomba ndugu yake mdogo kumtunza mkewake na watoto wake"

Pia aliwaomba msamaha mashabiki wa timu ya mpira Simba, kwa uamuzi wake wa kujinyonga, aliwaomba masamaha waendesha bodaboda na kuwaasa kufanya kazi halali na kutowaamini waganga wa kienyeji.

Kamanda amesema Mwili wa marehemu ulipelekwa katika Hospitali ya Wilaya ya Tarime na kufanyiwa uchunguzi kisha kuchukuliwa na ndugu zake kwa mazishi.

Sunday, November 10, 2019

AWAOMBA RADHI MASHABIKI WA SIMBA KWA KUJIUA GESTI... ATAKA MAZISHI YAKE WATU WACHEZE MPIRA


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Polisi Tarime/Rorya Henry Mwaibambe

Dinna Maningo - Malunde1 blog Rorya
Mkazi wa kijiji cha Kowaki Wilayani Rorya mkoani Mara Juma Okora amewataka Mashabiki wa timu ya  Simba SC,ndugu na marafiki kumsamehe baada ya kufanya maamuzi ya kujinyonga kutokana na ugumu wa maisha.


Akizungumza na Waandishi wa Habari Kamanda wa Polisi Mkoa wa Polisi Tarime/Rorya Henry Mwaibambe amesema kuwa marehemu alikutwa kwenye chumba cha kulala wageni akiwa amejinyonga kwa kutumia kamba huku akiwa ameacha karatasi yenye ujumbe mrefu wa maandishi.

"Polisi walifika wakakuta ameshakufa na alikuwa kaandika barua ndefu, awali tulidhani labda kauawa na mtu na akaandika ujumbe kwa kujifanya ni marehemu, lakini tulivyofatilia kwa undani kwa kuangalia mwandiko na kumbukumbu za maandishi ya nyuma aliyokuwa akiyaandika wakati wa uhai wake tukagundua mwandiko ni wake na ameandika mwenyewe",amesema Kamanda Mwaibambe.

Mwaibambe amesema barua hiyo iliyoandikwa na marehemu ambayo ujumbe wake ulijikita kuwaomba watu msamaha na kuwashauri vijana kutafuta mali kwa njia za halali na si za kishirikina kwa kile alichodai kuwa kajiua kutokana na ugumu wa maisha na amekuwa akitafuta mali kwa njia za kishirikina bila mafanikio.

Baadhi ya ujumbe uliosomwa na Kamanda ulieleza"Nawaomba Washabiki wa Simba mnisamehe kwa maauzi haya ugumu wa Maisha umenifanya nijinyonge,Mke wangu Helen naomba unisamehe kwa kukuacha na mzigo wa kulea watoto peke yako,mdogo wangu......naomba uwatunze wanangu,Babu samahani".

"Bodaboda mnisamehe,rafiki zangu akina......mnisamehe na ninawaomba vijana mtafute mali kwa njia za halali nimetafuta kwa njia za kishirikina lakini sijafanikiwa nilipewa masharti magumu yamenishinda nimeamua kujinyonga naomba siku ya mazishi yangu watu wacheze Mpira",alisema Mwaibambe

Hata hivyo Kamanda Mwaibambe amewataka wananchi kutochukua maamuzi ya kujiua huku akieleza kuwa ujumbe wa marehemu nifundisho kwa vijana nakwamba wanapaswa kuwa wavumivu katika Maisha .

Source

Mfahamu kiundani mwanamuziki Pepe Kalle


Novemba 28,kila mwaka ndugu,  jamaa na wapenzi wa muziki wa dansi Afrika Mashariki, Kati, Magharibi na Ulimwenguni kwa ujumla, itakuwa ni siku ya majonzi tukiomboleza kifo cha mwanamuziki Pepe Kalle aliyefariki Novemba 28, 1998 kwa ugonjwa wa moyo akiwa na umri wa miaka 47.

Jitu la miraba minne Pepe Kalle  baada ya kuzaliwa Novemba 30, 1951 katika Jiji la Kinshasa huko Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo  alipewa jina Kabasele Yampanya.

Alikuwa mtunzi, mwimbaji wa muziki wa soukous na kiongozi wa bendi ya Empire Bakuba. Umbo lake kubwa lilikuwa limebeba uzito wa Kilo 136 na urefu wake ulikuwa  Sentimeta 190 ambazo ni sawa na Futi Sita na Inchi tatu.

Pepe Kale alikuwa bingwa wa miondoko ya soukous na kiongozi wa bendi ya Empire Bakuba, ambayo ilikuwa maarufu katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

 Sauti yake nyembamba iliyokuwa na uwezo mkubwa wa kughani, alikuwa anauwezo mkuwa wa kucheza jukwaani akitikisa umbo lake licha ya kuwa na uzito mkubwa.

Watanzania wengi tutaendelea kumkumbuka mwanamuziki huyu hasa wakati alipokuja nchini mwetu na kutikisa majiji ya Arusha, Dar es Salam na Mbeya.

Wakati wa ujio wake hapa Tanzania, Pepe Kalle ambaye sauti yake ilikuwa nyembemba na nyororo, alifuatana  na wanamuziki akiwemo mipiga wa gita la besi Lofombo na waimbaji akina Papy Tax, Dilu Dilumona na Djo Djo Ikomo.


Rapa wake mahiri na kiongozi wa  wacheza Shoo Bileku Mpasi na  mbilikimo wawili Emoro na Jolly Bebbe walitoa burudani tosha kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam mwaka 1991. Mwaka uliofuatia wa 1992,  Emoro alifariki dunia  akiwa na bendi yake nje ya nchi  kwa safari za kikazi ya muziki.

'Kizuri huigwa' usemi huo ulijionyesha dhahiri baada ya msanii mmoja aliyejulikana kwa jina la Kokoriko, kuweza kuiga miondoko ya uchezaji wa Bileku Mpasi. Msanii huyo alipachikwa jina la Bileku Mpasi wa Tanzania.

Pepe wakati wa uhai wake alirekodi nyimbo zaidi wa 300 na kufyautua album 20 katika miongo miwili ya muziki wake na alijulikana kama 'Tembo wa Afrika'. 

Historia yake katika muziki inaeleza kwamba alianza muziki rasmi katika bendi  ya Afrikan Jazz ya  Baba yake mzazi Joseph Kabasele 'Grand Kalle'  aliyemtengeneza mwanaye huyo.

Baada ya kukomaa kimuziki akatimka na kwenda kujiunga na bendi ya Lipua Lipua iliyokuwa ikimilikiwa na Kiamunagana Mateta  Wanzo la Mbonga 'Verkeis'
Akipotua Lipua Lipua, haikuchukua kipindi kirefu  akafanywa kuwa  mwimbaji kiongozi  akishirikiana na mwimbaji wengine Nyboma Mwandido.

Safari yake katika muziki haikuishia hapo kwani mwaka 1973  Pepe kale akiwa na Dilu Dilumona na Papy Tax waliondoka katika bendi hiyo ya na  kuunda bendi yao iliyopewa jina la Empire Bakuba.
Jina la Empire Bakuba lilitokana na mashujaa wapiganaji wa makabila ya  Kongo.

Katika miaka hiyo ya 1970 Empire Bakuba na Zaiko Langa Langa ndizo zilikuwa zakitikisa jiji la Kinshasa vilivyo na kujizolea umaarufu mkubwa kwa wapenzi wa muziki wa dansi.

Vibao vya Dadou cha  Pepe Kalle na  Sango ya Mwa ya Papy Tex, iliiweka Empire Bakuba kwenye chati na ikaanzisha mtindo wa Kwasakwasa.

Mwaka 1982 yalipofanyika maadhimisho ya miaka kumi ya bendi hiyo, Empire Bakuba ilipigiwa kura na ikashinda kuwa bendi bora huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zamani Zaire.

Miaka ya 1980 Bakuba ilijizolea wapenzi na mashabiki lukuki ikishirikiana na Nyboma Mwandido kurekodi wimbo wa Moyibi mwaka 1988 wimbo ambao uliiongeza bendi hiyo umaarufu katika nchi zinazozungumza lugha ya kifaransa huko Afrika ya Kati na Magharibi.

Album ya Roger Milla iliyokuwa ikimuenzi na kumsifia mchezaji wa mpira wa miguu Roger Milla ambaye alichezea timu yake ya taifa ya Cameroon akiwa na umri mkubwa kuliko wote mwaka 1990.

Miaka ya 1990 Pepe Kale alitoa album zingine za Gigant Afrique Lager than Life na Cocktail. Nyimbo zingine zilikuwa za Hidaya, Sintia,  Reovisie, Guy guy na Yanga Afrika. Nyimbo zingine zilizotikisa masikio ya wapenzi zilikuwa La- rhumba,Don't Cry  Yaja, Zouke Zouke Nakutuna na Pon moun Paka Buoge.


 Empire Bakuba ilifanya ziara  sehemu mbalimbali za nchi hiyo ya  Kongo (DRC) na hata nje ya nchi hiyo.

Kama wanamuziki wengine Pepe Kalle ailiwashirikisha wanamuziki wengine wakongwe katika tasnia ya muziki akina Simaro Lutumba na Nyoka Longo.

Bendi ya hiyo ya Empire Bakuba ilitoweka katika sura muziki baada ya kifo cha kiongozi wake Pepe Kalle.

Watanzania tutaendelea kumukumbuka Pepe Kalle ambaye alipotua Tanzania, ilitunga nyimbo kupitia lugha ya Kiswahili, za Yanga Afrika, akisifia Klabu ya  Yanga iliyokuwa ikitajwa mfadhili wa klabu hiyo  Abbas Gulamali, Hidaya, wimbo alioimba akilalamika kupoteza mkanda wake wa kiuno na  mpenzi Bupe, aliutunga alipotoka jijini la Mbeya kufanya onyesho.

Wizkid, Tiwa Savege Kwenye Ardhi ya Tanzania



Staa wa muziki kutoka Nchini nigeria Ayodeji Ibrahim maarufu kama Wizkid aneyetamba na wimbo wa Joro amethibitisha kuwepo kwenye grand final ya wasafi festival katika viwanja vya posta kijitonyama usiku wa leo Jijini Dar es Salaam.

Staa huyo amethibitisha kupitia insta srory ya ukurasa wake wa instagram kwa kuandika "Tanzania see you"

Kwake ni mara ya pili kuja kutumbiza Tanzania ambapo kwa  mara ya kwanza alitumbuiza katika tamasha la Fiesta mwaka 2016 na mwaka 2019 anatumbuiza katika tamasha la wasafi Festival.

Mpenzi mpya wa vanessa mdee aanza kuposti mashemeji
Staa huyo atakamilisha orodha ya mastaa wawili kutoka nchini Nigeria ambapo tayari Tiwa savage ameshawasiri nchini jana usiku kwaajili ya kutumbuiza katika tamasha hilo.

Makala: WCB watembea na PENSELI, jibu la Ali Kiba litawasogeza au kuwavuruga?
Aidha msanii kutoka nchini Congo Innos B anayetamba na wimbo wa Yope aliomshirikisha Diamond Platnumz anatarajiwa kutumbuiza katika tamasha hilo huku akiungana na wasanii wengine wa bongo fleva.

Saturday, November 9, 2019

Friday, November 8, 2019

Zijue sifa za mwanaume ambaye hana malengo na wewe katika mahusiano ya kimapenzi


Mara nyingi unapokuwa katika mahusiano ya kimapenzi basi mwanaume ambaye hana malengo na wewe katika mahusiano yenu basi utmajua kwa kuangalia mambo yafuatayo;

Anakwepa mazungumzo ya ndoa.
Haonyeshi kufurahi unapoanzisha mazungumzo kuhusu suala la kufunga ndoa na wala hapendi kuzungumzia hilo. Wakati mwingine hata kukutambulisha kwa ndugu zake au rafiki inakuwa shida.

Anagharamia anasa kuliko mambo muhimu.
Anakuwa ni mtu wa kukununulia mapambo ya gharama na vitu vyote vya anasa, lakini hana mawazo ya kuzungumzia maisha yenu ya baadaye wala kukununulia vitu ambavyo vitakuwa na manufaa katika maisha ya mbeleni. Haangalii masuala ya elimu wala kukutafutia mtaji au kazi.

Hajali machozi yako.
Unaweza kugundua ni jinsi gani hana mpango mzuri na maisha yako, kwani hata anapokuudhi anakuwa hajali wala haumizwi na machozi yako, ni busara kuwa makini kwa sababu huyo atakuwa ni mtu wa kukupa maumivu wakati wote.

Hajitokezi hadharani
Mwanaume ambaye malengo yake ni kukuchezea huwa hataki mapenzi yenu yajulikane hadharani atakuwa mtu wa kutaka mambo yaende kwa siri. Hajitambulishi kwa rafiki wala kwa ndugu zako. Hatoi nafasi ya wewe kumtembelea nyumbani kwake wala kuwajua wale wa karibu yake na familia yake.

Hana mpango na watu wako
Mwanamume anayekupenda atajishughulisha na mambo yanayohusiana na watu wako wa karibu, hususan ndugu, jamaa na marafiki zako.  Utabaini kuwa mwanamume huyu haulizi swali lolote kuhusiana na familia yako au marafiki zako, basi tambua kuwa hana mpango wowote wa maana na wewe. Kumbuka mwanamume akikupenda hujaribu kuwafahamu na kuwapenda watu wako, maana amependa boga na sheria ni kwamba lazima upende na ua lake.

Hakumbuki lolote la maana
Ni wazi kuwa hujakaa sana na mwanamume huyu, lakini angalau kuna mambo muhimu umefanya naye ambayo anapaswa kuyakumbuka. Kama hawezi kukumbuka tarehe muhimu za uhusiano wenu,  basi yamkini mwanamume huyu hana mpango wowote wa dhati wa kuendelea kuwa nawe.
Source

Kwanii Wanaume Waaminifu Kwenye Uhusiano Huachwa.....


Kuachwa na mpenzi kwa sababu umekuwa ni muaminifu sana yaonekane ni jambo lisiloingia akilini lakini linatokea.

Moja ya mambo ya ajabu unayoweza kuwa ushawahi kuyasikia ni kwamba mara nyingine uamuzi wako wa kuwa mwanaume mwema sana na unayejitahidi kufanya uhusiano wako wa kimapenzi uwe mzuri muda wote unaweza kukugharimu na kujikuta unaachwa kabisa.

Haitakiwi kuwa hivyo lakini mara nyingine inatokea, na inatokea kwa sababu wazo la mwenza wako kuhusu uhusiano wa kimapenzi laweza likawa tofauti na ulionao wewe. Wengine wana mawazo hasi kuhusu jinsi uhusiano/ndoa inavyotakiwa kuwa.

Hii ndio sababu hutakiwi kuanzisha uhusiano wa kimapenzi na mtu asiye na vipaumbele sawa na vya kwako au asiye na mtazamo mmoja wa kimaisha kama ulionao wewe.

Usipozingatia hilo, utajikuta unaingia kwenye uhusiano na mtu ambaye hatakujali vya kutosha kwakuwa labda humfokei au kumpiga anapokukosea – au utajikuta ameshakupanda kichwani na kuanza kukudai mambo ambayo huwezi kuyatimiza lakini ukajikuta unajitutumua kumtimizia kwa sababu unataka kumfurahisha mpenzi wako na analijua jambo hilo.

Kwa sababu baadhi ya wanaume wanapenda kulinda siri na kuwaachia uhuru wapenzi wao, wanajikuta wakiwapa ruhusa wanawake zao kwenda popote wanapojisikia bila kuwafatilia wanachofanya.

Nini kinafata baada ya hapo? Mwanamke anatoka, anatafuta mchepuko na kukusaliti. Mwisho inakufanya wewe mwanaume uonekane mjinga mbele ya wengine.

Tatizo ni kwamba tabia hii inaibuka kutokana na mazoea ya watu kuingia kwenye uhusiano wakiwa wameficha tabia zao halisi na kuja kufungua makucha yao baada ya kuona ameshaishi na wewe kwa muda mrefu kiasi kwamba huwezi tena kumuacha.

Hii inasababisha wanaume walioathirika kutokana na tabia kama hizi kutoka kwa waliokuwa wapenzi wao wasiweze kuwaamini wanawake wengine tena kwa kuona kwamba wote ni sawa na wale waliowaumiza na kusababisha wasiweze kuwaonesha wenza wao wapya mapenzi kwa kiwango cha juu wakihofia kuumizwa tena.

Kuwa mpole, mkarimu na mwenye upendo wa hali ya juu kwa mpenzi wako ndio jambo linalotarajiwa kwenye uhusiano. Mtu hatakiwi kufanywa ajisikie vibaya kwa kumuonesha mapenzi ya kweli mwenza wake.

Kama wewe unakuwa muaminifu na mwema kwa mpenzi wako lakini umekuwa unadharauliwa au ukaachwa kutokana na tabia hiyo, kaa ukiwa na amani kabisa kwamba lawama za kuvunjika kwa uhusiano huo hazikuhusu wewe – lawama ni za mpenzi wako aliyeshindwa kujua wewe umekuwa mwema kiasi gani kwake.

CHADEMA WATANGAZA KUTOSHIRIKI UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA KWA MADAI YA KUFANYIWA RAFU


Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetangaza  kujitoa katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika November 24, mwaka huu. Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe ametangaza uamuzi huo leo kwa madai kuwa uchaguzi huo ni batili na wakishiriki watahalalisha ubatili huo.


Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe ametangaza uamuzi huo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma ambapo amesema sababu kubwa ni wagombea wa chama hicho kuenguliwa kwa sababu mbalimbali.

Mbowe amesema mara baada ya kikao cha Kamati Kuu ya chama hicho na wabunge, maazimio waliyokubaliana ni kugomea uchaguzi huo sababu majina ya wagombea wengi kukatatwa.

"Sisi kama chama tumeamua hatutashiriki zoezi hili na ninatoa amri kama Mwenyekiti wa viongozi na wagombea nchi nzima wasitishe kugombea na wasitishe kukata rufaa.

"Waachane na kuweka mapingamizi hatupo tayari kubariki ubatili." amesema Mbowe.

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unatarajiwa kufanyika Novemba 24, mwaka huu.


Wednesday, November 6, 2019

Dalili kuu 7 zinazoonyesha mtu ambaye atachelewa sana kufanikiwa

1. Siku zote ana pesa za kununua vocha na kuweka vifurushi,ana pesa za kununua nguo  lakini hana PESA za kununua kitabu kitakachomuongezea maarifa.

2. Siku Zote ana muda wa kuchart watsapp, kuangalia Movie, kusoma magazeti na Kupiga stori za mpira ama za wasanii lakini hana MUDA wa Kusoma kuhusu taaluma yake ama mambo ya kumuongezea ujuzi.

3. Siku zote akiona waliofanikiwa anawatuhumu aidha wameiba, ni freemason ama wana bahati katika maisha. Huwachukia na hataki kujifunza Kwao.

4. Siku zote hupenda kuhalalisha kufeli kwake kwa kujitetea, kulaumu uchumi, wazazi, serikali au amerogwa.

5. Siku Zote Hujiona anajua Kuliko Mtu Yeyote Yule na hapendi Kujifunza kwa wengine. Huongea sana Kuliko Kusikiliza.

6. Kila anachoingiza anatumia, ukimwambia kusave ama kuwekeza anasema ngoja nipate cha ziada nitaanza kesho.

7. Anajua mambo mengi sana, anajua stori za mafanikio, anasoma vitabu lakini hafanyii kazi ama anafanyia kazi kidogo sana katika kile anachokijua.

Je Unayo dalili mojawapo kati ya hizo? Amua kubadilika ishi au fanya ukijua kesho ipo .... NDOTO YAKO INAWEZEKANA, CHUKUA HATUA.
Source

China, Ufaransa zasaini mikataba ya kibiashara

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron na Rais wa China Xi Jinping wametangaza leo kusaini mikataba mikuu ya kibiashara mjini Beijing ya kiasi cha thamani ya dola bilioni 15.

Mikataba iliyosainiwa ni ya sekta za usafiri wa angani, nishati na kilimo. Kampuni 20 za Ufaransa zilipewa idhini ya kuuza nyama ya kuku, ng'ombe na nguruwe nchini China.

Macron na Xi wametangaza mikataba hiyo katika kikao cha wanahabari kama sehemu ya ziara ya kiongozi huyo wa Ufaransa nchini China.

Habari hizo zimekuja wakati kukiwa na ongezeko la mivutano ya kiuchumi kati ya China na Marekani.

Xi amesema katika taarifa kuwa viongozi hao wawili wametuma ujumbe thabiti kwa ulimwengu kuhusu umuhimu wa kuhimiza ushirikiano wa kimataifa na biashara huru pamoja na kushirikiana katika kujenga demokrasia za wazi.

Aidha, Viongozi hao wawili walitoa taarifa ya pamoja wakielezea kuunga mkono Mkataba wa Paris kuhusu Mazingira uliotiwa saini 2015 wakiutaja kuwa usioweza kubatilishwa.

Marekani ilianza rasmi mchakato wa kujitoa rasmi wiki hii.

Naombeni Msinilaumu kwa Uamuzi Huu Niliouchukua kwa Mume Wangu

Mimi nimeolewa miaka 15 sasa na tumejaaliwa watoto 4. Ndoa yetu ilipofikisha miaka 4-5 mume wangu alicheat, nikamkamata through sms akapinga sn lakini baadae alikubali akakiri kosa na kuomba msamaha. nikamsamehe

Tumeendelea kuishi na nilipopata mtoto wa tatu akanicheat tena, safari hii alikuwa nje ya nchi kimasomo, napo alikiri na kuomba msamaha, nikamsamehe

wakati niko mjamzito mimba ya mtoto wa nne alinicheat tena, kibaya zaidi alinicheat na house girl wng akampa ujauzito. kwa ivo wkt mimi nina mimba na House girl naye mjamzito(japo sikujua km house girl alikuwa mjamzito kwani aliondoka nyumbani) niligundua baadae kuwa mtt wa aliyekuwa house Girl wangu ni wa mume wangu

kama kawaida yake akaomba msamaha safari hii hadi kupiga goti na kulia ili nimsamehe...na mimi kwa kuwa bado nampenda na nimemvumilia kwa mengi nikaamua kumsamehe tena..ila tulikubailana masharti mengi na akakubali masharti yote niliyompa..mwanzoni alibehave vizuri sn akawa muwazi kwng hanifichi chochote kuhusu huyo mtt.. na tuliishi maisha ya furaha kwn alinijali mno na alionekana kweli amerigrate.
sasa cha kushangaza siku za karibuni amebadilika san, amekuwa msiri na hasemi chochote kuhusu huyo mtt wa nje..siku hizi anatuma hela kwa siri na pia anawasiliana na huyo mama wa mtoto kwa siri haniambii chochote..

nilipoona mabadiliko niliamua kumuuliza imekuwaje tena mbona siri tena wkt tulikubaliana kila kitu kiwe open? hakunijibu isipokuwa alikuwa mkali na kufoka na kusema hilo swala tumeshamalizana nalo sitaki kulisikiasikia tena..
nikajaribu tena siku nyingine kumuuliza na majibu ndio hayo hayo, kwa kifupi hataki na anakwepa kuzungumzia hilo suala kabisa...sasa najiuliza kwa nini anafanya siri? km hakuna jambo lolote baya basi anaficha nini? ina maana kuna kitu zaidi ya mtoto.

Sasa jamani mimi nimeamua km ifuatavyo
1. Na mimi nimeamua kuwa na mahusiano nje ya ndoa, jamani msinilaumu nami pia nahitaji kuliwazwa na kufarijiwa kwa kifupi nimechoka na mastress yasiykuwa na mwisho, sikuwahi kumcheat mume wng ktk maisha yote ya ndoa. ila sasa atanisamehe tu ht akijua wl sijali, nipo tayari kwa lolote..
2. Sina mpango wa kuondoka kwenye nyumba tuliyojenga pamoja nitaishi hapa hapa kwani sipendi wtt wng walelwe na mzazi mmoja..wtt hawajui kinachoendelea in fact hata ndugu na jamaa hawajui chochote kwani mimi sijawaambia na wala sijawahi kuwaeleza matatizo ya ndoa yng..kwa nje tunaonekana familia iliyobarikiwa na ina furaha lkn wenyewe ndio tunaojua ndani kukoje
3. Kwa sababu sisemagi matatizo yangu kwa ndugu na marafiki nimeamua kuweka hapa labda nitapunguza kitu fulani kichwani kwani sometime naona km nazidiwa mawazo vile

Tuesday, November 5, 2019

ZANTEL YAZINDUA SIMU JANJA IJULIKANAYO KAMA SMARTA YENYE UWEZO WA 4G NA GHARAMA NAFUU



Mkuu wa Bidhaa na Bei wa Zantel, Aneth Jamila Muga (Julia),akionyesha simu janja na ya gharama nafuu ya SMARTA iliyozinduliwa na Zantel mjini Zanzibar. Simu hii inayonunuliwa ikiwa na GB 12 intaneti inayowezesha matumizi ya mwaka mzima inapatikana kwa shilingi 39,999/- nchini pote. Wengine pichani ni wafanyakazi wa Zantel 

**
Katika jitihada zake za kuongeza wigo wa watumiaji wa simu janja nchini Tanzania, Zantel imezindua simu janja yenye uwezo wa 4G na gharama nafuu sana sokoni ijulikanayo kama SMARTA.

Akiongea wakati wa hafla ya uzinduzi, Mkuu wa Bidhaa na Bei wa Zantel, Aneth Jamillah Muga, alisema simu iliyozinduliwa imetengenezwa kwa teknojia zinazowezesha matumizi ya programu za simu janja zinazowezesha kupata programu za kuelimisha na kuburudisha kama vile, WhatsApp, Facebook, YouTube, Google na inapatikana kwa bei nafuu ya shilingi 39,999/-.

Alisema simu ya SMARTA ni aina mpya ya simu katika soko la Tanzania inayowezesha kuongeza idadi ya watumiaji wa simu janja nchini kote na kuleta mabadiliko ya kidigitali kwenye jamii.

"Tumezindua simu aina ya SMARTA katika soko kuwezesha wananchi wengi kumudu kumiliki simu janja sambamba na kuwapatia fursa ya kufurahia maisha ya kidigitali kupitia mtandao wa 4G+ wa Zantel". Alisema Muga.
Muga, alisema kuanzia sasa simu janja zijulikazo kama SMARTA zinapatikana katika maduka yote ya Zantel yaliyopo Pemba, Unguja, na Tanzania bara na zinanunuliwa zikiwa tayari zimeunganishwa na intaneti ya bure yenye GB 12 itakayowezesha mteja kuitumia kwa kipindi cha miezi 12.

Mkuu wa Zantel Zanzibar,Mohammed Mussa Buacha, alisema kuzinduliwa kwa simu mpya za SMARTA ni moja ya mkakati wa Zantel kuleta mapinduzi ya kidigitali na kuwezesha kupatikana teknolojia za kisasa kwa gharama nafuu nchini kote. Alisema Zantel inaamini kuwepo kwa bidhaa za kisasa kwa matumizi ya huduma za kidigitali kunabadilisha maisha ya wananchi kuwa bora.

''Kupitia mapinduzi ya kidigitali yanawezesha kupata elimu, taarifa za afya, burudani, huduma za kifedha na kwenye intaneti inawezesha kujua mambo mbalimbali yanayotokea katika maisha yetu ya kila siku. Dira ya Zantel ni kuwezesha upatikanaji wa huduma za kidigitali kwa manufaa ya wateja wetu wapya na wa zamani". alisisitiza Mussa.

Alisema kupatikana kwa simu za gharama nafuu za SMARTA, ni suluhisho la kuwezesha watanzania wengi kuweza kumudu kumiliki simu janja nchini na kuwezesha kuendeleza matumizi ya huduma za kidigitali Zanzibar "Kuanzia sasa Watanzania hawana sababu ya kuwa na vikwazo wanapotaka kununua simu janja".

Zantel imekuwa mstari wa mbele kuwekeza katika ubunifu kwendana na ongezeko la watumiaji wa huduma za data na kuunganishwa kwenye intaneti yenye kasi kubwa ambapo ili wengi wafurahie huduma hizo kunatakiwa kuwepo simu janja za gharama nafuu.

Monday, November 4, 2019

Rais Magufuli " Usijifanye Muhimili, Kaliheshimu Bunge"



Rais Dkt. John Pombe Magufuli amemuapisha Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali, Charles Kichere, leo Novemba 4 Ikulu Jijini Dar es Salaam na kumpa maagizo katika kazi yake mpya.

Moja ya maagizo aliyompa ni kuhakikisha anasuka upya uongozi ndani ya taasisi hiyo ili kuhakikisha kuwa inafanya kazi kulingana na sheria na maagizo  ya mihimili inayoongoza nchi.

Maagizo mengine aliyopewa ni, "CAG nenda kafanye kazi huko, usije ukajifanya na wewe ni muhimili mwingine, mihimili ni mitatu na umeshaiona hapa. Nafasi yako ni Mkaguzi Mkuu wa Serikali, kafanye kazi zako vizuri bila ya kuonea watu.

 "Unapopewa kazi na mihimili mingine kama Bunge au Mahakama kaitekeleze usibishane nao wewe ni mtumishi. Kasimamie hiyo ofisi kuna baadhi ya watendaji wako wanapokwenda kukagua kwenye balozi wanaomba fedha, sasa nenda kawachambue." Amesema Rais Magufuli.

Aidha, amesema Rais ana mamlaka ya kumtoa CAG kulingana na Katiba na Sheria akieleza kuwa upo uwezekano wa mtumishi wa nafasi hiyo kutolewa muda wowote hata chini ya miaka mitano.

"Unaweza kumaliza miaka yako mitano au ukaishia mmoja. katika maisha ya duniani huwezi ukapewa mamlaka ya kuteua halafu usiwe na mamlaka ya kutengua, sikutishi lakini wewe nenda kafanye kazi zako"

Kuhusu suala la rushwa, Rais Magufuli amesema, "lakini pia kasimamie hiyo ofisi kuna baadhi ya watendaji wako wanapotumwa kwenda kukagua kwenye balozi wanalipwa pesa hapa na wakifika huko nako wanaomba pesa, ofisi ya CAG sio safi kama mnavyofikiri".

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...