Kampuni ya #Boeing imeanza kushughulikia muundo wa ndege mpya
ya abiria yenye uwezo wa kwenda kasi mara tano ya sauti #Hypersonic.
Tangu kustaafishwa kwa ndege za abiria aina #Concord (supersonic transport) ambazo zilikuwa na uwezo wa kufanya safari zake kwa nusu ya muda unaochukua ndege za sasa, kampuni nyingi zinazo jishughulisha na uundaji wa vyombo vya usafiri wa anga vinajaribu kubuni ndege tofauti tofauti zenye uwezo wa kwenda kasi zaidi ya Concord huku zikitoa udhaifu ulikuwepo wa kelele, uchafuzi mazingira na ulaji mdogo wa mafuta.
Kitendo cha kuunda umbile na injini zitakazoweza kufanya kazi katika kasi inayozidi mara tano ya sauti (zaidi ya 5500km/h) imekuwa ni suala gumu kwani linahitaji fedha nyingi na muda katika uwekezaji na utafiti.
Chombo chochote cha usafiri wa anga kinachotaka kufika mwendokasi huo inahitajika malighafi tofauti katika uundaji wake kama #Titanium ili kukabiliana na joto kali linalosababishwa na msuguano wa chombo husika na hewa.
Kampuni Boeing imekuja na mchoro wa ubunifu wa ngamizi kuonesha ndege hiyo ambayo inategemea kufika mwendokasi zaidi ya 6000km/saa huku ikitumia injini ya #TurboRamjet ambayo ni 'modification' ya ile ambayo awali ilitumika kwenye ndege ya kijasusi aina ya #SR71 "Blackbird" ambayo itakuwa inafanya kazi kama injini ya kawaida ikiwa #Supersonic chini ya mwendokasi wa 4000km/saa na baadae kufanya kazi kama #Ramjet ikifika kasi mara tano ya sauti 'Hypersonic speed' (kuanzia 5000km/saa) kwa kufunga vidirisha upande wa feni za injini hiyo kwakuwa haziwezi tena kufanya kazi katika mwendokasi huo na kuruhusu hewa yenye kasi kuingia moja kwa moja kwenye injini na kuchomwa pasipo kuhitaji mkamizo 'compression' ya injini za kawaida.
Wanasema ndege hiyo itakuwa inaenda usawa wa futi 95,000 kutoka usawa wa bahari na kasi ya 6000km/saa.
Ndege za kisasa kama #Boeing787 #Dreamliner na #Airbus350 #XWB zina uwezo wa kwenda hadi futi 43,000 kutoka usawa wa bahari na kasi ya 930-950km/saa
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
