Friday, August 30, 2019

MWENDESHA BODABODA ALIYEFARIKI KWA AJALI AZUA GUMZO KUACHA WAJANE 'Wake' 6 NA WATOTO 30

Siri nyingi hufichuka wakati ambapo binadamu anafariki kwani licha ya kuwa ni kinyume na itikadi kumuanika aliyeaga dunia, mambo mengine hasa ya kifamilia huwa vigumu kuyaficha. 


Hayo ndiyo yalifichuka baada ya dereva mmoja wa bodaboda aitwaye Hassan Mafabi (51) mkazi wa Nakatundu Kangulumira nchini Uganda kufariki dunia kwenye ajali ya barabarani pikipiki yake kugongana na gari siku ya Jumamosi wiki iliyopita.

Bodaboda huyo alikuwa na wake 6 na watoto 30 licha ya kazi yake yenye malipo ya wastani hali iliyosababisha watu wengi kushangaa ni vipi aliweza kutekeleza mahitaji ya wake hao wote. 

 Wengi wamepigwa na butwaa baada ya matangazo kuwafikia kuhusu mchango wa kusaidia familia ya marehemu kwani ameacha wajane sita na watoto 30.


Hassan Mafabi mwenye umri wa miaka 51 alikuwa akiishi na wake hao sita na watoto wake na kuchapa kazi kama kawaida huku wengi wasijue kuwa alikuwa na familia kiasi hicho.

 Kulingana na Ugandanz.com, Mafibi aliishi katika kijiji kimoja nchini humo tangu kifo chake barabarani ambapo aligongwa na gari. 


Askofu wa kanisa la Mukono nchini humo alidhibitisha kisa hicho na kuwataka marafiki kujitokeza kuisaidia familia ya Mafibi kwani yeye ndiye alitegemewa kuilisha. 

Wengi hata hivyo walishangaa ni vipi mwendesha bodaboda huyo aliweza kuwalisha wake hao pamoja na watoto 30 ikizingatiwa mapato ya biashara ya bodaboda ni ya wastani tu.

Harmonize Huu ni muda wa kuungana Na Clouds (CMG),Utafika mbali Bro.


Hey Guys...

I Hope mko poa wakubwa,,,Ryt,,??

Okay Fresh

Najua watu wengi nikiwemo Mimi wanajiuliza,Je Ngoma za Harmonize zitaanza kupigwa Clouds baada ya kujitoa kwenye lebo ya hasimu wao?

Hilo swali wengi hatuna majibu.

Nakumbuka kipindi bifu la Diamond na Alikiba linaanza lilikuwa ni bifu kubwa sana Kutokana na ushindani ulio kuwepo,Clouds walijitahid kukuza bifu lile ili angalau kumpunguza nguvu Diamond,kweli kipindi cha mwanzoni lile bifu Nahisi Hata Mond Mwenyewe lilimtetemesha kidogo japo hakutaka kujionyesha wazi,

Hilo bifu liliendelelea ila mwisho wa siku mshindi alikuja kupatikana ambaye kila mmoja anamjua Ni Simba AKA Dangote,Moja ya sababu kubwa za Alikiba kushindwa ni Kutokana na mziki wake kutokuwa na ubunifu,pia utoaji wa nyimbo ukawa ni hafifu kwa madai kuwa nyimbo zake zina ishi so hawez kutoa track kila muda,Hali hiyo ilikuwa tofauti kwa upande wa pila ambaye ni mshindani wake,Diamond Platnumz,yeye aliamini kabisa mziki ni biashara na kama ni biashara lazima ahakikishe walaji wake (Mashabiki) kila baada ya muda flani awape Chakula kipya,Mtindo huo wa Alikiba ilifikia hatua Hata wanao msapoti waachane naye wakiwemo clouds wenyewe wakabaki wanamsapoti kishingo upande,

Mpaka Muda huu Mziki huu wa bongo hauna ushindani tena Bali wamebaki wale wanao mchukia Diamond na kujifanya eti wao ni team mziki mzuri (Team kiba).

Kwa mtazamo wangu hapo juu ni kuwa Harmonize kwa uwezo alionao ni kwamba ana uwezo kwa 70℅ kumtetelesha Diamond endapo akichanga karata zake vizuri,Harmonize anacho takiwa kufanya ni kuwa karibu na clouds na kwa uwezo alio nao wa kuimba na kuachia song back to back naona kabisa Clouds wanamhitaji Konde boy kuliko Alikiba,Alikiba hakuwa chaguo sahihi Bali Jamaa alibebwa na wanao mchukia Diamond ila hawakuwa mashabiki.

Simaanishi Harmonize Anaweza kuwa Sawa na Diamond ila akicheza vizuri Anaweza fika mbali coz Jamaa tayari ana connections na wasanii wengi kwa sasa tofauti na Rich mavoko aliye ondoka akiwa hajajijenga vizuri.

Harmonize Najua kwa Muda huu mfupi atayumba ila akichanga karata zake vizuri Anaweza kuwa mkubwa zaid ya alivyo kuwa WCB,Anacho takiwa kukifanya ni kusimama mwenyewe na kutumia njia zile alizo jifunza kwenye chuo (Lebo yake WCB).

Harmonize Hizo views ulizo kuwa unapata kule You tube hazikuwa zako Bali zilikuwa za Diamond so zisikuteteleshe na kukukatisha tamaa baada ya kuona zimepungua,Huu ni Muda wa kutengeneza views zako ili uone ukubwa wako.

JF
Source

Nogesha mahusiano yako ya kimapenzi kwa kufanya mambo haya



Kutengeneza uhusiano wenye nguvu ni moja ya mambo yenye changamoto kubwa. Japo hakuna maelekezo maalum, kuna mambo machache na rahisi ambayo unaweza kumwambia mpenzi wako yakaujenga zaidi. Weka desturi ya kusema mambo haya kwa mpenzi wako na muda mfupi tu mtakuwa couple itakayowapa wivu marafiki zetu.

Nakupenda
Nakupenda ni kitu rahisi na cha wazi cha kumwambia mpenzi wako. Hakikisha tu kuwa unamaanisha. Jaribu kulisema neno hilo pindi mpenzi wako anapokuchekesha au pale anapofanya kitu kinachokukumbusha kwanini mko pamoja.

Nilikuwa nakuwaza
Ni muhimu kumjulisha mpenzi wako kuwa unamuwaza hata kama hamko sehemu moja. Ukiona kitu kizuri au cha kuchekesha katika siku yako ambacho kinakufanya umkumbuke, mjulishe.

Siku yako ilikuaje?
Muulize masuala ambayo mpenzi wako anakutana nayo katika shughuli za kila siku. Muulize kuhusu huyo mfanyakazi mwenzie anayemkera au kazi kubwa waliyokuwa wakifanya. Kumpa nafasi mpenzi wako kushare sehemu zingine za maisha yake kutasaidia kuunganisha dots kati ya muda mnaokuwa pamoja.

Nakuunga mkono
Mpe moyo mpenzi wako kwa kumjulisha kuwa unaunga mkono maamuzi yake. Unaweza ukaenda mbali zaidi kwa kujaribu kumsaidia afanikishe malengo aliyojiwekea. Maisha yamejaa vikwazo vingi, na ile hisia kuwa una mtu mwingine upande wako zinaweza kukusaidia kuvivuka. Msiwe couple tu, kuweni timu. Kumkumbusha mpenzi wako kuwa upo nyuma yake kutaimarisha uhusiano wenu.

Umependeza
Kama umekuwa kwenye uhusiano kwa muda mrefu, ni rahisi kujisahau katika mengi. Ni muhimu kumkumbusha mpenzi wako kuwa anakuvutia. Kumjulisha kuwa 'gauni hilo limekupendeza sana' kutamfanya ajisikie vizuri na kukumbusha kwanini ulimchagua yeye.

Samahani
Kila mtu hukosea wakati fulani. Wakati mwingine hujikuta tukiongea maneno kwa hasira na baadaye kugundua kuwa hatukuwa sahihi. Ubishi hauna nafasi kwenye uhusiano wenye furaha, hivyo omba msamaha unapofanya kosa. Omba msamaha kwa kukasirika. Omba msamaha kwa kuumiza hisia za mpenzi wako. Omba msamaha hata kwa vitu ambavyo sio kosa lako.
Hakuna kama wewe
Mpenzi wako anatakiwa kuwa rafiki yako. Kama hautaki kutembea naye, basi hamkupaswa kuwa kwenye uhusiano. Mfanye mpenzi wako ajue kuwa yeye ni bora na hakuna kama yeye.

Napenda mawazo yako
Mwambie mpenzi wako kuwa unapenda mawazo yake. Mjulishe kuwa unaona ana akili, mcheshi, anajua kupenda na ana kipaji.

Nakuheshimu
Kama ulivyo uhusiano wa marafiki, heshima ni kitu muhimu kwako na mpenzi wako. Mpe nafasi ya kukushauri au kukupa mawazo kwenye mambo yanayokutatiza. Mtu anapohisi anaheshimiwa, hujisikia pia furaha na salama, vitu ambavyo ni muhimu kwenye uhusiano wowote mzuri.

Usiku mwema
Tunaishi kwenye wakati ambapo mawasiliano ni rahisi mno. Kwa kubonyeza tu kitufe tunaweza kutuma ujumbe kuvuka bahari, hivyo hakuna kisingizio cha kushindwa kusema 'usiku' mwema.
Haimjulishi mpenzi wako tu kuwa unataka kulala, bali pia inamjulisha kuwa unamfikiria. Hata kama hamjaongea siku nzima na hasa kama mmejibizana, maliza siku na kishindo chanya.

Friday, August 23, 2019

WAZEE WATANO WAKAMATWA WAKIFANYA NGONO HADHARANI WAKIMCHANGIA MWANAMKE MMOJA


Wazee sita wenye umri wa kuanzia miaka 62 hadi 85 wamekamatwa na polisi baada ya kukutwa wakifanya mapenzi kwa kuchangia mwanamke mmoja hadharani.



Wazee hao, wanaume watano walikamatwa wakifanya mapenzi na mwanamke pekee mwenye umri wa miaka 85.

Mume wa mwanamke huyo naye alikuwa kwenye kundi la wanaume watano walioshiriki mapenzi hadharani.

Kwa mujibu wa polisi watuhumiwa hao ni Daniel Dobbins(67)OttoWilliams(62), Charles Ardito(75), John Linartz (62), Richard Butler(82) na mkewe JoyceButler (85).

Watuhumiwa hao walikamatwa wakifanya uhalifu huo kwenye Hifadhi ya Grace Richardson iliyopo mji wa Fairfield na wamefunguliwa mashitaka kwa kufanya vitendo vyenye kuvuruga amani.

Hata hivyo, watuhumiwa wote hao waliachiwa kwa dhamana baada ya kuahidi kufika mahakamani wenyewe.

Dobbins aliwahi kukamatwa 2017 baada ya polisi kupata taarifa za kuonekana akitembea uchi kwenye hifadhi nyingine.


Polisi walipofika eneo la bustani walimkuta Dobbins akiwa uchi kwenye gari yake na walipomuhoji alidai anafanya hivyo kwa lengo la kupata tiba.

Uchaguzi Wa Serikali Za Mitaa Kufanyika November 24,2019

Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.

Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemani Jafo amesema uchaguzi wa serikali za mitaa utafanyika Novemba 24, 2019.

Jafo ametangaza tarehe ya uchaguzi huo leo Ijumaa Agosti 23, 2019 wakati wa mkutano wake na wakuu wa mikoa, makatibu tawala na wadau mbalimbali uliolenga kutoa maelekezo na tangazo la uchaguzi huo.



Amesema kuwa tangazo hilo ni kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi ibara ndogo ya 4,1 hadi 3 chini ya tangazo la serikali number 371  na kuendelea huku akisisitiza muhimu elimu ya mpiga kura  kutolewa  kwa wakati.

Amesema kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi uandikishaji wapiga kura utaanza siku 47 kabla ya siku ya uchaguzi na utadumu kwa siku saba.

Amesema upigaji kura utaanza saa 2.00 asubuhi na kuhitimishwa saa 12.00 jioni.

Waziri Jafo amesema viongozi watakoma uongozi wao  siku saba kabla ya siku ya  kuchukua fomu za kugombea.

Amesema waangalizi wa uchaguzi wataruhusiwa baada ya kupata kibali kutoka kwa katibu mkuu Tamisemi na maombi yatatakiwa  kupata kibali kwa katiba mkuu ndani ya siku 21 baada ya tangazo la uchaguzi kutoka.

Amesema kampeni sitafanyika siku saba kabla ya tarehe ya uchaguzi wa serikali za mitaa.



Awali akimkaribisha mgeni rasmi kutoa tangazo hilo katibu mkuu wa TAMISEMI Mhandisi  Joseph Nyamuhanga amesema kanuni zote za uchaguzi zimekamilika  hadi sasa.

Akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wakuu wote wa mikoa nchini mkuu wa mkoa wa singida Dkt.Rehema Nchimbi amesema wako tayari katika maswala ya kiusalama,ulinzi na Amani sanjari na taarifa sahihi na za wakati kwa watu wote bila upendeleo na ubaguzi na utakuwa uchaguzi wa uhuru ,haki na uwazi. 



Wakizungumza mara baada ya tangazo hilo baadhi ya viongozi wa vyama tofauti wamesema kuwa huu ndiyo wakati muafaka wa kujipanga kwaajili ya uchaguzi huo. 



Ikumbukwe kila baada ya miaka mitano Tanzania bara  hufanya uchaguzi wa serikali za mitaa katika ngazi ya kata ,vijiji na mitaa kabala ya uchaguzi mkuu wa wabunge na rais miezi michache baadaye.


Thursday, August 22, 2019

Wasafi Tuwekeni Wazi Mashabiki Kwa Hili

 

Moja kati ya vitu ambavyo mashabiki tulivipokea kwa furaha sana ni hatua ambayo @diamondplatnumz 

alipoamua kuanzisha lebo ya #WCB lengo kubwa lilikuwa ni kuinua sanaa ya Tanzania na kuwapa nafasi 

vijana wenzake waliopo mtaani. Watanzania tulilipokea kwa mikono miwili na mpaka sasa Wasafi ndiyo 

lebo kubwa ya muziki Afrika Mashariki na kati hili halina ubishi

.

Lakini ndani ya miezi miwili mitatu hii kumekuwa na sintofahamu juu ya kinachoendelea kati ya uongozi 

wa WCB na mtoto wenu wakwanza kimuziki @harmonize_tz Uvumi ni kuwa uongozi na msanii wao hawapo sawa japo kila mtu anajaribu kukwepa kuanika ukweli. Tetesi zaidi zilianza kuvuma baada ya kumkosa @harmonize kwenye 

baadhi ya mikoa inapofanyika tamasha la Wasafi Festival. Inawezekanaje msanii aliyeko chini ya lebo kama Harmonize afanye show moja tu ya Wasafi Fesival?, inamaana uongozi haukuwa na ratiba ya 

msanii mpaka apate mkoa mmoja tu na iko wazi kuwa Harmonize ni miongoni mwa wasanii pendwa 

zaidi kwenye lebo ya WCB?. Mashabiki tunaumia juu ya hili tupo njiapanda

.

Mzazi akikosea hasemwi kwa hali ilivyo sasa mashabiki tunamnyooshea kidole @harmonize_tz kila kukicha. Kinachofuata ni matusi kwenye ukurasa wa Harmonize je kama uongozi mmelitafakari hili?. Msanii anayaoga matusi kila kukicha hamuoni kama mnavunja kitu mlichokijenga 

kwa miaka mingi?, @babutale @sallam_sk @diamondplatnumz mko wapi kutoa maelezo ya kina kwa 

mashabiki?.

.

.

Pia inasemekana kuwa (Taarifa zisizo rasmi) meneja wa Country Boy @petimanwakuache alikutana na maneno makali baada ya kushutumiwa kwamba alitaka kumpandisha Harmonize kama Surprise kwenye tamasha la Wasafi Festival Dodoma. Sasa kwa hali hii tutafika?, WCB mnanguvu kubwa kwenye muziki wa Tanzania na tunawategemea sana sasa kama mnaanza kuvuruga mashabiki wapi tutaelekea?, jitafarini juu ya hili kama ni kiki mnaitengeneza basi jueni hasara zake ni kubwa kuliko faida

Wednesday, August 21, 2019

Faida za kufanya mazoezi nyakati za asubuhi


Mazoezi ya viungo ni muhimu sana kwa afya yako, kuna namna mbalimbali za kufanya mazoezi, Unaweza kufanya mazoezi ya viungo fulani vya mwili wako kama miguu, mikono, mgongo.
        
Lakini pia kuna mazoezi ambayo ukifanya utakuwa umefanya zoezi lilojumuisha kiungo zaidi ya kimoja mfano mazoezi ya kukimbia, kuruka kamba na mengineyo.

Licha ya kuwa unaweza kutumia muda kidogo kufanya mazoezi kwa takribani dakika (30-45) kwa siku iwe asubuhi au jioni lakini pia unaweza kupata faida nyingi za kiafya kwa kufanya mazoezi hayo.
                                              
Kwa kuwa kuna faida nyingi za kufanya mazoezi basi leo nimeona nikupatie hizi chache kwa manufaa na ufahamu wa afya yako.
Mazoezi hukufanya uchangamke na kuwa shupavu.
Mazoezi huboresha ufahamu wako uwezo wa kuelewa na kufikiri mambo katika mazingira yanayokuzunguka.
Mazoezi huboresha uwezo wako wa kuhifadhi kumbukumbu.
Mazoezi husaidia kupunguza msongo wa mawazo.
Mazoezi huimarisha moyo hivyo hukuepusha na maradhi mengi yatokanayo na mapigo mabaya ya moyo.
Mazoezi humfanya mtu ajiamini.
Mazoezi hupasha mwili joto hivyo husaidia kuzuia baridi.
Mazoezi husaidia kuweka sawa kiwango cha cholesterol au mafuta yaliyopo mwilini.
Mazoezi hupunguza uwezekano wa mtu kupata ugonjwa wa kisukari.
Mazoezi hushusha kupanda kwa shinikizo la damu. (high blood pressure)
Mazoezi hupunguza uwezekano wa mtu kupata baadhi ya maradhi ya saratani.
Mazoezi humsaidia mtu kuondokana na baadhi ya matatizo ya akili.
Mazoezi huboresha hamu ya mtu kuweza kula.
Mazoezi hupunguza uzito wa ziada wa mwili na kufanya mwili wako kuwa mwepesi.

Mpendwa msomaji hizi ni baadhi ya faida za kufanya mazoezi, yote ya yote mazoezi hurefusha maisha kwa kukufanya uwe mwenye afya njema.

Ni vyema ukajiuliza, hivi ni kweli ukifanya mazoezi na kula vyakula bora kunaweza kuboresha maisha yako? Jibu ni ndiyo mazoezi na vyakula ni dawa pekee ya kutibu au kukuepusha na magonjwa mengi yanayoweza kuzuilika. Fanya mazoezi kuimarisha afya yako!

Monday, August 19, 2019

MUME ACHINJA MKE KISHA NAYE KUJIUA ..... 'WALITISHIANA KUUANA'

 Mwanaume mmoja amemchinja mke wake na kisha yeye mwenyewe kujinyonga, wakiwa nyumbani kwao katika kijiji cha Nakunga, nchini Kenya.



Polisi nchini Kenya walisema tukio hilo lilitokea jana Jumapili asubuhi Agosti 18,2019.

Jirani wa wanafamilia hao, Kennedy Barasa alisema saa 3 asubuhi alisikia mayowe kutoka kwa Stephen Kagumo na mkewe Caren Chebet yaliyodumu kwa dakika kadhaa hivyo kuamua kwenda eneo la tukio kwa lengo la kutoa msaada.

Hata hivyo, Barasa alisema walipofika katika nyumba hiyo walikuta mlango umefungwa kwa ndani.

"Tulivunja mlango na kumkuta mwanamke yuko katika dimbwi la damu na mwili wa mumewe ulikuwa ukining'inia katika chumba kingine,"alisema.

Dada wa mwanaume huyo ambaye anaishi nyumba moja na wanandoa hao pamoja na mtoto wa miaka 18, alisema alipoamka alisikia shemeji yake akilumbana na mkewe.

"Nilijaribu kusogea na kumuona shemeji akiwa ameshika panga huku akigombana na mke wake. Nilisikia wakitishiana kuuana lakini baada ya muda mfupi sikusikia kitu," alisisitiza.

Alisema baada ya majirani kufika katika chumba hicho walivunja mlango na kukuta wote wamefariki dunia.

Miili hiyo ilipelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Rufaa ya Kitale.
Via > Mwananchi

Saturday, August 17, 2019

Jela Miaka 30 Kwa Kumpa Mimba Mwanafunzi


Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoani Kigoma imemuhukumu miaka 30 jela mkazi wa kata ya Mwanga manispaa ya Kigoma Ujiji, Isack Balayabala (25)  baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kumpa ujauzito mwanafunzi wa kidato cha nne shule ya Sekondari Kaulananga.

Akisoma hukumu hiyo jana Ijumaa Agosti 16, 2019  hakimu wa mahakama hiyo, Eliya Baha alisema mshtakiwa alitenda kosa hilo Desemba 2018 kwa  kumpa ujauzito mwanafunzi huyo.

Katika kesi hiyo ya  jinai namba 46 ya mwaka 2019 mahakama hiyo imesema  imeridhishwa na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na hivyo kwa kuzingatia  kifungu cha sheria cha 60A kifungu kidogo cha (3) cha sheria ya elimu namba 353 ya mwaka 2002 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2016, mtuhumiwa atatumikia kifungo cha miaka 30 Jela

Thursday, August 15, 2019

Huwezi Amini Huyu ni Mwanaume Shoga Tajiri Huko Nigeria, Anaitwa Bobrisky

Shoga maarufu kutoka pande za +234 , Idris okuneye(28), maarufu kama BOBRISKY, ndiye staa shoga aliyeamua kujiweka wazi nchini Kwao kwa kuvaa na kuishi kama mwanamke, unaambiwa hutumia mamillion ya pesa kujiremba na ku maintain muonekano wa kike.

Shoga huyo ambaye pia ni rafiki wa muigizaji mkongwe, Tontoh Dikeh, amekua akivutia watu mbali mbali kwa umahiri wake wa kujiremba na kuishi maisha expensive pengine kuliko mastaa wengine nchini humo.

Bobrisky anajihusisha na biashara ya vipodozi ambayo anadai ndo iliyompa utajir wa kutisha mpaka sasa, ingawa hata yeye mwenyewe pia amewahi kusema mara kwa mara kuwa anatoka na ma politician na watu wazito wenye pesa zao nchini humo ambao pia wanampa jeuri ya kuishi maisha ya kifahari huko Lagos state


Muonekano wa zamani kabla hajabadili muonekano wake


Source

Wednesday, August 14, 2019

Mwalimu Mkuu atuhumiwa kubaka na kumpa mimba mwanafunzi wa darasa la tano

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Nyantore, iliyopo Kigoma, Jason Rwekaza (Katikati) amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kigoma na kusomewa mashitaka saba.

Sita kati ya mashtaka hayo ni ubakaji na moja kumtia mimba mwanafunzi wake wa darasa la tano.

Mtuhumiwa huyo amekana mashitaka hayo na ametoka kwa dhamana hadi kesi yake itakaposomwa Agosti 19 2019.

Monday, August 12, 2019

Esma Platnumz "Namshukuru Mungu Wifi Yangu Tanasha Hana Mambo ya Kiswahili Kama Waliopita"


"Ninachoshukuru mimi Tanasha hana mambo ya Kiswahili kabisa wala muda wa kuangalia nini kimepostiwa mtandaoni kwa sababu anajua watu wengi wanazungumza tu wala hawajui maisha ya kweli ya mtu binafsi," - Esma Platnumz

Thursday, August 8, 2019

JKT Yaja na Habari Njema kwa Wananchi wa Kanda ya Kusini

JKT Yaja na Habari Njema kwa Wananchi wa Kanda ya Kusini
Wananchi wa mikoa ya Kusini( Lindi na Mtwara) wameombwa kutumia maonesho ya nane nane na  kanda ya ujenzi ya kanda ya Kusini kupata msaada wa kitaalamu wa mambo mbalimbali yahusuyo shuguli za maendeleo.

Wito huo ambao ni habari njema kwa wananchi wa kanda ya hii ulitolewa jana na Luteni Kanali Juma Mrai alipozungumza na Muungwana Blog katika viwanja vya Ngongo, manispaa ya Lindi, yanapofanyika maonesho ya wakulima( Nanenane) kanda ya Kusini.

Luteni Kanali Mrai ambae amemuwakilisha mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa ( JKT) alipotembelea mabanda ya maonesho ya jeshi hilo wajifunze kupitia mambo wanayoyaona katika mabanda hayo, ili maonesho hayo yawanufaishe.

Katika maonesho hayo, alisema wananchi hawanabudi kutumia kanda hiyo ya ujenzi kupata ushauri wa kitaalamu katika shughuli zao za maendeleo na ujenzi wa taifa.

Alisema jeshi hilo ni mali yao na lipo kwa ajili yao, kwahiyo wana haki na sababu ya kulitumia, Ikiwemo kupata ushauri kuhusu kilimo, ufugaji, uvuvi na fani nyingine zinazoweza kuwafanya wanufaike na kazi wanazofanya.

Mbali na kutoa  ushauri, kamanda huyo alisema kanda  ya ujenzi ina toa huduma za ujenzi kwa taasisi za umma,taasisi binafsi na mtu mmoja mmoja. Hivyo wasisite kuwatumia katika kazi zao.

 ''Waendelee kuliamiani jeshi lao, kwani gharama za ujenzi ni nafuu, watakamilishiwa kazi zao kwa wakati, kwamujibu wa mikataba na kwa ubora,'' alisisitiza kamanda Mrai.

''Lakini pia wananchi wanapata fursa ya kuona vijana wao kupitia jeshi lao wanafanya nini. Kwani ni dhahiri wanapata ujuzi na maarifa yanayoweza kuwafanya wajiajiri,'' alisema kamanda Mrai.

Mwanaheri Silitumii Vibaya Shepu Langu

Mwanaheri Silitumii Vibaya Shepu Langu
WANADADA anayekimbiza kwenye Tamthiliya ya Kapuni, Mwanaheri Ahmed amefunguka kwamba anajijua kuwa ameumbika lakini kamwe hawezi kujilengesha kwa wanaume wakware.  Akipiga stori na Gazeti la Amani, Mwanaheri alisema mara nyingi akikaa kwenye kioo huwa anajiangalia na kuishia kumshukuru Mungu kwa uumbaji wake lakini kamwe hawezi kujirahisi  licha na kutamaniwa na wanaume wengi.

"Ninajijua kuwa nina lishepu zuri, tena mara nyingi nikiwa najiangalia kwenye kioo najizungusha nyuma na mbele, kisha naishia kusema asante Mungu kwa uumbaji wako, ameniumba haswa na mimi ni mzuri bwana ndio maana niliwekwa ndani," alisema Mwanaheri ambaye aliolewa mapema mwaka jana na mfanyabiashara aliyefahamika kwa jina moja la Hamisi

MWAUWASA Yatangaza Bei Mpya za Maji




Kimenuka..Waziri Lukuvi Awasimamisha Kazi Watumishi 183 Wizara ya Ardhi


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi , William Lukuvi  amewasimamisha kazi watumishi 183 wa wizara hiyo kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazowakabili.

*Nafasi za Ajira na Scholarships Tanzania

Watumishi hao ambao waziri huyo amekabidhi majina yao Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kwa ajili ya uchunguzi, wanadaiwa  kuingilia mfumo wa kukadiria na kukusanya kodi ya pango ya ardhi kinyume na taratibu na kusababisha upotevu wa mapato ya Serikali.

Wednesday, August 7, 2019

WAZIRI MKUU MAJALIWA 'AKOSHWA' NA MAONESHO YA VIWANDA YA NCHI ZA SADC

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Ndege nchini (ATCL) Mhandisi Ladislaus Matindi katika Maonyesho ya Maadhimisho ya Nne ya Wiki ya Viwanda kwa Nchi za SADC kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu wa Tanzania,Mhe. Kassim Majaliwa, akipata maelezo kuhusu ya Reli ya Kisasa kutoka kwa Afisa Habari wa  Shirika la Reli Tanzania (TRC), Jamila Mbarouk alipotembelea banda la Shirika la Reli Tanzania(TRC)  katika maonesho ya Wiki ya Viwanda SADC, yanayoendelea Jijini Dar es Salaam, kulia kwake ni Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Innocent Bashungwa.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitembelea mabanda katika Maonyesho ya Maadhimisho ya Nne ya Wiki ya Viwanda kwa Nchi za SADC kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam, Agosti 6, 2019. Wapili kulia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa George Lous Chuwa kuhusu bidhaa mbalimbali wakati alipotembelea banda la Sekretarieti ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) katika Maonyesho ya Maadhimisho ya Nne ya Wiki ya Viwanda kwa Nchi za SADC kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam, Agosti 6, 2019. Wapili kulia ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza na wanahabari mara baada ya kutembelea Maonyesho ya Maadhimisho ya Nne ya Wiki ya Viwanda kwa Nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam, Wa pili kulia ni Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocenti Bashungwa na kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza na wanahabari mara baada ya kutembelea Maonyesho ya Maadhimisho ya Nne ya Wiki ya Viwanda kwa Nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam, Agosti 6, 2019. Wa pili kushoto ni Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocenti Bashungwa. Wengine kutoka kushoto ni Waziri wa Afya wa Zanzibar, Hamad Rashid, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi, Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega.

Na Mwandishi Wetu.

 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa amewataka watanzania kuchangamkia fursa zitokanazo na maonesho ya Viwanda ya Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) ili kuwezesha ukuaji wa uchumi wa viwanda ambao Serikali inaujenga.

 Akizungumza mara baada ya kutembelea maonesho hayo yanayoendelea katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Julius Nyerere, Viwanja vya Karimjee na Gymkana, Waziri Mkuu amesema kuwa maandalizi ya Mkutano Mkuu wa 39 wa Wakuu wa Nchi za SADC yamekamilika yakihusisha kuwepo kwa maonesho ambayo nchi wanachama wataonesha teknoloji, Ubunifu na bidhaa zao kutoka katika Viwanda vya nchi za SADC.

 Waziri Mkuu alisema kuwa Serikali imetoa fursa kwa wafanyabiashara Wakubwa, wa kati, wadogowadogo na wenye bidhaa zinazozalishwa kwa mikono kuja kuonesha na kuchukua teknolojia kutoka nchi wageni ambao wapo nchini kwa maonesho hayo ya wiki moja.

 "Sisi kama Serikali tumetoa Fursa kwa wale ambao wanafanya kazi na kuzalisha bidhaa zao kwa kutumia mikono kuja kuonesha bidhaa zao ili ziweze kupata masoko kwa nchi wanachama wa SADC kwani nchi zote zinakuja hapa kuleta bidhaa mbalimbali kwa hiyo watanzania wanatakiwa kutumia fursa hii kuwauzia wageni bidhaa zetu", Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Tazama VIDEO ya Rosa Ree Anayosema Ananguvu za Kiume...Chaa Kali ya Mwaka


Tazama VIDEO ya Rosa Ree Anayosema Ananguvu za Kiume...Chaa Kali ya Mwaka

Bonyeza Play Kutazama:


YESU FEKI HAJAFARIKI.... KATUPIA PICHA NA VIDEO FACEBOOK

Michael Job, muhubiri wa Marekani na muigizaji ambaye hivi majuzi alizuru Kenya na kuitwa 'Yesu bandia' hajafariki kama ilivyoangaziwa na vyombo mbalimbali vya habari nchini Tanzania na Kenya.

Kulingana na uchunguzi wetu jamaa huyo yupo hai na mzima kama kigongo.

Kadhalika, muhubiri huyo yupo nchini Kenya na kwamba hajatimuliwa kama ilivyodaiwa na vyombo hivyo vya habari.

Taarifa za vyombo hivyo ambazo zilianza kuenezwa siku tano zilizopita zinadai, Yesu huyo bandia alifariki siku chache tu baada ya kuhudhuria ibada ya kidini.


Inadaiwa kwamba alifariki siku chache tu baada ya kutembelea taifa hilo la Afrika mashariki baada ya kuuguwa ugonjwa wa mapafu.

Hata hivyo mhubiri huyo ameendelea kupakia mtandaoni picha na video ya shughuli zake siku baada ya siku.

Picha na video za karibuni zaidi alizipakia kwenye ukurasa wake wa Facebook saa nne usiku wa kuamkia leo.

Katika chapisho hilo na kanda za video alizoweka katika akaunti yake ya facebook Bwana Job anaonekana katika gari moja akihubiri Kiingereza huku akisaidiwa na mkalimani huku watu wakifuatilia mahubiri yake.

Aliandika: Leo mimi na Paul Maurer tulipata fursa ya kuhubiri juu ya gari la CFAN . mamia ya watu walifanya uamuzi wa yesu kuwa muokozi wa maisha yao. watoto wengi walimkaribisha Yesu na

Katika chapisho lake katika ukurasa wake wa facebook siku ya Jumatatu, muhuburi huyo aliandika: Ahsante Marc na Catrice mioyo yenu na utumishi wenu na Ahsanteni kwa kuja Kenya! Mungu aliwatumia ninyi kuokoa maisha ya watoto wengi. Kuhubiri Ukristo kwa masikini , kuwaponya wale waliovunjika moyo kuwaachilia waliotekwa, kuwafungulia waliokandamizwa, kuwaponya wengi na kuwaleta wengi karibu katika moyo wa Yesu. Ahsanteni kwa kanisa lenu na urafiki wenu. Waombeeni watu hawa wa Mungu! Tumsifu bwana! Nendeni duniani ili kuhubiri neno kwa viumbe vyote .Nenda ukahubiri injili kwa mtu hii leo. Mungu atakupatia ujasiri huu unavyozungumza . Anakusubiri. Ubarikiwe Ahsante kwa kutuombea!


Anaonekana akitangaza mkutano wa kidini utakaofanyika kuanzia Alhamisi wiki hii jijini Nakuru.

Picha za kanda za video zilizomuonyesha amevalia kama Yesu Kristozilisambazwa katika mitandao ya kijamii kote barani Afrika.

Lakini jamaa huyu ni nani haswa na anafanya nini?

Mwanamume huyo ni mhubiri kutoka Marekani na muigizaji anayeitwa Michael Job, aliyekuwa anahudhuria misa ya madhehebu mbalimbali ya kikristo ambako alialikwa kuzungumza.

Anaishi Orlando, Florida, ambako amekuwa akiigiza kuwa Yesu katika bustani maalum The Holy Land Experience theme park, inayojitambulisha kama "jumba halisi la biblia la ukumbusho".

Watu wamekuwa wakifanya mzaha katika mtandao wa Twitter kuhusu picha zake na namna wachungaji barani Afrika wanapenda kudai kufanya miujiza.

Hii sio ziara yake ya kwanza barani Afrika, mapema mwaka huu alikuwa nchini Togo, licha ya kwamba picha alizoweka kutoka huko hakuonekana akiwa amevaa mavazi ya kuiga - bali alikuwa amevaa suti.

Alizuru pia Nigeria.
Chanzo - BBC

Tuesday, August 6, 2019

Njia zitakazowasiaidia muweze kudumu katika mahusiano yenu ya kimapenzi

Hakuna binadamu asiyefahamu nini maana ya mapenzi na kama wapo basi ni wachache sana na wanaweza kuwa hawafahamu kwa maneno lakini kivitendo wanakuwa wanafahamu aidha kwa kuona, kusikia na hata kwa wao wenyewe kushiriki kwenye mapenzi hayo.

Na hakuna binadamu yeyote asiyependa kupenda au kupendwa, wote tunapenda kupenda na pia tunapenda kupendwa pia. Na siku zote ukipenda na usipopendwa pale unapopenda huwa inakuwa ni huzuni sana na wengine hufikia hatua mbaya sana za kufikiria mengine mengi tu ya hatari pale mapenzi yanapokuwa machungu kwao.

Hii ndio sababu wengi wetu huwa tunakaa pale tunapoona kweli kuna mapenzi na si kukaa pale ambapo unaona unadanganywa au kuzungushwa kila siku. Lakini kuna wakati tunaweza kujikuta hata pale tunapopenda na kupendwa pia panaharibika baada ya muda na kunakuwa na ugomvi na kukosa maelewano baina yenu na wakati mwingine usifahamu kwa nini hamuelewani au ukaelewa lakini ukakosa njia za kutatua.

Zifuatazo ni baadhi tu ya njia mbalimbali za kufanya ukae na mpenzi wako kwa muda mrefu kwenye mahusiano na mkafurahia mapenzi yenu popote pale mtakapokuwa na mtakapoishi.

1. Kuwa na muonekano chanya kwa mpenzi wako.
Ukiwa ni mtu wa kuangalia mabaya/kasoro sana kwa mpenzi wako kuliko mazuri yake hautakuja kukaa kwenye mahusiano kwa muda mrefu hata siku moja, utaendelea kubadilisha wanaume/Wanawake kila siku na mwisho wa siku utajiona huna bahati kwenye mapenzi na wakati Unayeyaharibu mapenzi yako ni wewe Mwenyewe…kakuna asiye na kasoro (ukiwemo wewe mwenyewe).

Kwa hiyo muonyeshe mpenzi wako mapenzi bora na umrekebishe pale anapokosea Bila kuwa na lawama mara kwa mara, kuna makosa mengine ni hakuna binadamu asiyefahamu nini maana ya mapenzi na kama wapo basi ni wachache sana na wanaweza kuwa hawafahamu kwa maneno lakini kivitendo wanakuwa wanafahamu aidha kwa kuona, kusikia na hata kwa wao wenyewe kushiriki kwenye mapenzi hayo.

Na hakuna binadamu yeyote asiyependa kupenda au kupendwa, wote tunapenda kupenda na pia tunapenda kupendwa in return. Na siku zote ukipenda na usipopendwa pale unapopenda huwa inakuwa ni huzuni sana na wengine hufikia hatua mbaya sana za kufikiria mengine mengi tu ya hatari pale mapenzi yanapokuwa machungu kwao.

Hii ndio sababu wengi wetu huwa tunakaa pale tunapoona kweli kuna mapenzi na si kukaa pale ambapo unaona unadanganywa au kuzungushwa kila siku. Lakini kuna wakati tunaweza kujikuta hata pale tunapopenda na kupendwa pia panaharibika baada ya muda na kunakuwa na ugomvi na kukosa maelewano baina yenu na wakati mwingine usifahamu kwa nini hamuelewani au ukaelewa lakini ukakosa njia za kutatua.

2. Mpe nafasi na uhuru mpenzi wako.
Mnapokuwa kwenye mahusiano jitahidini kwa hali na mali kupeana nafasi/uhuru kwenye mambo mengi hasa yale ya kitaaluma zaidi na kimaisha. Anapokwambia yupo kwenye kikao cha kikazi jaribu kumuelewa na umpe support ya kutosha kwenye kazi zake au biashara zake au hata masomo yake. Usipende sana kulalamika pale anapochelewa kurudi kazini au kutoka kwenye biashara zake bali mpokee kwa upole na baada ya kupumzika ndipo muulize kwa upole na kimahaba zaidi kwanini siku hizi anachelewa sana kurudi au kwenye biashara zake au shuleni tofauti na zamani.

Hii itajenga zaidi kuliko kubomoa kwa kulalamika na kupayuka mbele yake na huku yeye akiwa hata hajapumzika na itamfanya siku nyingine aione nyumba chungu kitu ambacho si kizuri kwenu wote wawili.

3. Mfanye mwenza wako ajivunie kuwa nawe kila wakati.
Hakikisha katika mapenzi yenu kila siku unamfanya mpenzi wako ajivunie kuwa nawe na hakikisha humfanyi ajute kwa kukuchagua wewe miongoni mwa wote aliowaona. Usijidanganye hata siku moja kuwa kwa kumpata tu na kwa yeye kukupenda basi hajaona mwingine wa kuweza kuwa naye.

Wapo wengi sana anaoweza kuwa nao lakini amekuchagua wewe katika hao wote, kwa hiyo usimfanye aanze kuwafikiria wale wengine wanaomfuatilia kila siku na kumsumbua. Ukianza kumwacha aanze kuwafikiria wengine aidha kwa wewe kuwa unamkosesha amani ya mapenzi kila mara au kwa mengine mabaya ndani ya mapenzi basi ipo siku utaishia pabaya.

4. Msadie kwa hali na mali kila inapowezekana.
Kwenye mahusiano huwa kuna kupanda na kushuka miongoni mwa wapenzi na hasa kiuchumi na hata kisaikolojia. Hakuna kitu kizuri kwenye mapenzi kama mtu kupata tatizo na akasaidiwa na mpenzi wake katika hali ambayo hakuitegemea, namaanisha mpenzi wako akipata tatizo lolote hakikisha wewe ndo unakuwa wa kwanza kulifahamu na kulifanyia kazi.

Sio matatizo yote yanamalizwa kwa pesa so hata ushauri na kumpa mawazo chanya inasaidia sana na kumfanya awe na furaha kuwa nawe. Kama unampenda usione tabu kumsaidia kwa kuogopa kuonekana eti unahonga, huyo ni mpenzi wako kwa hiyo jiamini na umpe kile anachostahili kusaidiwa na mpenzi wake.

Yapo mambo mengi sana ambayo kama mkiyafanya kwenye mapenzi basi uhusiano wenu utakuwa wa kudumu na wenye furaha sana ingawa hapa nimezungumzia kwa uchache sana lakini nina imani itasaidia sana kwa wote walio kwenye mahusiano .

Mapenzi hayana ndumba au limbwata hata siku moja, unapoona wapenzi wengi wana furaha kwenye mapenzi yao ni kwa sababu wanavumiliana kwa mengi na kusameheana kwa mengi. sana na unaweza kuyarekebisha kwa kukaa chini na mpenzi wako mkayamaliza kwa dakika 5 tu lakini wengine huwa issue kubwa kwao na kusababisha mwisho mbaya.

CCM KAHAMA YANG'OA WANACHAMA WA CHADEMA....MWENYEKITI ATAKA KUCHAGUA VIONGOZI BORA



Na Salvatory Ntandu - Malunde1 blog Kahama
Kuelekea katika uchanguzi wa serikali za mitaa hapa nchini wananchi wilayani Kahama mkoani Shinyanga wametakiwa kuchagua viongozi bora na sio bora kiongozi ambao wataweza kusimamia fedha na miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na serikali.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wilaya ya Kahama Thomas Myonga wakati akizungumza kwenye mkutano maalum wa chama hicho wa kuwapokea wanachama sita wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) uliofanyika katika kijiji cha Ufala kata ya Kilago.

Amesema katika uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka huu ni vyema wananchi wakafanya maamuzi sahihi ya kuchagua viongozi wenye sifa, wasiokuwa watoa rushwa na walevi ambao siyo waadilifu wanaotaka madaraka kwa maslahi yao binafsi.

Amefafanua kuwa wanachama hao sita wakiongozwa na aliyekuwa mwenyekiti wa kijiji hicho Daniel Makoye wamefanya uamuzi sahihi ya kuhamia (CCM) kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya Tano chini ya Dk John Pombe Magufuli katika kuwaletea maendeleo wananchi.

Ameongeza kuwa CCM mpya haina makundi hivyo ni jukumu lao kushirikiana nao katika juhudi za kuhakikisha chama hicho kinapata ushindi katika uchaguzi huo na mbinu pekee ya kushinda ni pamoja na kuweka wagombea wanaokubalika katika jamii ambao hawana sifa mbaya kama vile walevi,wazembe na wasiopenda kufanya kazi.

Myonga amewakabidhi wanachama hao wapya kadi za CCM ambao ni Daniel Makoye mwenyekiti wa kijiji cha Ufala,Bundala Busuli,Paschal Gulamali,Masanja Peter,Luhende Kaswaki na Hasan Athuman ambao wote walikuwa wanachama wa CHADEMA.

Uchaguzi wa serikali za mitaa utafanyika mwezi Oktoba nchi nzima.











Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...