NA REBECCA DUWE TANGA
Wadau wa maendeleo wameombwa kushirikiana na Mamlaka ya mapato Tanzania TRA mkoa wa Tanga kutoa elimu kwa makundi ya wanawake ili waweze kuzikia fursa mbalimbali na hatimaye waweze kulipa kodi kwa maendeleo ya nchi.
Meneja wa Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Tanga CPA Castro John ametoa kauli hiyo leo may 14, 2026 alipokuwa akifungua jukwaa la wanawake na kodi lililoandaliwa na Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Tanga na kufadhiliwa na shirika la GIZ lenye kauli mbiu isemayo "Wanawake na kodi nguzo ya maendeleo ya Taifa"
"Kwa wadau wetu wa taasisi za kifedha tunaomba muendelee kushirikiana nasi katika kuwawezesha wanawake ili kukuza biashara zao kwa misingi ya sheria na kodi" Amesema Meneja Castro
Katika hatua nyingine Castro alisema Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA Mkoa wa Tanga, ina jukumu la kutoa Elimu ya mlipakodi pamoja na fursa mbalimbali zinazowazunguka Wanawake Wafanyabiashara na Wajasiriamali ili kumuwawezesha kutanua uelewa juu ya mifumo na Sheria za Kodi Nchini.
"TRA inatambua mchango wa Wanawake katika ulipaji wa Kodi na kwasasa Wanawake wamekuwa mstari wa mbele katika ulipaji wa Kodi Nchini,hivyo naomba muendelee kuwa mstari wa mbele katika ulipaji wa Kodi ili tulijenge Taifa letu"Aliongeza Castro
Castro aliwataka Wanawake kuendelea kudumisha nidhamu ya ulipaji wa Kodi Nchini nakwamba Mamlaka hiyo ipo tayari wakati wowote kutoa msaada kwa mfanyabiashara anayepitia changamoto yoyote,
"Niwaombe muendelee kudumisha nidhamu ya ulipaji wa Kodi mliyonayo ili tuondoe usumbufu wowote unaoweza kujitokeza endapo mtu atakwepa kulipa Kodi,TRA ipo tayari wakati wowote kutoa msaada kwa mfanyabiashara anayepitia changamoto yoyote, niwaombe ukiwa na changamoto yoyote tuambie tukusaidia usikae nayo alafu baadae unakuja kulalamika" Alisisitiza Castro
Kwaupande wake,Naibu Katibu wa Jumuiya ya Nchini Wafanyabiashara, Ismail Masoud aliwataka watumishi wa TRA kuwasaidia kutoa Elimu Wafanyabiashara mkoani Tanga ili kuondoa kasoro nyingi zinazowakabili Wafanyabiashara,
"Niwaombe TRA iendelee kutoa Elimu ya mlipakodi ili changamoto za Wafanyabiashara hususani zinazotokana na Elimu ziishe, lakini pia kwasisi Wafanyabiashara,tuache janja janja zakukwepa Kodi, tunataka twende pamoja ili tuweze kufanikisha dira ya Taifa 2050" Alisisitiza Masoud.
Kwa upande wake Afisa maendeleo mkoa wa Tanga Charles Mtali amesema wanawake wana mchango mkubwa wa maendeleo ya kiuchumi .
tofauti na wanaume hivyo wasipowezeshwa itakuwa ni vigumu nchi kufikia malengo yake.


















































