Na OWM - TAMISEMI, Kahama














Na OWM - TAMISEMI, Kahama














Hospitali ya Rufani KCMC ,imetangaza kuwa imeanza ujenzi wa Taasisi ya Moyo KCMC ili kusadia na kupunguza gharama inayotokana na safari ya umbali mrefu na foleni ya huduma kwa Wagonjwa wanaotibiwa katika Taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete JKCI wakiwemo wale wanaosafirishwa nje ya Nchi .
Sambamba na wadau wa Maendeleo Mkoa wa Tanga wanatarajiwa kusaidia kuchangia kiasi cha Sh.Bil 3 kwaajili ya ununuzi wa vifaa kati ya Bil.25 zinazohitajika katika ujenzi wa Hospitali hiyo ambapo mpaka sasa kiasi cha Sh.22 Bil kimeshapatikana kutoka kwa Wadau wa Maendeleo nje ya Nchi.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake ,Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt.Batilda Buriani, alisema ujenzi wa Taasisi hiyo unakwenda kuwasaidia wakazi wa Mikoa ya Kanda ya kaskazini Tanga, Kilimanjaro, Arusha na Manyara kuwapunguzia gharama kubwa wanayotumia ya kwenda katika Taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete JKCI pamoja na kuokoa gharama kubwa,
"Ujenzi wa Taasisi hii ya magonjwa ya moyo utawasaidia wakazi wa Tanga na Mikoa ya Kanda ya kaskazini lakini pia hata watu wengine kutoka Mikoa mingine ya jirani, kwasasa Wagonjwa wa moyo wanalazimika kusafiri hadi jijini Dar e S salaam katika Taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete JKCI lakini wengine wanapata rufani yakwenda nje ya Nchi, lakini ujio wa Taasisi hiyo utaongeza upana wa huduma za moyo Nchini na kupunguza idadi ya Wagonjwa katika Taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete JKCI" Alisisitiza Dkt.Batilda
Dkt.Batilda alisema asilimia 60 ya Wagonjwa wanaotibiwa katika Taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete JKCI wanatoka Kanda ya kaskazini na kuwataka wadau wa Maendeleo mkoani Tanga kujitokeza kwa wingi May 30 kwenye harambee na wadau wa Maendeleo ukumbi wa Tanga Beach resort ili kuchangia pamoja na kupea fursa za ujenzi wa Taasisi ya moyo KCMC,
"Niwaombe sana wadau wa Maendeleo Mkoa wa Tanga tujitokeze kwa wingi kwenye harambee maalumu ili tuweze kuchangia ujenzi wa Taasisi ya moyo KCMC,lakini pia kwa wale ambao hawatoweza kufika naomba tujitokeze kwa michango"Balozi Batilda
Kwa upande wake afisa miradi na mipango wa KCMC Emanuel Biyanchi alisema kuputia hafla hiyo wadau watapata taarifa sahihi kuhusu fursa kwenye sekta ya Afya uwekezaji,huduma za Afya miradi ya maendeleo na maeneo ya mashirikiano ya kibiashara na kijamii ndani KCMC na taasisi zake.
Aliongeza kusema kuwa sekta ya Afya si tu eneo huduma pekee bali ni fursa kwa wawekezaji , ajira,ubunifu na Tahiti na maendeleo ya jamii.
samabamba na hayo alisema hafla hiyo itatoa nafasi majadiliano yankaribu kati y wadau, wawekezaji Viongozi na Taasisi mbalimbali kuhusu namna bora ya kushirikiana kati ya miradi ya maendeleo inayolenga kuboresha huduma za Afya na ustawi wa jamii.
Mwalimu ametoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam wakati wa mjadala wa kitaifa kuhusu hatima ya nchi ulioandaliwa na Chama cha ACT Wazalendo.
.Mwalimu alieleza kuwa kila mtu anajua kilichotokea siku hiyo ya uchaguzi, ikiwemo mauaji na uwepo wa changamoto kubwa ya ajira kwa vijana, lakini akasisitiza kuwa kikwazo kikubwa kwa sasa imekuwa ni wanasiasa kushindana maneno majukwaani na kuonyesha umahiri wa kusema badala ya kugusa kiini cha tatizo na kutoa majawabu ya kuivusha nchi.
Kutokana na hali hiyo, Salum Mwalimu alimpongeza Mwenyekiti wa ACT Wazalendo, Othman Masoud Othman, kwa kuitisha mjadala huo na kumtaka asione aibu kusimamia jawabu aliloliwasilisha kupitia kijitabu chake kilichosisitiza haja ya kuanzisha jukwaa la majadiliano ya kitaifa yatakayoongozwa na misingi ya ukweli, haki na uwajibikaji.
Mwalimu alimshauri Othman kuchukua uongozi na kuunda kamati itakayojumuisha watu mbalimbali ili kuanzisha jukwaa hilo, si kama mwenyekiti wa chama bali kama kiongozi mwandamizi wa kisiasa atakayeungwa mkono na vyama vingine, kwa lengo la kupata ukweli na kuweka mifumo ya jinsi viongozi wa kisiasa wanavyopaswa kuwajibika.
Kwa upande wake, mwandishi na mchambuzi wa masuala ya siasa, Ezekiel Kamwaga, alisema kuwa nchi inahitaji utashi wa kisiasa kabla ya kuanza kuzungumza ukweli, huku akionya kuwa viongozi wengi wa sasa wanaonekana kuwa wepesi kukimbilia mitandao ya kijamii badala ya kuonyesha uongozi thabiti.
Kamwaga alifafanua kuwa kiongozi mzuri ni yule anayesimama mbele na kuwa tayari kupokea lawama au kuzomewa, lakini anakaa nyuma wakati wa kupokea sifa, sifa ambayo kwa sasa inaonekana kupotea miongoni mwa viongozi.
Naye mwanasiasa Odero Odero aliwataka viongozi wa upinzani kuacha kulia na badala yake watafute suluhu ya kweli kwa kukabiliana na Rais Samia Suluhu Hassan kwenye meza ya mazungumzo.
Odero aliwashauri viongozi hao akiwemo Othman Masoud, Zitto Kabwe, na John Heche kuondoa tabia ya kuogopana na kujificha kwani Rais Samia ni kama dada na mama yao, na njia pekee ya kuifikisha nchi mbali ni kukaa naye meza moja ili kieleweke.
Suala hili la maridhiano ni sehemu ya falsafa ya uongozi ya Rais Samia kupitia '4R' zake ambazo ni Maridhiano, Ustahmilivu, Mabadiliko na Kujenga upya, ambapo hivi karibuni aliahidi kuunda kamati ya maridhiano baada ya kupokea ripoti ya Tume ya Kuchunguza Matukio Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.
Wadau wa maendeleo wameombwa kushirikiana na Mamlaka ya mapato Tanzania TRA mkoa wa Tanga kutoa elimu kwa makundi ya wanawake ili waweze kuzikia fursa mbalimbali na hatimaye waweze kulipa kodi kwa maendeleo ya nchi.
Meneja wa Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Tanga CPA Castro John ametoa kauli hiyo leo may 14, 2026 alipokuwa akifungua jukwaa la wanawake na kodi lililoandaliwa na Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Tanga na kufadhiliwa na shirika la GIZ lenye kauli mbiu isemayo "Wanawake na kodi nguzo ya maendeleo ya Taifa"
"Kwa wadau wetu wa taasisi za kifedha tunaomba muendelee kushirikiana nasi katika kuwawezesha wanawake ili kukuza biashara zao kwa misingi ya sheria na kodi" Amesema Meneja Castro
Katika hatua nyingine Castro alisema Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA Mkoa wa Tanga, ina jukumu la kutoa Elimu ya mlipakodi pamoja na fursa mbalimbali zinazowazunguka Wanawake Wafanyabiashara na Wajasiriamali ili kumuwawezesha kutanua uelewa juu ya mifumo na Sheria za Kodi Nchini.
"TRA inatambua mchango wa Wanawake katika ulipaji wa Kodi na kwasasa Wanawake wamekuwa mstari wa mbele katika ulipaji wa Kodi Nchini,hivyo naomba muendelee kuwa mstari wa mbele katika ulipaji wa Kodi ili tulijenge Taifa letu"Aliongeza Castro
Castro aliwataka Wanawake kuendelea kudumisha nidhamu ya ulipaji wa Kodi Nchini nakwamba Mamlaka hiyo ipo tayari wakati wowote kutoa msaada kwa mfanyabiashara anayepitia changamoto yoyote,
"Niwaombe muendelee kudumisha nidhamu ya ulipaji wa Kodi mliyonayo ili tuondoe usumbufu wowote unaoweza kujitokeza endapo mtu atakwepa kulipa Kodi,TRA ipo tayari wakati wowote kutoa msaada kwa mfanyabiashara anayepitia changamoto yoyote, niwaombe ukiwa na changamoto yoyote tuambie tukusaidia usikae nayo alafu baadae unakuja kulalamika" Alisisitiza Castro
Kwaupande wake,Naibu Katibu wa Jumuiya ya Nchini Wafanyabiashara, Ismail Masoud aliwataka watumishi wa TRA kuwasaidia kutoa Elimu Wafanyabiashara mkoani Tanga ili kuondoa kasoro nyingi zinazowakabili Wafanyabiashara,
"Niwaombe TRA iendelee kutoa Elimu ya mlipakodi ili changamoto za Wafanyabiashara hususani zinazotokana na Elimu ziishe, lakini pia kwasisi Wafanyabiashara,tuache janja janja zakukwepa Kodi, tunataka twende pamoja ili tuweze kufanikisha dira ya Taifa 2050" Alisisitiza Masoud.
Kwa upande wake Afisa maendeleo mkoa wa Tanga Charles Mtali amesema wanawake wana mchango mkubwa wa maendeleo ya kiuchumi .
tofauti na wanaume hivyo wasipowezeshwa itakuwa ni vigumu nchi kufikia malengo yake.