Tanzania Daily Eye
Sunday, June 21, 2026
TARURA KUENDELEA KUJENGA MADARAJA YA MAWE NCHI NZIMA -SUNGURA
Saturday, June 20, 2026
TBA YATEKELEZA MPANGO WA NYUMBA ZA GHARAMA NAFUU KWA WANANCHI
POLISI WAFICHUA MPANGO WA UHALIFU JULAI 7
Friday, June 19, 2026
JUMLA YA MIRADI 73 YA MWENGE WA UHURU YENYE THAMANI YA SH BILIONI 27.7 KUKAGULIWA,KUWEKEWA MAWE YA MSINGI NA KUZINDULIWA
Na Rebeca Duwe Tanga
Mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian amewataka wananchi wa Mkoa waTanga kutokeza kupoke mwenge wa uhuru ili kuweza kuukimbiza ili kuhakikisha nuru inamulika kila mahali na kuimarisha umoja na mshikamano, ambapo utakimbizwa katika halmashauri zote 11 za mkoa huo na kukagua, kuzindua pamoja na kuweka mawe ya msingi katika miradi 73 yenye thamani ya zaidi ya 27.7
Hayo aliyasema wakati akizungumza na waandishi wa habari ,kuhusu maandalizi ya Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu ambapo alisema Mwenge wa Uhuru utapokelewa katika Viwanja vya Shule ya Msingi Mji Mpya, Kijiji cha Mtoro, Kata ya Tunguli wilayani Kilindi ukitokea Mkoa wa Morogoro.
Alisema baada ya mapokezi hayo, Mwenge utakimbizwa kwa umbali wa kilometa 1,340 kupitia halmashauri zote za Mkoa wa Tanga kabla ya kukabidhiwa Mkoa wa Kilimanjaro Juni 28 mwaka huu katika Uwanja wa Shule ya Msingi Hedaru.
Dk. Burian alisema kati ya miradi 73 itakayofanyiwa kazi na Mwenge wa Uhuru, miradi 34 itawekewa mawe ya msingi, miradi 26 itafunguliwa na kuzinduliwa, miradi 11 ya vijana itakaguliwa pamoja na miradi miwili ya sekta ya maji.
Alifafanua kuwa miradi hiyo ina thamani ya Sh bilioni 27.76, ambapo Sh milioni 300.6 ni nguvu za wananchi, Sh bilioni 1.27 ni michango ya halmashauri, Sh bilioni 10.7 ni fedha za Serikali Kuu na Sh bilioni 15.47 ni mchango wa wahisani.
Akizungumzia kaulimbiu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu inayosema, “Tanzania ni Yetu Sote, Tushikamane kwa Pamoja Kuleta Maendeleo,” Dk. Burian alisema mkoa umejipanga kuhakikisha wananchi wa makundi mbalimbali wanashiriki kikamilifu katika shughuli zote za Mwenge.
Alisema viongozi wa serikali, watumishi wa umma, viongozi wa dini, wanawake, vijana, watu wenye mahitaji maalumu pamoja na makundi mengine wamehamasishwa kushiriki kikamilifu kuanzia mapokezi hadi makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru.
Aidha, wananchi watapata fursa ya kuushika na kuukimbiza Mwenge huo kama sehemu ya kuimarisha mshikamano, umoja wa kitaifa na ushiriki wa wananchi katika shughuli za maendeleo.
Mbali na kuhamasisha maendeleo, Mwenge wa Uhuru utaendelea kutoa elimu kuhusu mapambano dhidi ya rushwa, malaria, VVU/UKIMWI, matumizi ya dawa za kulevya pamoja na umuhimu wa lishe bora kwa jamii.
Dk. Burian aliwataka wananchi wa Mkoa wa Tanga kujitokeza kwa wingi katika maeneo ya mapokezi, miradi na mikesha mbalimbali ili kushiriki shughuli za Mwenge wa Uhuru na kufaidika na ujumbe wake.
Alisema mkoa umejipanga kikamilifu kuhakikisha wananchi wanapata burudani na hamasa kupitia ushiriki wa wasanii na vikundi vya sanaa vitakavyoshiriki katika maeneo yote ambayo Mwenge wa Uhuru utakesha.
Sunday, June 14, 2026
PROF. SHEMDOE AIELEKEZA KAMPUNI YA CRBC KUKAMILISHA UJENZI WA BARABARA 7 UBUNGO IFIKAPO AGOSTI 14, 2026








STAMICO YATAMBULIWA KAMA SHIRIKA BORA LA MADINI TANZANIA
Saturday, June 13, 2026
SHEIKH PEMBE ASISITIZA KUHUSU UMUHIMU WA AMANI, ATAKA WAISLAMU KUILINDA NCHI YAO
Friday, June 12, 2026
SERIKALI YAOMBA AWAMU YA PILI YA MRADI WA MAZIWA FAIDA KUANZA MWAKA 2027
NA REBECA DUWE TANGA
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeomba kuendelea kwa ushirikiano kati ya Tanzania na Ireland kupitia utekelezaji wa Awamu ya Pili ya Mradi wa Maziwa Faida kuanzia mwaka 2027 hadi 2032, ili kuendeleza mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kuimarisha uzalishaji wa maziwa, kuongeza tija na kuboresha maisha ya wafugaji nchini.
Ombi hilo limetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Fabian Madele, wakati akifungua rasmi Maonesho ya Ubunifu na Teknolojia katika Sekta ya Maziwa (TALIRI Open Day 2026) yaliyofanyika katika Kituo cha Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) Kanda ya Mashariki, jijini Tanga.
Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Madele amesema Mradi wa Maziwa Faida unaotekelezwa kwa ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania kupitia TALIRI na Taasisi ya Maendeleo ya Kilimo na Chakula ya Ireland (TEAGASC), kwa ufadhili wa Serikali ya Ireland kupitia Ubalozi wa Ireland nchini Tanzania, umeleta mageuzi makubwa katika sekta ya maziwa, hususani katika Mkoa wa Tanga.
Dkt. Madele amesema kabla ya kuanza kwa mradi huo, wafugaji wengi walikuwa wakizalisha wastani wa lita 3 hadi 5 za maziwa kwa ng’ombe mmoja kwa siku. Kupitia matumizi ya teknolojia bora za ufugaji, malisho bora, huduma za ugani zilizoimarishwa na mafunzo kwa wafugaji, uzalishaji umeongezeka hadi wastani wa lita 15 kwa ng’ombe mmoja kwa siku katika maeneo mengi yaliyofikiwa na mradi.
“Matokeo haya yanaonesha wazi mchango mkubwa wa utafiti, ubunifu na ushirikiano wa kimataifa katika kuongeza tija, kuboresha kipato cha wafugaji na kuimarisha usalama wa chakula na lishe nchini,” alisema Dkt. Madele.
Aidha, Dkt. Madele amesema kuwa Tanzania kwa sasa inazalisha takribani lita bilioni 4.1 za maziwa kwa mwaka, wakati mahitaji ya taifa yanakadiriwa kufikia lita bilioni 13 kwa mwaka, amesema hali hiyo inaonesha uwepo wa fursa kubwa ya kuwekeza zaidi katika uzalishaji wa maziwa ili kupunguza pengo la mahitaji na kuongeza mchango wa sekta hiyo katika uchumi wa taifa.
Kwa upande wake, Mwakilishi wa Balozi wa Ireland nchini Tanzania, Bi. Suzanne Keatinge, ameipongeza TALIRI kwa utekelezaji mzuri wa Mradi huo na kuwatambua watafiti, wataalamu wa ugani na wadau wote waliochangia mafanikio ya mradi huo.
Nae Mkurugenzi Mkuu wa TALIRI Prof. Erick Komba, ameishukuru Serikali ya Ireland kwa ufadhili wake na kueleza kuwa mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa Awamu ya Kwanza ya Mradi wa Maziwa Faida (2021/2022–2025/2026) yameweka msingi imara wa kuendelea kuleta mabadiliko chanya katika sekta ya maziwa nchini.
Prof. Komba alisema TALIRI itaendelea kuhakikisha kuwa matokeo ya tafiti, ubunifu na teknolojia zilizozalishwa kupitia mradi huo zinawafikia wafugaji wengi zaidi nchini kwa lengo la kuongeza uzalishaji, tija na ushindani wa sekta ya maziwa.
Aliongeza kuwa Mradi wa Maziwa Faida, uliogharimu zaidi ya Euro milioni 3 sawa na zaidi ya Shilingi bilioni 7 za Kitanzania, umenufaisha zaidi ya wanawake na vijana 3,000 katika ukanda wa pwani ya mashariki, hususan Wilaya ya Muheza mkoani Tanga.
Kwa mujibu wa Prof. Komba, mafanikio makubwa ya mradi huo ni pamoja na kufanya tafiti za malisho bora yanayostahimili mazingira ya ukanda wa pwani, kubaini aina bora za ng’ombe wa maziwa, kuwajengea uwezo maafisa ugani, kutoa mafunzo kwa wafugaji, kuimarisha vyama vya ushirika vya wafugaji, kuboresha miundombinu ya utafiti pamoja na kuanzisha mashamba darasa ambayo yamekuwa vituo muhimu vya kujifunzia na kusambaza teknolojia za kisasa za ufugaji wa ng’ombe wa maziwa.
Mradi wa Maziwa Faida unatajwa kuwa mfano bora wa ushirikiano wa maendeleo unaochochea matumizi ya utafiti na ubunifu katika kutatua changamoto za uzalishaji wa maziwa na kuchangia ukuaji endelevu wa sekta ya mifugo nchini Tanzania.
TANZANIA NA GIZ ZASAINI MAKUBALIANO YA KUIMARISHA USHIRIKISHWAJI WA WANAWAKE KATIKA TEKNOLOJIA ZA KIDIJITALI.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...





















