Tanzania Daily Eye
Tuesday, May 5, 2026
ROSTAM AZIZI : KENYA -TANZANIA NA KENYA ZIWE NA MFUMO MMOJA WA KIBIASHARA KUPATA MAFANIKIO ZAIDI YA BIASHARA
MBUNGE MWAKIOJA ATANGAZA NEEMA YA SOKA WILAYA MKINGA
>Agawa vifaa vya michezo kwa timu zote zinazoshiriki Ligi ya wilaya ya Mkinga
Na Oscar Assenga, MKINGA
Mbunge wa Jimbo la Mkinga mkoani Tanga, Twaha Mwakioja, ameahidi kushirikiana na wadau mbalimbali wa michezo kuinua kiwango cha soka wilayani humo kwa kuwekeza katika elimu na maendeleo ya waamuzi pamoja na makocha.
Akizungumza wakati wa mchezo wa Ngao ya Jamii uliokwenda sambamba na uzinduzi wa Ligi ya Wilaya ya Mkinga, uliofanyika katika Uwanja wa Chamazi, Kata ya Matamba, Mwakioja alisema lengo lao ni kuwekeza katika michezo kwa vijana ili kuwapatia ajira, kuboresha afya zao, pamoja na kuimarisha amani, mahusiano mema na ushirikiano miongoni mwao.
Alieleza kuwa dhamira yao ni kuwashika mkono vijana ili waweze kupiga hatua kutoka ngazi ya wilaya, kwenda mkoa, kanda na hatimaye ligi za juu, huku yeye akiwa bega kwa bega nao kuhakikisha wanafikia malengo yao.
Mbunge huyo alibainisha kuwa wamepata taarifa ya kuwepo kwa changamoto mbalimbali, ikiwemo uhaba wa makocha na waamuzi wenye sifa. Hivyo, wamejipanga kuwekeza katika mafunzo ya makocha ili kila kata iwe na angalau kocha mmoja mwenye ujuzi na mafunzo rasmi, pamoja na kuandaa waamuzi wenye vyeti ili kuboresha usimamizi wa michezo.
Alisisitiza kuwa uwekezaji huo utaenda sambamba na ushirikiano na Chama cha Soka Wilaya ya Mkinga katika kukuza na kuendeleza vipaji vya vijana.
Aidha, alisema mpango wao ni kuhakikisha kila kata na kijiji kinakuwa na timu ya mpira wa miguu inayoshiriki ligi ya wilaya. Aliongeza kuwa watawekeza zaidi ili kuibua timu imara zitakazoweza kushiriki ligi za ngazi ya mkoa, kanda na hatimaye Ligi Kuu, hatua itakayosaidia kuitangaza Mkinga katika ramani ya soka nchini.
Katika kuonyesha dhamira hiyo, Mwakioja alikabidhi jezi na mipira kwa timu zinazoshiriki ligi hiyo, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha na kusaidia maendeleo ya michezo wilayani humo.
Kwa upande wake, Katibu wa Chama cha Soka Wilaya ya Mkinga, Fadhili Habibu, alisema ratiba ya ligi hiyo imeanza Mei 4 katika kituo cha Mkinga, huku kituo cha Maramba kikitarajiwa kuanza Mei 6 (Jumatano), ambapo kutakuwa na vituo vinne vitakavyochezwa katika Kijiji cha Maramba, ikiwa ni pamoja na mechi kati ya Viva Dynamo na Maramba FC.
Habibu alisema lengo la ligi hiyo ni kusimamia na kuibua vipaji vya vijana, pamoja na kuwapa mwelekeo wa maendeleo yao kisoka. Alimshukuru mbunge kwa kujitoa na kushirikiana nao katika kufanikisha malengo hayo.
Naye Mwenyekiti wa Chama cha Soka Wilaya ya Mkinga, Hassan Zumo, alimpongeza mbunge kwa juhudi zake za kuendeleza michezo wilayani humo, akieleza kuwa hatua hiyo imeongeza hamasa na matarajio ya ushindani mkubwa katika ligi hiyo, hasa baada ya timu kukabidhiwa vifaa.
Zumo aliongeza kuwa tangu kuanzishwa kwa chama hicho mwaka 2008, wamekuwa wakipeleka vilabu katika mashindano ya ngazi ya mkoa lakini wamekuwa wakikwama kutokana na changamoto za kifedha. Hata hivyo, alisema kupitia uongozi wa Mbunge Mwakioja, wana matumaini ya kupata timu itakayoweza kufika hadi Ligi Kuu.
Aidha, timu zinazoshiriki mashindano hayo zimeahidi kujituma na kupambana kwa juhudi zote ili kuhakikisha ligi hiyo inaleta mafanikio na tija kwa vijana wa Wilaya ya Mkinga.
Monday, May 4, 2026
RAIS RUTO AMPONGEZA RAIS SAMIA KWA KUUNDA TUME YA JAJI CHANDE
MCHENGERWA: BIMA YA AFYA KWA WOTE IWE KIPAUMBELE BAJETI YA 2026/27
Source
Thursday, April 30, 2026
Oraimo Watch 6 Lite: Smartwatch mpya inayotingisha sokoni
Soko la smartwatch linaendelea kukua kwa kasi, na sasa limepokea nyongeza mpya yenye ushindani mkubwa, Oraimo Watch 6 Lite. Ikiwa imebuniwa kwa kuzingatia mahitaji ya mtumiaji wa kisasa, saa hii inaleta mchanganyiko wa teknolojia ya hali ya juu, muonekano wa kuvutia, na utendaji bora kwa matumizi ya kila siku, ikiambatana na kauli mbiu yake “Kuwa Fiti Kimtindo.”
Moja ya vitu vinavyoifanya Oraimo Watch 6 Lite kuwa ya kipekee ni skrini yake kubwa ya 2.01 HD, inayotoa mwonekano ulio wazi na wa kuvutia. Pia inakuja na kipengele cha Bluetooth HD Calling, kinachokuwezesha kupokea na kupiga simu moja kwa moja kupitia saa yako kwa urahisi wa hali ya juu ukiwa popote ulipo.
Kwa upande wa uimara, saa hii inajivunia hadi siku 30 za matumizi thabiti, hivyo kukuondolea usumbufu wa kuchaji mara kwa mara. Aidha, ikiwa na kiwango cha IP68 (waterproof & dustproof), Oraimo Watch 6 Lite iko tayari kukabiliana na mazingira tofauti bila wasiwasi.
Uzinduzi rasmi wa bidhaa hii ulifanyika tarehe 4/4/2026 katika duka la Kinondoni, ambapo wadau na wapenzi wa teknolojia walipata nafasi ya kuiona na kuijaribu kwa karibu. Baadaye, uzinduzi wa pili wa kipekee (soft launch) ulifanyika kwa kushirikiana na jamii ya wakimbiaji ya iRun, ambapo washiriki walipata uzoefu halisi wa kutumia saa hii wakati wa mazoezi. Hii ilikuwa njia ya kuonyesha jinsi vipengele vya afya na ufuatiliaji wa mwili vinavyofanya kazi kwa ufanisi.
Kwa matumizi ya kila siku, Oraimo Watch 6 Lite ina uwezo mkubwa wa kusaidia katika ufuatiliaji wa usingizi, mazoezi, pamoja na kukuza mtindo bora wa maisha. Pamoja na muonekano wake wa kisasa na UI interface iliyo rafiki kwa mtumiaji, saa hii inakuwa chaguo sahihi kwa yeyote anayehitaji msaidizi wa kidijitali mkononi.
Kwa sasa, Oraimo Watch 6 Lite inapatikana sokoni kwa ununuzi, ikiwa tayari kuleta mabadiliko katika maisha ya watumiaji wake. Kwa kifupi, ni zaidi ya saa ni mshirika wako wa kila siku katika afya, mawasiliano, na mtindo wa maisha, ukiakisi kikamilifu kauli mbiu yake: “Kuwa Fiti Kimtindo.”
Saturday, April 18, 2026
CCM Mkoa wa Tanga ya gundua ubadhirifu Saruji 150 ikiwa ni poamoja uwizi wa saruji katika Hospitali ya wilaya Kilindi mkoani Tanga
Na Rebeca Duwe ,Kilindi
Mwenyekiti wa CCM Mkoa waTanga Rajabu Abdrahman amesema Chama cha Mapinduzi hakitaweza kuwafumbia Macho wale wote wanaohusika na ubadhirifu wa Fedha za serikali kwa kuyafanyia mambo yao binafsi badala ya kufanya kazi iliyo kusudiwa ya kuondoa changamoto za wananchi .
Hayo aliyasema wakati wa ziara yake ya kukagua ujenzi wa Hospitali ya wilaya ya Kilindi ambapo kulitokea ubadhirifu wa saruji 145 iliyohifadhiwa kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali hiyo ili kuondoa changamoto ya huduma za afya .
Aidha alisema kwa msistizo kuwa amesikia uwizi wa saruji na kuharibika saruji iliyoganda kutokana kukaa kwa muda mrefu bila kutumika kwa kazi iliyokusudia jambo ambalo inaonyesha kuwa ni uzembe wa wataalamu waliopewa kazi hiyo.
"Mradi huu wa Hospitali ya wilaya Kilindi pesa yake imetolewa na Rais Dkt Samia Suluhu Hasan hivyo kutokutumia ipasavyo ni ubadhitifu wa Pesa za serikali na kuwakosesha wananchi haki zao za kupata huduma ya Afya,kwani kabla ya kutokuwepo kwa Hospitali hiyo wananchi wa Kilindi walikuwa wanaifuata huduma hiyo Morogoro ,Handeni au Tanga mjini jambo ambalo inawatia gharama kubwa ya usafiri wananchi hao."
Alisema Rajabu
Sambamba na hayo Mwenyekiti huyo CCM aliagiza watu wote waliofanya ubadhirifu kwa njia moja ama nyingine wachukuliwe hatua kali za sheria ili miradi iweze kukamilika kwa wakati kama ambavyo mhe Rais amelekeza na kutaka kuondoa changamoto za wananchi anaowaongoza.
Kwa upande wake MKurugenzi wa halmashauri ya Wilaya Kilindi mkoani Tanga John Mgalula alisema walipata taarifa za uwizi wa saruji na kumkamata bodaboda akiwa na mifuko mitano ya saruji na kuwapeleka polisi ambapo mpaka sasa kuna mlinzi yuko polisi na fundi pamoja na bodaboda ambapo uchunguzi bado unaendelea kwa mujibu wa taratibu za kisheria.
Aliongeza kuwa baada ya kugundua hivyo walianza kuhesabu na kagundua kuwa kuna mifuko ya aina tatu ambayo ni iliyoibiwa,iliyoganda na ambayo ni mizima ambayo jumla ilikuwa ni mifuko 193 ambayo kuna iliyotumika kati ya hiyo na iliyopo na ambayo imeharibika sana.
Hata hivyo alisema kuwa bado wanaendelea kufuatilia kujua ni mifiko mingapi inafaa na iliyopo ndani ya stoo kwa ujenzi kugundua mifkuko mi ngapi haifai kabisa ili kuendaelea ujenzi Hospitali kwa ajili ya kuwahudumia u wananchi wa kilindi.
Thursday, April 16, 2026
SERIKALI YAJIPANGA KUZIFANYIA UKARABATI SHULE ZOTE KONGWE NCHINI - PROF. SHEMDOE






Wednesday, April 15, 2026
WAZIRI SANGU: RAIS SAMIA AWEZESHA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII KUWA HIMILIVU
KAMATI YA FUM KISHAPU YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO YENTE THAMANI YA TSH. BILION 1.2
Ziara hiyo imefanyika Aprili 15 hadi 16, 2026, ikiongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Mhe. Enock Reuben, ambapo wajumbe wa kamati walitembelea na kujionea hali halisi ya utekelezaji wa miradi hiyo ya maendeleo katika maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo.
Miradi iliyokaguliwa inagusa moja kwa moja maisha ya wananchi, ikiwemo miradi ya afya, umeme wa jua, ujenzi wa vyumba vya madarasa, matundu ya vyoo kwenye baadhi ya zahanati na maegesho ya magari mnada wa Mhunze, ujenzi wa nyumba mpya ya Mkurugenzi Mtendaji, ujenzi wa vichomea taka katika zahanati, pamoja na maendeleo ya kikundi cha Vijana na Wanawake waliopewa mikopo ya asilimia 10 wa Halmashauri hiyo.
Kwa mujibu wa kamati hiyo, lengo kuu la ziara lilikuwa ni kufuatilia kwa karibu matumizi ya fedha za miradi, kutathmini hatua za utekelezaji, pamoja na kubaini changamoto zinazoweza kukwamisha ukamilishaji wa miradi hiyo.
Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, Mhe. Reuben amesisitiza umuhimu wa kuhakikisha kila shilingi ya umma inaleta thamani halisi kwa wananchi (value for money), huku akiwataka watendaji kusimamia miradi kwa weledi na uwajibikaji mkubwa.
Kamati haikuishia kukagua tu, bali pia ilitoa maelekezo na ushauri muhimu kwa watendaji. Miongoni mwa mambo yaliyosisitizwa ni, usimamizi makini wa fedha za miradi, uzingatiaji wa viwango vya ubora wa ujenzi, kukamilika kwa miradi ndani ya muda uliopangwa pamoja na utatuzi wa changamoto kwa wakati.
Hatua hizi zinalenga kuhakikisha miradi hiyo inaleta manufaa yaliyokusudiwa kwa wananchi bila kuchelewa wala kupoteza rasilimali.
Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango ina nafasi muhimu katika kusukuma maendeleo ya wilaya. Kupitia ziara kama hizi, kamati inaendelea kuhakikisha uwajibikaji unaimarika, fedha zinatumika ipasavyo, na miradi inatekelezwa kwa ufanisi.
Kwa ujumla, ziara hii ni ishara ya dhamira ya dhati ya viongozi wa Kishapu katika kusimamia maendeleo na kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora zinazotokana na miradi hiyo.Makamo mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga na Diwani wa Kata ya Masanga Mhe. Enock Reuben akisikiliza maelezo kwenye ziara ya kamati ya Fedha Utawala na Mipango iliyofanyika Aprili 14-15, 2026 ya ukaguzi wa miradi 7 ya maendeleo yenye thamani ya Tsh. bilioni 1.2
Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga Emmanuel Johnson akiielezea jambo kamati ya Fedha Utawala na Mipango wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi 8 ya maendeleo yenye thamani ya Tsh. bilioni 1.2 Aprili 14-15, 2026
Diwani wa Kata ya Mwamalasa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga Mhe. Bushi Mpina ambaye pia ni Mjumbe wa kamati ya Fedha, Utawala na Mipango wa Halmashauri ya wilaya hiyo
Diwani wa viti maalumu Kata ya Ukenyenge Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga Mhe. Sophia Masele ambaye pia ni Mjumbe wa kamati ya Fedha, Utawala na Mipango wa Halmashauri ya wilaya hiyo
Diwani wa Kata ya Songwa wilayani Kishapu mkoani Shinyanga Mhe. Abdul Ngoromole ambaye pia ni Mjumbe wa kamati ya Fedha, Utawala na Mipango wa Halmashauri ya wilaya hiyo
Diwani wa Kata ya Kishapu Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga Mhe. Joel Ndettoson ambaye pia ni Mjumbe wa kamati ya Fedha, Utawala na Mipango wa Halmashauri ya wilaya hiyo
Picha za Miradi
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...













































