Tanzania Daily Eye
Friday, August 14, 2026
WATUMISHI WA WIZARA WATEMBELEA OFISI ZA UBALOZI WA TANZANIA NCHINI INDIA
Monday, June 29, 2026
VIJANA WAHIMIZWA KULINDA NA KUDUMISHA AMANI
Sunday, June 28, 2026
TRA YAPANDA MITI 1000 KATIKA SHULE UMMY MWALIMU KUADHIMISHA MIAKA 30 YA KUANZISHWA KWAKE
NA REBECA DUWE TANGA
Katika kuendeleza shughuli za uwajibikaji kwa jamii, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) leo imepanda miti isiyopungua 1,000 katika Shule ya Sekondari Ummy Mwalimu iliyopo Kata ya Maweni, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 30 tangu kuanzishwa kwa mamlaka hiyo.
Akizungumza wakati wa zoezi hilo, mgeni rasmi ambaye ni Naibu Kamishna wa Shughuli za Ufundi – Kodi za Ndani, Ted Frank Silkiluwasha, alisema pamoja na jukumu la kukusanya mapato ya Serikali, TRA imeendelea kushiriki shughuli mbalimbali za kijamii zinazoleta maendeleo kwa wananchi.
Alisema zoezi la upandaji miti linaonesha ushirikiano mzuri uliopo kati ya TRA na jamii, huku akisisitiza umuhimu wa kuitunza miti hiyo ili iweze kukua na kutoa manufaa kwa vizazi vya sasa na vijavyo.
"Utunzaji wa miti ni muhimu kwa sababu huchangia kulinda tabaka la ozone, kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi na kulinda afya ya binadamu pamoja na viumbe wengine," alisema Silkiluwasha.
Aidha, alimtaka Meneja wa TRA Mkoa wa Tanga kuendelea kutoa elimu ya kodi kwa wananchi, akieleza kuwa elimu hiyo inapaswa kuwa endelevu. Pia alipendekeza Shule ya Sekondari Ummy Mwalimu kuingizwa katika mpango wa Tax Club, unaolenga kuwajengea wanafunzi uelewa na utamaduni wa kulipa kodi.
"Ukubwa wa taifa haupimwi kwa wingi wa watu au silaha, bali kwa uchumi imara. Uchumi huo hujengwa kupitia ukusanyaji wa mapato ya Serikali ambayo huwezesha kuboresha sekta za elimu, afya, miundombinu na hata kuimarisha ulinzi na usalama," alisema.
Kwa upande wake, Meneja wa TRA Mkoa wa Tanga, Castrol John, aliwataka wafanyabiashara kuzingatia sheria za kodi na kuacha kutumia njia zisizo halali wanapoingiza bidhaa nchini.
Pia alihimiza wananchi kuwafichua wakwepa kodi, akibainisha kuwa TRA ina utaratibu wa kutoa zawadi kwa watu watakaotoa taarifa zitakazosaidia kuokoa mapato ya Serikali yanayopotea.
Naye Mhifadhi kutoka Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Michael Charles, aliipongeza TRA kwa hatua hiyo na kuzitaka taasisi nyingine kuiga mfano huo.
Alisema miti ina mchango mkubwa katika kuhifadhi mazingira, kuboresha ubora wa hewa, kuhifadhi viumbe hai, kuongeza vivutio vya utalii, kutoa matunda na kuchangia afya bora ya jamii.
Akitoa shukrani kwa TRA, Mkuu wa Shule ya Sekondari Ummy Mwalimu, Asha Kitundu, alisema shule hiyo ina eneo la takribani ekari 700, hivyo miti iliyopandwa itasaidia kutoa kivuli, kuzuia mmomonyoko wa udongo na kuboresha mazingira ya kujifunzia.
Aidha, aliwahamasisha wadau wengine kujitokeza kuisaidia shule hiyo, akieleza kuwa bado ni changa na inahitaji ushirikiano wa jamii katika kuendeleza maendeleo yake.
Shule ya Sekondari Ummy Mwalimu ilianzishwa mwaka 2022 ikiwa na wanafunzi 316 waliohamishwa kutoka Shule ya Sekondari Maweni. Kwa sasa shule hiyo ina wanafunzi 916 na walimu watatu, huku ikitarajia kupokea wanafunzi 83 wa Kidato cha Tano mwezi Julai mwaka huu.
Saturday, June 27, 2026
ZAIDI YA WANUFAIKA 17,000 WA KAYA MASKINI RUVUMA WAFIKIWA NA BIMA YA AFYA KWA WOTE.
Meneja wa mfuko wa bima ya Afya Mkoa wa Ruvuma Hansi John Akizungumza na waandishi wa habari waliomtembelea ofisini kwake kuhusu mipango ya serikali kuzifikia kaya zisizo na uwezo na utekelezaji wake kwa awamu kupitia mpango wa TASAF.
Na Regina Ndumbaro Songea-Ruvuma
Mfuko wa Bima ya Afya Mkoa wa Ruvuma umefanikiwa kuwafikia zaidi ya wanufaika 17,000 kutoka kaya zisizo na uwezo katika utekelezaji wa awamu ya kwanza ya mpango wa Bima ya Afya kwa Wote unaotekelezwa na Serikali kupitia mpango wa TASAF.
WADAU KILOLO WAJADILI FURSA ZA KUIMARISHA UCHUMI KUPITIA MRADI WA INUA II
Hand in Hand Eastern Africa–Tanzania imekutana na viongozi na wadau wa Wilaya ya Kilolo kwa lengo la kujadili fursa za ushirikiano katika utekelezaji wa Mradi wa INUA II, unaolenga kuwawezesha wanawake, vijana na makundi yaliyo katika mazingira ya uhitaji kujenga uchumi endelevu.
Thursday, June 25, 2026
ALIYEDANGANYA FAMILIA YA MUMEWE KUWA NI MJAMZITO AKAMATWA KWA UWIZI WA MTOTO MCHANGA LUSHOTO.
Na Rebeca Duwe , Lushoto.
Jeshi la polisi Mkoa wa Tanga linamshikilia mwanamke mmoja aliyejulikana kwa jina la Habiba Seleman Fundi kwa tuhuma za wizi wa mtoto mchanga katika hospitali ya wilaya ya Lushoto Mkoani Tanga.
Akithibitisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo Kamanda wa polisi mkoa wa Tanga Almachius Mchunguzi alisema mtuhumiwa huyo alikamatwa mnamo tarehe 21juni mwaka huu Majira ya saa 1 usiku katika kitongoji cha Garekaya Wiliyani Lushoto akiwa na mtoto huyo.
Kamanda Mchunguzi alisema alisema kuwa manamo juni 19 mwaka huu saa 11jioni mama mzazi wa mtoto huyo Mwanaidi Juma Nyaki mkazi wa Kijiji cha Kwemakame aliripoti kupotea kwa mwanae wa siku moja .
Aidha aliongeza kusema kuwa mtuhumiwa huyo alitumia mbinu ya kujenga urafiki wa karibu na mama mzazi wa mtoto huyo pamoja ndugu waliokuwa wakimhudumia hospitalini hapo.
Alisema baada ya kupata imani yao alichukua fursa hiyo na kumweka mtoto ndani ya beseni lenye nguo kisha kutoweka na mtoto bila kufahamika kwa wakati huo.
Sambamba na hayo alisema uchunguzi wa kina umebaini kuwa mtuhumiwa alikuwa akidai kwa muda mrefu kuwa ni mjamzito na kuwahakikishia ndugu,jama wa mume wake kuwa alikuwa akisubiri kujifungua.
Hata hivyo baadaya muda ameuweka kufika aliamua kufanya mpango huo wa kuiba mtoto ili kuwathibitishia madai yake kwa familia ya mumewe na watu waliokuwa wakimzunguka kuwa alikuwa mjamzito na amejifungua.
mwisho
Wednesday, June 24, 2026
UVCCM SHINYANGA: TUSIHANGAIKE NA MATUSI YA WAPINZANI MTANDAONI, TUWAJIBU KWA MATOKEO YA KAZI
SHILATU AZINDUA MASHINDANO YA KUSAKA VIPAJI KANDA YA KUSINI, SERIKALI YAIMARISHA MKAKATI WA KUKUZA SANAA NA MICHEZO KWA VIJANA
Tuesday, June 23, 2026
SERIKALI YABADILI GIA, SASA KUWA RAFIKI WA BIASHARA NA SIO WADHIBITI-KAPINGA
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Mara nyingi wanawake wamekuwa watu wa kukaa kimya bila kusema wanataka nini ili kuridhishwa katika mapenzi na mbaya zaidi katika swala zima ...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...



























