Tanzania Daily Eye
Monday, April 13, 2026
SEKTA YA VIWANDA YASHIRIKIANA NA VETA, ENABEL KUANDAA WATAALAMU
TANESCO Hanang Yapokea Gari Jipya la Kisasa Kuimarisha Huduma za Umeme
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Wilaya ya Hanang’ mkoani Manyara limepokea gari jipya aina ya Isuzu FRR lenye mitambo ya kisasa kwa ajili ya kuboresha huduma za umeme wilayani humo.
Gari hilo limekabidhiwa leo rasmi na Mkuu wa Wilaya ya Hanang’, Almish Hazal, katika hafla iliyofanyika kwenye ofisi za TANESCO Hanang’.
Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Hazal amesema gari hilo lina uwezo mkubwa wa kubeba vifaa vizito, kubadilisha nguzo pamoja na transfoma kwa urahisi, hivyo litasaidia kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya TANESCO.
Hazal amesema kuwa hatua hiyo ni sehemu ya mafanikio ya serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuboresha huduma za umeme, akieleza kuwa vijiji vyote 96 vya Wilaya ya Hanang’ tayari vimepata umeme, na sasa juhudi zinaelekezwa kwenye vitongoji 116 vilivyopo katika kata 33 za wilaya hiyo.
“Gari hili litasaidia sana utendaji kazi wa TANESCO, hasa kuwafikia wananchi kwa haraka pale changamoto za umeme zinapotokea,” amesema Hazal.
Kwa upande wake, Kaimu Meneja wa TANESCO Wilaya ya Hanang’, Mhandisi Mwitondi Charles Rugembe, amesema kabla ya kupatikana kwa gari hilo walilazimika kukodi gari kwa gharama kubwa, hali iliyoongeza matumizi yasiyo ya lazima.
“Awali tulikuwa tunakodi gari na kutumia gharama kubwa, lakini sasa serikali imeokoa fedha hizo kupitia upatikanaji wa gari hili jipya,” amesema Rugembe.
Ameongeza kuwa gari hilo litasaidia kupunguza changamoto ya kukatika kwa umeme mara kwa mara, kwani sasa wataalamu wataweza kufika kwa wakati kwenye maeneo yenye hitilafu na kufanya matengenezo haraka.
Naye Mbunge wa Jimbo la Hanang’, Asia Halamga, amesema kuwa TANESCO wilayani humo tayari imepata gari la kutembelea pamoja na gari hilo jipya la kazi nzito, jambo linaloonesha dhamira ya serikali katika kuboresha miundombinu ya huduma za umeme.
Asia amewataka wananchi kuendelea kumuombea Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ili aendelee kupeleka miradi zaidi ya maendeleo katika Wilaya ya Hanang’.
Saturday, April 11, 2026
BAYI: AMANI NDIO MUHIMILI WA MAFANIKIO KATIKA MICHEZO
Amani na michezo vimetajwa kuwa ni vitu vyenye uhusiano wa karibu, ambapo kila kimoja kinakiimarisha kingine katika kujenga jamii na taifa imara.
Michezo hustawi zaidi katika mazingira yenye utulivu, huku ikiwa ni chombo muhimu cha kukuza umoja, mshikamano wa kijamii, na maelewano miongoni mwa watu wenye asili na tamaduni tofauti.
Kupitia michezo, jamii hujenga jukwaa la pamoja lenye ushindani unaoambatana na heshima, nidhamu, na urafiki, hali inayopunguza hofu na kuongeza kuaminiana.
Mmoja wa wanamichezo mashuhuri na sauti yenye heshima duniani katika riadha, Filbert Bayi, anaamini kuwa amani na michezo haviwezi kutenganishwa.
Katika mahojiano maalum, Bayi ambaye amewahi kushikilia rekodi ya dunia, alibainisha kuwa hakuna nchi inayoweza kukuza vipaji vya michezo bila kuwepo kwa amani na utulivu. Alisisitiza kuwa michezo si burudani pekee, bali ni chanzo kikubwa cha ajira, huduma za kijamii, na undugu miongoni mwa watu wa mataifa mbalimbali.
Bayi alieleza kuwa amani huweka mazingira rafiki kwa wanamichezo kufanya mazoezi na kuonesha vipaji vyao bila hofu ya usalama.
Alitolea mfano Tanzania kama kioo cha namna amani inavyochochea maendeleo ya michezo, kwani wanamichezo wana nafasi ya kushindana katika hali ya utulivu. Aliongeza kuwa katika ngazi ya kimataifa, michezo imekuwa ikitumika kupunguza uhasama kati ya mataifa yaliyowahi kuwa kwenye migogoro, akitolea mfano wa mataifa hayo kutembea pamoja wakati wa ufunguzi wa michezo mikubwa.
Mbali na hayo, Bayi alikumbusha tukio la kihistoria la kususia michezo ya Olimpiki ya mwaka 1976 kupinga ubaguzi wa rangi kama ujumbe wa kusisitiza haki, usawa, na amani. Alihitimisha kwa kutoa rai kwa serikali, vyombo vya michezo, na jamii kwa ujumla kuendelea kuwekeza katika michezo kama njia ya kukuza amani, hasa kwa vijana. Alisisitiza kuwa kudumisha amani na umoja ndiyo siri ya kujenga Tanzania imara na yenye ustawi kwa vizazi vijavyo.
CCM MKOA WA TANGA YAWAPA MWEZI MMOJA VIONGOZI WA JIJI LA TANGA KUHAKIKSHA SOKO LA MGANDINI LINABORESHWA NA KUIMARISHWA USAFI.
Na Rebeca Duwe Tanga
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga na mjumbe wa kamati kuu ya Halmashauri kuu ya CCM TaifaRajab Abdurhaman ametoa maelekezo kwa Halmashauri ya Jiji la Tanga kuhakikisha maeneo ya kukusanyia taka katika soko la Mgandini yanaboreshwa kwa kujazwa kifusi ikiwemo kurekebisha barabara za ndani ili kuimarisha usafi.
Hayo aliyasema wakati wa ziara yake ya kufuatilia utekelezajia wa magagizo aliyoyatoa awali kuhusu kuboresha usafi wa soko hilo lilipo jijini Tanga ambapo viongozi wa jiji walianza kuyafanyia kazi ikiwemo kuondosha uchafuzi uliokuwepo awali .
Aidha alisisitiza umuhimu wa kuhakikisha maji ya mvua yanaelekezwa ipasavyo kwenye mifereji ili kuepusha mafuriko na uharibifu wa miundombinu katika soko hilo ili kuweza kuondoa changamoto ya tope kwa wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla.
Awali, wakati wa ziara yake ya kukagua hali ya usafi, Mwenyekiti huyo hakuridhishwa na mazingira ya soko hilo na kutoa muda wa mwezi mmoja kwa uongozi wa Jiji kuhakikisha hali ya usafi inaboreshwa.
Akizungumza baada ya kufanya ziara ya ufuatiliaji, Rajab aliwapongeza Mstahiki Meya pamoja na viongozi wa Jiji kwa kuchukua hatua na kuanza kutekeleza maelekezo yaliyotolewa na Chama cha Mapinduzi.
“Hatuhitaji viongozi wa kulalamika, tunahitaji viongozi wanaochukua hatua kutatua changamoto za wananchi. Mlichokifanya ni kutimiza wajibu wenu,” alisema.
Alisema kuwa hali ya uchafu iliyokuwepo awali haikuwafurahisha viongozi wala wafanyabiashara, hivyo hatua zilizochukuliwa zinaonesha uwajibikaji wa uongozi.
Sambamba na hayo wa Mwenyekiti CCM Rajab alisisitiza kuwa atarejea kukagua maendeleo hayo baada ya wiki mbili na kuonya kuwa hataki kusikia visingizio badala ya utekelezaji.
“Ndani ya mwezi mmoja kuanzia Aprili 9 hadi Mei 9, tunatarajia kuona kazi imeanza. Hatutaki hadithi, tunataka vitendo,” alisisitiza.Rajab
Aidha, alieleza kuwa Jiji la Tanga ni taswira ya mkoa huo, hivyo linapaswa kuwa safi na lenye mpangilio mzuri.
Alikumbusha kuwa zamani Tanga ilikuwa mji unaojulikana kwa usafi na ustaarabu, hivyo ipo haja ya kurejesha hali hiyo.
Kuhusu huduma za vyoo katika soko hilo, Mwenyekiti alieleza kutoridhishwa na hali iliyopo, akibainisha kuwa choo kilichopo hakitoshelezi mahitaji kutokana na idadi kubwa ya watumiaji.
Alisema kuwa hali hiyo inasababisha baadhi ya watu kulazimika kujisaidia katika maeneo yasiyofaa, jambo linalohatarisha afya za wananchi na wafanyabiashara.
Alisisitiza umuhimu wa Jiji kutafuta suluhisho la kudumu, ikiwemo kuboresha mfumo wa maji taka ili kuendana na ongezeko la watumiaji.
Hata hivyo, aliwapongeza viongozi kwa kuanza mpango wa kujenga choo kipya chenye matundu 12 kitakachosaidia kupunguza changamoto hiyo, hasa katika kipindi hiki ambacho soko linatarajiwa kujengwa upya.
Pia alizungumzia changamoto ya msongamano wa magari yanayoleta bidhaa sokoni hapo, akielekeza kuwepo kwa utaratibu maalum wa magari kuingia na kushusha mizigo kwa mpangilio ili kupunguza msongamano na kuboresha usafi.
Alipendekeza magari yapaki katika maeneo maalum yaliyo nje ya soko, kisha yaingie kwa zamu kushusha bidhaa.
Katika hatua nyengine alisisitiza umuhimu wa kujenga mifereji ya maji ili kuzuia maji ya mvua kutuama au kuingia sokoni, hali inayochangia uchafu na uharibifu wa mazingira.
Alimalizia kwa kuwataka viongozi wa Jiji kuwa karibu na wananchi na kushughulikia changamoto zao kwa vitendo, akibainisha kuwa wananchi hao ndio chanzo cha mapato ya Jiji kupitia kodi.
Kwa upande wake, Naibu Meya ambaye pia ni Diwani wa kata ya mwanzange ambalo eneo lililopo soko hilo, Khalid Rashid alisema kuwa Jiji lina mpango wa kuboresha miundombinu ya ndani ya soko, ikiwemo njia za kupita ili kuondoa changamoto ya matope wakati wa mvua. Alibainisha kuwa kazi hiyo inatarajiwa kuanza ndani ya wiki moja.
Friday, April 10, 2026
AMANI NI SILAHA YA KUTIMIZA NDOTO NA MAONO YETU- MSIGWA
Thursday, April 9, 2026
SAMAMBA ATOA WITO GST KUBORESHA MAZINGIRA YA KAZI, KUIMARISHA USHIRIKIANO

Na Mwandishi Wetu - Dodoma
Wednesday, April 8, 2026
TRA TANGA YAVUKA MALENGO KATIKA UKUSANYAJI WA MAPATO NDANI YA MIEZI TISA KUANZIA JULAI 2025 HADI MACH 2026.
MAMLAKA ya mapato (TRA)mkoani Tanga imeweka rekodi mpya ya ukusanyaji wa mapato baada ya kukusanya jumla ya Shilingi Bilioni 406.17 katika kipindi cha miezi tisa (Julai 2025 – Machi 2026), ikiwa ni ongezeko la asilimia 137 ya lengo lililowekwa.
Katika kipindi hicho, Mkoa ulikadiriwa kukusanya kiasi cha Shilingi Bilioni 296.3, ambapo ufanisi huo mkubwa uliovuka lengo kwa takriban Shilingi Bilioni 110, umetajwa kuwa ni matokeo ya ushirikiano wa karibu kati ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), walipakodi, na vyombo vya ulinzi na usalama mkoani Tanga.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa, Meneja wa TRA Mkoa wa Tanga, Castro John, amewashukuru walipakodi wa Tanga kwa kulipa kodi kwa hiari na kushirikiana na taasisi mbalimbali kama Chama cha Wafanyabiashara (JWT) na Chama cha Wafanyabiashara, Viwanda na Kilimo (TCCIA).
"Huu ni ufanisi mkubwa ambao haujawahi kutokea. Tunamshukuru Mkuu wa Mkoa na vyombo vya usalama kwa kuhakikisha mazingira ya ukusanyaji kodi yanakuwa salama. Sifa hizi ni za walipakodi wa Tanga ambao wamekuwa wasikivu na wazalendo kwa nchi yao," alisema John.
Licha ya mafanikio hayo, John ametoa onyo dhidi ya wafanyabiashara wanaotumia njia zisizo rasmi (njia za panya) kuingiza bidhaa nchini. Alibainisha kuwa bidhaa za magendo siyo tu zinaikosesha serikali mapato, bali ni hatari kwa afya ya mlaji kwani hazijapita katika taasisi za udhibiti wa ubora.
Aliongeza kuwa operesheni dhidi ya magendo zinaendelea na wafanyabiashara kadhaa wameshakamatwa na kutozwa faini kubwa (Penalties), huku akisisitiza kuwa chombo chochote kitakachokutwa kimebeba bidhaa za magendo kitataifishwa kulingana na sheria. Aidha, aliwataka wananchi kudai risiti za EFD na wafanyabiashara kutoa risiti halali katika kila manunuzi.
Meneja huyo, amewahimiza wafanyabiashara kutumia Bandari ya Tanga ambayo sasa inafanya kazi kwa ufanisi mkubwa na kutoa mizigo kwa wakati, jambo linalochochea ukuaji wa biashara mkoani hapa.
Kuhusu wafanyabiashara wenye madeni makubwa, TRA imewataka kufika ofisini kwa ajili ya majadiliano (Negotiations) ili kuwekewa utaratibu wa kulipa kwa awamu. Mamlaka hiyo imebainisha kuwa imeweka "Dawati la Wafanyabiashara" kwa ajili ya kutoa elimu na kusaidia kukuza biashara ndogo ziweze kufikia hatua ya kuwa walipakodi wakubwa.
Meneja huyo ametoa wito kwa wafanyabiashara kujitokeza kukadiriwa mapato yao ili kuepuka changamoto wakati wa zoezi la ukaguzi barabarani.
Tuesday, March 24, 2026
DUNIA YAIPIGIA SALUTE TANZANIA: TUZO ZA STANBIC JIJINI LONDON NI JIBU KWA WANAOBWABWAJA MITANDAONI

Monday, March 23, 2026
MIRADI YA SHILINGI BILIONI 85 KUCHOCHEA USHIRIKIANO WA TANZANIA NA AUSTRIA
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...

































