Friday, May 15, 2026

WANAWAKE WAPEWA ELIMU YA MLIPA KODI ILI KUICHANGAMKIA FURSA

 


NA REBECCA DUWE TANGA 


Wadau wa maendeleo wameombwa kushirikiana na Mamlaka ya mapato Tanzania TRA mkoa wa Tanga kutoa elimu kwa makundi ya wanawake ili waweze kuzikia fursa mbalimbali na hatimaye waweze kulipa kodi kwa maendeleo ya nchi.


Meneja wa Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Tanga CPA Castro John ametoa kauli hiyo leo may 14, 2026 alipokuwa akifungua jukwaa la wanawake na kodi lililoandaliwa na Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Tanga na kufadhiliwa na shirika la GIZ lenye kauli mbiu isemayo "Wanawake na kodi nguzo ya maendeleo ya Taifa"


"Kwa wadau wetu wa taasisi za kifedha tunaomba muendelee kushirikiana nasi katika kuwawezesha wanawake ili kukuza biashara zao kwa misingi ya sheria na kodi" Amesema Meneja Castro 

Katika hatua nyingine Castro alisema Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA Mkoa wa Tanga, ina jukumu la  kutoa Elimu ya mlipakodi pamoja na fursa mbalimbali zinazowazunguka Wanawake Wafanyabiashara na Wajasiriamali ili kumuwawezesha kutanua uelewa juu ya mifumo na Sheria za Kodi Nchini.


"TRA inatambua mchango wa Wanawake katika ulipaji wa Kodi na kwasasa Wanawake wamekuwa mstari wa mbele katika ulipaji wa Kodi Nchini,hivyo naomba muendelee kuwa mstari wa mbele katika ulipaji wa Kodi ili tulijenge Taifa letu"Aliongeza Castro 


Castro aliwataka Wanawake kuendelea kudumisha nidhamu ya ulipaji wa Kodi Nchini nakwamba Mamlaka hiyo ipo tayari wakati wowote kutoa msaada kwa mfanyabiashara anayepitia changamoto yoyote,


"Niwaombe muendelee kudumisha nidhamu ya ulipaji wa Kodi mliyonayo ili tuondoe usumbufu wowote unaoweza kujitokeza endapo mtu atakwepa kulipa Kodi,TRA ipo tayari wakati wowote kutoa msaada kwa mfanyabiashara anayepitia changamoto yoyote, niwaombe ukiwa na changamoto yoyote tuambie tukusaidia usikae nayo alafu baadae unakuja kulalamika" Alisisitiza Castro 


Kwaupande wake,Naibu Katibu wa Jumuiya ya Nchini Wafanyabiashara, Ismail Masoud aliwataka watumishi wa TRA kuwasaidia kutoa Elimu Wafanyabiashara mkoani Tanga ili kuondoa kasoro nyingi zinazowakabili Wafanyabiashara,


"Niwaombe TRA iendelee kutoa Elimu ya mlipakodi ili changamoto za Wafanyabiashara hususani zinazotokana na Elimu ziishe, lakini pia kwasisi Wafanyabiashara,tuache janja janja zakukwepa Kodi, tunataka twende pamoja ili tuweze kufanikisha dira ya Taifa 2050" Alisisitiza Masoud.


Kwa upande wake Afisa maendeleo mkoa wa Tanga Charles Mtali amesema wanawake wana mchango mkubwa wa maendeleo ya kiuchumi .

tofauti na wanaume hivyo wasipowezeshwa itakuwa ni vigumu nchi kufikia malengo yake.

MRADI WA BARRICK-TWIGA FUTURE FORWARD EDUCATION KUBORESHA SEKTA YA ELIMU NYANG’HWALE


Meneja Mkazi wa Barrick nchini Dkt. Melkiory Ngido (kulia) akiweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Mabweni mawili, vyumba vitano vya madarasa na vyoo matundu nane shule ya sekondari Nyang'hwale
Meneja Mkazi wa Barrick nchini Dkt. Melkiory Ngido (kulia) akiwa na viongozi mbalimbali wakati wa hafla ya uwekaji Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Mabweni mawili, vyumba vitano vya madarasa na vyoo matundu nane shule ya sekondari Nyang'hwale.
Muonekano wa sehemu ya madarasa
Muonekano wa sehemu ya vyoo
Meneja Mkazi wa Barrick nchini Dkt. Melkiory Ngido (kulia) akizungumza wakati akiweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Mabweni mawili, vyumba vitano vya madarasa na vyoo matundu nane shule ya sekondari Nyang'hwale.

***
Wakazi wa Halmashauri ya Nyang’hwale ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakinufaika na miradi ya fedha za CSR kutoka mgodi wa Barrick Bulyanhulu, kipindi hiki tena wamefikiwa neema ya kupata fedha kiasi cha shilingi 401,800,000/= za mradi wa ‘Barrick-Twiga Future Forward Education Program, ambazo zitafanikisha kuboresha miundo mbinu ya wanafunzi wa Kidato cha tano na sita katika shule ya Sekondari ya Serikali ya Nyang’hwale iliyopo mkoani Geita.

Hafla ya uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Mabweni mawili, vyumba vitano vya madarasa na vyoo matundu nane shule ya sekondari Nyang'hwale ambapo mgeni rasmi alikuwa Meneja Mkazi wa Barrick nchini Dkt. Melkiory Ngido.

Katika hotuba aliyoitoa katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na viongozi wa serikali,wananchi na wanafunzi, Dkt. Ngido amesema Barrick itaendelea kushirikiana na Serikali katika kuchochea maendeleo ya jamii kupitia sekta mbalimbali, hususani sekta ya elimu kwa lengo la kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia.

Amesema Barrick-Twiga inaamini kuwa elimu ni msingi wa maendeleo ya mtu mmoja mmoja, jamii na taifa kwa ujumla na taifa lolote linalotaka kujenga uchumi imara, jamii yenye maarifa, na kizazi chenye ushindani, halina budi kuwekeza kwa makusudi katika elimu na ndio maana kampuni inaiona elimu siyo tu kama eneo la uwajibikaji kwa jamii, bali kama nguzo ya kimkakati ya maendeleo ya taifa.

“Tunafahamu kuwa darasa bora hujenga ufaulu bora. Bweni salama hujenga utulivu wa mwanafunzi. Mazingira safi ya usafi hulinda afya, heshima na hadhi ya mtoto wa Kitanzania. Hivyo basi, tunapojenga miundombinu ya elimu, tunakuwa tunajenga zaidi ya majengo; tunakuwa tunajenga ndoto, uwezo, fursa na maisha ya baadaye”,amesema.

Dkt. Ngido amesema katika kuthibitisha dhamira hiyo, mwezi Machi mwaka 2023, Barrick iliahidi kutoa Dola za Marekani milioni 30 kuunga mkono ajenda ya Serikali ya Tanzania ya kuboresha miundombinu ya elimu nchini.

Kupitia mpango wa Barrick-Twiga Future Forward Education Programme, lengo ni kujenga madarasa 1,090, mabweni 270 na matundu ya vyoo 1,640 katika shule 161 nchini kote, zenye uwezo wa kuhudumia takribani wanafunzi 49,000 zitakapokamilika.

Amesema katika awamu ya kwanza ya mpango huu, yenye thamani ya Dola za Marekani milioni 10, ilianza Julai 2023 na kukamilika Desemba 2024, ambapo shule 64 zilinufaika kupitia ujenzi wa madarasa 396, mabweni 97 na vyoo 600.

Aidha, awamu ya pili, pia yenye thamani ya Dola za Marekani milioni 10, ilianza Machi 2025, na kufikia Aprili 2026 ilikuwa imefikia zaidi ya asilimia 83 ya utekelezaji.

Katika awamu hii, takribani shilingi bilioni 19 zimeshatolewa, sawa na asilimia 79 ya bajeti ya awamu hiyo, kwa ajili ya shule 65, zikiwemo madarasa 318, mabweni 116 na vyoo 542.

“Katika utekelezaji wa awamu hii ya pili, Shule ya Sekondari Nyang’hwale ni miongoni mwa shule zinazopata manufaa ya moja kwa moja kupitia ushirikiano huu. Napenda kuweka bayana kuwa, kwa shule hii pekee, Barrick-Twiga imeshalipa shilingi 304,930,973, sawa na asilimia 76 ya fedha za mradi, kwa ajili ya ujenzi wa madarasa matano, mabweni mawili na vyoo vinane”, amesema Dkt. Ngido.

Akifafanua zaidi faida za Mradi huu katika jamii ya Nyang'hwale alisema utawezesha na kuongeza nafasi za wanafunzi kujifunzia katika mazingira bora zaidi, kupunguza msongamano madarasani,kuimarisha mazingira ya malazi kwa wanafunzi, hususan wa kike na kuboresha usafi, afya na hadhi ya shule kwa ujumla.

Kwa upande wake , Katibu Tawala wa Halmashauri ya Nyang’hwale,Bw.. Kaunga Amani amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuweka mazingira bora kwa wawekezaji wa nje na ndani ambao kupitia uwekezaji wanaendelea kuwanufaisha watanzania.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale Ndg. Husna Toni ameishukuru Barrick Tanzania kwa mchango mkubwa uliowezesha ujenzi wa miundombinu hiyo ambao itasaidia kuongeza kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi sambamba na kuwawezesha kusoma katika mazingira rafiki.

Wednesday, May 13, 2026

DC NDILE AWATAKA VIJANA SONGEA KUDUMISHA UZALENDO NA KULINDA AMANI

Mkuu wa Wilaya ya Songea mheshimiwa Wilman Kapenjama Ndile Akizungumza na vijana waliojitokeza katika kongamano hilo leo mei 13 2026 katika ukumbi wa Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma
Mkuu wa Wilaya ya Songea mheshimiwa Wilman Kapenjama Ndile akiwa pamoja na viongozi wa chama wakati alipowasili ukumbi wa Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma leo tarehe 13 mei 2026 katika kongamano la vijana lenye kauli mbiu isemayo "vijana tuyajenge Tanzania ni yetu "
Daktari wa mifugo Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma Dkt Seria Masole akizungumzia umuhimu wa kujiajiri badala ya kusubiri qjira katika kongamano la vijana leo ukumbi wa Manispaa ya Songea 

Na Regina Ndumbaro Songea-Ruvuma 


Mkuu wa Wilaya ya Songea, Kapenjama Ndile, amewataka vijana nchini kuwa wazalendo na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa huku wakiepuka vitendo vinavyoweza kusababisha uvunjifu wa amani.

AFCON 2027: JKCI NA ALMC WAANZA MAANDALIZI YA HUDUMA ZA DHARURA


Na Mwandishi Wetu, Arusha

HOSPITALI ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) chini ya menejimenti ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) wamefanikuwa kutoa huduma za matibabu bure kwa zaidi ya watu 2,000 kuelekea kilele cha maadhimisho ya wauguzi duniani.

Hospitali hizo pia zimekuwa wadhamini wakuu wa Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani yaliyofanyika jijini Arusha, yakihusisha shughuli mbalimbali za kijamii pamoja na utoaji wa huduma za matibabu bure kwa wananchi.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa maadhimisho hayo, Dk Saleh Hamisi Mwinchete ambaye ni Daktari Bingwa wa Moyo pamoja na Mkurugenzi wa Tiba wa Hospitali ya ALMC, alisema maadhimisho hayo ambayo hufanyika kila tarehe 15 Mei kila mwaka ikiwa ni kumbukumbu ya kuzaliwa kwa mwanzilishi wa huduma za uuguzi duniani Florence Nightingale, yaliwakutanisha wauguzi kutoka maeneo mbalimbali nchini katika viunga vya Hospitali ya ALMC.

Alisema kabla ya kufikia kilele cha maadhimisho hayo, wauguzi pamoja na madaktari bingwa walitoa huduma za matibabu bure kwa wakazi wa jiji la Arusha kupitia vituo maalum vilivyowekwa katika Hospitali ya ALMC na Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Arusha (AICC).

Alisema zaidi ya wananchi 1,400 walipata huduma mbalimbali za uchunguzi wa afya hususan magonjwa yasiyoambukiza, huku wauguzi 600 nao wakinufaika na huduma hizo, na kufanya jumla ya watu 2,000 kufaidika na huduma za matibabu bure zilizotolewa na Arusha Lutheran Medical Centre chini ya menejimenti ya JKCI.

Alisema lengo la huduma hizo ni kuwasaidia wananchi kufahamu hali ya afya zao kupitia uchunguzi wa mapema wa presha ya damu, kiwango cha sukari, mapigo ya moyo pamoja na viashiria vingine muhimu vya magonjwa yasiyoambukiza.

Alisema wananchi wengi hupata madhara makubwa ya magonjwa ya moyo kutokana na kutofanya uchunguzi mapema na kutofahamu viwango vya afya zao.

“Tunataka wananchi wajue namba zao. Kufahamu presha yako, kiwango cha sukari pamoja na hali ya afya ya moyo wako ni hatua muhimu ya kujikinga dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza,” alisema Dk. Mwinchete.

Aidha, alisema katika maadhimisho hayo pia kulifanyika tukio maalum la kuwasha mshumaa lililofanyika katika viunga vya Hospitali ya ALMC kwa mara ya kwanza katika historia ya maadhimisho hayo jijini Arusha. Tukio hilo lilikuwa ishara ya upendo, matumaini na amani kwa wagonjwa wanaopatiwa huduma katika hospitali mbalimbali nchini.

Baada ya kuwashwa, mshumaa huo wa upendo na matumaini ulipelekwa katika wodi mbalimbali za wagonjwa waliolazwa hospitalini hapo, ambapo wauguzi walitembelea wagonjwa na kutoa zawadi maalum kama sehemu ya kuwafariji na kuwapa moyo katika kipindi cha matibabu yao

Baada ya zoezi hilo, wauguzi wote waliongozwa na bendi ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika maandamano maalum kuelekea Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Arusha (AICC), ambako walipokelewa mgeni rasmi wa maadhimisho hayo pamoja na viongozi mbalimbali wa sekta ya afya.

Dkt. Mwinchete alisema wauguzi wana mchango mkubwa katika utoaji wa huduma za afya kwani zaidi ya asilimia 60 ya huduma zote anazozipata mgonjwa hospitalini hutolewa kupitia kada hiyo.

Kutokana na umuhimu huo, alisema JKCI pamoja na ALMC zimeendelea kuwekeza katika kuwajengea uwezo wauguzi kupitia mafunzo ya kitaaluma, huduma kwa wateja na mbinu bora za utoaji huduma ili kuongeza ubora wa huduma kwa wagonjwa.

Aidha, alisema taasisi hizo zimeanza maandalizi kuelekea mashindano ya Africa Cup of Nations ambapo ALMC inatarajiwa kuwa miongoni mwa vituo vya kutoa huduma za dharura kwa wageni, mashabiki na washiriki wa mashindano hayo sambamba na kutoa mafunzo maalumu kwa wauguzi na madaktari kuhusu utoaji wa huduma za dharura.

Kwa mujibu wa Dkt. Mwinchete, maandalizi hayo yanahusisha mafunzo maalum kwa wauguzi na wataalamu wengine wa afya ili kuhakikisha Tanzania inakuwa tayari kutoa huduma za afya zenye viwango vya kimataifa wakati wa mashindano hayo makubwa ya bara la Afrika.


Tuesday, May 12, 2026

TPDC YAONGOZA UCHIMBAJI WA GESI SONGO SONGO, SERIKALI YAANZA MAZUNGUMZO YA KUONGEZA LESENI YA PAET


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba amesema Kitalu cha Gesi Asilia cha Songo Songo kina jumla ya visima 12, ambapo Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) imechimba visima tisa, huku Kampuni ya Pan African Energy Tanzania (PAET) ikichimba visima vitatu.

Mhe. Makamba amesema hayo leo Mei 12, 2026, wakati akijibu swali la Mbunge wa Kilwa Kusini, Mhe. Hasnain Gulamabbas Dewji, katika Mkutano wa Tatu, Kikao cha 27 cha Bunge la 13 mjini Dodoma, aliyehoji idadi ya visima vya gesi asilia vilivyochimbwa hadi sasa katika Kisiwa cha Songo Songo.

Amesema kuwa Kitalu cha Songo Songo kinaendelea kuzalisha wastani wa futi za ujazo milioni 84.7 za gesi asilia kwa siku, kulingana na mahitaji yaliyopo.

Aidha, Mhe. Makamba amesema kuwa kutokana na leseni ya sasa ya uendelezaji wa gesi asilia kufikia ukomo mwezi Oktoba 2026, timu ya majadiliano ya Serikali inaendelea na mazungumzo na kampuni ya PAET kuhusu uwezekano wa kuongeza muda wa leseni hiyo ili kuendelea na shughuli za uzalishaji katika kitalu hicho.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...