Thursday, April 16, 2026

SERIKALI YAJIPANGA KUZIFANYIA UKARABATI SHULE ZOTE KONGWE NCHINI - PROF. SHEMDOE



Na OWM – TAMISEMI, Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI, Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amesema Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI imeandaa andiko la mradi unaoitwa SIFA yaani (School Infrastructure Facelifting Programme) na kuliwasilisha Wizara ya Mipango, ili kuwezesha upatikanaji wa fedha za kufanyia ukarabati wa shule zote kongwe za awali, msingi na sekondari nchini.

Prof. Shemdoe amesema hayo Aprili 15, 2026 wakati akijibu hoja za Waheshimiwa Wabunge walizoziwasilisha wakati wa kujadili Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka 2026/27.

“Namshukuru Mheshimiwa Prof. Kitila Mkumbo na timu yake ya Wizara ya Mipango kwa kulipokea andiko tulilowasilisha ili tupate fedha za kutekeleza mradi wa ukarabati wa shule kongwe nchi nzima,” amesema Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe amefafanua kuwa, tathmini iliyofanyika imebaini ukarabati unahitajika kwenye shule za msingi ikihusisha vyumba vya madarasa ni 42,716 na nyumba za walimu 31,813 na kwa upande wa shule za sekondari inajumuisha vyumba vya madarasa 6,889, nyumba za walimu 3,518, maktaba 91 na mabweni 309. 

Prof. Shemdoe ameanisha kuwa, Serikali imekuwa ikitoa fedha kwa ajili ya kufanya ukarabati kwa awamu ambapo kati ya mwaka 2021/22 hadi 2025/26, Serikali imetumia shilingi bilioni 237.9 kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa miundombinu mipya ya shule za msingi na Sekondari kongwe na chakavu nchini.





Wednesday, April 15, 2026

WAZIRI SANGU: RAIS SAMIA AWEZESHA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII KUWA HIMILIVU

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu akitoa ufafanuzi kwa Waheshimiwa Wabunge, wakati akichangia mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Taasisi zake na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2026/2027 katika Bunge la 13, Mkutano wa Tatu, kikao cha Tisa leo Aprili 15, 2026 Jijini Dodoma.

************

Na: OWM (KAM) – Bungeni, Dodoma

Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa kuchukua hatua madhubuti katika kuimarisha Mifuko ya Hifadhi ya Jamii nchini kwa lengo la kuhakikisha ustawi wa wananchi, pamoja na kuhakikisha utoaji wa pensheni kwa wakati.

Pongezi hizo zimetolewa Bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mheshimiwa Deus Clement Sangu, leo Aprili 15, 2026 wakati akichangia mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Taasisi zake na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2026/2027.

Aidha, Mhe. Sangu amesema thamani ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii imeendelea kuongezeka ikiwemo Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) thamani yake imeongezeka kutoka Shilingi Trilioni 4.36 hadi Shilingi Trilioni 10.3. Mfuko wa PSSSF thamani yake iliongezeka kutoka Shilingi Trilioni 5.74 hadi Shilingi Trilioni 12.96.

Waziri Sangu amefafanua kuwa deni la Serikali katika mfuko wa PSSSF ilikuwa Trilioni 4.46, mwaka 2022/2023 Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alitoa hati fungani ya shilingi trilioni 2.17 kwa ajili ya kuulipa mfuko wa PSSSF deni lililodumu kwa muda mrefu la shilingi trilioni 4.6 la michango kabla ya 1999. Pia, Serikali imeendelea kulipa Trilioni 2.09 ambayo imesaidia thamani ya Serikali kulipa mfuko huo wa PSSSF kufikia asilimia 95.

Vilevile, Mhe. Sangu amesema kuwa kutokana na mifuko ya hifadhi ya jamii kuwa himilivu imepelekea kwa sasa watumishi wa umma wanaostafu wanalipwa mafao yao ndani ya siku ishirini na tano huku kiwango cha kima cha chini cha pesheni kuongezeka toka shilingi 100,000 hadi kufikia shilingi 250,000 kwa wastaafu.

Kadhalika, Waziri Sangu amesema Mifuko ya hifadhi ya jamii imeendelea kuwekeza katika miradi yenye tija kwa lengo la kuongeza thamani ya michango ya wanachama na kukuza uchumi pamoja na kuongeza ajira kwa wananchi.

Akihitimisha mchango wake, Mheshimiwa Sangu aliwahakikishia wabunge kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano itaendelea kusimamia utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2026/2027 kwa ufanisi, ili kuleta manufaa kwa Watanzania katika sekta zote za kiuchumi na kijamii.

Kwa upande wake, Spika wa Bunge, Mheshimiwa Mussa Azan Zungu, amewapongeza wabunge kwa kupitisha bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu na kusisitiza umuhimu wa wizara na taasisi husika kusimamia utekelezaji wake ili kuchochea maendeleo ya wananchi.

KAMATI YA FUM KISHAPU YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO YENTE THAMANI YA TSH. BILION 1.2

Na Sumai Salum- Kishapu

Katika jitihada za kuhakikisha fedha za umma zinaleta matokeo chanya kwa wananchi, Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga imefanya ziara maalum ya kukagua miradi 7 ya maendeleo yenye thamani ya shilingi Bilioni 1, 278,000,000.

Ziara hiyo imefanyika Aprili 15 hadi 16, 2026, ikiongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Mhe. Enock Reuben, ambapo wajumbe wa kamati walitembelea na kujionea hali halisi ya utekelezaji wa miradi hiyo ya maendeleo katika maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo.


Miradi iliyokaguliwa inagusa moja kwa moja maisha ya wananchi, ikiwemo miradi ya afya, umeme wa jua, ujenzi wa vyumba vya madarasa, matundu ya vyoo kwenye baadhi ya zahanati na maegesho ya magari mnada wa Mhunze, ujenzi wa nyumba mpya ya Mkurugenzi Mtendaji, ujenzi wa vichomea taka katika zahanati, pamoja na maendeleo ya kikundi cha Vijana na Wanawake waliopewa mikopo ya asilimia 10 wa Halmashauri hiyo.


Kwa mujibu wa kamati hiyo, lengo kuu la ziara lilikuwa ni kufuatilia kwa karibu matumizi ya fedha za miradi, kutathmini hatua za utekelezaji, pamoja na kubaini changamoto zinazoweza kukwamisha ukamilishaji wa miradi hiyo.


Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, Mhe. Reuben amesisitiza umuhimu wa kuhakikisha kila shilingi ya umma inaleta thamani halisi kwa wananchi (value for money), huku akiwataka watendaji kusimamia miradi kwa weledi na uwajibikaji mkubwa.


Kamati haikuishia kukagua tu, bali pia ilitoa maelekezo na ushauri muhimu kwa watendaji. Miongoni mwa mambo yaliyosisitizwa ni, usimamizi makini wa fedha za miradi, uzingatiaji wa viwango vya ubora wa ujenzi, kukamilika kwa miradi ndani ya muda uliopangwa pamoja na utatuzi wa changamoto kwa wakati.


Hatua hizi zinalenga kuhakikisha miradi hiyo inaleta manufaa yaliyokusudiwa kwa wananchi bila kuchelewa wala kupoteza rasilimali.


Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango ina nafasi muhimu katika kusukuma maendeleo ya wilaya. Kupitia ziara kama hizi, kamati inaendelea kuhakikisha uwajibikaji unaimarika, fedha zinatumika ipasavyo, na miradi inatekelezwa kwa ufanisi.


Kwa ujumla, ziara hii ni ishara ya dhamira ya dhati ya viongozi wa Kishapu katika kusimamia maendeleo na kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora zinazotokana na miradi hiyo.Makamo mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga na Diwani wa Kata ya Masanga Mhe. Enock Reuben akisikiliza maelezo kwenye ziara ya kamati ya Fedha Utawala na Mipango iliyofanyika Aprili 14-15, 2026 ya ukaguzi wa miradi 7 ya  maendeleo yenye thamani ya Tsh. bilioni 1.2Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga Emmanuel Johnson akiielezea jambo kamati ya Fedha Utawala na Mipango wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi 8 ya maendeleo yenye thamani ya Tsh. bilioni 1.2  Aprili 14-15, 2026 Diwani wa Kata ya Mwamalasa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga  Mhe. Bushi Mpina ambaye pia ni Mjumbe wa kamati ya Fedha, Utawala na Mipango wa Halmashauri ya wilaya hiyoDiwani wa viti maalumu Kata ya Ukenyenge Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga  Mhe. Sophia Masele ambaye pia ni Mjumbe wa kamati ya Fedha, Utawala na Mipango wa Halmashauri ya wilaya hiyoDiwani wa Kata ya Songwa wilayani Kishapu mkoani Shinyanga Mhe. Abdul Ngoromole ambaye pia ni Mjumbe wa kamati ya Fedha, Utawala na Mipango wa Halmashauri ya wilaya hiyoDiwani wa Kata ya Kishapu Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga  Mhe. Joel Ndettoson ambaye pia ni Mjumbe wa kamati ya Fedha, Utawala na Mipango wa Halmashauri ya wilaya hiyoPicha za Miradi

                     Tazama picha za matukio mbalimbali













  




























Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...