Tanzania Daily Eye
Sunday, May 17, 2026
HISTORIA NA MAFANIKIO YA TANZANIA PRISONS SC YAWEKWA WAZI KWA MASHABIKI, JIJINI DODOMA
Saturday, May 16, 2026
WADAU WA SIASA WATAKA MARIDHIANO KUNUSURU NCHI
Mwalimu ametoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam wakati wa mjadala wa kitaifa kuhusu hatima ya nchi ulioandaliwa na Chama cha ACT Wazalendo.
.Mwalimu alieleza kuwa kila mtu anajua kilichotokea siku hiyo ya uchaguzi, ikiwemo mauaji na uwepo wa changamoto kubwa ya ajira kwa vijana, lakini akasisitiza kuwa kikwazo kikubwa kwa sasa imekuwa ni wanasiasa kushindana maneno majukwaani na kuonyesha umahiri wa kusema badala ya kugusa kiini cha tatizo na kutoa majawabu ya kuivusha nchi.
Kutokana na hali hiyo, Salum Mwalimu alimpongeza Mwenyekiti wa ACT Wazalendo, Othman Masoud Othman, kwa kuitisha mjadala huo na kumtaka asione aibu kusimamia jawabu aliloliwasilisha kupitia kijitabu chake kilichosisitiza haja ya kuanzisha jukwaa la majadiliano ya kitaifa yatakayoongozwa na misingi ya ukweli, haki na uwajibikaji.
Mwalimu alimshauri Othman kuchukua uongozi na kuunda kamati itakayojumuisha watu mbalimbali ili kuanzisha jukwaa hilo, si kama mwenyekiti wa chama bali kama kiongozi mwandamizi wa kisiasa atakayeungwa mkono na vyama vingine, kwa lengo la kupata ukweli na kuweka mifumo ya jinsi viongozi wa kisiasa wanavyopaswa kuwajibika.
Kwa upande wake, mwandishi na mchambuzi wa masuala ya siasa, Ezekiel Kamwaga, alisema kuwa nchi inahitaji utashi wa kisiasa kabla ya kuanza kuzungumza ukweli, huku akionya kuwa viongozi wengi wa sasa wanaonekana kuwa wepesi kukimbilia mitandao ya kijamii badala ya kuonyesha uongozi thabiti.
Kamwaga alifafanua kuwa kiongozi mzuri ni yule anayesimama mbele na kuwa tayari kupokea lawama au kuzomewa, lakini anakaa nyuma wakati wa kupokea sifa, sifa ambayo kwa sasa inaonekana kupotea miongoni mwa viongozi.
Naye mwanasiasa Odero Odero aliwataka viongozi wa upinzani kuacha kulia na badala yake watafute suluhu ya kweli kwa kukabiliana na Rais Samia Suluhu Hassan kwenye meza ya mazungumzo.
Odero aliwashauri viongozi hao akiwemo Othman Masoud, Zitto Kabwe, na John Heche kuondoa tabia ya kuogopana na kujificha kwani Rais Samia ni kama dada na mama yao, na njia pekee ya kuifikisha nchi mbali ni kukaa naye meza moja ili kieleweke.
Suala hili la maridhiano ni sehemu ya falsafa ya uongozi ya Rais Samia kupitia '4R' zake ambazo ni Maridhiano, Ustahmilivu, Mabadiliko na Kujenga upya, ambapo hivi karibuni aliahidi kuunda kamati ya maridhiano baada ya kupokea ripoti ya Tume ya Kuchunguza Matukio Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.
SWICA YAIBUA MATOKEO CHANYA KISESA
Friday, May 15, 2026
WANAWAKE WAPEWA ELIMU YA MLIPA KODI ILI KUICHANGAMKIA FURSA
NA REBECCA DUWE TANGA
Wadau wa maendeleo wameombwa kushirikiana na Mamlaka ya mapato Tanzania TRA mkoa wa Tanga kutoa elimu kwa makundi ya wanawake ili waweze kuzikia fursa mbalimbali na hatimaye waweze kulipa kodi kwa maendeleo ya nchi.
Meneja wa Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Tanga CPA Castro John ametoa kauli hiyo leo may 14, 2026 alipokuwa akifungua jukwaa la wanawake na kodi lililoandaliwa na Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Tanga na kufadhiliwa na shirika la GIZ lenye kauli mbiu isemayo "Wanawake na kodi nguzo ya maendeleo ya Taifa"
"Kwa wadau wetu wa taasisi za kifedha tunaomba muendelee kushirikiana nasi katika kuwawezesha wanawake ili kukuza biashara zao kwa misingi ya sheria na kodi" Amesema Meneja Castro
Katika hatua nyingine Castro alisema Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA Mkoa wa Tanga, ina jukumu la kutoa Elimu ya mlipakodi pamoja na fursa mbalimbali zinazowazunguka Wanawake Wafanyabiashara na Wajasiriamali ili kumuwawezesha kutanua uelewa juu ya mifumo na Sheria za Kodi Nchini.
"TRA inatambua mchango wa Wanawake katika ulipaji wa Kodi na kwasasa Wanawake wamekuwa mstari wa mbele katika ulipaji wa Kodi Nchini,hivyo naomba muendelee kuwa mstari wa mbele katika ulipaji wa Kodi ili tulijenge Taifa letu"Aliongeza Castro
Castro aliwataka Wanawake kuendelea kudumisha nidhamu ya ulipaji wa Kodi Nchini nakwamba Mamlaka hiyo ipo tayari wakati wowote kutoa msaada kwa mfanyabiashara anayepitia changamoto yoyote,
"Niwaombe muendelee kudumisha nidhamu ya ulipaji wa Kodi mliyonayo ili tuondoe usumbufu wowote unaoweza kujitokeza endapo mtu atakwepa kulipa Kodi,TRA ipo tayari wakati wowote kutoa msaada kwa mfanyabiashara anayepitia changamoto yoyote, niwaombe ukiwa na changamoto yoyote tuambie tukusaidia usikae nayo alafu baadae unakuja kulalamika" Alisisitiza Castro
Kwaupande wake,Naibu Katibu wa Jumuiya ya Nchini Wafanyabiashara, Ismail Masoud aliwataka watumishi wa TRA kuwasaidia kutoa Elimu Wafanyabiashara mkoani Tanga ili kuondoa kasoro nyingi zinazowakabili Wafanyabiashara,
"Niwaombe TRA iendelee kutoa Elimu ya mlipakodi ili changamoto za Wafanyabiashara hususani zinazotokana na Elimu ziishe, lakini pia kwasisi Wafanyabiashara,tuache janja janja zakukwepa Kodi, tunataka twende pamoja ili tuweze kufanikisha dira ya Taifa 2050" Alisisitiza Masoud.
Kwa upande wake Afisa maendeleo mkoa wa Tanga Charles Mtali amesema wanawake wana mchango mkubwa wa maendeleo ya kiuchumi .
tofauti na wanaume hivyo wasipowezeshwa itakuwa ni vigumu nchi kufikia malengo yake.
MRADI WA BARRICK-TWIGA FUTURE FORWARD EDUCATION KUBORESHA SEKTA YA ELIMU NYANG’HWALE
Wednesday, May 13, 2026
DC NDILE AWATAKA VIJANA SONGEA KUDUMISHA UZALENDO NA KULINDA AMANI
Daktari wa mifugo Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma Dkt Seria Masole akizungumzia umuhimu wa kujiajiri badala ya kusubiri qjira katika kongamano la vijana leo ukumbi wa Manispaa ya Songea
AFCON 2027: JKCI NA ALMC WAANZA MAANDALIZI YA HUDUMA ZA DHARURA
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...














































