Wednesday, February 18, 2026

WAANDISHI WA HABARI GEITA WAPEWA MBINU ZA KUTHIBITISHA NA KUHAKIKI TAARIFA; UTPC YAHAMASISHA UANDISHI WA HABARI ZENYE TIJA


Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya
akizungumza wakati kifungua mafunzo maalum kuhusu Uthibitishaji na Uhakiki wa taarifa kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita.
Mwezeshaji wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News), Misinformation na Disinformation, Kadama Malunde – Mkurugenzi wa Malunde 1 Blog akifundisha mbinu za uthibitishaji wa taarifa (fact-checking), matumizi ya Akili Unde (AI) katika kuhakiki habari, pamoja na namna ya kutambua asili ya picha na video.
Afisa kutoka JamiiAfrica, Innocent Mangu, akizungumza wakati wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News), Misinformation na Disinformation, akisema JamiiAfrica inaamini kuwa bila taarifa sahihi hakuna maamuzi sahihi, ndiyo maana wanashirikiana na Ubalozi wa Uholanzi pamoja na UTPC kuhakikisha waandishi wa habari wanapatiwa mbinu bora za kuhakiki taarifa na kukabiliana na propaganda.
Picha ya kumbukumbu washiriki wa mafunzo


Na Mwandishi wetu - Geita

Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya, amesema waandishi wa habari wana wajibu mkubwa wa kuhakikisha jamii inapata taarifa sahihi badala ya taarifa potofu, akisisitiza kuwa mapambano dhidi ya upotoshaji wa habari yanahitaji weledi, maadili na matumizi sahihi ya teknolojia.

Akifungua mafunzo maalum kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita kuhusu Uthibitishaji na Uhakiki wa Taarifa yaliyofanyika Jumatano, Februari 18, 2026 mjini Geita, Simbaya amesema katika dunia ya sasa yenye wingi wa taarifa, ni rahisi kwa jamii kupotoshwa iwapo waandishi hawatakuwa makini katika uchambuzi na uthibitishaji wa habari.

"Wananchi wanahitaji taarifa sahihi zitakazowasaidia kufanya maamuzi sahihi. Jukumu la mwandishi ni kuhakikisha jamii inapata ukweli. Ndiyo maana tumeona umuhimu wa kuandaa mafunzo haya. Nendeni mkatumie elimu hii kwa vitendo. Tunataka muandike habari zenye uwezo wa kubadili jamii na kujenga taifa," amesema Simbaya.

Ameongeza kuwa UTPC inataka kuona waandishi wakiendelea kushikilia misingi ya maadili ya taaluma yao na kuandika habari zenye tija zisizopotosha umma.

Lengo kuu ni kuwajengea waandishi uwezo wa kukabiliana na changamoto za fake news, misinformation na disinformation ambazo zimekuwa tishio kubwa duniani.

Washiriki wamepatiwa mbinu mbalimbali za uthibitishaji wa habari, ikiwemo matumizi ya Akili Unde (Artificial Intelligence – AI), kugundua asili ya picha na video, kulinganisha taarifa na vyanzo vinavyoaminika, pamoja na kusoma zaidi ya vichwa vya habari ili kuepuka kupotoshwa.

Mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa "Ukweli Kwanza" unaolenga kuongeza weledi wa waandishi wa habari na kuimarisha uwezo wa wananchi kupambana na upotoshaji wa taarifa. Kupitia mradi huo, waandishi wanafundishwa mbinu za fact-checking, matumizi sahihi ya teknolojia na namna ya kutambua na kukabiliana na misinformation na disinformation.

Aidha, mradi huo unalenga kuwawezesha waandishi chipukizi, hususan wanawake, kuwa mstari wa mbele katika kulinda ukweli na kuimarisha uaminifu wa vyombo vya habari nchini.

Kupitia mafunzo haya, UTPC na wadau wake wanaamini kuwa waandishi wa habari wataendelea kuwa nguzo muhimu ya ukweli, uwazi na uwajibikaji katika jamii.

Mafunzo hayo yameandaliwa na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) chini ya ufadhili wa Ubalozi wa Uholanzi. 

UTPC pia imeshirikiana na taasisi ya JamiiAfrica katika kupata wataalamu wanaoweza kutoa mafunzo haya kwa weledi.
Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya
akizungumza wakati wa mafunzo maalum kuhusu Uthibitishaji na Uhakiki wa taarifa kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita.
Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya
akizungumza wakati wa mafunzo maalum kuhusu Uthibitishaji na Uhakiki wa taarifa kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita.
Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya
akizungumza wakati wa mafunzo maalum kuhusu Uthibitishaji na Uhakiki wa taarifa kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita.
Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya
akizungumza wakati wa mafunzo maalum kuhusu Uthibitishaji na Uhakiki wa taarifa kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita.
Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya
akizungumza wakati wa mafunzo maalum kuhusu Uthibitishaji na Uhakiki wa taarifa kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita.
Mwezeshaji wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News), Misinformation na Disinformation, Kadama Malunde – Mkurugenzi wa Malunde 1 Blog akifundisha mbinu za uthibitishaji wa taarifa (fact-checking), matumizi ya Akili Unde (AI) katika kuhakiki habari, pamoja na namna ya kutambua asili ya picha na video.
Mwezeshaji wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News), Misinformation na Disinformation, Kadama Malunde – Mkurugenzi wa Malunde 1 Blog akifundisha mbinu za uthibitishaji wa taarifa (fact-checking), matumizi ya Akili Unde (AI) katika kuhakiki habari, pamoja na namna ya kutambua asili ya picha na video.
Mwezeshaji wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News), Misinformation na Disinformation, Kadama Malunde – Mkurugenzi wa Malunde 1 Blog akifundisha mbinu za uthibitishaji wa taarifa (fact-checking), matumizi ya Akili Unde (AI) katika kuhakiki habari, pamoja na namna ya kutambua asili ya picha na video.
Mwezeshaji wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News), Misinformation na Disinformation, Kadama Malunde – Mkurugenzi wa Malunde 1 Blog akifundisha mbinu za uthibitishaji wa taarifa (fact-checking), matumizi ya Akili Unde (AI) katika kuhakiki habari, pamoja na namna ya kutambua asili ya picha na video.

Afisa kutoka JamiiAfrica, Innocent Mangu, akifundisha mbinu za uthibitishaji na uhakiki wa taarifa wakati wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News) kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita
Afisa kutoka JamiiAfrica, Innocent Mangu, akifundisha mbinu za uthibitishaji na uhakiki wa taarifa wakati wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News) kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita
Afisa kutoka JamiiAfrica, Innocent Mangu, akifundisha mbinu za uthibitishaji na uhakiki wa taarifa wakati wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News) kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita
Afisa kutoka JamiiAfrica, Innocent Mangu, akifundisha mbinu za uthibitishaji na uhakiki wa taarifa wakati wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News) kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita



Monday, February 16, 2026

Picha : SHANGWE ZATAWALA KIKUNDI CHA 'BETTER TOGETHER' KIKIZINDULIWA KWA KISHINDO, DC MTATIRO ATAKA MSHIKAMANO ZAIDI


 Mwenyekiti wa Kikundi cha Better Together Mussa Ngangala akikata keki wakati wa uzinduzi rasmi wa Kikundi cha Better Together katika Ukumbi wa CCM Mkoa wa Shinyanga

Na Mwandishi wetu - Malunde 1 blog

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Julius Mtatiro, ameongoza uzinduzi rasmi wa Kikundi cha Better Together katika hafla iliyogubikwa na shamrashamra, nderemo na vifijo vya wanachama waliojaa matumaini na mshikamano huku akikipongeza kikundi hicho kwa maono yake ya kuimarisha umoja, ustawi wa kijamii na kukuza maendeleo ya kiuchumi miongoni mwa wanachama wake.

Uzinduzi huo ulifanyika tarehe Februari 14, 2026 ulitanguliwa na shughuli za kijamii na kiafya zikiwemo mbio za amani (jogging) zilizoanzia Ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga na kuhitimishwa katika Uwanja wa CCM Kambarage, sambamba na mazoezi ya viungo (aerobic na cardio). 

Wanachama pia walitembelea Kituo cha Afya Kambarage na kutoa matendo ya huruma kwa wagonjwa na wahitaji, kabla ya kuhitimisha siku hiyo kwa sherehe rasmi ya uzinduzi jioni katika ukumbi wa CCM Mkoa wa Shinyanga.
Akizungumza wakati wa uzinduzi, Mtatiro alisema kuwa vikundi vya kijamii kama Better Together vina mchango mkubwa katika kuimarisha mtaji wa kijamii, kusaidiana wakati wa changamoto na kujenga utamaduni wa uwajibikaji.

"Nawapongeza sana waanzilishi na wanachama wa Better Together kwa maono yenu. Kuanzisha na kuendesha kikundi chenye wanachama zaidi ya 400 ndani ya muda mfupi ni ishara ya uongozi makini na imani ya watu. Serikali inaamini katika nguvu ya umoja wa wananchi. Endeleeni kushikamana, kudumisha nidhamu ya fedha na uwazi ili kikundi chenu kiwe mfano bora wa kuigwa," alisema Mtatiro.
Aliongeza kuwa, vikundi vinapojengwa katika misingi ya uaminifu, husaidia kupunguza mzigo wa kijamii kwa familia na kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika ngazi ya chini.

Mwenyekiti wa Kikundi cha Better Together, Mussa Jonas Ngangala, alisema uzinduzi huo ni hatua muhimu katika safari ya kuimarisha taasisi yao na kuongeza wigo wa huduma kwa wanachama.

"Tulianza kama wazo la kuinuana katika changamoto za maisha, lakini leo tumekuwa familia kubwa yenye wanachama zaidi ya 400. Dhamira yetu ni kujenga mfumo imara wa kusaidiana kijamii na kiuchumi, kuhakikisha kila mwanachama anahisi kuthaminiwa na kulindwa katika nyakati za shida na furaha," alisema Ngangala.

Alibainisha kuwa kikundi kitaendelea kuandaa programu za kijamii, kuhamasisha utunzaji wa afya, pamoja na kuendeleza utamaduni wa kuchangia na kusaidiana kwa uwazi na uwajibikaji.
Better Together ni muunganiko wa wanachama zaidi ya 400, wengi wao wakiishi Mkoa wa Shinyanga huku wengine wakitoka nje ya mkoa huo. Kikundi hicho kilianzishwa mwezi Oktoba 2025 kwa lengo la kusaidiana katika nyakati za shida na raha, pamoja na kufanya matendo ya huruma katika jamii.

Katika hafla hiyo, wanachama pia walifanya harambee ya kuchangia mfuko wa kikundi ili kuimarisha uwezo wake wa kutekeleza majukumu kwa ufanisi zaidi mwaka 2026.

Uzinduzi wa Better Together umeweka msingi wa kuendelea kujenga mshikamano, kuimarisha mtandao wa kijamii na kukuza ustawi wa wanachama wake, huku ukiwa mfano wa namna vikundi vya kijamii vinavyoweza kuwa chachu ya maendeleo katika jamii.
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Julius Mtatiro akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa Kikundi cha Better Together katika Ukumbi wa CCM Mkoa wa Shinyanga
 Mwenyekiti wa Kikundi cha Better Together Mussa Ngangala akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa Kikundi cha Better Together katika Ukumbi wa CCM Mkoa wa Shinyanga
 Mwenyekiti wa Kikundi cha Better Together Mussa Ngangala (kulia) akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Julius Mtatiro wakati wa uzinduzi rasmi wa Kikundi cha Better Together katika Ukumbi wa CCM Mkoa wa Shinyanga
 Mwenyekiti wa Kikundi cha Better Together Mussa Ngangala (kulia) akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Julius Mtatiro wakati wa uzinduzi rasmi wa Kikundi cha Better Together katika Ukumbi wa CCM Mkoa wa Shinyanga



























































































































Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...