Monday, March 9, 2026

DKT. GWAJIMA AWAHIMIZA WANANCHI KUUPOKEA NA KUULINDA MRADI WA PAMOJA KWA USTAWI WA KIUCHUMI



Na Mwandishi wetu, GEITA

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima, amewataka wananchi waliopo katika Halmashauri 40 zilizopo katika Mikoa 10 ya Arusha, Mwanza, Kagera, Mara, Singida, Shinyanga, Geita, Rukwa,Tabora na Simiyu waupokee na kuulinda Mradi wa Kukuza Usawa wa Kijinsia Tanzania (PAMOJA) ili kuwanufaisha wanawake kiuchumi pamoja na kuzuia na kukabiliana na ukatili wa kijinsia (GBV).

Dkt. Gwajima ametoa wito huo  Machi 08, 2026 Mkoani Geita kwa wananchi wa mikoa hiyo 10 na Halmashauri zake 40 ambazo zinatekeleza mradi huo wa PAMOJA, mara baada ya kuuzindua rasmi mradi  wakati wa kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani.

"Mradi huu wa PAMOJA wa miaka mitano (5), wananchi na waratibu  mkiupokea,  kuutekeleza na kuulinda ipasavyo, utakuwa ni nyenzo muhimu ya kuwawezesha wanawake kiuchumi pamoja na kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia nchini," amesisitiza Dkt. Gwajima.

Aidha, Waziri Gwajima amemuelekeza Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. John Jingu, kuhakikisha Sekretarieti ya Uratibu wa Mradi wa PAMOJA inaendelea kutimiza wajibu wake kwa weledi na ufanisi ili fursa za mradi ziwafikie na kuwanufaisha walengwa na kumtaka atoe taarifa za mradi kwa umma ili waujue kwani ni mradi uliowalenga wananchi.

Dkt. Gwajima amesema katika kuendeleza azma ya kuwawezesha wanawake kiuchumi, Serikali ya Awamu ya Sita ikiongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inashirikiana na Mdau wa Maendeleo Benki ya Dunia ambayo imetoa mkopo wa  Dola za Marekani Milioni 100 na Ruzuku ya Dola za Kimarekani  Millioni nne (4) sawa na Shilingi Bilioni 262 ili kuwezesha utekelezaji wa mradi huo nchini. 

Mradi huo wa PAMOJA uliozinduliwa na Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima unatekelezwa na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kwa kushirikiana Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI  pamoja na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto - Zanzibar ambapo utekelezaji wake ulianza rasmi 30 Aprili, 2025 na utafikia tamati Februari 28, 2029.






Saturday, February 28, 2026

AGIZO LA RC MANYARA KUHUSU TAA, LAANZA KUTEKELEZWA BABATI.



Na John Walter-Manyara

Hatimaye kazi ya ukarabati wa taa za barabarani zilizokuwa haziwaki katika Mji wa Babati imeanza kutekelezwa kufuatia agizo la Mkuu wa Mkoa wa Manyara Region kwa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA).

Kwa muda mrefu baadhi ya wakazi wa Babati walilalamikia tatizo la taa za barabarani kuzimika hali iliyokuwa ikisababisha hofu ya usalama nyakati za usiku.

Kufuatia malalamiko hayo, Mkuu wa Mkoa kupitia kikao cha bodi ya Barabara mkoa kilichofanyika hivi karibuni, aliiagiza TARURA kuhakikisha taa zote zilizokuwa haziwaki zinarejeshwa katika hali ya kufanya kazi haraka iwezekanavyo.

Kupitia jukwaa la mitandao la Manyara Mpya, Mkuu huyo wa Mkoa amethibitisha kuanza kwa utekelezaji wa agizo hilo kwa kuchapisha picha zinazoonesha mafundi wakiendelea na kazi ya matengenezo ya miundombinu ya taa hizo.

Akiandika katika ujumbe wake, amesema:

"Ndugu viongozi mliopo mitaani huko Naimani mnaona kazi inaendelea, taa zilizozima ni nyingi na kazi yote itakamilika, tuwe na subra tu. Nawashukuru kwa uvumilivu.
Naimani kwenye hili kikombe kimeniepuka
🙇🏽‍♀️
Nawapenda sana
❤️"

Kauli hiyo imepokelewa kwa hisia chanya na wananchi wengi, wakionesha matumaini kuwa kukamilika kwa kazi hiyo kutaimarisha usalama, kuongeza mwanga katika maeneo ya biashara pamoja na kurahisisha shughuli za kijamii nyakati za usiku.

Utekelezaji huo unaonekana kuwa sehemu ya juhudi za uongozi wa mkoa katika kusimamia na kuboresha miundombinu ya huduma za kijamii ndani ya Manispaa ya Babati.

 

Thursday, February 19, 2026

Halmashauri ya Wilaya ya Babati yapitisha bajeti ya bilioni 71 kwa miaka 2026–2030


Na John walter-Babati

Baraza la madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Babati limepitisha mapendekezo ya bajeti ya shilingi bilioni 71 kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2026 hadi 2030, ikiwa ni sehemu ya mipango ya kuimarisha utoaji wa huduma na utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa wananchi.

Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, John Noya, amesema bajeti hiyo inahitaji usimamizi madhubuti na utekelezaji mzuri wa ukusanyaji wa mapato ili iweze kuleta matokeo yaliyokusudiwa.

"Tusiposimamia vyema mapato yetu, bajeti haitafanya kazi kama ilivyopangwa lakini tukisimamia kwa umakini, itawezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa ufanisi," amesema Noya.

Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Anna Mbogo amesema kuwa baada ya bajeti hiyo kupitishwa na Bunge, baraza la madiwani kwa kushirikiana na wataalamu wa halmashauri litatoa ushirikiano mkubwa katika hatua za utekelezaji ili kuhakikisha malengo yaliyowekwa yanafikiwa.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Babati, Emmanuela Kaganda, amesisitiza umuhimu wa kuwepo kwa uwiano wa miradi ya maendeleo katika kata zote, akibainisha kuwa wananchi wote wanastahili kunufaika kwa usawa.

Naye Naibu Waziri wa Utumishi na Utawala Bora, Regina Ndege Qwaray, amesema Serikali chini ya uongozi wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, tayari imeanza utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2025–2030, hivyo amezitaka halmashauri kuhakikisha mipango yao inaendana na Dira ya Maendeleo ya Taifa ya mwaka 2025–2050.

Amesisitiza kuwa upangaji na utekelezaji wa bajeti za halmashauri unapaswa kulenga maendeleo endelevu yatakayoboresha maisha ya wananchi kwa muda mrefu.

 

 

Wednesday, February 18, 2026

WAANDISHI WA HABARI GEITA WAPEWA MBINU ZA KUTHIBITISHA NA KUHAKIKI TAARIFA; UTPC YAHAMASISHA UANDISHI WA HABARI ZENYE TIJA


Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya
akizungumza wakati kifungua mafunzo maalum kuhusu Uthibitishaji na Uhakiki wa taarifa kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita.
Mwezeshaji wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News), Misinformation na Disinformation, Kadama Malunde – Mkurugenzi wa Malunde 1 Blog akifundisha mbinu za uthibitishaji wa taarifa (fact-checking), matumizi ya Akili Unde (AI) katika kuhakiki habari, pamoja na namna ya kutambua asili ya picha na video.
Afisa kutoka JamiiAfrica, Innocent Mangu, akizungumza wakati wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News), Misinformation na Disinformation, akisema JamiiAfrica inaamini kuwa bila taarifa sahihi hakuna maamuzi sahihi, ndiyo maana wanashirikiana na Ubalozi wa Uholanzi pamoja na UTPC kuhakikisha waandishi wa habari wanapatiwa mbinu bora za kuhakiki taarifa na kukabiliana na propaganda.
Picha ya kumbukumbu washiriki wa mafunzo


Na Mwandishi wetu - Geita

Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya, amesema waandishi wa habari wana wajibu mkubwa wa kuhakikisha jamii inapata taarifa sahihi badala ya taarifa potofu, akisisitiza kuwa mapambano dhidi ya upotoshaji wa habari yanahitaji weledi, maadili na matumizi sahihi ya teknolojia.

Akifungua mafunzo maalum kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita kuhusu Uthibitishaji na Uhakiki wa Taarifa yaliyofanyika Jumatano, Februari 18, 2026 mjini Geita, Simbaya amesema katika dunia ya sasa yenye wingi wa taarifa, ni rahisi kwa jamii kupotoshwa iwapo waandishi hawatakuwa makini katika uchambuzi na uthibitishaji wa habari.

"Wananchi wanahitaji taarifa sahihi zitakazowasaidia kufanya maamuzi sahihi. Jukumu la mwandishi ni kuhakikisha jamii inapata ukweli. Ndiyo maana tumeona umuhimu wa kuandaa mafunzo haya. Nendeni mkatumie elimu hii kwa vitendo. Tunataka muandike habari zenye uwezo wa kubadili jamii na kujenga taifa," amesema Simbaya.

Ameongeza kuwa UTPC inataka kuona waandishi wakiendelea kushikilia misingi ya maadili ya taaluma yao na kuandika habari zenye tija zisizopotosha umma.

Lengo kuu ni kuwajengea waandishi uwezo wa kukabiliana na changamoto za fake news, misinformation na disinformation ambazo zimekuwa tishio kubwa duniani.

Washiriki wamepatiwa mbinu mbalimbali za uthibitishaji wa habari, ikiwemo matumizi ya Akili Unde (Artificial Intelligence – AI), kugundua asili ya picha na video, kulinganisha taarifa na vyanzo vinavyoaminika, pamoja na kusoma zaidi ya vichwa vya habari ili kuepuka kupotoshwa.

Mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa "Ukweli Kwanza" unaolenga kuongeza weledi wa waandishi wa habari na kuimarisha uwezo wa wananchi kupambana na upotoshaji wa taarifa. Kupitia mradi huo, waandishi wanafundishwa mbinu za fact-checking, matumizi sahihi ya teknolojia na namna ya kutambua na kukabiliana na misinformation na disinformation.

Aidha, mradi huo unalenga kuwawezesha waandishi chipukizi, hususan wanawake, kuwa mstari wa mbele katika kulinda ukweli na kuimarisha uaminifu wa vyombo vya habari nchini.

Kupitia mafunzo haya, UTPC na wadau wake wanaamini kuwa waandishi wa habari wataendelea kuwa nguzo muhimu ya ukweli, uwazi na uwajibikaji katika jamii.

Mafunzo hayo yameandaliwa na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) chini ya ufadhili wa Ubalozi wa Uholanzi. 

UTPC pia imeshirikiana na taasisi ya JamiiAfrica katika kupata wataalamu wanaoweza kutoa mafunzo haya kwa weledi.
Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya
akizungumza wakati wa mafunzo maalum kuhusu Uthibitishaji na Uhakiki wa taarifa kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita.
Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya
akizungumza wakati wa mafunzo maalum kuhusu Uthibitishaji na Uhakiki wa taarifa kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita.
Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya
akizungumza wakati wa mafunzo maalum kuhusu Uthibitishaji na Uhakiki wa taarifa kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita.
Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya
akizungumza wakati wa mafunzo maalum kuhusu Uthibitishaji na Uhakiki wa taarifa kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita.
Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya
akizungumza wakati wa mafunzo maalum kuhusu Uthibitishaji na Uhakiki wa taarifa kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita.
Mwezeshaji wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News), Misinformation na Disinformation, Kadama Malunde – Mkurugenzi wa Malunde 1 Blog akifundisha mbinu za uthibitishaji wa taarifa (fact-checking), matumizi ya Akili Unde (AI) katika kuhakiki habari, pamoja na namna ya kutambua asili ya picha na video.
Mwezeshaji wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News), Misinformation na Disinformation, Kadama Malunde – Mkurugenzi wa Malunde 1 Blog akifundisha mbinu za uthibitishaji wa taarifa (fact-checking), matumizi ya Akili Unde (AI) katika kuhakiki habari, pamoja na namna ya kutambua asili ya picha na video.
Mwezeshaji wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News), Misinformation na Disinformation, Kadama Malunde – Mkurugenzi wa Malunde 1 Blog akifundisha mbinu za uthibitishaji wa taarifa (fact-checking), matumizi ya Akili Unde (AI) katika kuhakiki habari, pamoja na namna ya kutambua asili ya picha na video.
Mwezeshaji wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News), Misinformation na Disinformation, Kadama Malunde – Mkurugenzi wa Malunde 1 Blog akifundisha mbinu za uthibitishaji wa taarifa (fact-checking), matumizi ya Akili Unde (AI) katika kuhakiki habari, pamoja na namna ya kutambua asili ya picha na video.

Afisa kutoka JamiiAfrica, Innocent Mangu, akifundisha mbinu za uthibitishaji na uhakiki wa taarifa wakati wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News) kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita
Afisa kutoka JamiiAfrica, Innocent Mangu, akifundisha mbinu za uthibitishaji na uhakiki wa taarifa wakati wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News) kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita
Afisa kutoka JamiiAfrica, Innocent Mangu, akifundisha mbinu za uthibitishaji na uhakiki wa taarifa wakati wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News) kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita
Afisa kutoka JamiiAfrica, Innocent Mangu, akifundisha mbinu za uthibitishaji na uhakiki wa taarifa wakati wa Mafunzo ya Kupambana na Habari Potoshi (Fake News) kwa waandishi wa habari Mkoa wa Geita



Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...