Monday, June 22, 2026

TRA YATOA MSAADA KWA WATOTO NJITI HOSPITALI YA RUFAA BOMBO KATIKA MAADHIMISHO YA. MIAKA 30

 


Rebeca Duwe Tanga 


Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imetoa msaada wa vifaa mbalimbali katika Hospitali ya Rufaa ya Bombo mkoani Tanga kwa ajili ya kuwasaidia watoto wenye changamoto mbalimbali, wakiwemo watoto njiti, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 30 ya mamlaka hiyo.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, Naibu Kamishna wa Huduma za Kiufundi kutoka Makao Makuu ya TRA, Ted Silkiluwasha, alisema kuwa katika jamii ya Watanzania kuna watu wenye mahitaji maalum wanaohitaji kusaidiwa, hivyo mamlaka imeona umuhimu wa kuwafikia na kuwasaidia.






Alisema Kamishna Mkuu wa TRA, Yusuph Mwenda, amesisitiza kuwa ukusanyaji wa mapato ndio unaochangia maendeleo na kuimarisha uwepo wa taifa, hivyo ni muhimu kuhakikisha hakuna mwananchi anayeachwa nyuma katika juhudi za maendeleo.

“Sambamba na kuimarisha taifa, hatupendi kumuacha mtu yeyote nyuma. Miaka 30 ya TRA imewezekana kutokana na walipa kodi, na mamlaka inatambua kuwa uhai wa walipa kodi ndio uhai wa TRA. Ndiyo maana tumeamua kutoa msaada huu kwa watoto njiti kama sehemu ya kurudisha kwa jamii inayochangia maendeleo ya taifa kupitia kodi,” alisema Silkiluwasha.

Aliongeza kuwa Julai 1 mwaka huu TRA itatimiza miaka 30 tangu kuanzishwa kwake, ikiwa na kaulimbiu ya “Tanzania kwa Pamoja Tunajenga Taifa Letu.” Alisema mamlaka imeona umuhimu wa kufika Hospitali ya Rufaa ya Bombo kwa kuwa inahudumia watu wenye mahitaji makubwa, ili kuwajulisha kuwa wao ni sehemu muhimu ya jamii.

Kwa upande wake, Meneja wa TRA Mkoa wa Tanga, Castro John, alisema kuwa mamlaka hiyo inaamini kila Mtanzania ni mlipa kodi wa sasa au wa baadaye, hivyo hata watoto waliotembelewa ni walipa kodi wa kesho na pengine watumishi wa baadaye wa TRA.



Alisema mtazamo huo ndio uliowasukuma kushiriki katika shughuli za kijamii na kusaidia makundi yenye mahitaji maalum.

Aidha, alizitaka taasisi nyingine, hususan mkoani Tanga, kujitokeza kusaidia watu wenye uhitaji na kushiriki katika shughuli za kijamii zinazolenga kuwatia moyo na kuboresha maisha yao.

Naye Nuru Hamisi Omari alisema kuwa hospitali hiyo hupokea watoto njiti kutoka maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Tanga. Alieleza kuwa watoto hao hupatiwa huduma mbalimbali ikiwemo kuongeza kiwango cha sukari mwilini na kusaidiwa kupumua kwa kutumia mashine maalum hadi wanapofikia uzito unaoruhusiwa.

Alifafanua kuwa mtoto anaporuhusiwa kwenda nyumbani anatakiwa kuendelea kuhudhuria kliniki maalum ya ufuatiliaji wa ukuaji hadi atakapofikia uzito wa kilo tatu, ndipo huendelea na huduma za kawaida za kliniki.

Kwa upande wake, Muuguzi Kiongozi wa Wodi ya Watoto, Sister Rukia Mbega, ameishukuru TRA kwa kuguswa na mahitaji ya watoto njiti na kutoa msaada utakaosaidia kuboresha huduma kwa watoto hao.

Alisema msaada uliotolewa unajumuisha sabuni, nepi (pampers), dawa na makopo ya maziwa ya unga, vitu ambavyo ni muhimu katika kuwahudumia watoto njiti.


Sunday, June 21, 2026

VIJANA WANAOISHI MAZINGIRA MAGUMU WAJITENGA NA MAANDAMANO YA 7/7





Na mwandishi wetu

Wakati baadhi ya wanaharakati na watumiaji wa mitandao ya Kijamii wakihamasisha maandamano kupitia mitandao ya kijamii kuelekea Julai 7, 2026, vijana wanaoishi katika mazingira magumu ambao walijikuta katikati ya vurugu zilizotokea Oktoba 29, 2025 wameeleza namna walivyobeba mzigo mkubwa wa madhara, wakisema hawatamani kuona hali kama hiyo ikijirudia.

Vijana hao wanasema kipindi hicho kilisababisha kukosekana kwa amani, chakula, sehemu za kulala na shughuli za kujipatia kipato, huku baadhi ya wenzao wakijeruhiwa, kupata ulemavu wa kudumu na wengine kupoteza maisha.

Mmoja wao, Juma Maftah, mkazi wa Ilala Dar Es Salaam amesema siku za vurugu zilikuwa ngumu zaidi kwa watu wanaoishi mitaani kuliko kundi lolote lingine.

“Tarehe 29, 2025 wakati ule kilichotokea ilikuwa changamoto sana kwangu, amani hakuna, kula ilikuwa tabu, sehemu za kulala pia kwa sisi tunaolala nje ilikuwa changamoto sana, wengine walivunjika miguu na ndugu zetu wengine walikufa.

 Ilifika hatua mpaka tukawa tunakamata mbwa mtaani na kuwala kwa siku siku ambazo zilikuwa na ukosefu wa amani kwa sisi tunaoishi katika mazingira magumu. Mimi niombe vijana wenzangu tusikubali hata kidogo kushawishika tukaingia kwenye kufanya vurugu kwani tutaishia jela, kujisababishia ulemavu au kifo. Amani ndio kila kitu kwenye maisha,” alisema.

Kwa upande wake, Baraka Richard amesema wakati wa vurugu hizo hakuweza kufanya shughuli zake za kubeba mizigo sokoni, akiwataka Vijana wengine Nchini kutokubali kushawishiwa na wito wa kushiriki maandamano au vurugu zinazoweza kuhatarisha maisha yao, wakisema uzoefu wao unaonesha kuwa matokeo yake huacha majeraha ya muda mrefu kwa watu wa kawaida.

Ripoti ya Tume ya Uchunguzi iliyoongozwa na Jaji Mkuu mstaafu Mohamed Othman Chande kuhusu matukio ya vurugu yaliyotokea baada ya uchaguzi wa mwaka 2025 ilibainisha kuwa baadhi ya vijana wanaoishi katika mazingira magumu, maeneo ya stendi na masokoni walirubuniwa kushiriki maandamano kwa kuahidiwa fedha pamoja na ajira. 

Ripoti hiyo ilionya kuhusu matumizi ya vijana walio katika mazingira magumu kwa maslahi ya kisiasa, ikisisitiza umuhimu wa kuongeza uelewa na fursa za kiuchumi ili kuwakinga dhidi ya ushawishi unaoweza kuwaingiza kwenye migogoro na vitendo vya vurugu.

TARURA KUENDELEA KUJENGA MADARAJA YA MAWE NCHI NZIMA -SUNGURA



Na Mwandishi wetu, Dodoma

Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) inaendelea na uboreshaji wa miundombinu ya barabara nchini huku serikali ikiwa imetoa takribani ya Dola Milioni 65 kwa ajili ya kurejesha mawasiliano yaliyoharibika kutokana na mvua za El Nino za mwaka 2023/2024.

Akizungumza na Wanahabari Kwenye Maadhimisho ya wiki ya utumishi wa umma mkoani Dodoma Mkuu wa kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma Tarura, Catherine Sungura amesema TARURA wanahudumia barabara za wilaya zenye urefu wa Kilomita 144,429 nchi nzima zikiwemo barabara za lami,mawe,changarawe na udongo.

Tunaendelea kujenga Madaraja nchi nzima katika kuhakikisha jamii inapata huduma za maendeleo kupitia barabara hizo hivyo kufikia sasa tunaMadaraja ya Mawe yapatayo 490 .

" Kutokana na mvua Za mwaka 2023/2024 Tarura tulipokea fedha kutoka benki ya dunia takribani ya dola Milioni 65 kwa ajili ya kurejesha mawasiliano ya barabara ambazo ziliathirika na Mvua za Elnino ambapo kwa sasa tumerudisha Mawasiliano ya barabara hizo kwa asilimia 70 katika Vijiji,Wilaya na Mikoa." Amesema Mkuu wa kitengo Sungura"

Aidha, mameneja wa mikoa hususani mkoa wa tabora wilaya ya sikonge na urambo huduma zimerejea kwa wananchi kama kawaida hivyo tarura tunaendelea kuboresha miradi mbalimbali ukiwemo mradi wa TACTIC katika miji 45 ambapo tunajenga masoko, barabara za lami na Mradi wa DMDp 2 ambao tunajenga takribani kilomita 250 katika wilaya 5 za mkoa wa Dar es Salaam.

Vilevile kwa mkoa wa Dar esalaam tuwatoe hofu Wananchi kuwa wakandarasi wamerejea kukamilisha miundombinu ya barabara hiyo hivyo Mtaa wa majohe kivule kuna kilomita 2 za barabara za zege vilevile kigamboni.

Katika Hatua nyingine tarura tumetoa ajira kwa kikundi cha maafisa usafirishaji (bodaboda) mkoani morogoro wilaya ya ifakara na ambapo wanafanya matengenezo ya kawaida ya miundombinu na hivyo wanaenda kuinuka kiuchumi kupitia miradi wa RISE.

Kwa upande wake afisa utumishi mkuu Speransia Mhapa ameongeza kuwa tarura imefanya mabadiliko mbalimbali kwenye sekta ya miundombinu nchini ambapo tunatambua katika maendeleo hayo watumishi wa umma wamekuwa na mchango mkubwa katika kukamilisha suala hilo la miundombinu.

Nitoe wito Kwa wananchi wote wanaoendelea kutembelea kwenye maadhimisho haya wafike kwenye banda la Tarura kupata elimu na huduma mbalimbali zinazotolewa na Wakala wa barabara za mijini na Vijijini (TARURA)

Saturday, June 20, 2026

TBA YATEKELEZA MPANGO WA NYUMBA ZA GHARAMA NAFUU KWA WANANCHI



Katika kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2050 inayolenga kuhakikisha wananchi wanapata makazi bora na ya gharama nafuu, Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) umeendelea kutekeleza mpango wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu ili kuwawezesha wananchi, hususan vijana, kumudu kumiliki makazi.

Akizungumza katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika kitaifa katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Huduma Saidizi wa TBA, Bi. Amina Lumuli, amesema kuwa TBA tayari imeanza kutekeleza miradi ya nyumba za gharama nafuu katika mkoa wa Dar es Salaam.

Bi. Lumuli ametaja Mradi wa Temeke Kota kuwa ni miongoni mwa miradi hiyo, akibainisha kuwa utekelezaji wa mpango huo utaendelea katika maeneo mbalimbali nchini.


"Tunawakaribisha wawekezaji kuja kushirikiana nasi ili kwa pamoja tuweze kufanikisha lengo la Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050 la kuhakikisha wananchi wanapata makazi bora na ya gharama nafuu," amesema Bi. Lumuli.

Aidha, Bi. Lumuli amesema utekelezaji wa mradi huu unatokana na dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ya kuhakikisha wananchi wanapata makazi bora na yenye gharama nafuu.

Amesema TBA itaendelea kuhakikisha makundi yote, yakiwemo makundi maalum, yanafikiwa na kunufaika na programu hii ya nyumba za gharama nafuu.



POLISI WAFICHUA MPANGO WA UHALIFU JULAI 7

Jeshi la Polisi limetoa onyo kali kwa watu wote wanaohamasisha na kupanga kutekeleza vitendo vya uvunjifu wa amani na uhalifu nchini, wakiwemo wale wanaochochea kufanyika kwa maandamano mnamo tarehe 7 Julai mwaka huu.
Onyo hilo limetolewa kufuatia kuwepo kwa maswali mengi kutoka kwa baadhi ya wananchi hivi karibuni, wakitaka kujua jinsi jeshi hilo linavyofuatilia na kushughulikia uhamasishaji huo wa uvunjifu wa amani unaoendelea kufanywa na baadhi ya watu kupitia majukwaa mbalimbali ya mitandao ya kijamii.

Kupitia taarifa yake, Jeshi la Polisi limesema linafuatilia kwa karibu sana shughuli hizo zote kupitia mifumo yake mbalimbali pamoja na mitandao ya kijamii, ambapo imegundulika kuwa watu hao wameacha ajenda ya awali ya maandamano yasiyozingatia sheria na sasa wanahamasishana kufanya vitendo vizito vya kihalifu.

Miongoni mwa vitendo vya hatari vinavyohamasishwa ni pamoja na kufunga barabara, kuchoma moto shule kwa lengo la kusababisha taharuki kwa wazazi na walezi, kushambulia wananchi, kukata watu vichwa na kuua, pamoja na kuharibu mali za umma na za binafsi.

Aidha, watu hao wamediriki kwenda mbali zaidi kwa kuchocheana kupitia mitandao hiyo kuvamia askari wa vyombo vya ulinzi na usalama ili kuwapora silaha kwa ajili ya kwenda kuzitumia kutekeleza uhalifu wanaoupanga.

Jeshi la Polisi limesisitiza kuwa uhamasishaji huo wa jinai unaofanyika chini ya kivuli cha kile wanachokiita haki ya kufanya maandamano ya amani haukubaliki hata kidogo, kwani ni kinyume kabisa na sheria za nchi, misingi ya utawala wa sheria, mikataba ya kikanda na kimataifa, na unahatarisha usalama wa Taifa.

Jeshi hilo limefafanua kuwa hakuna haki yoyote inayomruhusu mtu kuhamasisha uhalifu unaokusudia kuhatarisha usalama wa maisha ya watu na mali zao, au unaokiuka haki za wengine kwa kuwajengea hofu kila siku na kuwanyima uhuru wao wa kufanya shughuli zao za kila siku za kujitafutia kipato.

Kwa sababu hiyo, Jeshi hilo limesema hatua stahiki za kisheria zinaendelea kuchukuliwa dhidi ya wahusika wote, na jeshi linaendelea kuwafuatilia kwa karibu sana kwa mujibu wa sheria za nchi.

Jeshi la Polisi limetoa wito kwa wananchi wote nchini kuungana kwa pamoja katika kushirikiana kukataa na kupinga kwa nguvu zote vitendo hivyo vya kihalifu vinavyolenga kuhatarisha maisha ya wananchi, mali zao, mali za umma, pamoja na amani ya nchi.

Vilevile, limetoa ushauri kwa mtu yeyote anayepokea ujumbe unaohamasisha uhalifu wa aina hiyo kutousambaza kabisa, bali kuufuta mara moja na kutoa taarifa kwa vyombo husika ili hatua zichukuliwe.

Jeshi limewahakikishia wananchi wote kuwa hali ya usalama nchini itaendelea kuwa shwari, yenye amani, utulivu na usalama kamili, kwani mambo hayo yatalindwa na kudumishwa kwa ushirikiano wa karibu sana kati ya Jeshi la Polisi pamoja na vyombo vingine vyote vya ulinzi na usalama.

Friday, June 19, 2026

JUMLA YA MIRADI 73 YA MWENGE WA UHURU YENYE THAMANI YA SH BILIONI 27.7 KUKAGULIWA,KUWEKEWA MAWE YA MSINGI NA KUZINDULIWA

 


Na Rebeca Duwe  Tanga


Mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian amewataka wananchi wa  Mkoa waTanga kutokeza kupoke mwenge wa uhuru  ili kuweza kuukimbiza ili kuhakikisha nuru inamulika kila mahali na kuimarisha umoja na mshikamano, ambapo utakimbizwa katika halmashauri zote 11 za mkoa huo na kukagua, kuzindua pamoja na kuweka mawe ya msingi katika miradi 73 yenye thamani ya zaidi ya 27.7


Hayo aliyasema wakati akizungumza na waandishi wa habari ,kuhusu maandalizi ya Mbio za Mwenge wa Uhuru  mwaka huu ambapo alisema Mwenge wa Uhuru utapokelewa katika Viwanja vya Shule ya Msingi Mji Mpya, Kijiji cha Mtoro, Kata ya Tunguli wilayani Kilindi ukitokea Mkoa wa Morogoro.



Alisema baada ya mapokezi hayo, Mwenge utakimbizwa kwa umbali wa kilometa 1,340 kupitia halmashauri zote za Mkoa wa Tanga kabla ya kukabidhiwa Mkoa wa Kilimanjaro Juni 28 mwaka huu katika Uwanja wa Shule ya Msingi Hedaru.


Dk. Burian alisema kati ya miradi 73 itakayofanyiwa kazi na Mwenge wa Uhuru, miradi 34 itawekewa mawe ya msingi, miradi 26 itafunguliwa na kuzinduliwa, miradi 11 ya vijana itakaguliwa pamoja na miradi miwili ya sekta ya maji.


Alifafanua kuwa miradi hiyo ina thamani ya Sh bilioni 27.76, ambapo Sh milioni 300.6 ni nguvu za wananchi, Sh bilioni 1.27 ni michango ya halmashauri, Sh bilioni 10.7 ni fedha za Serikali Kuu na Sh bilioni 15.47 ni mchango wa wahisani.


Akizungumzia kaulimbiu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu inayosema, “Tanzania ni Yetu Sote, Tushikamane kwa Pamoja Kuleta Maendeleo,” Dk. Burian alisema mkoa umejipanga kuhakikisha wananchi wa makundi mbalimbali wanashiriki kikamilifu katika shughuli zote za Mwenge.


Alisema viongozi wa serikali, watumishi wa umma, viongozi wa dini, wanawake, vijana, watu wenye mahitaji maalumu pamoja na makundi mengine wamehamasishwa kushiriki kikamilifu kuanzia mapokezi hadi makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru.


Aidha, wananchi watapata fursa ya kuushika na kuukimbiza Mwenge huo kama sehemu ya kuimarisha mshikamano, umoja wa kitaifa na ushiriki wa wananchi katika shughuli za maendeleo.


Mbali na kuhamasisha maendeleo, Mwenge wa Uhuru utaendelea kutoa elimu kuhusu mapambano dhidi ya rushwa, malaria, VVU/UKIMWI, matumizi ya dawa za kulevya pamoja na umuhimu wa lishe bora kwa jamii.


Dk. Burian aliwataka wananchi wa Mkoa wa Tanga kujitokeza kwa wingi katika maeneo ya mapokezi, miradi na mikesha mbalimbali ili kushiriki shughuli za Mwenge wa Uhuru na kufaidika na ujumbe wake.


Alisema mkoa umejipanga kikamilifu kuhakikisha wananchi wanapata burudani na hamasa kupitia ushiriki wa wasanii na vikundi vya sanaa vitakavyoshiriki katika maeneo yote ambayo Mwenge wa Uhuru utakesha.



Sunday, June 14, 2026

PROF. SHEMDOE AIELEKEZA KAMPUNI YA CRBC KUKAMILISHA UJENZI WA BARABARA 7 UBUNGO IFIKAPO AGOSTI 14, 2026

Na OWM - TAMISEMI, Dar es Salaam

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe ametaka Mkandarasi kampuni ya China Railways and Bridges Corporation (CRBC) inayojenga barabara tisa (9) za lami zenye urefu wa kilometa 5.42 kukamilisha ujenzi wa barabara saba (7) zilizosalia ifikapo Agosti 14, 2026, barabara hizo zinajengwa kupitia Mradi wa Uboreshaji wa Jiji la Dar es Salaam Awamu ya Pili (DMDP II) katika kata za Sinza, Mburahati, Mabibo na Makurumla wilayani Ubungo.

Prof. Shemdoe ametoa maelekezo hayo Juni 13, 2026 Katika Manispaa ya Ubungo jijini Dar es Salaam wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua ujenzi wa barabara 23 zenye urefu wa kilometa 52.37 zinazojengwa wilayani Ubungo katika kata 11 kupitia utekelezaji wa Mradi wa Uboreshaji wa Jiji la Dar es Salaam Awamu ya Pili (DMDP II).

Prof. Shemdoe amesitiza kuwa, mkandarasi huyo anayesuasua katika ujenzi wa barabara hizo kwa kisingizio cha lami kuchelewa kufika kutokana na vita ya Mashariki ya Kati, hatopewa muda wa nyongeza wa kukamilisha ujenzi wa barabara hizo iwapo atashindwa kukamilisha ifikapo Agosti 14, 2026 kwa mujibu wa mkataba.

“TARURA hakuna kumuongezea muda mkandarasi huyu, atafute lami popote atakapoipata na afanye kazi usiku na mchana kukamilisha barabara hizi 7 zilizosalia ili kuwaondolea adha wananchi,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Katika kuhakikisha barabara zinakamilika kwa wakati, Prof. Shemdoe ameitaka TARURA na Mshauri Elekekezi (NIMETA Consult (T) kumshauri mkandarasi CRBC kwa kuangalia uwezekano wa kukabidhi baadhi ya barabara hizo kwa mkandarasi mwingine (sub contract) ili ujenzi ukamilike kwa wakati.

Aidha, Prof. Shemdoe amemuelekeza Mtendaji Mkuu wa TARURA Mhandisi Victor Seff kumuondoa Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Uhasibu Bw. Evans Mgeusa anayesimamia Fedha za Miradi ya Benki ya Dunia kwa kitendo cha kuchelewesha malipo na kumleta mwingine ambaye atafanya kazi kwa weledi na wakati.

Sanjari na hilo, Prof. Shemdoe amemuelekeza Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI Bw. Adolf Ndunguru kuwaondoa Wahasibu Bw. Julius Bashuta na Mbwana Mkembe wa kitengo hicho cha Fedha na Uhasibu kinachosimamia  fedha za miradi ya Benki ya Dunia, na kuwaleta wengine ambao watafanya kazi vizuri na kwa uaminifu. 

Akizungumzia jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita, Prof. Shemdoe amempongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha utiaji saini wa mikataba minne ya ujenzi wa barabara za wilaya ya Ubungo yenye thamani ya shilingi bilioni 77, 457,169,172.73 kupitia Mradi wa Uboreshaji wa Jiji la Dar es Salaam Awamu ya Pili (DMDP II).

Kwa upande wake Mkazi wa Sinza Bw. Jawa Waziri amemshukuru Prof. Shemdoe kwa kufanya ziara ya ukaguzi wa barabara ya mtaa wake wa Sinza Lion na kumpongeza kwa kumuelekeza mkandarasi CRBC kukamilisha kwa wakati barabara hiyo ambayo imekuwa ni kero kwa wakazi wa eneo hilo.










STAMICO YATAMBULIWA KAMA SHIRIKA BORA LA MADINI TANZANIA


DAR ES SALAAM

Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) limeendelea kuthibitisha ubora wake barani Afrika baada ya kutwaa tuzo mbili muhimu katika Tuzo za Kampuni Bora za Mwaka Afrika (Africa Company of the Year Awards - ACOYA).

Katika hafla ya utoaji wa tuzo hizo iliyofanyika Juni 12, 2026 katika Ukumbi wa Superdome, Oysterbay jijini Dar es Salaam, STAMICO iliibuka mshindi mkubwa wa usiku huo kwa kujinyakulia tuzo ya Shirika Bora la Madini la Mwaka Tanzania pamoja na Tuzo Kuu ya Mshindi wa Jumla wa ACOYA, ambayo ndiyo tuzo kubwa zaidi ya hafla hiyo.

Tuzo hizo zilipokelewa kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO, Dkt. Venance Mwasse, na Meneja wa Masoko na Uhusiano wa Umma wa shirika hilo, Deus Alex Ntukamazina.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kupokea tuzo hizo, Ntukamazina alisema ushindi huo ni wa pili mfululizo kwa STAMICO katika tuzo hizo za bara la Afrika, jambo linaloonesha mafanikio makubwa ya mabadiliko yanayoendelea ndani ya shirika hilo.

Alisema tuzo hizo ni uthibitisho wa kutambuliwa kwa juhudi, ubunifu na kujitolea kwa watendaji wa STAMICO katika kuligeuza shirika hilo kuwa miongoni mwa taasisi zenye ufanisi na kuaminika zaidi katika sekta ya madini.

“Kwa shirika letu, huu ni ushahidi kwamba kazi kubwa inayofanyika katika kulibadilisha STAMICO inatambuliwa na kuthaminiwa. Ni matokeo ya juhudi za pamoja za kuhakikisha tunatoa mchango mkubwa katika maendeleo ya sekta ya madini nchini,” alisema Ntukamazina.

Alipoulizwa kuhusu siri ya mafanikio ya STAMICO kutoka kuwa shirika lililokuwa likikabiliwa na changamoto miaka iliyopita hadi kuwa taasisi inayoshinda tuzo za kimataifa, Ntukamazina alieleza kuwa uongozi bora na mipango ya kimkakati ndiyo msingi wa mafanikio hayo.

Alimpongeza Dkt. Mwasse kwa uongozi wake thabiti, bunifu na wenye maono ambao umewezesha STAMICO kupanua shughuli zake za kibiashara, kuongeza gawio kwa Serikali na kuimarisha ushirikiano na wachimbaji wadogo pamoja na wawekezaji wakubwa katika sekta ya madini.

Kwa ushindi huo wa tuzo mbili za bara la Afrika, STAMICO imeendelea kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania na kuweka viwango vya juu vya utendaji kwa mashirika ya umma barani Afrika.

Saturday, June 13, 2026

SHEIKH PEMBE ASISITIZA KUHUSU UMUHIMU WA AMANI, ATAKA WAISLAMU KUILINDA NCHI YAO



Imamu Mkuu Masjid Mtambani Sheikh Shabani Pembe amewataka Waislamu na Watanzania wote kwa ujumla kuendelea kudumisha na kuilinda amani ya Tanzania, akisisitiza kuwa ikiwa serikali ingeruhusu kufanyika kwa kile kilichokuwa kimepangwa, kuratibiwa na kuhamasisha Oktoba 29, 2025 basi Tanzania isingeweza kukalika tena kutokana na uvunjifu wa amani ambao ungetokea wakati ule wa Uchaguzi.

Sheikh Shabani Pembe amebainisha hayo wakati akitoa hotuba yake kwa waumini wa Dini ya Kiislamu Mkoani Dar Es Salaam na kuwataka Waislamu kuhukumu kile kilichotokea kwa uadilifu pamoja na kupima athari ambazo zingeweza kujitokeza ikiwa serikali ingewaaacha wale waliokuwa wamejitokeza barabarani kuendelea na matukio yao ya uvunjifu wa amani Nchini.

"Kituo chetu cha mwendokasi tumeshuhudia kikichomwa, Vituo vya Polisi vilichomwa, ATM pale Manyanya imechomwa na hata maduka ya watu yamechomwa na kuibiwa, hawa watu wangeachiwa wafanye wanavyotaka hii Nchi ingekuwa wapi? Ndugu zangu tunapohukumu tuhukumu kwa uadilifu, kwamba lengo lilikuwa waachiwe wafanya wanavyotaka? Au ilikuwa nini? Baadae wale wote waliowachochea wanaanza kuiona dola mbaya, Tunapohukumu mambo tuhukumu kwa uadilifu." Amesema Sheikh Pembe.

"Tunapohukumu mambo tuhukumu kwa uadilifu, amani ni tunu ndugu zangu, ikiondoka hii hata sisi hatuwezi kukusanyika. Ile Ijumaa ile kutoka Tegeta mpaka hapa nililipa Elfu sitini kwa bodaboda na nimefika hapa naambiwa Mufti ametangaza hakuna ibada hapa, sasa waislamu niwaombe kuipenda Nchi yako ni katika Imani. Wale wote waliokuwa wanahamasisha yale ya Oktoba 29 hakuna hata mtoto wao aliyeguswa na kiwembe, tafsiri yake ni kuwa wao na familia zao zilibaki salama, kinyume chake familia za maskini na fukara ndio waliotolewa kafara." Ameongeza kusema.

Sheikh Pembe amewakosoa vikali pia wale wanaokosoa Tume zilizoundwa kuchukua matukio hayo ya wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, akisisisitiza kuwa Tanzania ni huru na Watanzania wanapaswa kuunga mkono busara na hekima za Viongozi wao katika kupata muafaka na suluhu ya kudumu dhidi ya kile kinachotajwa kama sababu ya matukio ya Oktoba 29, 2025.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...