Monday, May 4, 2026

MCHENGERWA: BIMA YA AFYA KWA WOTE IWE KIPAUMBELE BAJETI YA 2026/27

Waziri wa Afya, Mohamed Mchengerwa akizungumza kwenye ufunguzi wa kikao cha baraza kuu la wafanyakazi wa wizara hiyo kilichofanyika jijini Mwanza.
Waziri wa Afya, Mohamed Mchengerwa amesisitiza kwamba bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2026/27 inapaswa kutoa mwelekeo wa Taifa katika utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote.

Mchengerwa amesema hayo Jumapili Mei 03, 2026 wakati akizungumza kwenye ufunguzi wa kikao cha Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Wizara ya Afya kilichofanyika ukumbi wa Rock City Mall jijini Mwanza.

"Lazima tujiandae kikamilifu kwa utekelezaji wa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote. Hili si suala la kadi pekee bali lazima kuwe na utayari wa miundombinu, mifumo, dawa na rasilimali watu imara" alisema Mchengerwa.

Mchengerwa alisisitiza kwamba lazima mifumo ya TEHAMA iwe imara, upatikanaji wa dawa na vifaa tiba uimarishwe huku akiweka mkazo kwa buzalishaji wa ndani kupewa kipaumbele na Wizara ya Afya.

"Lazima mifumo ya manunuzi itoe kipaumbele kwa wazalishaji wa ndani. Katibu Mkuu nakuagiza usimamie hilo, ununuzi kupitia MSD na mifumo yetu ya manunuzi lazima izingatie hilo lakini kwa kuzingatia ubora" ameongeza.

Mchengerwa aliongeza kuwa katika mwaka wa fedha 2025/2026, Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imefanikiwa kupiga hatua ikiwemo kuongeza upatikanaji wa dawa muhimu kufikia wastani wa asilimia 73 kwa mwezi Februari, 2026.

"Pia tumeendelea kupunguza vifo vya akina mama wajawazito kupitia uwekezaji katika vituo vya afya, hospitali za wilaya, vifaa tiba na rasilimali watu. Haya ni mafanikio ya pamoja chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan" alisema Mchengerwa.

Pia alitoa wito kwa kila mtumishi, kuanzia makao makuu hadi hospitali za rufaa, kutoka idara hadi kituo cha afya, kuhakikisha wanatoa huduma kwa weledi na huruma kwa wananchi.

"Hatutavumilia ucheleweshaji wa huduma usio na sababu. Hatutavumilia upendeleo unaodhalilisha haki za mwananchi" alisisitiza Mchengerwa huku akiagiza Katibu Mkuu kufanyia kazi malalamiko ya wagonjwa kukaa muda mrefu bila kupata huduma katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt Seif Shekalaghe alisema kikao hicho kimelenga kujadili na kupitisha mwelekeo wa bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2026/27 yenye lengo la kuboresha huduma za afya kwa wananchi pamoja na ustawi wa watumishi.

Naye Katibu wa Baraza hilo, Vivian Joseph ambaye ni Afisa Tawala Mkuu Wizara ya Afya alisema kupitia kikao hicho kitasaidia upatikanaji wa bajeti ambayo ni shirikishi kutekelezwa na watumishi wa wizara hiyo baada ya kupitishwa na bunge.
Waziri wa Afya, Mohamed Mchengerwa akizungumza kwenye ufunguzi wa kikao cha baraza kuu la wafanyakazi wa wizara hiyo kilichofanyika jijini Mwanza.
Waziri wa Afya, Mohamed Mchengerwa akizungumza kwenye ufunguzi wa kikao cha baraza kuu la wafanyakazi wa wizara hiyo kilichofanyika jijini Mwanza.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalaghe akizungumza kwenye kikao cha baraza la wafanyakazi wa wizara hiyo kilicholenga kujadili na kupitisha bajeti ya mwaka 2026/27.
Mganga Mkuu wa Serikali, Dkt. Grace Magembe akizungumza kwenye kikao cha baraza la wafanyakazi Wizara ya Afya kilichoketi jijini Mwanza.
Wafanyakazi wa Wizara ya Afya wakifuatilia kikao cha baraza la wafanyakazi wa wizara hiyo.
Wafanyakazi wa Wizara ya Afya wakifuatilia kikao cha baraza la wafanyakazi wa wizara hiyo.
Wafanyakazi wa Wizara ya Afya wakifuatilia kikao cha baraza la wafanyakazi wa wizara hiyo.

Source

Thursday, April 30, 2026

Oraimo Watch 6 Lite: Smartwatch mpya inayotingisha sokoni


Soko la smartwatch linaendelea kukua kwa kasi, na sasa limepokea nyongeza mpya yenye ushindani mkubwa, Oraimo Watch 6 Lite. Ikiwa imebuniwa kwa kuzingatia mahitaji ya mtumiaji wa kisasa, saa hii inaleta mchanganyiko wa teknolojia ya hali ya juu, muonekano wa kuvutia, na utendaji bora kwa matumizi ya kila siku, ikiambatana na kauli mbiu yake “Kuwa Fiti Kimtindo.”

Moja ya vitu vinavyoifanya Oraimo Watch 6 Lite kuwa ya kipekee ni skrini yake kubwa ya 2.01 HD, inayotoa mwonekano ulio wazi na wa kuvutia. Pia inakuja na kipengele cha Bluetooth HD Calling, kinachokuwezesha kupokea na kupiga simu moja kwa moja kupitia saa yako kwa urahisi wa hali ya juu ukiwa popote ulipo.

Kwa upande wa uimara, saa hii inajivunia hadi siku 30 za matumizi thabiti, hivyo kukuondolea usumbufu wa kuchaji mara kwa mara. Aidha, ikiwa na kiwango cha IP68 (waterproof & dustproof), Oraimo Watch 6 Lite iko tayari kukabiliana na mazingira tofauti bila wasiwasi.


Uzinduzi rasmi wa bidhaa hii ulifanyika tarehe 4/4/2026 katika duka la Kinondoni, ambapo wadau na wapenzi wa teknolojia walipata nafasi ya kuiona na kuijaribu kwa karibu. Baadaye, uzinduzi wa pili wa kipekee (soft launch) ulifanyika kwa kushirikiana na jamii ya wakimbiaji ya iRun, ambapo washiriki walipata uzoefu halisi wa kutumia saa hii wakati wa mazoezi. Hii ilikuwa njia ya kuonyesha jinsi vipengele vya afya na ufuatiliaji wa mwili vinavyofanya kazi kwa ufanisi.

Kwa matumizi ya kila siku, Oraimo Watch 6 Lite ina uwezo mkubwa wa kusaidia katika ufuatiliaji wa usingizi, mazoezi, pamoja na kukuza mtindo bora wa maisha. Pamoja na muonekano wake wa kisasa na UI interface iliyo rafiki kwa mtumiaji, saa hii inakuwa chaguo sahihi kwa yeyote anayehitaji msaidizi wa kidijitali mkononi.

Kwa sasa, Oraimo Watch 6 Lite inapatikana sokoni kwa ununuzi, ikiwa tayari kuleta mabadiliko katika maisha ya watumiaji wake. Kwa kifupi, ni zaidi ya saa ni mshirika wako wa kila siku katika afya, mawasiliano, na mtindo wa maisha, ukiakisi kikamilifu kauli mbiu yake: “Kuwa Fiti Kimtindo.”

Saturday, April 18, 2026

CCM Mkoa wa Tanga ya gundua ubadhirifu Saruji 150 ikiwa ni poamoja uwizi wa saruji katika Hospitali ya wilaya Kilindi mkoani Tanga


 Na Rebeca Duwe ,Kilindi


Mwenyekiti wa CCM Mkoa waTanga Rajabu Abdrahman amesema Chama cha Mapinduzi hakitaweza kuwafumbia Macho wale wote wanaohusika na ubadhirifu wa Fedha za serikali kwa kuyafanyia mambo yao binafsi badala ya kufanya kazi iliyo kusudiwa ya kuondoa changamoto za wananchi .


Hayo aliyasema wakati wa ziara yake ya kukagua ujenzi wa Hospitali ya wilaya ya Kilindi ambapo kulitokea ubadhirifu wa saruji 145 iliyohifadhiwa kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali hiyo ili kuondoa changamoto ya huduma za afya .


Aidha alisema kwa msistizo kuwa amesikia uwizi wa saruji na kuharibika saruji iliyoganda kutokana kukaa kwa muda mrefu bila kutumika kwa kazi iliyokusudia jambo ambalo inaonyesha kuwa ni uzembe wa wataalamu waliopewa kazi hiyo.

"Mradi huu wa Hospitali ya wilaya Kilindi pesa yake imetolewa na Rais Dkt Samia Suluhu Hasan hivyo kutokutumia ipasavyo ni ubadhitifu wa Pesa za serikali na kuwakosesha wananchi haki zao za kupata huduma ya Afya,kwani kabla ya kutokuwepo kwa Hospitali hiyo wananchi wa Kilindi walikuwa wanaifuata huduma hiyo Morogoro ,Handeni au Tanga mjini jambo ambalo inawatia gharama kubwa ya usafiri wananchi hao."


 Alisema Rajabu

Sambamba na hayo Mwenyekiti huyo CCM aliagiza watu wote waliofanya ubadhirifu kwa njia moja ama nyingine wachukuliwe hatua kali za sheria ili miradi iweze kukamilika kwa wakati kama ambavyo mhe Rais amelekeza na kutaka kuondoa changamoto za wananchi anaowaongoza.


Kwa upande wake MKurugenzi wa halmashauri ya Wilaya Kilindi mkoani Tanga John Mgalula alisema walipata taarifa za uwizi wa saruji na kumkamata bodaboda akiwa na mifuko mitano ya saruji na kuwapeleka polisi ambapo mpaka sasa kuna mlinzi yuko polisi na fundi pamoja na bodaboda ambapo uchunguzi bado unaendelea kwa mujibu wa taratibu za kisheria.


Aliongeza kuwa baada ya kugundua hivyo walianza kuhesabu na kagundua kuwa kuna mifuko ya aina tatu ambayo ni iliyoibiwa,iliyoganda na ambayo ni mizima ambayo jumla ilikuwa ni mifuko 193 ambayo kuna iliyotumika kati ya hiyo na iliyopo na ambayo imeharibika sana.


Hata hivyo alisema kuwa bado wanaendelea kufuatilia kujua ni mifiko mingapi inafaa na iliyopo ndani ya stoo kwa ujenzi kugundua mifkuko mi ngapi haifai kabisa ili kuendaelea ujenzi Hospitali kwa ajili ya kuwahudumia u wananchi wa kilindi.

Thursday, April 16, 2026

SERIKALI YAJIPANGA KUZIFANYIA UKARABATI SHULE ZOTE KONGWE NCHINI - PROF. SHEMDOE



Na OWM – TAMISEMI, Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI, Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amesema Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI imeandaa andiko la mradi unaoitwa SIFA yaani (School Infrastructure Facelifting Programme) na kuliwasilisha Wizara ya Mipango, ili kuwezesha upatikanaji wa fedha za kufanyia ukarabati wa shule zote kongwe za awali, msingi na sekondari nchini.

Prof. Shemdoe amesema hayo Aprili 15, 2026 wakati akijibu hoja za Waheshimiwa Wabunge walizoziwasilisha wakati wa kujadili Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka 2026/27.

“Namshukuru Mheshimiwa Prof. Kitila Mkumbo na timu yake ya Wizara ya Mipango kwa kulipokea andiko tulilowasilisha ili tupate fedha za kutekeleza mradi wa ukarabati wa shule kongwe nchi nzima,” amesema Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe amefafanua kuwa, tathmini iliyofanyika imebaini ukarabati unahitajika kwenye shule za msingi ikihusisha vyumba vya madarasa ni 42,716 na nyumba za walimu 31,813 na kwa upande wa shule za sekondari inajumuisha vyumba vya madarasa 6,889, nyumba za walimu 3,518, maktaba 91 na mabweni 309. 

Prof. Shemdoe ameanisha kuwa, Serikali imekuwa ikitoa fedha kwa ajili ya kufanya ukarabati kwa awamu ambapo kati ya mwaka 2021/22 hadi 2025/26, Serikali imetumia shilingi bilioni 237.9 kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa miundombinu mipya ya shule za msingi na Sekondari kongwe na chakavu nchini.





Wednesday, April 15, 2026

WAZIRI SANGU: RAIS SAMIA AWEZESHA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII KUWA HIMILIVU

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu akitoa ufafanuzi kwa Waheshimiwa Wabunge, wakati akichangia mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Taasisi zake na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2026/2027 katika Bunge la 13, Mkutano wa Tatu, kikao cha Tisa leo Aprili 15, 2026 Jijini Dodoma.

************

Na: OWM (KAM) – Bungeni, Dodoma

Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa kuchukua hatua madhubuti katika kuimarisha Mifuko ya Hifadhi ya Jamii nchini kwa lengo la kuhakikisha ustawi wa wananchi, pamoja na kuhakikisha utoaji wa pensheni kwa wakati.

Pongezi hizo zimetolewa Bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mheshimiwa Deus Clement Sangu, leo Aprili 15, 2026 wakati akichangia mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Taasisi zake na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2026/2027.

Aidha, Mhe. Sangu amesema thamani ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii imeendelea kuongezeka ikiwemo Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) thamani yake imeongezeka kutoka Shilingi Trilioni 4.36 hadi Shilingi Trilioni 10.3. Mfuko wa PSSSF thamani yake iliongezeka kutoka Shilingi Trilioni 5.74 hadi Shilingi Trilioni 12.96.

Waziri Sangu amefafanua kuwa deni la Serikali katika mfuko wa PSSSF ilikuwa Trilioni 4.46, mwaka 2022/2023 Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alitoa hati fungani ya shilingi trilioni 2.17 kwa ajili ya kuulipa mfuko wa PSSSF deni lililodumu kwa muda mrefu la shilingi trilioni 4.6 la michango kabla ya 1999. Pia, Serikali imeendelea kulipa Trilioni 2.09 ambayo imesaidia thamani ya Serikali kulipa mfuko huo wa PSSSF kufikia asilimia 95.

Vilevile, Mhe. Sangu amesema kuwa kutokana na mifuko ya hifadhi ya jamii kuwa himilivu imepelekea kwa sasa watumishi wa umma wanaostafu wanalipwa mafao yao ndani ya siku ishirini na tano huku kiwango cha kima cha chini cha pesheni kuongezeka toka shilingi 100,000 hadi kufikia shilingi 250,000 kwa wastaafu.

Kadhalika, Waziri Sangu amesema Mifuko ya hifadhi ya jamii imeendelea kuwekeza katika miradi yenye tija kwa lengo la kuongeza thamani ya michango ya wanachama na kukuza uchumi pamoja na kuongeza ajira kwa wananchi.

Akihitimisha mchango wake, Mheshimiwa Sangu aliwahakikishia wabunge kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano itaendelea kusimamia utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2026/2027 kwa ufanisi, ili kuleta manufaa kwa Watanzania katika sekta zote za kiuchumi na kijamii.

Kwa upande wake, Spika wa Bunge, Mheshimiwa Mussa Azan Zungu, amewapongeza wabunge kwa kupitisha bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu na kusisitiza umuhimu wa wizara na taasisi husika kusimamia utekelezaji wake ili kuchochea maendeleo ya wananchi.

KAMATI YA FUM KISHAPU YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO YENTE THAMANI YA TSH. BILION 1.2

Na Sumai Salum- Kishapu

Katika jitihada za kuhakikisha fedha za umma zinaleta matokeo chanya kwa wananchi, Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga imefanya ziara maalum ya kukagua miradi 7 ya maendeleo yenye thamani ya shilingi Bilioni 1, 278,000,000.

Ziara hiyo imefanyika Aprili 15 hadi 16, 2026, ikiongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Mhe. Enock Reuben, ambapo wajumbe wa kamati walitembelea na kujionea hali halisi ya utekelezaji wa miradi hiyo ya maendeleo katika maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo.


Miradi iliyokaguliwa inagusa moja kwa moja maisha ya wananchi, ikiwemo miradi ya afya, umeme wa jua, ujenzi wa vyumba vya madarasa, matundu ya vyoo kwenye baadhi ya zahanati na maegesho ya magari mnada wa Mhunze, ujenzi wa nyumba mpya ya Mkurugenzi Mtendaji, ujenzi wa vichomea taka katika zahanati, pamoja na maendeleo ya kikundi cha Vijana na Wanawake waliopewa mikopo ya asilimia 10 wa Halmashauri hiyo.


Kwa mujibu wa kamati hiyo, lengo kuu la ziara lilikuwa ni kufuatilia kwa karibu matumizi ya fedha za miradi, kutathmini hatua za utekelezaji, pamoja na kubaini changamoto zinazoweza kukwamisha ukamilishaji wa miradi hiyo.


Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, Mhe. Reuben amesisitiza umuhimu wa kuhakikisha kila shilingi ya umma inaleta thamani halisi kwa wananchi (value for money), huku akiwataka watendaji kusimamia miradi kwa weledi na uwajibikaji mkubwa.


Kamati haikuishia kukagua tu, bali pia ilitoa maelekezo na ushauri muhimu kwa watendaji. Miongoni mwa mambo yaliyosisitizwa ni, usimamizi makini wa fedha za miradi, uzingatiaji wa viwango vya ubora wa ujenzi, kukamilika kwa miradi ndani ya muda uliopangwa pamoja na utatuzi wa changamoto kwa wakati.


Hatua hizi zinalenga kuhakikisha miradi hiyo inaleta manufaa yaliyokusudiwa kwa wananchi bila kuchelewa wala kupoteza rasilimali.


Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango ina nafasi muhimu katika kusukuma maendeleo ya wilaya. Kupitia ziara kama hizi, kamati inaendelea kuhakikisha uwajibikaji unaimarika, fedha zinatumika ipasavyo, na miradi inatekelezwa kwa ufanisi.


Kwa ujumla, ziara hii ni ishara ya dhamira ya dhati ya viongozi wa Kishapu katika kusimamia maendeleo na kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora zinazotokana na miradi hiyo.Makamo mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga na Diwani wa Kata ya Masanga Mhe. Enock Reuben akisikiliza maelezo kwenye ziara ya kamati ya Fedha Utawala na Mipango iliyofanyika Aprili 14-15, 2026 ya ukaguzi wa miradi 7 ya  maendeleo yenye thamani ya Tsh. bilioni 1.2Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga Emmanuel Johnson akiielezea jambo kamati ya Fedha Utawala na Mipango wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi 8 ya maendeleo yenye thamani ya Tsh. bilioni 1.2  Aprili 14-15, 2026 Diwani wa Kata ya Mwamalasa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga  Mhe. Bushi Mpina ambaye pia ni Mjumbe wa kamati ya Fedha, Utawala na Mipango wa Halmashauri ya wilaya hiyoDiwani wa viti maalumu Kata ya Ukenyenge Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga  Mhe. Sophia Masele ambaye pia ni Mjumbe wa kamati ya Fedha, Utawala na Mipango wa Halmashauri ya wilaya hiyoDiwani wa Kata ya Songwa wilayani Kishapu mkoani Shinyanga Mhe. Abdul Ngoromole ambaye pia ni Mjumbe wa kamati ya Fedha, Utawala na Mipango wa Halmashauri ya wilaya hiyoDiwani wa Kata ya Kishapu Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga  Mhe. Joel Ndettoson ambaye pia ni Mjumbe wa kamati ya Fedha, Utawala na Mipango wa Halmashauri ya wilaya hiyoPicha za Miradi

                     Tazama picha za matukio mbalimbali













  




























Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...