Tanzania Daily Eye
Saturday, March 14, 2026
MFUMO WA “ONGEA NA WAZIRI” WAIMARISHA MAWASILIANO KATI YA SERIKALI NA WANANCHI
Wednesday, March 11, 2026
WAKAZI MRUKI NA MSASANI WAILILIA SERIKALI DARAJA LA KUDUMU MTO FAHHAY
Na John Walter-Babati
Wakazi wa mitaa ya Mruki na Msasani katika Halmashauri ya Mji wa Babati mkoani Manyara wameiomba serikali kuwajengea daraja la kudumu katika Mto Fahhay ili kuondoa hatari inayowakabili wanafunzi wa Shule ya Msingi Mruki wanaolazimika kuvuka daraja la mbao kila siku wanapoenda shuleni.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wakazi hao wamesema daraja hilo la muda limekuwa likitumika kwa zaidi ya miaka mitatu, lakini kwa sasa limeanza kuwa hatari kutokana na baadhi ya mbao na miti iliyotumika kulijenga kuoza na idadi ya watumiaji kuongezeka.
Shule shikizi ya Msingi Mruki yenye takribani wanafunzi 200 ilianzishwa na Halmashauri ya Mji wa Babati kwa lengo la kupunguza umbali mrefu waliokuwa wakitembea wanafunzi kutoka mitaa ya Mruki na Msasani kwenda katika shule mama ya Msingi Msasani na Darajani.
Mwenyekiti wa Bodi ya Shule ya Msingi Mruki, Bakari Said, amesema licha ya daraja hilo kuwa mkombozi kwa wanafunzi kwa kipindi cha zaidi ya miaka mitatu, sasa limekuwa tishio kwa usalama wao hasa wakati wa msimu wa mvua.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mruki, Abdilahi Rajabu, amesema daraja hilo ni kiungo muhimu kinachounganisha mitaa ya Sinai na Mruki, ambapo asilimia kubwa ya watoto kutoka maeneo hayo husoma katika shule hiyo shikizi ya Mruki.
Naye Mariam Hamis, mkazi wa Mruki, ameiomba serikali kuharakisha ujenzi wa daraja la kudumu ili kuwaepusha watoto na wakazi wa eneo hilo na hatari ya kuanguka mtoni wanapovuka.
Baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo akiwemo Samia Issa Ramadhani na Halima Idd wamesema hulazimika kuvuka daraja hilo kila siku kwenda na kurudi shuleni, hali inayowatia hofu hasa wakati daraja linapokuwa na utelezi au kuharibika.
Aidha, Agostino Balohho, ambaye ni mlinzi wa Shule ya Msingi Mruki, amesema daraja hilo la mbao ni njia fupi inayotumiwa na wanafunzi kutoka Mtaa wa Sinai kufika shuleni na pia hutumiwa na wakazi wa Mruki kama njia ya mkato kwenda mjini Babati kufuata huduma mbalimbali.
Kutokana na hali hiyo, wakazi hao wameiomba serikali pamoja na wadau wa maendeleo kuwasaidia kujenga daraja la kudumu litakalohakikisha usalama wa wanafunzi na wananchi wanaolitumia kila siku.
Monday, March 9, 2026
DKT. GWAJIMA AWAHIMIZA WANANCHI KUUPOKEA NA KUULINDA MRADI WA PAMOJA KWA USTAWI WA KIUCHUMI







Saturday, February 28, 2026
AGIZO LA RC MANYARA KUHUSU TAA, LAANZA KUTEKELEZWA BABATI.
Na John Walter-Manyara
Hatimaye kazi ya ukarabati wa taa za barabarani zilizokuwa haziwaki katika Mji wa Babati imeanza kutekelezwa kufuatia agizo la Mkuu wa Mkoa wa Manyara Region kwa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA).
Kwa muda mrefu baadhi ya wakazi wa Babati walilalamikia tatizo la taa za barabarani kuzimika hali iliyokuwa ikisababisha hofu ya usalama nyakati za usiku.
Kufuatia malalamiko hayo, Mkuu wa Mkoa kupitia kikao cha bodi ya Barabara mkoa kilichofanyika hivi karibuni, aliiagiza TARURA kuhakikisha taa zote zilizokuwa haziwaki zinarejeshwa katika hali ya kufanya kazi haraka iwezekanavyo.
Kupitia jukwaa la mitandao la Manyara Mpya, Mkuu huyo wa Mkoa amethibitisha kuanza kwa utekelezaji wa agizo hilo kwa kuchapisha picha zinazoonesha mafundi wakiendelea na kazi ya matengenezo ya miundombinu ya taa hizo.
Akiandika katika ujumbe wake, amesema:
"Ndugu viongozi mliopo mitaani huko Naimani mnaona kazi inaendelea, taa zilizozima ni nyingi na kazi yote itakamilika, tuwe na subra tu. Nawashukuru kwa uvumilivu.
Naimani kwenye hili kikombe kimeniepuka 🙇🏽♀️
Nawapenda sana ❤️"
Kauli hiyo imepokelewa kwa hisia chanya na wananchi wengi, wakionesha matumaini kuwa kukamilika kwa kazi hiyo kutaimarisha usalama, kuongeza mwanga katika maeneo ya biashara pamoja na kurahisisha shughuli za kijamii nyakati za usiku.
Utekelezaji huo unaonekana kuwa sehemu ya juhudi za uongozi wa mkoa katika kusimamia na kuboresha miundombinu ya huduma za kijamii ndani ya Manispaa ya Babati.
Thursday, February 19, 2026
Halmashauri ya Wilaya ya Babati yapitisha bajeti ya bilioni 71 kwa miaka 2026–2030
Na John walter-Babati
Baraza la madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Babati limepitisha mapendekezo ya bajeti ya shilingi bilioni 71 kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2026 hadi 2030, ikiwa ni sehemu ya mipango ya kuimarisha utoaji wa huduma na utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa wananchi.
Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, John Noya, amesema bajeti hiyo inahitaji usimamizi madhubuti na utekelezaji mzuri wa ukusanyaji wa mapato ili iweze kuleta matokeo yaliyokusudiwa.
"Tusiposimamia vyema mapato yetu, bajeti haitafanya kazi kama ilivyopangwa lakini tukisimamia kwa umakini, itawezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa ufanisi," amesema Noya.
Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Anna Mbogo amesema kuwa baada ya bajeti hiyo kupitishwa na Bunge, baraza la madiwani kwa kushirikiana na wataalamu wa halmashauri litatoa ushirikiano mkubwa katika hatua za utekelezaji ili kuhakikisha malengo yaliyowekwa yanafikiwa.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Babati, Emmanuela Kaganda, amesisitiza umuhimu wa kuwepo kwa uwiano wa miradi ya maendeleo katika kata zote, akibainisha kuwa wananchi wote wanastahili kunufaika kwa usawa.
Naye Naibu Waziri wa Utumishi na Utawala Bora, Regina Ndege Qwaray, amesema Serikali chini ya uongozi wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, tayari imeanza utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2025–2030, hivyo amezitaka halmashauri kuhakikisha mipango yao inaendana na Dira ya Maendeleo ya Taifa ya mwaka 2025–2050.
Amesisitiza kuwa upangaji na utekelezaji wa bajeti za halmashauri unapaswa kulenga maendeleo endelevu yatakayoboresha maisha ya wananchi kwa muda mrefu.
Wednesday, February 18, 2026
WAANDISHI WA HABARI GEITA WAPEWA MBINU ZA KUTHIBITISHA NA KUHAKIKI TAARIFA; UTPC YAHAMASISHA UANDISHI WA HABARI ZENYE TIJA
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...



















































