Tanzania Daily Eye
Wednesday, June 10, 2026
DKT. MAULID: UONGOZI WA KIMKAKATI NI MSINGI WA MAFANIKIO YA SEKTA YA ELIMU
CBE YAHUISHA MITAALA TISA KUENDANA NA TEKNOLOJIA NA MAHITAJI YA SOKO LA AJIRA
Tuesday, June 9, 2026
CWM Yasisitiza Malezi ya Maadili kwa Wafanyakazi wa Majumbani
Chama wa wafanyakazi wakatoliki CWM kinaendelea na mchakato wa kutoa semina kwa wanawake wa makundi mbali ili kupaza sauti kwa jamii kutambua thamani,wajibu na haki za wafanyakazi wa majumbani
Mkakati wa kuyafikia makundi hayo ni sehemu ya utekelezaji wa maono na misingi ya Chama hicho kuwa sauti kwa wasio na sauti hasa wafanyakazi wa majumbani ambao katika utekelezaji wa majukumu yao hukutana na vikwazo mbalimbali
Aidha leo June 5 CWM imekutanisha kundi la wanawake wakatoliki na makundi mengine ya wanawake katika parokia ya Teule ya Mtakatifu Benedict Mkundi Jimboni Morogoro
Miongoni mwa mambo yanayojadiliwa katika mafunzo hayo ni kukazia mchakato wa uwepo wa mikataba ya ajira kwa wafanyakazi wa majumbani, haki na wajibu wao kama zilivyo kazi nyingine
EDSON YEYEYE ni Mratibu CWM Taifa,amewaagiza washiriki hao kuimarisha malezi ya kimaadili kwa wafanyakazi hao, ili kulinda heshima na utu wa Mfanyakazi wa nyumbani.
Kwa upande wake Frola Ng'eni Katibu wa CHODAWU mkoa wa Morogoro amesema mfanyakazi ana haki ya kushikishwa kujiunga na mfuko wa jamii,Nssf kwa ajili ya akiba yake ya baadaye.
Hata hivyo amesema kuwa sekta ya wafanyakazi wa majumbani ni sekta muhimu katika kukuza pato la familia na taifa, hivyo wanatakiwa kupewa haki wanazostahili bila kunyanyaswa
CWM inalenga kuyafikia makundi mengi ya wanawake Jimboni Morogoro ambapo hivi karibuni wanatarajia kukutana na kundi la wafanyakazi wa Majumbani ili kukamilisha mkakati wa kuwapeleka katika mafunzo ya ufundi stadi katika chuo cha Veta Mikumi
Wednesday, June 3, 2026
Airtel Yaongeza Uwekezaji Zanzibar, Yaingia Ushirikiano na ZECO Kuimarisha Huduma za Kidigitali
DKT. RAJABU SEIF AIPONGEZA NEMC KWA ELIMU YA UHIFADHI WA MAZINGIRA
Tuesday, June 2, 2026
Breaking : UMMY MWALIMU ALAMBA UTEUZI..SASA MSHAURI WA RAIS SAMIA
VINGOZI WA DINI WATAKIWA KUWA MSTARI WA MBELE KATIKA MALEZI.
Na Rebeca Duwe Tanga
Viongozi wa Dini wametakiwa kushirikiana na Jamii kwa kuzingatia suala la malezi ya watoto na vijana ili kuweza kupata kizazi kilicho bora katika jamii kwa maslahi mapana ya taifa kwa ujumla.
Haya aliyasema mwanyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga ustdh Rajabu Abdrahman wakati akizungumza na waandishi wa habari wilayani Pangani katika kijiji cha Stahabu Pwani wakati dua ya kuombea dua ya kuwaombe ndugu waliotangualia mbele ya haki, ambapo alisema Suala la malezi na makuzi ya watoto ni jukumu la jamii kuweza kushirikia na viongozi wa dini ili kupata jamii ambayo ina msimamo mzuri wa kiimani na kimaadili.
Aidha Mwenyekiti Rajabu alisema kwamba ni vyema kushirikiana na viongozi wa Dini ili waweze kukemea mmomnyoko wa maadlii uliokitithiri katika Jamii kwani kwa kufanya hivyo itasaidia kupunguza wimbi la wahalifu na kuwa na jamii salama.
"Viongozi wa dini wana nafasi kubwa ya kuijenga jamii salama kwa kuwa wao ndio wanakaa na watu kwenye nyumba za ibada hivyo tukashirikana nao wote kujenga kizazi kijacho kwa kuweza kuwakemea maadili mabovu ili tuwe na kizazi kijacho "
alisema Mwenyekiti Rajabu.
Hata hivyo Mwenyekiti Rajab alisisitiza umuhimu wa malezi bora katika jamii hasa viongozi wa dini kuwa mstari wa mbele kukemea uovu kwa sababu ndio nguvu kazi ya baadaye na viongozi wa baadaye kwa aajili ya jami ijayao.
Kwa upande wake Mkuu Balozi Batilda Burian alimpongeza Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga kwa kufanya jambo la kuwaunganisha viongozi mbalimbali kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa na nje ya mkoa kwa ajili dua ya kuwombea ndugu waliotangulia mbele ya haki.
Friday, May 29, 2026
MADIWANI WAASWA KUWA CHACHU YA MAENDELEO KISHAPU NA KUEPUKA MGONGANO WA MASLAHI
Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Peter Masindi akifungua mafunzo ya madiwani wa Halmashauri hiyo yakuwajengea uwezo katika masuala ya maadili,rushwa na kukumbushwa wajibu wao ambayo yametolewa na Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga
Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Peter Masindi, amewataka madiwani kusimamia kwa umakini miradi ya maendeleo katika maeneo yao huku akisisitiza kuwa wao ndiyo wawakilishi wa wananchi na nguzo muhimu ya maendeleo ya Taifa.
Akizungumza wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo madiwani kuhusu kujiepusha na vitendo vya rushwa, kubaini mianya ya rushwa pamoja na kuwakumbusha maadili na wajibu wao, Masindi amesema viongozi hao wanapaswa kuwa chachu ya mabadiliko kwa kuwajibika ipasavyo katika maeneo wanayoyaongoza.
Amesema wananchi wanawategemea madiwani kuwasimamia na kuwawakilisha vizuri, hivyo wanapaswa kuangalia changamoto zilizopo katika kata zao na kuchukua hatua kwa wakati ili kuhakikisha maendeleo yanapatikana.
“Wananchi watawapima baada ya miaka mitano kwa kazi mtakazozifanya, Maendeleo ya kata yanawategemea ninyi, msipofanya maamuzi sahihi kata zenu haziwezi kupata maendeleo,” amesema Masindi.
Aidha amewataka madiwani kufanya kazi kwa kuzingatia maadili, nidhamu pamoja na kutunza siri za vikao na majukumu yao, akieleza kuwa dhamana waliyopewa ni kubwa ndiyo maana Serikali imeamua kutoa mafunzo hayo ili kuwakumbusha wajibu wao kwa wananchi.
Kwa upande wake, Mwendesha Mashitaka wa TAKUKURU Mkoa wa Simiyu ambaye pia ni wakili Maximilian Kyabona, amewaasa madiwani kujiepusha kutanguliza maslahi binafsi mbele na kusahau kuwa wao ni wawakilishi wa wananchi.
Kyabona amesema madiwani ndiyo watakaowezesha Halmashauri ya Kishapu kupata maendeleo iwapo watawajibika ipasavyo, kupinga rushwa na kufichua mianya yote inayoweza kusababisha miradi ya maendeleo kushindwa kutekelezwa.
Alitaja baadhi ya mambo ambayo madiwani wanapaswa kuyaepuka kuwa ni pamoja na kubadili vifungu vya matumizi ya fedha, kuchukuliana posho pamoja na kujihusisha na zabuni mbalimbali zinazoweza kuleta mgongano wa maslahi.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...




















