Saturday, July 31, 2021

Kauli ya Manara baada ya Mo Dewji kutoa bilioni 20 Simba



Kupitia maelezo yake aliyoweka kwenye mtandano wa Instagram Haji Manara ameandika kuwa "Nikisoma baadhi ya Comments zenu toka jana mnauliza Bughatti Mbona husemi kitu kuhusu billioni 20, ndugu zangu kama kuna Muumini namba moja aliyeshiriki kuwashawishi wanasimba wakubali juu ya muundo huu mpya ni mimi"


"Nilizodolewa sana, nikatusiwa sana na nikagombana na wengi kuhusu uwekezaji huu, iweje nisiunge mkono jambo lenye maslahi kwa Simba na mpira wetu kwa ujumla"
"Na niwaambie jana ni siku kubwa kwangu kwa sababu nililotaka na kulipigania limekuwa, nitaunga mkono kila jitihada za kuifanya Simba iwe kubwa zaidi na zaidi na Insha'Allah wiki hii nitaongea nanyi kuwashukuru"

Polisi Yakata 15 Wakamatwa Na Viuatilifu Feki Mtwara


POLISI Mkoani Mtwara imikamata watu 15 kwa tuhuma za kuuza viuatilifu feki vya salpha na vya maji ambavyo vinatumika kudhibiti magonjwa ya zao la korosho.


Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Brigadia Jenerali Marco Gaguti amewaambia waandishi wa habari mjini hapa kuwa watu hao walikamatwa na viuatilifu vya salpha tani 84.3 na vya maji tani 292 ambavyo vimeisha muda wake wamatumizi.


"Watu hao walikamatwa katika zoezi lilofanywa na jeshi la polisi mkaoni hapa baada ya kupata taarifa za awali za uwepo wa viuatilifu feki katika baadhi ya maduka maeneo mbalimbali Mtwara," amesema.


Kufuatia hatua hiyo, Gaguti ameelekeza jeshi la polisi kukamilisha taratibu za kipolisi na watuhumiwa kufikishwa haraka kwenye vyombo vya sheria.


Pia ameagiza kufungwa kwa maduka pamoja na maghala ambayo yalihusika katika hujuma hiyo ya kuuza na kuhifadhi viuatilifu ambavyo vimeisha mda wake mpaka pale kesi ya msingi itakapokamilika.


Pia Gaguti amewaomba wananchi wa pamoja na wakulima kuwa waangalifu na kufuatilia kuhakikisha ubora wa viuatilifu na madawa mengine wayanyotumia katika kudhibiti magonjwa ya korosho.


"Ninawaomba wa Mtwara haswa wakulima kuwa macho wanapotafuta viuatiliu na madawa ya mikorosho, wawe makini kuangalia na kufuatilia ubora wa madwa wanayonunua na kutoa taarifa mapeam ili tuweze kukabiliana na uwepo wa madwa feki," amesema.


Viautilifu hivyo vilikamatwa katika maeneo ya Manispaa ya Mtwara Mikindani, Tandahimb, Newala  na Nanyumbu.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara Mark Njera amesema uchunguzi wa awali ulibaini kuwa watuhumiwa hao walitumia mbinu za kuwahadaa wakulima kwa kuwaambia kuwa wameruhusiwa na mamlaka husika kuuza hivyo viuatilifu pamoja na kuwa vimeharibika huku wakiwaambia kuwa havina tatizo.


Pia watuhumiwa hao walitumia barua ambayo walidai wamepewa na mamlaka husika ambazo ziliwapa idhini kuuza hivyo viuatilifu feki pia walitumia nyaraka za kughushi kuonyesha kwamba wamepewa idhini na mamlaka husika kuuza viuatilifu hivyo.

MWANZA FRIENDS WAKUTANA SHINYANGA MJINI KUZINDUA KATIBA ,KUSAKA FURSA ZA UWEKEZAJI


Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association, Patrick Joseph akionesha Katiba na Nyaraka mbalimbali za Kikundi cha Mwanza Friends Association.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Wanachama wa Kikundi cha Wafanyabiashara na Watumishi wa Umma  Marafiki kutoka Mwanza maarufu 'Mwanza Friends Association' wanaofanya shughuli zao kwenye mikoa mbalimbali nchini Tanzania wamekutana Mjini Shinyanga kwa ajili ya kikao na kuzindua rasmi Katiba yao pamoja na kutafuta fursa za uwekezaji katika Mkoa wa Shinyanga.

Wanachama hao wa Mwanza Friends Association wamefanya kikao chao kilichoambatana na ziara 'Tour' mkoani Shinyanga leo Jumamosi Julai 31 katika Hoteli ya Liga Mjini Shinyanga.

Akizungumza katika kikao hicho, Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association, Patrick Joseph amesema walianzisha kikundi hicho mwaka 2014 kwa lengo ya kusaidiana katika shida na raha.

"Kikundi cha Marafiki kutoka Mwanza 'Mwanza Friends Association' chenye Makao yake Makuu Jijini Mwanza kinaundwa na Wafanyabiashara na Watumishi wa Umma wanaotoka Mkoa wa Mwanza lakini sasa wanaishi kwenye mikoa mingine nchini",amesema Joseph.

"Sisi tunajihusisha na masuala ya kusaidiana kijamii katika shida na raha. Hivi sasa tuna wanachama 35 na tuna miradi ukiwemo mradi wa VIP Bar iliyopo Maduka Tisa Ilemela Jijini Mwanza",ameeleza.

Amesema wanachama wa Mwanza Friends Association kutoka mikoa mbalimbali nchini wameamua kufanya kikao chao Mjini Shinyanga na kuzindua rasmi Katiba yao ikiwa ni sehemu ya ziara yao ya kutafuta fursa za uwekezaji zilizopo mkoani Shinyanga.

Joseph ametumia fursa hiyo kuwakaribisha wanaotaka kujiunga na Mwanza Friends Association na kuwaomba wawasiliane na Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association kwa simu namba 0755 863 330 (Patrick Joseph) au Katibu Omary Haji (0653261226).

ANGALIA PICHA HAPA
Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association, Patrick Joseph akionesha Katiba ya Kikundi cha Mwanza Friends Association wakati wa kikao cha Wanachama wa kikundi hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Liga Hotel Mjini Shinyanga leo Jumamosi Julai 31,2021. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association, Patrick Joseph akizungumza wakati akifungua kikao cha Wanachama wa kikundi hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Liga Hotel Mjini Shinyanga leo Jumamosi Julai 31,2021. Kulia ni Mweka Hazina, Respicius Rwegoshora, kushoto ni Katibu, Omary Haji.
Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association, Patrick Joseph akizungumza wakati akifungua kikao cha Wanachama wa kikundi hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Liga Hotel Mjini Shinyanga leo Jumamosi Julai 31,2021.
Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association, Patrick Joseph akizungumza wakati akifungua kikao cha Wanachama wa kikundi hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Liga Hotel Mjini Shinyanga leo Jumamosi Julai 31,2021.
Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association, Patrick Joseph akiwakaribisha wanaotaka kujiunga na Mwanza Friends Association na kuwaomba wawasiliane na Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association kwa simu namba 0755 863 330 (Patrick Joseph) au Katibu Omary Haji (0653261226).
Katibu wa Mwanza Friends Association Omary Haji akizungumza kwenye kikao cha Wanachama wa kikundi hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Liga Hotel Mjini Shinyanga leo Jumamosi Julai 31,2021.
Mweka Hazina wa Mwanza Friends Association, Respicius Rwegoshora akizungumza kwenye kikao cha Wanachama wa kikundi hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Liga Hotel Mjini Shinyanga leo Jumamosi Julai 31,2021.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakiwa kwenye kikao
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakiwa kwenye kikao
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakiwa kwenye kikao
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakiwa kwenye kikao
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakiwa kwenye kikao
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakiwa kwenye kikao
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakiwa kwenye kikao
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakiwa kwenye kikao

Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Mweka Hazina wa Mwanza Friends Association, Respicius Rwegoshora akipata chakula
Katibu wa Mwanza Friends Association Omary Haji akipata chakula
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakipiga picha ya kumbukumbu Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakipiga picha ya kumbukumbu Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakipiga picha ya kumbukumbu Liga Hotel Mjini Shinyanga leo Jumamosi Julai 31,2021.


Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Meneja TTCL Atumbuliwa Kwa Kukwepa Ziara za Viongozi na Kupika Taarifa

 


Meneja wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) wa Mkoa wa Kagera, Irene Shayo ametenguliwa kuanzia Julai 30, 2021 kwa tuhuma za utumishi wake kusuasua na kukwepa ziara za viongozi katika eneo lake


Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Kundo Mathew amesema pia Meneja huyo amekuwa akipika Taarifa za Mapato na Matumizi


Naibu Waziri amesema Meneja huyo apangiwe majukumu mengine kulingana na wasifu wake kitaaluma ili aweze kufanya kazi vizuri kwasababu majukumu ya sasa hana uwezo nayo


Mwanariadha wa Kenya aondolewa Olimpiki kisa matumizi ya madawa




Mwanariadha wa Kenya Mark Otieno Odhiambo ameondoshwa nje ya mashindano ya Olimpiki ya Tokyo baada ya vipimo kuonesha ametumia dawa zilizopigwa marufuku michezoni.

Kijana huyo wa miaka 28 alikuwa ametakiwa kushindana katika mbio za mita 100 za wanaume Jumamosi lakini alishindwa katika hatua ya vipimo na kubainika alitumia dawa za kusisimua misuli.

Kwa mujibu wa mkuu wa msafara huko Tokyo Waithaka Kioni: "Hata hivyo amekataa kutambua madai ya ukiukaji huo na kuomba uchambuzi wa sampuli yake ya mkojo ."

Kipimo kilifanyika tarehe 28 mwezi Julai wakati mwanariadha huyo alipokuwa Tokyo, kabla ya hapo alikuwa kwenye kambi ya mazoezi nchini Japan kati ya tarehe 15 na tarehe 24 mwezi Julai.

Otieno Odhiambo alishiriki kwenye Mashindano ya Dunia ya 2017 na Michezo ya Jumuiya ya Madola ya 2018.

Ni mwanariadha wa pili wa Kiafrika kuondolewa kwenye michuano hiyo baada ya Mnaijeria Blessing Okagbare.

Kioni alisisitiza kwamba maafisa wa michezo na bodi zinazosimamia michezo nchini Kenya wameazimia kuendeleza vita yao dhidi ya dawa zilizopigwa marufuku michezoni

"Haya ni mambo ambayo labda yanaweza kuepukika hii ndio sababu inaendelea kuwasiliana na mashirikisho ya michezo na ADAK kwa hivyo tunaendelea kutoa elimu juu ya kupambana na dawa zilizopigwa marufuku kwa wanariadha wetu, "aliiambia BBC Sport Africa.

"Lakini sio kwamba wanariadha hawajui na ndio sababu tunachukulia kuwa hana hatia hadi tutakapochunguza tena sampuli B ya mkojo.

"Nilizungumza naye mchana huu na ananiambia hawezi kukumbuka kama alitumia kitu chochote ambacho kitatoa matokeo ya aina hiyo.

"Kinachonisumbua ni kwamba Kenya tayari imekuwa kwenye orodha ya waliowekewa alama nyekundu na tulitarajia tutatoka katika orodha hiyo lakini tukio kama hili linaweza kuvuruga mpango wa kujinasua."

Japan yakanusha madai kwamba kuna uhusiano kati ya Olimpiki ya Tokyo na ongezeko la maambukizi ya virusi vya corona




Japan imekanusha madai kwamba kuna uhusiano kati ya Olimpiki ya Tokyo na mwenendo unaoongezeka wa aina mpya za virusi vya corona (Kovid-19).

Waziri Mkuu Suga Yoshihide, katika mkutano na waandishi wa habari, alisema kwamba hakuona uhusiano kati ya ongezeko la kubwa la kesi za maambukizi katika siku za mwisho baada ya Michezo ya Olimpiki ya Tokyo, ambayo ilianza mnamo Julai 23.

Suga alisema,

"Tunatekeleza hatua za kinga ya virusi ambazo hupunguza trafiki ya binadamu pamoja na udhibiti mkali wa mipaka ili kuzuia kuenea kwa janga hilo kutoka kwa wageni. Nadhani hakuna uhusiano wowote."

Idadi kubwa zaidi ya kesi za maambukizi tangu mwanzo wa janga huko Japan ilirekodiwa jana. Kesi za maambukizi ya virusi kote nchini ziliongezeka kwa zaidi ya 10,000 kwa siku moja kwa mara ya kwanza.

Idadi ya vifo kutokana na virusi nchini iliongezeka hadi 15,188, na idadi ya wagonjwa iliongezeka hadi 904,036. Katika vitengo vya huduma za wagonjwa mahututi, watu 539 wanatibiwa Kovid-19.


Source

TVMC YATOA ELIMU UKATILI WA KIJINSIA, LISHE MAONESHO YA BIASHARA NA TEKNOLOJIA YA MADINI SHINYANGA


Mratibu wa Miradi wa Shirika lisilo Kiserikali la The Voice of Marginalized Community (TVMC) la Mjini Shinyanga, Mary Mahanya (kulia) akizungumza katika banda la TVMC kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga leo Jumamosi Julai 31,2021.

Shirika la TVMC limeshiriki Maonesho hayo  kwa kuelimisha wananchi kuhusu kupinga ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto, kutoa elimu ya masuala ya Lishe zikiwemo njia sahihi za kunyonyesha mtoto na kutoa msaada wa Kisheria  ili kusaidia kutatua migogoro mbalimbali kama vile ya ardhi na ndoa.

Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga yanayoongozwa na kauli mbiu "Uwekezaji wa Madini na Viwanda Shinyanga kwa Uchumi Endelevu" yameanza tarehe 23 Julai, yanatarajiwa kuhitimishwa tarehe 1 Agosti, 2021.

Mratibu wa Miradi wa Shirika lisilo Kiserikali la The Voice of Marginalized Community (TVMC) la Mjini Shinyanga, Mary Mahanya (kulia) akielezea huduma zinazotolewa na TVMC kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
 Afisa Utawala wa Shirika lisilo Kiserikali la The Voice of Marginalized Community (TVMC) la Mjini Shinyanga, Chiku Hamis akionesha kipeperushi kinachoelezea masuala ya Lishe kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
 Afisa Utawala wa Shirika lisilo Kiserikali la The Voice of Marginalized Community (TVMC) la Mjini Shinyanga, Chiku Hamis akionesha kipeperushi kinachoelezea masuala ya Lishe kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.

Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Blinken kuhusu mkataba wa nyuklia wa Iran


 

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken alisema kuwa mazungumzo ya nyuklia na Iran hayataendelea milele.

Blinken alifanya mkutano wa pamoja na waandishi wa habari na mwenzake Ahmed Nasser es-Sabah huko Kuwait, ambapo alienda kufanya mawasiliano rasmi.

Kwenye mkutano na waandishi wa habari uliotangazwa kwenye televisheni ya serikali ya Kuwait, Blinken alisema: "Tulikuwa na mazungumzo ya moja kwa moja na Wairani huko Vienna, kuonyesha nia yetu njema na ya kurudi kwenye makubaliano ya nyuklia. Mazungumzo na Iran hayataendelea milele. Mpira sasa upo kwa upande wa Iran na ndio wanaopaswa kufanya uamuzi. "

Waziri wa Mambo ya Nje wa Kuwaiti Sabah alisema kuwa Marekani ilionyesha umuhimu unaozingatia kuhakikisha usalama katika eneo hilo.

Sabah pia alibaini kuwa wanataka kuandaa mkutano wa tano wa mazungumzo ya kimkakati kati ya Kuwait na Marekani.

Mkutano wa kwanza wa Mazungumzo ya Mkakati wa Marekani na Kuwait ulifanyika Washington mnamo 2016 na wa pili mnamo 2018, na wa tatu ulifanyika Kuwait mnamo 2019, na wa nne ulifanyika kupitia video mwaka jana.

Mazungumzo hayo, yaliyokuwa yakiendelea kwa takriban miezi 3 huko Vienna, mji mkuu wa Austria, ambayo vyama vya Ulaya pia vilishiriki, yalikwama baada ya mgombea wa kihafidhina Ebrahim Reisi kushinda uchaguzi wa urais uliofanyika Iran mnamo Juni 19.

Mkuu huyo alisema kuwa Tehran haitakubali makubaliano ya nyuklia isipokuwa vikwazo vya Marekani vitakapoondolewa kikamilifu.

Washington pia ilisema kwamba sharti hili halikubaliki na kuonya kwamba "mazungumzo hayawezi kuendelea kwa muda usiojulikana".

CHUO CHA ROYAL KINATANGAZA NA FASI ZA MASOMO

 


Chuo cha Royal Training Institute Kilichopo Mbagala Jijini Dar es salaam kinawatangazia nafasi za masomo kwa kozi za mwezi April na Septemba mwaka huu.


 Usajili umeanza na Unaendelea chuoni Royal Training Institute.

Chuo kimesajiliwa na NACTE kwa usajili namba REG/HAS/103.


Kozi zinazotolewa na Royal Training Institute ni:-

Ordinary Diploma in Pharmaceutical Sciences(Kozi ya Ufamasia) miaka mitatu. Uwe na Alama D nne zikiwemo Kemia na Baiolojia.


Ordinary Diploma in Pharmaceutical Sciences (In Service) Mwaka 1-uwe umemaliza NTA Level 5


Pia Chuo cha Mafunzo Royal kwa kushirikiana Na Mamlaka ya Elimu ya ufundi (VETA) kingependa kuwajulisha wahitimu wa kidato cha nne  kwamba sasa Chuo kinatoa kozi ya msaidizi wa maabara (Certificate in Laboratory Assistants) ngazi ya 1, 2 na 3 Uwe umemaliza kidato Cha nne na kupata cheti  muhula utaanza Mwezi wa nne . Wahitimu watafanya kazi kwenye mashule, viwanda na taasisi mbalimbali. Chuo pia kitatoa punguzo kwako na kukusaidia kupata kazi.



Pia chuo Cha Royal  Institute kinatoa kozi ya Manunuzi na Ugavi(Procurement & Supply) ngazi ya cheti na Diploma. Uwe na ufaulu wa D 4 katika masomo ya kidato Cha nne.


Kwa Maelezo zaidi wasiliana na chuo Cha Royal kwa namba 0688353310, 0713325507, 0692972523, 0788083484

Au kwa barua pepe pharm_royal@yahoo.com, au tembelea tovuti yetu ya WWW.RTI.AC.TZ.


KUMBUKA KUNA PUNGUZO GHARAMA ZA HOSTELI KWA WALE WATAKAOWAHI..









Vikosi vya Rwanda vyafanya vema Msumbiji


Jeshi la Rwanda lililopelekwa Cabo Delgado nchini Msumbiji limetangaza kufanya vyema kwenye uwanja wa mapigano huku kukiwa na wasiwasi kuhusu kamanda wa kikosi hicho.

Msemaji wa jeshi la Rwanda ameliambia shirika la habari la Reuters kwamba wanamgambo 14 wameuliwa wiki hii na wanajeshi kutoka Rwanda waliopelekwa Msumbiji.

Ronald Rwivanga amesema operesheni za kijeshi zilizoendeshwa kwenye maeneo ya Mbau na Awese,mkoani Cabo Delgado, baada ya kikosi cha wanajeshi wake kuvamiwa, zilisababisha jumla ya wanamgambo 14 kuuliwa. Rwivanga amesema ni majeraha madogo yaliowapata wanajeshi wa Rwanda kufuatia operesheni hizo.

Mapema mwezi huu, Rwanda ilipeleka kikosi cha wanajeshi na polisi 1,000 nchini Msumbiji kusaidia katika kupamabana na kundi la waasi linaloendesha mashambulizi kaskazini mwa nchi hiyo.  Takriban raia laki nane waliyahama makaazi yao kwenye mkoa wa Cabo Delgado na mapigano hayo yalisababisha kampuni ya Mafuta ya Ufaransa ya Total kusitisha mradi wake wa dola bilioni 20 wa kuzalisha gesi asilia kwenye mkoa huo.

 Ikiwa kupelekwa kwa kikosi cha wanajeshi wa Rwanda nchini Msumbiji kunalenga kuwasaka wanamgambo wenye itikali kali. Lakini wakosoaji wa serikali ya Rwanda wanaoishi nchini humo wanahofia usalama wao pia. Jenerali Innoncent Kabandana anayeongoza kikosi hicho, ameelezwa na wapinzani kuwa ni mkono wa rais Paul Kagame katika kuwalenga wakosoaji wake.Mtandao wa TheRwandan.com, uliandaka kuwa Meja-jenerali Kabandana alihusika na mauwaji ya maaskofu wa kanisa katoliki wa Gakurazo mwaka 1994 nchini Rwanda na vilevile kuwalenga wakosoaji wa serikali ya Rwanda nchini Marekani na Canada ambako alifanya kazi kama mwambata wa kijeshi katika ubalozi wa Rwanda jijini Washington.

Cleophas Habiyareme, mkuu wa jamii ya wakimbizi wa Rwanda wanaoishi nchini Msumbiji amesema alisoma taarifa pia kwamba kamanda huyo anahusika na kuwalenga wapinzani wanaoishi nje ya nchi. Lakini amesema hilo haliwezi kuwatisha jamii ya wakimbizi wa Rwanda nchini Msumbiji. Habiyareme amesema Msumbiji ni nchi iliyosaini mkataba wa Geneva kwa jili ya kuwapa hifadhi wakimbizi. Amesema halitokuwa jambo la busara kwa kikosi kilicho alikwa kwa shughuli malumu baadae kuanza kuwalenga wakimbizi. Hata hivyo ameiomba serikali ya Msumbiji kuhakikisha usalama wao.

Nchini Msumbiji ambako jenerali Kabandana amepewa majukumu mapya, jamii ya wakimzizi wa Rwanda  ni takriban watu 4,000 ambao wamekuwa wakibughudhiwa na kuuliwa miaka ya hivi karibuni.  Kisa cha hivi karibuni ni kutoweka bila maelezo yoyote hadi sasa kwa mwandishi habari na mkosoaji wa serikali ya Rwanda Ntamuhanga Cassien aliyekuwa akiishi kwenye kisiwa cha Inhaca,nchini Msumbiji.

 

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...