Tuesday, July 31, 2018

Wakazi wa Kisarawe waeleza namna wanavyomfahamu Mhe Jokate Mwegelo (Video)

Wakazi wa Wilaya ya Kisarawe wamesema wanamsubiria kwa hamu Mkuu mpya wa wilaya hiyo, Mhe Jokate Mwegelo ambaye ameteuliwa na Rais Magufuli siku chache zilizopita.
The post Wakazi wa Kisarawe waeleza namna wanavyomfahamu Mhe Jokate Mwegelo (Video) appeared first on Bongo5.com.

Source

‘Wasanii wavivu kusoma sheria zetu, atakayekwenda nje bila kibali chetu faini mil.1 au kufutiwa usajili wake’-BASATA (+video)

Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) limeeleza wazi juu ya sheria zao na kanuni mpya ambazo zinawataka wasanii wote watakaokwenda nje ya nchi kwa lengo la kufanya show kuwa na kibali maalumu kutoka kwao kitakachomruhusu kufanya hivyo.


Kaimu Katibu Mtendaji BASATA, Onesmo Kayanda amesema kuwa sheria hiyo ipo wazi isipokuwa wasanii wakubwa huwa hawahudhurii kwenye semina na midahalo pia hawasomi sheria za BASATA ndio maana wanataharuki linapotokea suala la utekelezaji.
Akizungumzia suala la faini juu ya kibali hicho, Kayanda amesema kuwa endapo msanii atafanya show nje ya nchi bila kibali kwa mara ya kwanza ataonywa na kutozwa milioni 1 na akirudia tena faini itaongezeka na ikiendelea tabia hiyo basi atafutiwa usajili wake.
The post ‘Wasanii wavivu kusoma sheria zetu, atakayekwenda nje bila kibali chetu faini mil.1 au kufutiwa usajili wake’-BASATA (+video) appeared first on Bongo5.com.

Source

TANZIA: MWANAHABARI SHADRACK SAGATI AFARIKI DUNIA KATIKA AJALI YA GARI MKOANI GEITA




Source

Nina Mika 20 Sijawahi Fanya Mapenzi ila Nahisi Bikira yangu Haipo Je ni Kawaida?

Naitwa Nancy Naishi Kijitonyama , mimi ni Msichana na Miaka 20 nimekuwa nikijitunza kwa muda mrefu ili kutunza Bikira yangu kwa mwanaume atakaye nioa mungu akijalia ...so sijawahi fanya mapenzi na mtu yoyote japo napata vishawishi vingi....Saa zingine nikisikia hamu huwa najisugua kwa vidole sehemu zangu ili kutoa hamu....

Sasa hivi karibuni nimehisi huku chini hapako tight kama zamani hata nikiingiza kidole kinaingia bila shida sasa naogopa je Bikira yangu imeshatoka au ni kawaida? na je kujishika kwa vidole sehemu hizo kunaondoa bikira?

Please naomba ushauri.

Viongozi Wapya Walioteuliwa na Rais Magufuli Wataapishwa Kesho.

Viongozi Wapya Walioteuliwa na Rais Magufuli Wataapishwa Kesho.Rais John Magufuli Jumatano Agusti 1, 2018 atawaapisha viongozi mbalimbali aliowateua Jumamosi iliyopita.

Taarifa iliyotolewa  jana Julai 30, 2018 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Gerson Msigwa imesema viongozi hao ni, wakuu wa mikoa wanne na makatibu wakuu wawili.

Wengine ni, naibu makatibu wakuu wawili na makatibu tawala wa mikoa 13.


"Wakuu wa mikoa yote ya Tanzania Bara mnapaswa kuhudhuria tukio hili," imeeleza taarifa hiyo.

BBC DIRA YA DUNIA JUMATATU 30.07.2018


Source

Lionel Messi afanya mazoezi ya hatari (+Video)

Wakati baadhi ya wachezaji wa Barcelona wakiwa tayari wamerejea na kujiunga na klabu hiyo nyota wao Lionel Messi ameonekana akifanya mazoezi ya hatari na mbwa wake wakati akiwa nyumbani kwake. Kufuatia ushiriki wake kwenye michuano ya kombe la dunia nyota huyo wa Argentina, Messi amepatiwa muda wa kupumzika kabla ya kujiunga tena na Barcelona hivyo kutumia …

The post Lionel Messi afanya mazoezi ya hatari (+Video) appeared first on Bongo5.com.


Source

Monday, July 30, 2018

Unaniume Sana 'Baada ya Kwenda Mafunzo ya JKT Mpenzi Wangu Arudi Bila Bikira'

Hello Admin, naomba nisaidie hili
mimi ni kijana wa chuo mwaka wa pili, nilitokea kumpenda binti mmoja aliyemaliza kidato cha sita 2012 ambaye alikuwa ni jirani yangu na kwel tulipendana sana ,na tulipanga mimi na yeye tuje kuoana na kutokana na mazingira aliyolelewa baba yake akiwa mchungaji aliniambia kuwa yeye ni bikira na ataitunza hadi ndoa. kwakwel niliheshimu hayo mawazo yake kwa kuwa nlkw nampenda sana had wazazi wetu walikuwa wanalitambua hilo

Ila alipomaliza kidato cha sita alitakiwa aende kwenye mafunzo ya jkt kulingana na agizo la serikali hivyo alienda huko na nlikuwa nawasiliana nae mara kwa mara ingawa sio sana.


Kitu cha ajabu amebadilika sana kitabia tangu aliporudi ,nilipomuhoji vizur alikuja kuniambia kwa ss yeye sio bikira tena..nilipomuuliza kwa nn umechukua uamuzi huo? akaniambia alikuwa amechanganyikiwa kutokana na mazoez ya jkt had akafanya mapenz bila kujitambua ila akaomba msamaha na tuishi km zamani...kwakwel nimechanganyikiwa na sijui hata nimjibu nini? naomba ushaur kwako

Huyu Hapa Mzungu ndio Mpenzi wa Malia Obama, Mtoto wa Rais Mtaafu Barack Obama


Mtoto wa kwanza wa Rais Mstaafu wa Marekani Barack Obama, Malia Obama mwenye umri wa miaka 20 akiwa na Boyfriend wake Raia wa Uingereza, wawili hawa ni Wapenzi na familia zao zinatambua, walikutana Havard University wanakosoma wote.

Mbwana Samatta Wetu Awa Lulu Huko Ughaibuni, Club Zamgombania Kumsajili


SAMATTA 🔥🔥: Baada ya klabu ya Levante inayoshiriki Ligi kuu nchini Hispania kutuma ofa ya €4m kumtaka mshambuliaji wa Krc Genk Mbwana Samatta, imeelezwa kuwa vigogo wa Ujerumani Borrusia Dortmund nao wapo tayari kumchukua mchezaji huyo.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na meneja wa mchezaji huyo Jamal Kisongo zinadai kuwa kuna klabu kadhaa zinahitaji huduma yake zikiwemo Dortmund pamoja na Metz.
Licha ya kutakiwa na klabu hizo, ni Levante pekee ndiyo iliyoonesha nia zaidi kumtaka mshambuliaji huyo kutoka Tanzania .

Nandy Amwaga Radhi Jukwaani

KUONESHA mzuka umemkolea, msanii wa Kizazi Kipya zao kutoka Jumba la Kuibua Vipaji Tanzania (THT), Faustina Charles 'Nandy' amejikuta akishindwa kuzuia hisia zake mbele ya mashabiki na kulazimika kuvua 'kuchojoa' nguo ya juu pamoja na kiatu kimoja.

Ishu nzima ilijiri pande za Nyamongo, Tarime ambapo msanii huyo alikuwa akitumbuiza na baada ya kufika katikati ya shoo alisikika akiwaambia mashabiki wake kwamba avue nguo asivue ndipo akavua na kuwarushia akibakiwa na nguo moja ya ndani.

Baada ya muda tena aliwarushia kiatu mashabiki na kufanya umati uendelee kulipukwa kwa shangwe. Hata hivyo mara baada ya kushuka kwa shoo hiyo, Nandy aliingia katika mtandao wake wa Instagram na kuwashukuru mashabiki hao kwa kuandika; "Juhudi huzidi kipaji, asanteni sana Nyamongo

Mtoto wa miaka nane apata fistula baada ya kubakwa

Na John Walter -Babati

Mtoto wa Darasa la kwanza [jina tunalihifadhi] mwenye umri wa miaka nane (8) mwanafunzi wa shule ya Msingi Maganjwa iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Babati amefanyiwa kitendo cha ubakaji akiwa anaenda mashine kusaga unga wa ugali hali iliyomsababishia maumivu makali na kuwalazimu madaktari kumfanyia upasuaji.

Kwa mujibu wa mwenyekiti wa kijiji cha Maganjwa Petro Shauri alisema majira ya jioni mtoto huyo alitumwa mashineni kusaga mahindi kwa ajili ya chakula cha nyumbani na alipofika  msagaji alimwagiza arudi nyumbani kuchukua hela kwani alifika mashineni hapo akiwa hana hela na pia walikuwa wakidaiwa.

"Wakati akirejea nyumbani kumpa taarifa mama kwamba wanadaiwa ndipo alipokutana na mwanaume huyo na kufanyiwa kitendo hicho cha ubakaji',.alisema Mwenyekiti

Aliendelea kusema 'ilipofika usiku mama akastuka mbona mpaka sasa simwoni mwanangu ndipo  aliamua kwenda mashineni kumfuata na alipomuuliza Yule msagaji akamwambia nilishamuagiza muda mrefu aje umpe hela'.mwenyekiti alisimulia

Mwenyekiti alisema Mtuhumiwa alikamatwa usiku huo na kupelekwa katika ofisi ya kijiji hadi asubuhi na kupelekwa  kituo kidogo cha polisi Dareda.

Mama mzazi wa mtoto aliefanyiwa kitendo hicho Maria Domisiana amesema akiwa na majirani wakimtafuta alikumkuta mtoto wake akiwa na matope kichwani na alipomuuliza umepatwa na tatizo gani ndipo alipoanzanza kumsimulia kuwa alikutana   na Salao akamwambia twende tukachukue ndoo ya mama ana alipokataa akamkamata kwa na kmpeleka katika shamba la shule na kuanza kumvua nguo huku akimng'ata na kasha kumbaka huku akiwa amemziba mdomo.

Mganga mfawidhi wa hospitali ya Dareda Josef Lorry amesema kuwa mtoto huyo amepata ugonjwa wa Fistula kati ya sehemu yake ya haja ndogo na kubwa.

Lorry  amesema tukio hilo limemuathiri  mtoto huyo  kisaikolojia lakini pia athari za kihisia na kimaumbile kwa sababu ya kuharibiwa sehemu zake za siri.

Mtoto huyo kwa sasa yupo katika hospitali ya Wilaya, Dareda akiendelea kupata matibabu baada ya kufanyiwa upasuaji wa kumrudishia hali yake ya kawaida

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo


Job Opportunity at Brac Tanzania, Project Officer

Job Opportunity at Brac Tanzania, Product Development Officer

Job Opportunity at Brac Tanzania, Regional Project Officer

Job Opportunity at FHI 360 Tanzania, Senior Technical Specialist

Tailors and Sewing Teachers - Volunteer

Job Opportunity at CVPeople Africa, Administrator

Job Opportunity at Zanzibar College of Business & Management, Secretarial Position

Call for Application, CIVE Internship Programme at University of Dodoma (UDOM)

Nafasi zingine ingia www.ajirayako.co.tz

Tetesi za Barnaba Kurudiana Kimapenzi na Mama Steve, Ukweli Huu Hapa


Mzazi mwenza wa staa wa Bongo fleva anayefanya vyema na ngoma yake ya 'Chausiku' Barnaba Boy Classic, Zubeda amekataa kabisa Kurudisha Penzi kwa Baba watoto wake huyo.

Zubeda na Barnaba walikuwa Kwenye Mahusiano ya Kimapenzi kwa miaka mingi na hata kujaaliwa kuzaa mtoto mmoja wa kiume lakini penzi lao lilivunjika na kila mmoja kushika njia yake.

Siku chache zilizopita kulikuwa kuna tetesi kuwa wawili hao wameweka tofauti zao pembeni na kuamua kuwa pamoja tetesi ambazo Zubeda amezikataa na kudai hawezi kurudi kwa mzazi mwenziye kwa sababu kila mtu ana maisha yake mengine.

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Zubeda alisema kila mtu kwa sasa yuko kwenye uhusiano wa kimapenzi na wanaheshimiana katika hilo kilichobaki kwao kubaki kama wazazi na hakuna lingine zaidi ya hilo kwa sababu tangu wametengana ni muda mrefu sasa.

Watu wanadai tu kuwa nimerudi kwa Barnaba, lakini sio kweli kabisa yule ni mzazi mwenzagu tu na ataendelea kuwa hivyo na si kitu kingine kwa sababu nina mtu wangu na yeye ana mtu wake kilichobaki ni heshima tu ya mzazi mwenzangu".

Kidomo Domo Chawaponza Yanga Wachapwa Tena Kipigo cha Mbwa Mwizi na Gor Mahia

YANGA wameendeleza mwendo ambao siyo mzuri katika michuano ya kimataifa baada ya kuruhusu kupata kichapo kutoka kwa Gor Mahia cha mabao 3-2 kwenye mchezo wa hatua ya makundi wa Kombe la Shirikisho Afrika. Yanga wameshacheza michezo minne hadi sasa kwenye Kundi D ambalo lina timu nyingine ambazo ni USM Algers ya Algeria na Rayon Sports ya Rwanda, lakini hawajapata ushindi kwenye mchezo hata mmoja.

 Matokeo ya mchezo wa jana yanamaanisha kuwa sasa Yanga wamebakiza michezo miwili tu kwenye kundi lao na hawana matumaini ya kufuzu. Katika michezo miwili ambayo Yanga wamekutana na Gor Mahia hivi karibuni, wamefungwa jumla ya mabao saba, baada ya mchezo wa kwanza kufungwa 4-0 jijini Nairobi.

 Katika mchezo wa jana, kipa wa Yanga, Youth Rostand alifanya makosa kadhaa ambayo yalichangia mabao mawili ya mwanzo ya Gor Mahia.

Rostand alifanya kosa katika sekunde ya 35 tangu kuanzia kwa mchezo hu ambapo aliucheza mpira vibaya uliopigwa kichwa na George Ogutu na kujaa wavuni.

Hata hivyo, aliendelea kufanya makosa ya mara kwa mara ambapo dakika ya 41 kipa huyo aliudaka mpira akaurusha vibaya kabla haujaguswa na mchezaji mwingine akaudaka tena, mwamuzi akaamuru kuwa ni faulo ambapo Jacques Tuisenge aliifungia timu hiyo bao la pili.

 Dakika ya 55, Deus Kaseke, ambaye alicheza mchezo wake wa kwanza tangu asajiliwe na Yanga, hivi karibuni aliifungia timu yake bao moja baada ya kipa wa Gor Mahia, Boniface Oluoch kuutema mpira.

 Hata hivyo, matumaini ya Yanga hayakudumu kwani dakika ya 64, Gor Mahia walifunga bao la tatu kupitia kwa Haron Shakava baada ya mabeki wa Yanga kufanya uzembe. Dakika ya 75, Yanga walimtoa Rostand na nafasi yake kuchukuliwa Beno Kakolanya ambapo wakati anatoka mashabiki walikuwa wakimzomea.

 Dakika tano baadaye Raphael Daudi aliifungia timu hiyo bao la pili baada ya kipa kushindwa kukoa shuti lililopigwa na Ibrahim Ajibu. Hata hivyo, kocha wa Yanga, Mwinyi Zahera hakuonekana kwenye mchezo huo ambapo Noel Mwandila ndiye alikuwa anatoa maelekezo kwenye benchi.

Zimbabwe wanafanya uchaguzi mkuu leo, Mzee Mugabe akisaliti chama chake cha ZANU-PF


Wananchi nchini Zimbabwe leo Julai 30, 2018 wanafanya uchaguzi mkuu wa urais, serikali za mitaa na wabunge. Uchaguzi huo unakuwa wa kwanza katika historia ya Taifa hilo kufanyika bila kuwepo kwa kiongozi wa muda mrefu Robert Mugabe. Wagombea wakuu wenye nguvu katika uchaguzi huo wa urais ni Rais wa Sasa Emmerson Mnangagwa wa chama tawala cha Zanu-PF na kiongozi wa upinzani Nelson Chamisa.
Chamisa (40) ambaye anakiwakilisha Chama Cha Movement For Democratic Change (MDC) ameonekana kuwashawishi watu wengi hususani vijana nchini humo.
Kwa upande mwingine, Mzee Robert Mugabe jana Jumapili Julai 29, 2018 akizungumza na waandishi wa habari nyumbani amewashangaza watu wengi hususani wanachama wa Chama Cha ZANU-PF baada ya kusema kuwa atampigia kura kiongozi wa upinzani.
Akifunga Kampeni hapo jana Rais Mnangagwa (75) almaarufu kwa jina la MAMBA ameahidi kufanya mageuzi ya kiuchumi ikiwemo kutoa ajira kwa vijana.
Naye, Chamisa akiahidi kuijenga upya Zimbabwe ambapo alisikika akitilia mkazo wa kulibadilisha jina la Zimbabwe Kama alivyoahidi kwenye Kampeni zake zote alizofanya akidai jina la sasa lina laana.
The post Zimbabwe wanafanya uchaguzi mkuu leo, Mzee Mugabe akisaliti chama chake cha ZANU-PF appeared first on Bongo5.com.

Source

Sunday, July 29, 2018

Zitto Kabwe na Mbunge Bwege wamuibukia Rais Magufuli, wadai ameirudisha nyuma Tanzania (+video)

Mbunge wa Kigoma Mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo, Zitto Kabwe na mwezie Mbunge wa Kilwa Kusini, Selemani Bungara wamedai kuwa Tanzania ya sasa imekuwa kama ile ya Mwaka 1992 ambayo chama ilikuwa na Chama kimoja. Wakihutubia Wananchi katika viwanja vya Mkapa Garden mjini Kilwa Masoko jioni ya Leo Julai 29, 2018 wamesema kuwa kwa sasa CCM …

The post Zitto Kabwe na Mbunge Bwege wamuibukia Rais Magufuli, wadai ameirudisha nyuma Tanzania (+video) appeared first on Bongo5.com.


Source

Hii ndio show kali zaidi ya Diamond Platnumz kuwahi kutokea, awaimbisha kiswahili Wafaransa kisiwani Mayotte (picha+video)


Kwa sasa ukitaja majina ya wasanii 10 bora wanaofanya vizuri barani Afrika huwezi kuacha kumtaja Diamond Platnumz hii ni kutokana na kuongezeka kwa wigo mpana wa mashabiki wake.


Julai 28, 2018 Diamond Platnumz alikuwa katika visiwa vya Mayotte nchini Ufaransa ambapo aliweza kutumbuiza nyimbo zake zote tena zile ambazo hajafanya kolabo na jambo la kufurahisha licha ya asilimia 99% ya wananchi wa Mayotte kuzungumza Kifaransa lakini waliweza kuimba naye nyimbo zote kwa kiswahili.


The post Hii ndio show kali zaidi ya Diamond Platnumz kuwahi kutokea, awaimbisha kiswahili Wafaransa kisiwani Mayotte (picha+video) appeared first on Bongo5.com.

Source

Jux na Vanessa Mdee watangaza balaa lingine kwa mashabiki wao wa DR Congo, Rwanda na Burundi


Wakati mashabiki wa Vanessa Mdee na Jux nchini Tanzania wakiendelea kukata kiu ya burudani kupitia tamasha la wawili hao linalokwenda kwa jina la ‘In Love and Money Tour’, tayari wawili hao wametangaza habari njema kwa mashabiki wao wanaoishi nje ya nchi. Habari yenyewe ni kwamba wawili hao wameahidi kufanya ziara yao hiyo ya muziki nchini …
The post Jux na Vanessa Mdee watangaza balaa lingine kwa mashabiki wao wa DR Congo, Rwanda na Burundi appeared first on Bongo5.com.

Source

Rubani wa Boeing 787-8 Dreamliner afunguka viwanja ambavyo ndege hiyo inaweza kutua nchini Tanzania (+video)

Wakati Watanzania wakifurahia kuanza kwa safari za ndege ya Boeing 787-8 Dreamliner nchini Tanzania, ni vyema ungefahamu viwanja vya ndege hapa nchini Tanzania ambavyo ndege hiyo inaweza kutua. Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo jijini Mwanza kuhusu viwanja hivyo, Muongozaji wa ndege hiyo Kaptaini Richard Shaidi amesema ndege hiyo kwa sasa inaweza kutua Viwanja …

The post Rubani wa Boeing 787-8 Dreamliner afunguka viwanja ambavyo ndege hiyo inaweza kutua nchini Tanzania (+video) appeared first on Bongo5.com.


Source

Rais Dkt Magufuli afanya uteuzi na kuwahamisha vituo vya kazi viongozi wa Mikoa, Wizara na Wilaya




Source

Saturday, July 28, 2018

CCM Watangaza Kumpokea Rasmi Mwita Waitara, Tazama Hapa Alichokisema Polepole


Chama cha Mapinduzi CCM Kimetangaza kupokea rasmi Maombi ya Mbunge wa jimbo la ukonga kupitia CHADEMA kujiunga na chama hicho muda mfupi baada ya mbunge huyo kutangaza kujivua uanachama na nafasi zake zote kisha kujiunga CCM .


Akizungumza mbele ya vyombo vya habari katika ofisi za makao makuu CCM Limumba jijini Dar- es Salaam , Katibu wa itikadi na uenezi wa CCM Humphrey Polepole ameeleza kuwa Chama cha mapinduzi kinathamini sana mchango wa mbunge huyu kwani amekuwa ni mbunge anayeamini katika kusimamia ukweli.


Polepole  amesema pamoja na ndugu Mwita Waitara kuacha dhamana ya ubunge, mshahara,  na marupurupu yake, CCM kinatangaza rasmi moja kwa moja kuazia leo hii kitampeleka kwa watanzania kwa ajili ya kusema ukweli wote kwa kuwa ameonesha ujasiri mkubwa kisiasa.


"Wapo wengine ambao wangalikubali wauache ukweli wayaishi maslahi lakini wapo viongozi wachache ambao wapo radhi kupoteza yao ila umma upate kwa hiyo mimi nikupongeze sana ndugu Waitara" amesema Polepole.


Amesema baada ya kupata taarifa za mbunge huyo amezungumza na viongozi wa CCM akiwemo Katibu Mkuu Bashiru Ally, ambaye amempongeza sana Waitara kwa kujiamini kwake na kusimamia ukweli, hivyo CCM itaanza kwenda naye maeneo tofauti kwa hatua ya awali hasa kwenye maeneo ambayo kampeni za uchaguzi mdogo unafanyika ikiwemo jimbo la Buyungu mkoani Kigoma.


Polepole ameongeza kuwa wana-CCM wanayofuraha kushirikiri na Waitara katika kampeni zinazoendelea, na baada ya hapo atapata utambulisho na makaribisho rasmi ya wana-CCM wenzake katika eneo analoishi.


Awali akizungumza mbele ya Waandishi wa habari ndugu Waitara alisema moja kati ya vitu vilivyomuondoa ndani ya chama CHADEMA ni ugomvi wake na Mbowe ndani ya chama.


"Mimi nimeona kabla hawajanipiga chini nijiondoe mwenyewe. Sasa ndani ya CHADEMA, ukionekana na mtu wa CCM unaulizwa kwa nini unaonekana na watu hao. Mimi shida yangu siyo CCM shida yangu ni kuona wananchi wangu wa Ukonga wanatatuliwa shida zao. Wananchi wa Ukonga wavumilie natafuta namna bora ya kuweza kuwa na viongozi wa serikali bila kuhojiwa kama nimefumaniwa na mke wa mtu. Nimetaka kuwa huru" aliongeza. Waitara.


Ikumbukwe kuwa mwaka 1998 Mwita Waitara aliwahi kuwa mwanachama wa CCM  kisha kuhamia CHADEMA lakini leo hii amerejea tena CCM kwa mara nyingine akiwa miongoni mwa wabunge machache machachari wa upinzani waliotikisa kwa hoja nzito katika bunge 11.

Video: Jabu The Great – Maringo

Msanii wa muziki, Jabu M Maliamungu 'Jabu The Great' baada ya kufanya vizuri na video ya wimbo wake, My Women. Wiki hii ameachia video ya wimbo wake mpya uitwa ‘Maringo’. Video imeandaliwa na director Maji ya Vuguto. Muimbaji huyo ambaye ni raia wa Congo huku mama yake akiwa na asili ya Tanzania, amesema kabla ya …

The post Video: Jabu The Great – Maringo appeared first on Bongo5.com.


Source

Steve Nyerere awacharukia wanaombeza kukosa U-DC


Baada ya mwanamitindo Jokate Mwegelo pamoja na aliyekuwa msemaji wa Yanga Jerry Murro kuteuliwa na Rais Magufuli kuwa Wakuu wa Wilaya, mashabiki na wadau katika mitandao ya kijamii wanambeza Steve Nyerere kwa kuwa amekosa kuteuliwa. Muigizaji huyo amekuwa akionekana katika matukio mengi akitetea utendaji wa Rais Magufuli hali ambayo iliwajenga picha mashabiki hao kwamba anataka …
The post Steve Nyerere awacharukia wanaombeza kukosa U-DC appeared first on Bongo5.com.

Source

Video: Karen aeleza baba yake Gadner alivyompa masharti kwenye muziki, amtaja Jaydee

Binti Karen ambaye ni mtoto wa Gardner G Habashi mtangazaji mahiri wa Clouds FM, amefunguka kuzungumzia safari yake mpya kwenye muziki huku akidai kwamba ilikuwa ngumu kwa baba yake huyo pamoja na Mama yake kumruhusu kuingia kwenye muziki. Pia muimbaji huyo amemtaja mama yake mlezi, Lady Jaydee jinsi alimfanya kuwamsanii mzuri.

The post Video: Karen aeleza baba yake Gadner alivyompa masharti kwenye muziki, amtaja Jaydee appeared first on Bongo5.com.


Source

Ney wa Mitego Apaokonywa Magari 2 ya Mkopo, ni Baada ya Kushindwa Kulipa

Msanii nguli wa Hip Hop, Emmanuel Elibarik maarufu kama Ney wa Mitego anadaiwa kupokonywa magari mawili aliyokuwa ameyachukua kwa mkopo baada ya kushindwa kurejesha mkopo huo

VIDEO:

Video: Diamond apokewa kifalme Mayotte, akabidhiwa mrembo

Msanii wa muziki na rais wa WCB, Diamond Platnumz amepokewa kama mfalme katika kisiwa cha Mayotte ambapo anatarajia kufanya show ya nguvu weekend hii baada ya kumaliza tour yake ya Marekani. THANK YOU MAYOTTE!!! YOU GUYS MADE ME FEEL LIKE , AM AT HOME!!! I CAN'T WAIT TO PARTY WITH TOU TONIGHT!!!🙏🏻🙏🏻 #ABoyFromTandale #WCB4LIFE A …

The post Video: Diamond apokewa kifalme Mayotte, akabidhiwa mrembo appeared first on Bongo5.com.


Source

Timbulo awashangaa wadau wa muziki ‘huwezi shangaa mimi kumiliki IST’

Msanii wa muziki, Timbulo amesikitishwa na kitendo cha baadhi ya wadau wa muziki nchini Tanzania kushangaa mafanikio yake baada ya kusikia kwamba kuna watu wanaona hastahili kumiliki vitu kama nyumba na magari. Akiongea katika kipindi cha The Playlist cha Time Fm, Timbolo alidai wasanii wa watanzania wanatakiwa kuwa na mali nyingi sio watu kushangaa yeye …

The post Timbulo awashangaa wadau wa muziki ‘huwezi shangaa mimi kumiliki IST’ appeared first on Bongo5.com.


Source

Wengi washuhudia kupatwa kwa mwezi

Mamilioni ya watu duniani wameshuhudia tukio la kihistoria la kupatwa kamili kwa mwezi. Tukio hilo la muda mrefu zaidi katika karne hii limeshuhudiwa usiku wa kuamkia leo wa Julai 27 mwaka 2018 huku nchini Tanzani na Barani Afrika kwa ujumla, Australia, Asia, Ulaya na Amerika Kusini. Kupatwa huko kwa mwezi kumedumu kwa takriban saa 1 …

The post Wengi washuhudia kupatwa kwa mwezi appeared first on Bongo5.com.


Source

Real Madrid kuanza ligi bila mshindi wa tuzo ya Ballon d’Or

Klabu ya Real Madrid kwa jna la utani wakijulikana kama Los Blancos kutoka nchini Uhispania,ambao ni mabingwa wa mara 33 wa ligi hiyo pia washindi wa mara 13 wa ligi ya mbaingwa barani ulaya UEFA. Kwa mara ya kwanza tangu Florentino Perez awe rais wa klabu hiyo wanatarajia kuanza msimu mpya wa ligi 2018/2019 bila …

The post Real Madrid kuanza ligi bila mshindi wa tuzo ya Ballon d’Or appeared first on Bongo5.com.


Source

Soma Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Leo


Bonyeza links kusoma zaidi

2 Job Opportunities at Right To Play, Field Facilitators

Job Opportunity at Right To Play, Project Officer

Job Opportunity at Right To Play, Training Officer

Job Opportunity at Mohammed Enterprises Tanzania Limited - MeTL, Human Resources Officer

Job Opportunity at Kilimanjaro Dairy Cooperative, Marketing & Sales Officer

Job Opportunity at Kilimanjaro Dairy Cooperative, Dairy Specialist

Job Opportunity at Shugulika Recruitment, Operations Manager (Sales & Marketing)

Job Opportunity at Blue Recruits, Senior Procurement Specialist

Job Opportunity at Blue Recruits, Senior Environmental and Social Specialist (Energy sector)

Job Opportunity at Duma Works

Nafasi zingine ingia www.ajirayako.co.tz

Friday, July 27, 2018

Ukiamua Kuwa na Mahusiano na Mume wa Mtu Lazima Ukubali Kuwa Mtumwa wa Mambo Yafuatayo


“Wasanii Tupunguze Kiki Tufanye Kazi Zaidi”- Irene Paul


Muigizaji wa Bongo movie Irene Paul ameibuka na kuwashauri wasanii wenzake kuachana na kiki na kuanza kufanya kazi zao za sanaa kwa nguvu zaidi.

Wasanii wengi wamekuwa na mtindo wa kutengeneza skendo fulani (kiki) ziwe za kimapenzi au bifu lakini skendo zitakaziweza kuwaletea attention fulani kutoka Kwa vyombo vya habari au mitandao ya kijamii ili watakapotoa kazi zao zifanye vizuri.

Irene Paul amewataka wasanii wenzake kuacha kuzidisha sana kiki kama njia ya kutafuta attention kwani inakuwa inaharibu kazi zao kwani jitihada hivyo ya kiki wangeielekeza katika kutengeneza kazi Debye unitary basi mambo yangekuwa mazuri;

Nafikiri tumesha hustle sana Kwenye hii gemu kwa njia tofauti na umri haurudi nyuma bali unasogea so I think it's about time tufanye kazi zaidi kwani ndio kitu pekee kilichobaki.

Waliojiuza wamejiuza sana na waliokaa uchi wamekaa uchi sana na waliotengeneza skendo wametengeneza skendo za kutosha lakini wamepata nini out of it?.

Lakini pia Irene Paul amewataka Bongo movie wenzake waelekeze nguvu zao Kwenye kufanya kazi zaidi ili kuitudisha Bongo movie Kwenye ramani:

Umefika wakati tufanye kazi Bongo Movie Industry sio ya kipindi kile wakati inaanza kuna mapinduzi makubwa twende na wakati Tanzania tuna vipaji lakini tuna lack Knowledge na ubunifu kwaiyo cha muhimu kufanya kazi kwa bifu bidii ili kufika malengo".

BASATA watema cheche baada ya kumzuia Diamond kusafiri nje ya nchi ‘tumefanya kwake liwe fundisho kwa wengine’


Baraza la Sanaa Taifa, (BASATA) Julai 26, 2018  lilimzuia msanii wa muziki, Diamond Platnumz kwenda kufanya show nje ya nchi akiwa katika uwanja wa Mwl. JK Nyerere jijini Dar es salaam huku likieleza sababu kuwa hakuwa na kibali kutoka kwao cha kwenda kufanya show nje ya nchi.

Akielezea sakata hilo Katibu Mtendaji wa BASATA, Godfrey Mngereza amesema kuwa kwa sasa kuna utaratibu mpya ambao msanii akitaka kwenda kufanya show nje ya nchi ni lazima apitie BASATA wampe kibali na kisha akirudi pia anatakiwa kuripoti kwao.

BASATA wamesema wamemzuia Diamond ili liwe fundisho kwa wasanii wengine ambao wanamazoea ya kwenda nje ya nchi kufanya matamasha bila kila kibali kutoka kwao.


Utaratibu wa msanii kuwa na kibali anapoenda nje, yaani kutambua wapi anaelekea kikazi si mpya. Upo katika kanuni toka awali. Lengo ni kumhakikisha ulinzi wa haki na usalama wake pale kutakapotokea suala lisilo rafiki. Pia, kumuaga kwa kukabidhi bendera na mapokezi pindi anaporudi ikibidi,“amesema Mngereza kwenye mahojiano yake na TBC na kusisitiza kwanini wamemchukulia Diamond hatua hiyo.
Tumefanya hivi ili liwe fundisho kwa wasanii wetu wengine ambao bado wanakiuka jambo hili, wasanii wetu wanapoandaa vitu vya kwenda navyo vya kwenda kuonesha show nje ya nchi pale wanapoandaa tamasha. Tunawaasa wapitie taratibu, Kanuni na sheria za BASATA wala sio ngumu kiasi hicho.“amemaliza Mngereza.

Hata hivyo, Diamond Platnumz na timu yake alifanikiwa kuondoka nchini jana usiku na anatarajiwa kesho kutumbuiza katika visiwa vya Mayotte nchini Ufaransa.

Aunty Ezekiel Atoa Tamko, Hata Kama Wema Hataenda, yeye South Africa Ataenda Tu.


Aunty Ezekiel Atoa Tamko, Hata Kama Wema Hataenda, yeye South Africa Ataenda Tu.
Mwanadada Aunty Ezekiel amefunga mjadala uliokuwa ukiendelea baada ya kusemwa kwa maneno ya muda mrefu kuhusu uamuzi wa Diamond kuwataka yeye pamoja na Wema kwenda afrika ya kusini katika sherehe ya Tiffah.

Tamko la kwenda afrika ya kusini lilitolewa na Diamond mwenyewe na kusema kuwa katika watu kumi watakaokwenda ni lazima awepo Wema na Zari na ndipo Zari alipoanza kuwajibu katika mitandao kuwa hataki kuona watanzania watamchafulia nyumba.

Hata hivyo wengi walihisi kuwa tamko la Zari lingeweza kubadilisha mawazo ya wahusika lakini Aunty Ezekiel ameamua kujibu na kusema kuwa hata kama Wema hatokwenda Afrika ya kusini lakini yeye ataenda kwa sababu yeye ni  moja ya wanafamilia , lakini pia Zari pia ni wifi yake.

Ifike sehemu inabidi  tufunge mjadala maana kila siku ni aunt kuwa karibu na zari,wema na kama ni bethdei nitaenda tu.Hawa wote ni marafiki zangu kwa hiyo sasa siwezi kubagua eti kwa sababu wema aliachana na Diamond  wakati pia kule kwa Diamond kuna penzi wangu Iyobo  na isitoshe kwa upande mwingine Zari ni wifi yangu.

JEURI YA PESA: Diamond kutumia mil. 150 kwenye Birthday ya Tiffah, Harmonize akifanya ‘shopping’ ya mil. 100 Afrika Kusini

Kwa sasa ukizungumzia wasanii wenye fedha nchini Tanzania huwezi kuacha kuwataja Harmonize na Diamond Platnumz, na hili linaonekana wazi hata kwenye matumizi yao ya kawaida. Siku za hivi karibuni Diamond Platnumz ametangaza kuwapeleka watu 50 kutoka Tanzania kwenda Afrika Kusini ambapo kati ya watu hao 30 ni mashabiki wake na 10 watakuwa ni wanakamati wa …
The post JEURI YA PESA: Diamond kutumia mil. 150 kwenye Birthday ya Tiffah, Harmonize akifanya ‘shopping’ ya mil. 100 Afrika Kusini appeared first on Bongo5.com.

Source

Beyoncé shares new photos of Rumi & Carter!

Beyoncé and JAY-Z are sharing their adorable twins with the world. Rumi and Sir Carter made a rare appearance in a new photo posted on Beyoncé's official website. In the pic, a smiling Bey holds her 13-month-old babies in her lap while vacationing in Europe during the "On the Run II Tour." This is only …

The post Beyoncé shares new photos of Rumi & Carter! appeared first on Bongo5.com.


Source

Diamond Azuiwa Kwenda Kufanya Shoo Nje Akiwa Uwanja wa Ndege.

Baraza la Sanaa la Taifa, limemzuia Diamond Platinumz kwenda kufanya show nje ya nchi akiwa katika uwanja wa ndege wa kimaitafa wa mwl julius kambarage nyerere huku sababu kubwa ikiwa ni kwamba msanii huyo kukosa kibali cha kwenda kufanya show hiyo.
Akiongea na TBC  kaimu katibu mtendaji Onesmo Mabuye anasema kuwa Diamond amezuiwa kutokana na kukosa kibali cha BASATA cha kufanya show za nje.

Aunty Ezekiel: Wema Alinifanya Nimjue Iyobo


Aunty Ezekiel amefunguka na kuelezea jinsi alivyokutana na mzazi mwenzie moze iyobo ambae mpaka sasa wapo wote na wamekuwa pamoja katika kujenga familia.
Aunty anasema kuwa katika watu wakiosababisha mahusiano yake na moze kuendelea ni wema sepetu kutokana na ukweli kuwa kama asingekuwa na urafiki na wema na akawa anaenda kwa wema basi asingekutana kabisa na Iyobo.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...