Monday, March 20, 2023

Rais Ruto Sasa Asema Yuko Tayari Kwa Mazungumzo na Viongozi wa Upinzani



Rais William Ruto amesema kuwa yuko tayari kufanya mazungumzo yatakayo mnufaisha Mkenya wa kawaida
Ruto amesema kuwa hatoshurutishwa na kiongozi yeyote kufanya mazungumzo yanayolenga kunufaisha mtu binafsi
Awali kinara wa Azimio Raila Odinga alikuwa ameashiria kuwa mazungumzo yoyote yatafanyika baada ya maandamano ya Jumatatu 20


Rais William Ruto ameonekana kulegeza kamba kuhusu uwezekano wake wa kufanya mazungumzo na viongozi wa upinzani baada ya kusema kuwa yuko tayari kufanya mazungumzo yatakayoleta manufaa kwa taifa.


Rais William Ruto amesema yuko tayari kwa mazungumzo. Picha Twitter. Chanzo: Twitter
Ruto aliyesema kuwa hatoshurutishwa wala kutishwa ili kukubali mazungumzo alisema afisi yake inakaribisha kiongozi yeyote anayepania kufanya mazungumzo kwa manufa ya wananchi wa Kenya.

"Niko tayari kwa mazungumzo na viongozi wengine iwapo majadiliano yetu yatahusu maisha ya usoni ya taifa hili na yatazingatia sheria na kanuni zilizowekwa kikatiba," Rais alisema wakati wa ibadaa ya maombi Kapsabet.

Rais katika mazungumzo yake alionekana kumnyoshea kidole cha lawama kinara wa Azimio Raila Odinga na kumtaja kama kiongozi anayependa vurugu.


Ruto amesisitiza kuwa hatafanya mazungumzo na vyongozi wenye nia fiche na ambao ajenda yao kuu ni ya kujinufaisha wao binafsi na wala si ya kunufaisha Wakenya.

"Hatutakubali serikali isio na sheria zinazopaswa kufuatwa. Hamtatushia kwa kutupa makaata na kutumia vita ili kutushurutisha na mambo mnayoyafanya basi iwapo tutakubaliana nanyi tutakuwa tunazawadi ukaidi na hilo halitowezekana," Rais aliongezea.
Rais Ruto na viongozi wengine wa Kenya Kwanza siku za hivi karibuni wamekuwa wakishikilia kuwa hawatofanya mazungumzo ya maradhiano haswa na Odinga wakitaja ajenda ya kinara wa Azimio kama ya kibinafsi.

Viongozi wa makanisa akiwemo Askofu wa kanaisa Katoliki Philip Anyolo wamewaomba viongozi hawa wawili kuweka tofauti zao kando na kufanya mazungumzo yatakayohakikisha kuwa taifa linapata utulivu na linakosa migawanyiko.

Kwa upande wake kinara wa Azimio katika mahojiano na runinga ya Citizen alisema kuwa iwapo kutakuwa na mazungumzo ya aina yoyote basi yatafanyika baada ya maandamo ya Jumatatu 20.

Sunday, January 9, 2022

Country boy aondoka Konde Gang

upitia akaunti ya Konde Gang wameandima ujumbe huu:- TAARIFA: Mkataba Kati Ya Konde Music Worldwide Na @countrywizzy_tz Umemalizika Hii Leo Tar 8 January 2022. Kuanzia Leo Country Wizzy Atakuwa Msanii Anaejitegemea Baada Ya Kufikia Makubaliano Ya Pande Zote Mbili. Konde Music Worldwide Inamtakia Kila Lenye Kheri Country Wizzy Kwenye Career Yake Ya Music Pamoja Na …

The post Country boy aondoka Konde Gang appeared first on Bongo5.com.

Yasome Hapa Magazeti ya Leo Jumapili, Januari 9, 2022

Hapa tumekusogezea kurasa za mbele na za nyuma za magazeti yote ya Tanzania leo Januari 9, 2022 Usipitwe na Matukio, Install App Yako ya Kijanja...

The post Yasome Hapa Magazeti ya Leo Jumapili, Januari 9, 2022 appeared first on Global Publishers.

Orodha ya Mawaziri walioteuliwa na Rais Samia

Rais Samia afanya mabadiliko ya baraza la mawaziri na kubuni wizara mpya Akitangaza mabadiliko hayo, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Hussein Kattanga amesema Rais amefanya mabadiliko ya muundo katika wizara tatu. Rais Samia ”ameunganisha wizara tatu, iliyokuwa wizara ya uwekezaji iliyokuwa chini ya ofisi ya Waziri Mkuu na pia ameunganisha wizara ya biashara moja ambayo itaitwa …

The post Orodha ya Mawaziri walioteuliwa na Rais Samia appeared first on Bongo5.com.

Saturday, January 8, 2022

Simba Queens Yaichakaza Vibaya Yanga Princes

SIMBA Queens imeendeleza rekodi ya ubabe mbele ya Yanga Princess kwa kuendeleza vipigo kwenye msimu wao wa nne mfululizo baada ya kuibuka na ushindi wa...

The post Simba Queens Yaichakaza Vibaya Yanga Princes appeared first on Global Publishers.

Achomwa Moto na Rafiki Yake Kisa Mke

Daud Emanuel (27) mkazi wa Chamwino Manispaa ya Morogoro, amenusurika kifo baada ya kumwagiwa mafuta ya petroli kisha kuchomwa moto na rafiki yake aliyefahamika kwa...

The post Achomwa Moto na Rafiki Yake Kisa Mke appeared first on Global Publishers.

Rais Samia afanya mabadiliko ya baraza la mawaziri na kubuni wizara mpya

Rais wa Tanzani Samia Suluhu amefanya mabadiliko ya baraza la mawaziri na kubuni wizara mpya

Barabara Ndefu Zaidi Duniani Chini ya Ziwa Yaanza Kufanya Kazi

IKIWA ni takriban miaka minne ya ujenzi, barabara ndefu zaidi ya chini ya maji nchini China, hatimaye barabara hiyo imeanza kutumika kwa kupitisha magari chini...

The post Barabara Ndefu Zaidi Duniani Chini ya Ziwa Yaanza Kufanya Kazi appeared first on Global Publishers.

Je ni yapi manufaa viliyoyapata vyama vya upinzani Tanzania kwa kujiuzulu kwa Spika Ndungai?

Kung'atuka madarakani kwa Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai mnamo Januari 6, 2022 kumetajwa kuwa ni matokeo ya mwenendo wake na ndiye chanzo cha kuporomoka utendaji bora wa bunge miongoni mwa madoa ambayo yamechafua uongozi wake.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...