Wananchi wa mikoa ya Kusini( Lindi na Mtwara) wameombwa kutumia maonesho ya nane nane na kanda ya ujenzi ya kanda ya Kusini kupata msaada wa kitaalamu wa mambo mbalimbali yahusuyo shuguli za maendeleo.
Wito huo ambao ni habari njema kwa wananchi wa kanda ya hii ulitolewa jana na Luteni Kanali Juma Mrai alipozungumza na Muungwana Blog katika viwanja vya Ngongo, manispaa ya Lindi, yanapofanyika maonesho ya wakulima( Nanenane) kanda ya Kusini.
Luteni Kanali Mrai ambae amemuwakilisha mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa ( JKT) alipotembelea mabanda ya maonesho ya jeshi hilo wajifunze kupitia mambo wanayoyaona katika mabanda hayo, ili maonesho hayo yawanufaishe.
Katika maonesho hayo, alisema wananchi hawanabudi kutumia kanda hiyo ya ujenzi kupata ushauri wa kitaalamu katika shughuli zao za maendeleo na ujenzi wa taifa.
Alisema jeshi hilo ni mali yao na lipo kwa ajili yao, kwahiyo wana haki na sababu ya kulitumia, Ikiwemo kupata ushauri kuhusu kilimo, ufugaji, uvuvi na fani nyingine zinazoweza kuwafanya wanufaike na kazi wanazofanya.
Mbali na kutoa ushauri, kamanda huyo alisema kanda ya ujenzi ina toa huduma za ujenzi kwa taasisi za umma,taasisi binafsi na mtu mmoja mmoja. Hivyo wasisite kuwatumia katika kazi zao.
''Waendelee kuliamiani jeshi lao, kwani gharama za ujenzi ni nafuu, watakamilishiwa kazi zao kwa wakati, kwamujibu wa mikataba na kwa ubora,'' alisisitiza kamanda Mrai.
''Lakini pia wananchi wanapata fursa ya kuona vijana wao kupitia jeshi lao wanafanya nini. Kwani ni dhahiri wanapata ujuzi na maarifa yanayoweza kuwafanya wajiajiri,'' alisema kamanda Mrai.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, imetupilia mbali shauri lililokuwa limefunguliwa na Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina...