Wananchi wa mikoa ya Kusini( Lindi na Mtwara) wameombwa kutumia maonesho ya nane nane na kanda ya ujenzi ya kanda ya Kusini kupata msaada wa kitaalamu wa mambo mbalimbali yahusuyo shuguli za maendeleo.
Wito huo ambao ni habari njema kwa wananchi wa kanda ya hii ulitolewa jana na Luteni Kanali Juma Mrai alipozungumza na Muungwana Blog katika viwanja vya Ngongo, manispaa ya Lindi, yanapofanyika maonesho ya wakulima( Nanenane) kanda ya Kusini.
Luteni Kanali Mrai ambae amemuwakilisha mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa ( JKT) alipotembelea mabanda ya maonesho ya jeshi hilo wajifunze kupitia mambo wanayoyaona katika mabanda hayo, ili maonesho hayo yawanufaishe.
Katika maonesho hayo, alisema wananchi hawanabudi kutumia kanda hiyo ya ujenzi kupata ushauri wa kitaalamu katika shughuli zao za maendeleo na ujenzi wa taifa.
Alisema jeshi hilo ni mali yao na lipo kwa ajili yao, kwahiyo wana haki na sababu ya kulitumia, Ikiwemo kupata ushauri kuhusu kilimo, ufugaji, uvuvi na fani nyingine zinazoweza kuwafanya wanufaike na kazi wanazofanya.
Mbali na kutoa ushauri, kamanda huyo alisema kanda ya ujenzi ina toa huduma za ujenzi kwa taasisi za umma,taasisi binafsi na mtu mmoja mmoja. Hivyo wasisite kuwatumia katika kazi zao.
''Waendelee kuliamiani jeshi lao, kwani gharama za ujenzi ni nafuu, watakamilishiwa kazi zao kwa wakati, kwamujibu wa mikataba na kwa ubora,'' alisisitiza kamanda Mrai.
''Lakini pia wananchi wanapata fursa ya kuona vijana wao kupitia jeshi lao wanafanya nini. Kwani ni dhahiri wanapata ujuzi na maarifa yanayoweza kuwafanya wajiajiri,'' alisema kamanda Mrai.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
