







Sehemu ya wananchi wakimsikiliza Mgombea Ubunge jimbo la Bunda Mjini Esther Bulaya kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Chuo Kukuu cha Namibia kitengo cha dawa ya mifugo kinawafundisha mbwa kubaini virusi vya corona kwa kunusa.
Mpango wa nchi hiyo ni kuwapelea nbwa hao katikaviwanja vya ndegena vituo vya mpakani, kwa mujibu wa mtandao wa The Namibian.
Mbwa wamethibitishwa kuwa na uwezo wa kubaini virusi vya corona kwa aslimia 95, mhadiri wa somo la tiba ya wanyama Alma Raath anasema.
Mradi huo ulianzishwa miezi miezi miwili iliyopita, inarsema taarifa ya mtandao huo wa The Namibian, lakini haujataja ni lini mbwa hao watakuwa tayari kufanya kazi.
Mtandao wa The Namibian unasema nchi hiyo itakuwa ya kwanza kutumia mbwa kubaini virusi vya corona.
Mshambuliaji wa klabu bingwa Tanzania Bara (VPL) na Kombe la Shirikisho (ASFC) Simba SC, Meddie Kagere amesema amesikitishwa na taarifa zilizosambaa mtandaoni kuwa amempiga kocha wa timu hiyo, Sevn Vandenbroeck.
Jana taarifa za Kagere kudaiwa kumpiga kocha huyo kisa kikiwa ni kutopangwa kikosi cha kwanza cha Simba zilizagaa kwa kasi mitandaoni, na kuripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari mapema hii leo.
Akizungumza na E.A Radio mapema hii leo, mshambuliaji huyo kutoka Rwanda alisema ameshangaa baada ya kuona mambo hayo yanasambaa wakati yeye hajafanya tukio hilo na yuko freshi kabisa na kocha.
"Kuna mambo huwa yanasemwa kuhusu mimi ambayo siyo ya kweli yenye lengo la kunichafua ndiyo maana sijawahi kuwajibu."
"Lilianza la hirizi nikanyamaza na sasa limekuja la mimi kupigana na kocha kitu ambacho siyo kweli. Tangu tumefika Mbeya hatujafanya mazoezi na leo muda huu ndiyo tunafanya sasa nashangaa sijui mwalimu nimempiga wapi," alisema Kegere.
Hata hivyo Uongozi wa Simba SC kupitia idara ya habari na mawasiliano umekanusha taarifa hizo kwa kusema hazina ukweli, zidi ya kutaka kuvuruga amani ndani ya kikosi chao ambacho kipo tayari kuanza kutetea taji la Tanzania Bara mwishoni mwa juma hili dhidi ya Ihefu FC.
Mkuu wa Idara hiyo Haji Manara amesema: "Wanasema jana ugomvi uliotokea mazoezini, lakini Simba hawakuwa na mazoezi baada ya mchezo wa ngao ya jamii, hizo ni propaganda za kuvuruga utulivu uliopo ndani na nje ya Simba, wakitaka itokee kama upande wa pili yanayoendelea"
"Kama idara ya Habari na Mawasiliano hatutokubali kuona watu wanaandika uzushi kuhusu Klabu yetu na tutachukua hatua kali dhidi ya watakaohusika"
MGOMBEA ubunge Iramba Mashariki Mkoa wa Singida kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Mwigulu Nchemba, ameanza kumchokonoa Tundu Lissu, mgombea urais kupitia Chadema na Lazaro Nyalandu, mgombea ubunge wa Singida Kaskazini.
Akizungumza kwenye kampeni za Dk. John Magufuli, mgombea urais wa Tanzania kupitia chama hicho katika Uwanja wa Bombadier mkoani Singida leo tarehe 1 Septemba 2020 amesema, wawili hao hawana uzalendo.
Bila kuwataja majina, Mwigulu alimnanga Nyalandu kwamba, alipokuwa waziri (Waziri wa Maliasili na Utalii katika serikali ya awamu ya nne) alikuwa akienda Ulaya kunyoosha suti zake huku Lissu akisema amerejea nchini baada ya kupewa 'advance' (malipo ya awali).
Lissu ndiye aliyerejea nchini akitokea kwenye matibabu nchini Ubelgiji, ni baada ya watu wasiojulikana kushamabuliwa kwa risasi 'Area D,' jijini Dodoma tarehe 7 Septemba 2017.
Mara kadhaa Lissu alinukuliwa na vyombo vya habari akiwa ughaibuni, kwamba alishindwa kurudi Tanzania kwa kuwa sio sehemu salama kwake.
"Wengine wanakuja hapa wanajifanya watoto wa Singida, hawana uzalendo hata na wana Singida. Kuna mmoja tulikuwa mawaziri wote, hata suti zake alikuwa anaenda kunyoosha Ulaya, hana uchungu na Singida.
"Mwingine alisema Tanzania sio salama, sasa hivi amekuja sababu 'advance' amechukua baada ya uchaguzi tu atasema, Tanzania haiko salama, ataondoka," amesema Dk. Mwigulu.
Dk. Mwigulu ambaye ni Waziri wa Katiba na Sheria, amewataka Watanzania kumchagua Rais Magufuli. "Ioneeni huruma Tanzania, wale wagombea wengine wote mimi nawafahamu na nikiangalia janja janja yao, naona hata 'advance' wamechukua, nchi yetu itauzwa mkimuacha Dk. Magufuli," amesema Dk. Mwigulu.