Thursday, September 17, 2020

NKULILA AZINDUA RASMI KAMPENI ZA UCHAGUZI CCM NDEMBEZI..AOMBA APEWE MITANO TENA

Mgombea udiwani kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM kata ya Ndembezi manispaa ya Shinyanga mkoani Shinyanga David Nkulila  akiwaomba wananchi wa kata hiyo wamchague tena kuwa diwani wa kata ya Ndembezi. 

Na Suzy Butondo - Shinyanga
Mgombea udiwani kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM kata ya Ndembezi manispaa ya Shinyanga mkoani Shinyanga David Nkulila  amewaomba wananchi wa kata hiyo wamchague ili aweze kuzimalizia changamoto zilizopo ikiwemo kujenga soko la Kisasa na barabara za kata hiyo.

Nkulila ameyasema hayo leo wakati wa uzinduzi wa kampeni za udiwani iliyofanyika katika kata hiyo na kuhudhuriwa na wanachama wa CCM na wananchi wa kata hiyo.

"Nawaomba sana  wananchi wangu tarehe 28 mwezi wa kumi mnichague Mimi katika kuwakilisha kata, mmchague Patrobas Katambi katika kuwakilisha jimbo pia mchagueni Rais wetu John Pombe Magufuli katika kupeperusha bendera ya Chama Cha Mapinduzi mzee wa kuleta maendeleo kwa nchi yetu", amesema Nkulila.

Nkulila amesema kauli mbiu yake ni kuwasaidia wanyonge na kusimamia wafanyabiashara wote waweze kutendewa haki akisaidiana na mbunge wake Katambi pamoja na Rais Magufuli.

Baadhi ya wananchi wanaoishi kata ya Ndembezi, Jenifer Mahona na Shija Masanja wamesema wanamjua Nkulila ni mchapa kazi, hivyo hawana hofu na yeye watampigia kura na wanaamini atashinda kwani kazi zake zinajiekeza, na maendeleo aliyoyafanya yanaonekana.

"Sisi hatuna shaka na mgombea wetu udiwani kwani ni mchapa kazi mzuri na akisimamia hoja ya maendeleo inatendeka na anapenda haki si mtu wa kupindisha pindisha", amesema Masanja.

Mgombea udiwani kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM kata ya Ndembezi manispaa ya Shinyanga mkoani Shinyanga David Nkulila  akiwaomba wananchi wa kata hiyo wamchague tena kuwa diwani wa kata ya Ndembezi. Picha zote na Suzy Butondo
Mgombea udiwani kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM kata ya Ndembezi manispaa ya Shinyanga mkoani Shinyanga David Nkulila  akiwaomba wananchi wa kata hiyo wamchague tena kuwa diwani wa kata ya Ndembezi. 







Wednesday, September 16, 2020

Picha : TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI YAKUTANA NA WATOA HUDUMA YA HABARI MITANDAONI 'BLOGGERS'... 'YASISITIZA UMAKINI MTANDAONI'



Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa Uchaguzi Dkt. Wilson Mahera Charles akizungumza mbele ya Watoa Huduma ya Habari Mitandaoni (hawapo pichani),wakati akifungua Mkutano kati ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Watoa Huduma ya Habari Mitandaoni,uliofanyika leo katika kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, jijini Dar es salaam.

****

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imekutana na Watoa Huduma ya Habari Mitandaoni 'Online Content Service Providers' nchini Tanzania kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali ya mchakato wa uchaguzi mkuu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wabunge na Madiwani utakaofanyika Oktoba 28,2020.

Mkutano huo umefanyika leo Jumanne Septemba 15,2020 katika kituo cha mikutano cha kimataifa cha Julius Nyerere, jijini Dar es salaam .

Akifungua Mkutano huo, Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa Uchaguzi Dkt. Wilson Mahera Charles amesema Watoa Huduma ya Habari Mitandaoni ni wadau muhimu katika mchakato wa uchaguzi ndiyo maana wameamua kukutana nao ili kuwajengea uwezo kuhusu masuala ya uchaguzi ili waweze kuandika habari kwa usahihi na kulinda amani ya nchi.

"Tume ya Taifa ya Uchaguzi tunavipongeza vyombo vya habari mtandaoni kwa ushirikiano ambao mmekuwa mkitupatia.Tunathamini mchango wenu na tutaendelea kushirikiana nanyi ili kujenga nchi yetu. Tumewaita ili kuwajengea uelewa kuhusu mkachato wa uchaguzi,tunaamini kuwa mna nafasi kubwa ya kuelimisha jamii kuhusu taratibu mbalimbali za uchaguzi",amesema Dkt. Charles.

Aidha amewataka waandishi wa habari kuvipa nafasi sawa vyama vyote vya siasa na kuepuka kuandika habari zenye kuhamasisha vurugu na kusababisha uvunjivu wa amani.

"Kipindi cha Kampeni za uchaguzi huwa kuna joto la uchaguzi ambapo joto la kuvunja amani nalo huongezeka. Naomba tulinde amani ya nchi yetu kwa kuepuka kuandika habari zenye kuleta chuki",amesema.

Katika hatua nyingine alivitaka vyama vya siasa kufuata maadili ya uchaguzi na sheria za nchi na kuhakikisha wanafanya kampeni za kistaarabu huku akivikumbusha vyombo vya habari kuepuka kuandika kauli na matamshi ya kuvunja amani.

"Kuanzia sasa tutachukua hatua kali kwa viongozi wanaotoa matamshi ya kuvunja amani. Hata wewe mwandishi wa habari ukiandika habari zenye kuunga mkono matamshi hayo nawe utakuwa unavunja amani",ameongeza Dkt. Charles.

Dkt. Charles ametumia fursa hiyo kuviomba vyombo vya habari kuelimisha jamii kushiriki katika mchakato wa uchaguzi ikiwa ni pamoja na kuhamasisha wananchi kujitokeza kwenye mikutano ya kampeni kusikiliza sera za wagombea na kupiga kura Oktoba 28,2020 ili kupata viongozi wanaowataka watakaowaletea maendeleo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Habari na Mawasiliano kwa Umma, ambaye pia ni Mjumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Mh Asina Omari, amesema.

"Vyombo vya Habari mitandaoni vina nguvu kubwa katika masuala ya siasa hivyo ni muhimu watoa huduma ya habari mtandaoni kuhakikisha mnatumia vyanzo sahihi vya habari ili habari Mnazoziandika ziwe sahihi,Habari zitoke kwenye vyanzo sahihi ili habari ziwe sahihi".


Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa Uchaguzi Dkt. Wilson Mahera Charles akizungumza mbele ya Watoa Huduma ya Habari Mitandaoni (hawapo pichani),wakati akifungua Mkutano kati ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Watoa Huduma ya Habari Mitandaoni,uliofanyika leo katika kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa Uchaguzi Dkt. Wilson Mahera Charles akizungumza mbele ya Watoa Huduma ya Habari Mitandaoni (hawapo pichani),wakati akifungua Mkutano kati ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Watoa Huduma ya Habari Mitandaoni,uliofanyika leo katika kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, jijini Dar es salaam.
Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Habari na Mawasiliano kwa Umma, ambaye pia ni Mjumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Mh Asina Omari akizungumza mbele ya Watoa Huduma ya Habari Mitandaoni (hawapo pichani),wakati wa Mkutano na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC),uliofanyika leo katika kituo cha mikutano cha kimataifa cha Julius Nyerere, jijini Dar es salaam .
Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Elimu kwa Mpigakura, Giveness Aswile akifafanua jambo mbele ya Watoa Huduma ya Habari Mitandaoni (hawapo pichani),wakati wa Mkutano huo kati ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Watoa Huduma ya Habari Mitandaoni,uliofanyika leo katika kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, jijini Dar es salaam.
"Vyombo vya Habari mitandaoni vina nguvu kubwa katika masuala ya siasa hivyo ni muhimu watoa huduma ya habari mtandaoni kuhakikisha mnatumia vyanzo sahihi vya habari ili habari Mnazoziandika ziwe sahihi,Habari zitoke kwenye vyanzo sahihi ili habari ziwe sahihi", alisema Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Habari na Mawasiliano kwa Umma, ambaye pia ni Mjumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Mh Asina Omari.


Baaadhi ya Washiriki wa Mkutano huo wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri

Kushoto ni Mkurugenzi wa Kahama Tv Online, Shija Felician na Mkurugenzi wa Malunde Media, Kadama Malunde wakiwa kwenye Mkutano kati ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Watoa Huduma ya Habari Mitandaoni

Sehemu ye Meza kuu 
Baadhi ya Wageni waalikwa wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa kwenye mkutano huo.


Monday, September 7, 2020

ESTHER BULAYA TISHIO BUNDA…SHUHUDIA HAPA MKUTANO WAKE JIONI HII

  Sehemu ya wananchi wakimsikiliza Mgombea Ubunge jimbo la Bunda Mjini Esther Bulaya kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) 

Na Helena Magabe  -Bunda
Mgombea Ubunge jimbo la Bunda Mjini Esther Bulaya kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ameendelea na Kampeni zake za Uchaguzi ambapo leo Jumatatu Septemba 7,2020  amefanya Mkutano eneo la Stendi ya Zamani Bunda Mjini  huku mkutano wake ukihudhuriwa na maelfu ya wananchi waliofika kusikiliza sera zake.

Akizungumza katika mkutano huo Mgombea huyo wa Ubunge jimbo la Bunda Mjini Esther Bulaya amesema hatawaangusha wana Bunda endapo watamuongeza miaka mingine mitano huku akisisitiza kuwa wana Bunda wanataka Mwakilishi wa Wananchi sio wa Serikali.

Mgombea Ubunge jimbo la Bunda Mjini Esther Bulaya kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) akiwa kwenye msafara

Friday, September 4, 2020

Namibia kufundisha mbwa kugundua virusi vya corona



Chuo Kukuu cha Namibia kitengo cha dawa ya mifugo kinawafundisha mbwa kubaini virusi vya corona kwa kunusa.

Mpango wa nchi hiyo ni kuwapelea nbwa hao katikaviwanja vya ndegena vituo vya mpakani, kwa mujibu wa mtandao wa The Namibian.


Mbwa wamethibitishwa kuwa na uwezo wa kubaini virusi vya corona kwa aslimia 95, mhadiri wa somo la tiba ya wanyama Alma Raath anasema.


Mradi huo ulianzishwa miezi miezi miwili iliyopita, inarsema taarifa ya mtandao huo wa The Namibian, lakini haujataja ni lini mbwa hao watakuwa tayari kufanya kazi.


Mtandao wa The Namibian unasema nchi hiyo itakuwa ya kwanza kutumia mbwa kubaini virusi vya corona.

WAGOMBEA MULEBA KUSINI WAJINOA VIKALI


Mgombea Ubunge wa CCM Jimbo la Muleba Kusini Dr Oscar Kikoyo baada ya kupokea Ilani ya UchaguzI ya chama hicho kutoka kwa Mwenyekiti wa Mkoa Costancia Buhiye na kuhaidi kuinadi kwa wananchi.
 ***
Na Ashura Jumapili,Muleba
Wagombea wa Jimbo la Muleba Kusini katika nafasi ya Ubunge na Madiwani wameanza kunoa makali kupitia mikutano tofauti ya awali kabla ya uzinduzi rasmi wa kampeni utakaofanyika kesho siku ya Jumamosi Septemba 6,2020.

Mgombea Ubunge kupitia CCM Dr.  Oscar Kikoyo kwa nyakati tofauti ameshiriki mikutano iliyomkutanisha na wagombea wengine wa Ubunge na Udiwani kabla ya uzinduzi rasmi utakaofanyika katika uwanja wa Zimbihire mjini Muleba.

Katika uzinduzi wa kampeini ngazi ya Mkoa Dr. Kikoyo alihaidi kuinadi ilani ya CCM inayotoa mwelekeo wa ongezeko la miradi ya maendeleo na kutoa ufumbuzi wa changamoto zilizobaki katika awamu ya kwanza ya uongozi wa miaka mitano wa Rais John Magufuli.

Akiwa katika Kata ya Nshamba Dr. Kikoyo aliahidi kushirkiana na diwani wa Kata hiyo na wadau wengine kupata ufumbuzi wa kudumu wa tatizo la uhaba wa maji na kuinua elimu hasa ujenzi wa shule za kidato cha tano na sita katka Jimbo hilo.

Mkutano huo pamoja na viongozi mbalimbali pia unatarajiwa kupambwa na wasanii kutoka ndani na nje ya Wlaya ya Muleba ambapo wagombea udiwani wote wanatarajiwa kuhudhuria uzinduzi huo.
Mgombea Ubunge wa Muleba Kusini Dr Oscar Kikoyo akihutubia wananchi wa Kata ya Nshamba eneo la Muznga na kuwahaidi kasi ya maendeleo.
Baadhi ya wanachama na mashabiki wa CCM katika mkutano wa kampeni Kata ya Nshamba Jimbo la Muleba Kusini.
Mgombea Udiwani Kata ya Nshamba Gosbert Masilingi akijinadi kwa wananchi wa Kata hiyo kuomba achaguliwe tena kutekeleza ilani ya chama chake.
Mgombea Udiwani kata ya Kibanga Edson Issaya akinadi ilani ya CCM na mgombea wa chama hicho katika Kata ya Nshamba Gosbert Masilingi.
Mgombea Ubunge Muleba Kusini Dr Oscar Kikoyo akijadili jambo na baadhi ya wananchi baada ya mkutano katika eneo la Muzinga Kata ya Nshamba.
Mjumbe wa NEC kutoka Mkoa wa Kagera Wilbroad Mutabuzi akitoa nasaha kwa wagombea waliopita kwenye uteuzi wa vikao vya chama kunadi mafanikio ya awamu iliyopita na ilani ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka huu.
Mgombea Udiwani wa CCM Kata ya Mazinga iliyoko kwenye Ziwa Victoria Edson Alex akiwa tayari kusaka kura zake na wagombea wengine baada ya kukabidhiwa ilani na vitendea kazi vingine.
Mgombea udiwani kata ya Kishanda Helmes Mushumbusi akisisitiza jambo katika mkutano uliofanyika Kata ya Nshamba

Jamii ya Pwani na Utamaduni wa Sherehe za Kumtoa Binti Mwali.....


Katika baadhi ya Mikoa na Pwani ya Tanzania, wana utamaduni wa binti kupatiwa Mafunzo Maalumu ya Kimila au maarufu kama 'Kufundwa' na hujumuisha wasichana kuwekwa ndani kwa muda wa miezi kadhaa

Kwa binti ambaye hajapitia tukio hili huonekana kama atakuwa na hasara kubwa katika maisha yake ya ndoa ya baadaye kwani huonekana kama vile hajui mambo mengi ya kumridhisha mume kwa mujibu wa mila

Miongoni mwa Jamii inayotajwa kuendeleza mila hizi ni Wamakonde kutoka Kusini mwa Tanzania na baadhi ya wakazi wa Mkoa wa Pwani, ndani na hata nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam

Wazawa hawa wanamcheza binti kuanzia umri wa miaka 10 ambapo binti huelekezwa unyumba, namna ya kukaa na mume, nguo za kuvaa akiwa na mumewe, chakula cha kupika na kadhalika

Aidha, utamaduni huu umekuwa ukilaumiwa na baadhi ya watu kuwa ndio chanzo cha kusitisha masomo kwa wasichana wengi pamoja na mimba za utotoni kwani sherehe hizi zinafanyika wasichana wanapomaliza darasa la 7 au hata kabla hawajamaliza elimu hiyo

Ni tamaduni nyingine zipi zinazofanyika kwenye Jamii inayokuzunguka?

Wednesday, September 2, 2020

Mchezaji Ang'aka 'Mnanitengenezea Skendo Mlianza la Hirizi sasa Mnasema Nimemdunda Kocha'



Mshambuliaji wa klabu bingwa Tanzania Bara (VPL) na Kombe la Shirikisho (ASFC) Simba SC, Meddie Kagere amesema amesikitishwa na taarifa zilizosambaa mtandaoni kuwa amempiga kocha wa timu hiyo, Sevn Vandenbroeck.

Jana taarifa za Kagere kudaiwa kumpiga kocha huyo kisa kikiwa ni kutopangwa kikosi cha kwanza cha Simba zilizagaa kwa kasi mitandaoni, na kuripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari mapema hii leo.

Akizungumza na E.A Radio mapema hii leo, mshambuliaji huyo kutoka Rwanda alisema ameshangaa baada ya kuona mambo hayo yanasambaa wakati yeye hajafanya tukio hilo na yuko freshi kabisa na kocha.

"Kuna mambo huwa yanasemwa kuhusu mimi ambayo siyo ya kweli yenye lengo la kunichafua ndiyo maana sijawahi kuwajibu."
"Lilianza la hirizi nikanyamaza na sasa limekuja la mimi kupigana na kocha kitu ambacho siyo kweli. Tangu tumefika Mbeya hatujafanya mazoezi na leo muda huu ndiyo tunafanya sasa nashangaa sijui mwalimu nimempiga wapi," alisema Kegere.

Hata hivyo Uongozi wa Simba SC kupitia idara ya habari na mawasiliano umekanusha taarifa hizo kwa kusema hazina ukweli, zidi ya kutaka kuvuruga amani ndani ya kikosi chao ambacho kipo tayari kuanza kutetea taji la Tanzania Bara mwishoni mwa juma hili dhidi ya Ihefu FC.

Mkuu wa Idara hiyo Haji Manara amesema: "Wanasema jana ugomvi uliotokea mazoezini, lakini Simba hawakuwa na mazoezi baada ya mchezo wa ngao ya jamii, hizo ni propaganda za kuvuruga utulivu uliopo ndani na nje ya Simba, wakitaka itokee kama upande wa pili yanayoendelea"

"Kama idara ya Habari na Mawasiliano hatutokubali kuona watu wanaandika uzushi kuhusu Klabu yetu na tutachukua hatua kali dhidi ya watakaohusika"


Tuesday, September 1, 2020

Mwigulu: Nyalandu Alikuwa Akienda Kunyoosha Suti Ulaya, Lissu Amelipwa



MGOMBEA ubunge Iramba Mashariki Mkoa wa Singida kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Mwigulu Nchemba, ameanza kumchokonoa Tundu Lissu, mgombea urais kupitia Chadema na Lazaro Nyalandu, mgombea ubunge wa Singida Kaskazini.

Akizungumza kwenye kampeni za Dk. John Magufuli,  mgombea urais wa Tanzania kupitia chama hicho katika Uwanja wa Bombadier mkoani Singida leo tarehe 1 Septemba 2020 amesema, wawili hao hawana uzalendo.

Bila kuwataja majina, Mwigulu alimnanga Nyalandu kwamba, alipokuwa waziri (Waziri wa Maliasili na Utalii katika serikali ya awamu ya nne) alikuwa akienda Ulaya kunyoosha suti zake huku Lissu akisema amerejea nchini baada ya kupewa 'advance' (malipo ya awali).

Lissu ndiye aliyerejea nchini akitokea kwenye matibabu nchini Ubelgiji, ni baada ya watu wasiojulikana kushamabuliwa kwa risasi 'Area D,' jijini Dodoma tarehe 7 Septemba 2017.

Mara kadhaa Lissu alinukuliwa na vyombo vya habari akiwa ughaibuni, kwamba alishindwa kurudi Tanzania kwa kuwa sio sehemu salama kwake.

"Wengine wanakuja hapa wanajifanya watoto wa Singida, hawana uzalendo hata na wana Singida. Kuna mmoja tulikuwa mawaziri wote, hata suti zake alikuwa anaenda kunyoosha Ulaya, hana uchungu na Singida.

"Mwingine alisema Tanzania sio salama, sasa hivi amekuja sababu 'advance' amechukua baada ya uchaguzi tu atasema, Tanzania haiko salama, ataondoka," amesema Dk. Mwigulu.

Dk. Mwigulu ambaye ni Waziri wa Katiba na Sheria, amewataka Watanzania kumchagua Rais Magufuli. "Ioneeni huruma Tanzania, wale wagombea wengine wote mimi nawafahamu na nikiangalia janja janja yao, naona hata 'advance' wamechukua, nchi yetu itauzwa mkimuacha Dk. Magufuli," amesema Dk. Mwigulu.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...