Monday, September 7, 2020

ESTHER BULAYA TISHIO BUNDA…SHUHUDIA HAPA MKUTANO WAKE JIONI HII

  Sehemu ya wananchi wakimsikiliza Mgombea Ubunge jimbo la Bunda Mjini Esther Bulaya kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) 

Na Helena Magabe  -Bunda
Mgombea Ubunge jimbo la Bunda Mjini Esther Bulaya kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ameendelea na Kampeni zake za Uchaguzi ambapo leo Jumatatu Septemba 7,2020  amefanya Mkutano eneo la Stendi ya Zamani Bunda Mjini  huku mkutano wake ukihudhuriwa na maelfu ya wananchi waliofika kusikiliza sera zake.

Akizungumza katika mkutano huo Mgombea huyo wa Ubunge jimbo la Bunda Mjini Esther Bulaya amesema hatawaangusha wana Bunda endapo watamuongeza miaka mingine mitano huku akisisitiza kuwa wana Bunda wanataka Mwakilishi wa Wananchi sio wa Serikali.

Mgombea Ubunge jimbo la Bunda Mjini Esther Bulaya kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) akiwa kwenye msafara

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...