




























While in the past I was hard on TZ this time round we are on the wrong and we should quietly swallow our pride and fix this problem.
As long as we continue to exclude TZ from the list of the countries that can visit Kenya without being quarantined then they will continue doing this and I won't be surprised if this ended with border closure.
Firstly that list we gave out has a condition in that everyone must present a Covid free certificate which should have been issued less not more than 96 hours, why did we exclude TZ? It was an ill adviced move.
Now folks we cannot have our cake and at the same time eat it. If TZ are not good enough to be on the list then they just did the natural thing of stopping us also. We cannot be going to a neighbour as we wish but choose not to reciprocate.
Irony is that maids , trucks and bus drivers move without any restrictions at cross border points.
I feel for investors in the aviation industry...I feel for airlines.... I feel for our national carrier KQ. Our national carrier has its own challenges then add this where they cannot fly to a lucrative Nbi Dar route.
Finally it is not in our position to judge TZ on how they have handled the Corona crisis....we opted for more stringent measures which I support ...Sweden adopted a TZ similar approach as well and TZ continue with life. Last weekend popular simba sports club unveiled new players at parked Benjamin Mkapa Stadium where they played Vital O SC of Burundi.
KLM. Qatar. Emirates. Ethiopian.....all fly to Dar and Kili eating lunch meant for KQ as immediate neighbours.
TZ is our biggest trading partner and we share one of the longest borders and we speak the same national language.
I appeal to H.E to step in and help resolve this... with one call I believe he can do it.
Mohammed Hersi
Chairman
Kenya Tourism Federation
BAADA ya kupitishwa na Chama chao cha Mapinduzi (CCM) na kisha kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa leo wagombea wa Ubunge, Deo Ndejembi wa Jimbo la Chamwino na Livingstone Lusinde 'Kibajaji' wa Mvumi wamerudisha fomu kwa Msimamizi wa Uchaguzi ambaye pia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino, Dodoma, Athuman Masasi.
Wagombea hao wote majimbo yao yapo katika Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma ambapo wameahidi kufanya kampeni za kistaarabu huku wakiahidi kushughulika na kero za wananchi.
Akizungumza baada ya kurudisha fomu mgombea wa ubunge Chamwino, Deo Ndejembi amesema anaamini kwa mambo makubwa yaliyofanywa na Rais Dk John Magufuli ni wazi watapata kura nyingi za ndio kutokana na imani kubwa ambayo serikali imejenga kwa wananchi.
" Nakishukuru chama changu kwa kunipitisha niwaahidi ndugu zangu wa Chamwino kwamba ninakuja kufanya kazi ya kuwatumikia nyinyi, ninakuja kushirikiana na serikali yetu kuwaletea maendeleo ya kijamii na kiuchumi," Amesema Ndejembi.
Kwa upande wake Lusinde amewataka watanzania kumpigia kura nyingi za ndio Rais Magufuli ili kumpa heshima kwa utendaji wake uliovunja rekodi nchini na nje ya Nchi.
" Wananchi wenzangu wa Chamwino ni ahadi yetu kwenu kwamba tuna dhamira ya dhati ya kuwatumikia, mmeona namna ambavyo Rais wetu amefanya kazi kubwa ikiwemo kuifanya Nchi yetu kuwa na uchumi wa kati hata kabla ya 2025 ambapo tulikua tumejiwekea malengo," Amesema Lusinde.
Baada ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na kamati yake kupitisha majina ya wagombe wa Ubunge, Udiwa na viti maalumu kupitia chama cha mapinduzi CCM hivi leo.
Baadhi ya wadau wa muziki wameteuliwa ambao ni msanii wa muziki wa Bongo Fleva Mwana FA na meneja wa Diamond Platnumz Bbutale.
Baada ya uteuzi huo Mwana FA ameandika ujumbe huu
"Mungu ni mwema sana, Leo ni miongoni mwa zile siku chache, mimi nimeishiwa na sina la kusema, alama nyingine kuhusu ukubwa wa Mungu"
MTOTO mwingine wa kike mwenye umri wa siku tatu, ameopolewa na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwenye choo cha Zahanati ya Mshikamano wilayani Ngara mkoani Kagera akiwa hai.
Hilo ni tukio la pili kutokea wilayani humo, kwani Mei 21 mwaka huu, mtoto Isabela aliopolewa akiwa hai kwenye choo cha Shule ya Msingi Murganza wilayani humo na jeshi hilo.
Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani Kagera, Hamis Dawa, amesema walipata taarifa ya kutupwa kwa kichanga hicho katika choo cha Zahanati ya Mshikamano kupitia kwa Jeshi la Polisi wilayani humo.
"Baada ya taarifa hiyo, tuliwatuma askari wawili ambao ni ZM 3338 Sajenti Bahati Rudisha na FC 3802 Amos Mwita, ambao walifanikiwa kumuokoa mtoto huyo akiwa hai.
"Mtoto huyo tumemkabidhi kwenye Hospitali ya Mshikamano kwa ajili ya matibabu wakati huo Jeshi la Polisi likiendelea kumtafuta mama wa mtoto huyo aliyemtupa kwenye shimo la choo," alisema kamanda Hamisi Dawa.
Kwa mujibu wa Kamanda Dawa, kichanga hicho ambacho kilikuwa bado hakijakatika kitovu, kiliopolewa katika choo hicho kilichokuwa kinatumika, hivyo baada ya askari hao kubomoa mfuniko wa choo, walikiona kikiwa kinaelea.
"Mtoto hakukutwa na majeraha, bali alikuwa na afya njema, hivyo wahudumu wa afya hospitalini, wanaendelea kumfanyia uchunguzi wa kitabibu
"Tunashirikiana na watu wa Ustawi wa Jamii na wahudumu wa afya kitengo cha afya ya uzazi, ili kuweza kutoa elimu kwa akina mama ambao ndiyo wanaobeba ujauzito, jinsi ya kulea na kukabiliana na changamoto za kifamilia zinazowasababishia kutenda ukatili kwa watoto kama huu," alisema Kamanda Dawa.