Thursday, October 1, 2020

Picha : MAGUFULI AKIWAHUTUBIA WANANCHI WA MBALIZI MBEYA LEO ASUBUHI


Baadhi ya Wananchi wakimsikiliza Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Rais Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa akiwahutubia wakazi wa eneo hilo la Mbalizi mkoani Mbeya wakati akielekea Tundumba kwa ajili ya Mikutano ya Kampeni za Urais kwa upande wa CCM leo tarehe 01 Oktoba 2020. 
Mgombea Urais kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Rais Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wananchi wa Mbalizi mkoani Mbeya wakati akielekea Tundumba kwa ajili ya Mikutano ya Kampeni za Urais kwa upande wa CCM leo Oktoba 01,2020. 

Yanga Mwendo Mdundo Yampiga Mtu 2 Bola....Tonombe Mukoko Aibuka Shujaa



 KIKOSI cha Yanga leo Septemba 30 kimeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya timu ya KMKM kwenye mchezo wa kirafiki uliochezwa Uwanja wa Azam Complex.

Mabao ya Yanga yalifungwa na Tonombe Mukoko dakika 10 kwa kona ya Carols Carinhos kiungo ambaye amepewa jukumu la kupiga mipira iliyokufa ndani ya Yanga.

Dakika 20 mbele Mukoko tena alipachika bao la pili na la mwisho wa timu yake baada ya mabeki wa KMKM ya Zanzibar kujichanganya katika harakati za kuokoa hatari.

Kipindi cha pili mambo yalikuwa magumu kwa KMKM kuweza kuweka mzani sawa huku Yanga nao pia wakikwama kuongeza bao la pili. 


Mchezo wa leo ulikuwa ni wa kirafiki ambapo lengo kubwa ni kukiweka kikosi sawa cha Yanga fiti kwa kuwa hakikuwa na mazoezi ya muda mrefu kwa ajili ya maandalizi ya msimu wa 2020/21 kutokana na janga la Virusi vya Corona kutibua ratiba nyingi duniani. 


Akizungumza na Saleh Jembe, Kocha Msaidizi wa Yanga, Juma Mwambusi amesema kuwa malengo makubwa ni kukiandaa kikosi kwa ajili ya mechi zao zinazofuata.

"Kikosi kilikuwa na muda mfupi kwa ajili ya maandalizi ya ligi hivyo kwa sasa tunazidi kujiimarisha ili kuwa bora hasa ukizingatia kwamba tuna wachezaji wengi wapya," amesema.

BENKI YA CRDB YABORESHA HUDUMA KWA WASTAAFU WASTAAFU SASA KUHUDUMIWA KIDIJITALI

 

Afisa Mkuu wa Biashara wa Benki ya CRDB, Dkt. Joseph Witts (watatu kushoto) akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa mpango wa uwezeshaji kwa wastaafu uliyofanyika katika hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam, leo. Wengine pichani ni kutoka kulia ni Mwenyekiti wa makatibu Wakuu Wastaafu, Michael Mwanda, Balozi Mstaafu Salome Sijaona, Mkurugenzi wa Wateja Wadogo na Wakati wa Benki ya CRDB, Boma Raballa, Mwenyekiti wa Umoja wa Polisi Wastaafu, Kamishna wa Polisi Mstaafu Suleiman Kova na Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi Benki ya CRDB, Adili Stephen.

Afisa Mkuu wa Biashara wa Benki ya CRDB, Dkt. Joseph Witts (watatu kushoto) akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa mpango wa uwezeshaji kwa wastaafu uliyofanyika katika hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam, leo.  Kulia ni Mkurugenzi wa Wateja Wadogo na Wakati wa Benki ya CRDB, Boma Raballa na kushoto ni Mwenyekiti wa Umoja wa Polisi Wastaafu, Kamishna wa Polisi Mstaafu Suleiman Kova.

Benki ya CRDB imezindua mpango maalum wa uwezeshaji kwa wastaafu ambao unatoa fursa mbalimbali zinazolenga katika kuboresha maisha yao. Akizungumza katika uzinduzi wa mpango huo wenye kauli mbiu ya "Ndoto zako hazistaafu", Afisa Biashara Mkuu wa Benki ya CRDB, Dkt. Joseph Witts amesema mpango huo anajumuisha fursa za kujiwekea akiba, uwekezaji, pamoja na uwezeshaji wa kifedha kwa wastaafu.

Dkt. Witts alisema pamoja na uzinduzi wa mpango huo Benki ya CRDB pia imezindua huduma za akaunti maalum ya wastaafu "Pension Account" na huduma ya uwezeshaji kifedha kwa wastaafu kidijitali "Pension Advance" kupitia huduma ya SimBanking App.

Akielezea kuhusu akaunti ya wastaafu, Dkt. Witts alisema akaunti hiyo inawawezesha wastaafu kupokea pensheni zao kwa urahisi na usalama na kujiwekea akiba kutokana na vipato vinavyotokana na shughuli mbalimbali za kiuchumi wanazozifanya. Dkt. Witts alisema ili kutoa nafuu kwa wastaafu akaunti hiyo hufunguliwa bure, haina makato yoyote yale na hutoa fursa kwa wastaafu kuunganishwa bure na mifumo ya utoaji huduma kidijitalli ikiwamo SimBanking na Internet Banking. 

"Ninajivunia kuwajulisha kuwa hadi leo hii tukiwa tunazindua mpango huu wa uwezeshaji wastafu, tayari wastaafu zaidi ya 19,000 wameshafungua akaunti hii na wanafurahia huduma zetu," alisema Dkt. Witts huku akibainisha kuwa kupitia akaunti hiyo wastaafu wanapewa TemboCard inayowawezesha kupata huduma kwa CRDB Wakala na ATM zote nchi nzima.

Kwa upande wa huduma ya uwezeshaji wa kifedha kupitia "Pension Advance", Dkt. Witts alisema sasa hivi wastaafu wanaweza kupata uwezeshaji wa fedha za kujikimu na kuendesha maisha yao kuanzia shilingi 50,000 hadi shilingi milioni 1 popote pale walipo kidijitali kupitia SimBanking App, huku akibainisha kuwa mkopo huo wa Pension Advance unatolewa bila riba yoyote.

Akizungumzia kuhusu fursa za uwekezaji zinazotolewa na Benki ya CRDB kupitia mpango huo, Dkt. Witts alisema benki hiyo pia imeanzisha akaunti maalum ya uwekezaji ijulikanayo kama "Akaunti ya Thamani" ambayo inawawezesha wastaafu kujipatia kipato kila mwezi. "Akaunti hii ya Thamani inatoa fursa kwa wastaafu kuwekeza kwa kipindi cha miaka mitatu kwa riba ya hadi asilimia 8," alisema Dkt. Witts.

Naye Mkurugenzi wa Wateja Wadogo na Wakati wa Benki ya CRDB, Boma Rabala alisema kupitia mpango huo wa uwezeshaji kwa wastaafu benki hiyo pia imejipanga kuendelea kutoa mikopo kwa wastaafu ili kuwawezesha kuendeleza biashara na miradi yao ya maendeleo na hivyo kupunguza ukali wa maisha ya kila siku. Kupitia mkopo huo Wastaafu wanaweza kukopa kuanzia shilingi milioni 1 hadi shilingi milioni 100 kwa kipindi cha mwaka 1 hadi 7.

Mwenyekiti wa Makatibu Wakuu Wastaafu, Michael Mwanda aliishukuru Benki ya CRDB kwa kuwakumbuka wastaafu kupitia huduma na bidhaa zinazotolewa na benki hiyo. Mwanda alitoa rai kwa wastaafu wote kuchangamkia fursa hizo kuboresha maisha yao huku akiitaka Benki ya CRDB kutoa semina juu ya huduma hizo kwa wastaafu wote nchi nzima.

Naye Mwenyekiti wa Umoja wa Polisi Wastaafu, Kamishna wa Polisi Mstaafu, Suleiman Kova aliipongeza Benki ya CRDB kwa kuja na mpango huo wa uwezeshaji kwa wastaafu huku akibainisha kuwa zitasaidia kuleta chachu ya maendeleo na kufanya kustaafu kusiogopwe. "Na sisi wastaafu sasa tunajidai tuna benki yetu ambayo sio tu inausikiliza bali pia inatambua mchango wa wastaafu katika taifa letu, Asanteni sana Benki ya CRDB," alisema Kova huku akimuomba Afisa Biashara Mkuu wa Benki ya CRDB, Dkt. Joseph Witts kumsaidia kufungua akaunti ya Wastaafu ili aweze kufurahia huduma zote zinazotolewa katika mpango huo wa uwezeshaji wastaafu.









Wednesday, September 30, 2020

Benki ya CRDB yaboresha huduma kwa Wastaafu Wastaafu sasa kuhudumiwa kidijitali

 


Afisa Mkuu wa Biashara wa Benki ya CRDB, Dkt. Joseph Witts (watatu kushoto) akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa mpango wa uwezeshaji kwa wastaafu uliyofanyika katika hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam, leo. 


Wengine pichani ni kutoka kulia ni Mwenyekiti wa makatibu Wakuu Wastaafu, Michael Mwanda, Balozi Mstaafu Salome Sijaona, Mkurugenzi wa Wateja Wadogo na Wakati wa Benki ya CRDB, Boma Raballa, Mwenyekiti wa Umoja wa Polisi Wastaafu, Kamishna wa Polisi Mstaafu Suleiman Kova na Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi Benki ya CRDB, Adili Stephen.


Afisa Mkuu wa Biashara wa Benki ya CRDB, Dkt. Joseph Witts (watatu kushoto) akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa mpango wa uwezeshaji kwa wastaafu uliyofanyika katika hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam, leo.  Kulia ni Mkurugenzi wa Wateja Wadogo na Wakati wa Benki ya CRDB, Boma Raballa na kushoto ni Mwenyekiti wa Umoja wa Polisi Wastaafu, Kamishna wa Polisi Mstaafu Suleiman Kova.


Benki ya CRDB imezindua mpango maalum wa uwezeshaji kwa wastaafu ambao unatoa fursa mbalimbali zinazolenga katika kuboresha maisha yao. Akizungumza katika uzinduzi wa mpango huo wenye kauli mbiu ya "Ndoto zako hazistaafu", Afisa Biashara Mkuu wa Benki ya CRDB, Dkt. Joseph Witts amesema mpango huo anajumuisha fursa za kujiwekea akiba, uwekezaji, pamoja na uwezeshaji wa kifedha kwa wastaafu.


Dkt. Witts alisema pamoja na uzinduzi wa mpango huo Benki ya CRDB pia imezindua huduma za akaunti maalum ya wastaafu "Pension Account" na huduma ya uwezeshaji kifedha kwa wastaafu kidijitali "Pension Advance" kupitia huduma ya SimBanking App.


Akielezea kuhusu akaunti ya wastaafu, Dkt. Witts alisema akaunti hiyo inawawezesha wastaafu kupokea pensheni zao kwa urahisi na usalama na kujiwekea akiba kutokana na vipato vinavyotokana na shughuli mbalimbali za kiuchumi wanazozifanya. Dkt. Witts alisema ili kutoa nafuu kwa wastaafu akaunti hiyo hufunguliwa bure, haina makato yoyote yale na hutoa fursa kwa wastaafu kuunganishwa bure na mifumo ya utoaji huduma kidijitalli ikiwamo SimBanking na Internet Banking. 

"Ninajivunia kuwajulisha kuwa hadi leo hii tukiwa tunazindua mpango huu wa uwezeshaji wastafu, tayari wastaafu zaidi ya 19,000 wameshafungua akaunti hii na wanafurahia huduma zetu," alisema Dkt. Witts huku akibainisha kuwa kupitia akaunti hiyo wastaafu wanapewa TemboCard inayowawezesha kupata huduma kwa CRDB Wakala na ATM zote nchi nzima.


Kwa upande wa huduma ya uwezeshaji wa kifedha kupitia "Pension Advance", Dkt. Witts alisema sasa hivi wastaafu wanaweza kupata uwezeshaji wa fedha za kujikimu na kuendesha maisha yao kuanzia shilingi 50,000 hadi shilingi milioni 1 popote pale walipo kidijitali kupitia SimBanking App, huku akibainisha kuwa mkopo huo wa Pension Advance unatolewa bila riba yoyote.


Akizungumzia kuhusu fursa za uwekezaji zinazotolewa na Benki ya CRDB kupitia mpango huo, Dkt. Witts alisema benki hiyo pia imeanzisha akaunti maalum ya uwekezaji ijulikanayo kama "Akaunti ya Thamani" ambayo inawawezesha wastaafu kujipatia kipato kila mwezi. "Akaunti hii ya Thamani inatoa fursa kwa wastaafu kuwekeza kwa kipindi cha miaka mitatu kwa riba ya hadi asilimia 8," alisema Dkt. Witts.


Naye Mkurugenzi wa Wateja Wadogo na Wakati wa Benki ya CRDB, Boma Rabala alisema kupitia mpango huo wa uwezeshaji kwa wastaafu benki hiyo pia imejipanga kuendelea kutoa mikopo kwa wastaafu ili kuwawezesha kuendeleza biashara na miradi yao ya maendeleo na hivyo kupunguza ukali wa maisha ya kila siku. Kupitia mkopo huo Wastaafu wanaweza kukopa kuanzia shilingi milioni 1 hadi shilingi milioni 100 kwa kipindi cha mwaka 1 hadi 7.

Mwenyekiti wa Makatibu Wakuu Wastaafu, Michael Mwanda aliishukuru Benki ya CRDB kwa kuwakumbuka wastaafu kupitia huduma na bidhaa zinazotolewa na benki hiyo. Mwanda alitoa rai kwa wastaafu wote kuchangamkia fursa hizo kuboresha maisha yao huku akiitaka Benki ya CRDB kutoa semina juu ya huduma hizo kwa wastaafu wote nchi nzima.


Naye Mwenyekiti wa Umoja wa Polisi Wastaafu, Kamishna wa Polisi Mstaafu, Suleiman Kova aliipongeza Benki ya CRDB kwa kuja na mpango huo wa uwezeshaji kwa wastaafu huku akibainisha kuwa zitasaidia kuleta chachu ya maendeleo na kufanya kustaafu kusiogopwe. "Na sisi wastaafu sasa tunajidai tuna benki yetu ambayo sio tu inausikiliza bali pia inatambua mchango wa wastaafu katika taifa letu, Asanteni sana Benki ya CRDB," alisema Kova huku akimuomba Afisa Biashara Mkuu wa Benki ya CRDB, Dkt. Joseph Witts kumsaidia kufungua akaunti ya Wastaafu ili aweze kufurahia huduma zote zinazotolewa katika mpango huo wa uwezeshaji wastaafu.

Waliomuua Kada wa CCM Njombe Wakiri Kutekeleza Mauaji Hayo



Kamanda wa Polisi mkoani Njombe, Hamis Issa amesema gari namba T 457 DAB, Toyota Gaiya, mali ya George Sanga ambaye ni mgombea Udiwani Kata ya Ramadhani kwa tiketi ya CHADEMA ilitumika wakati wa utekelezaji wa mauaji ya kada wa CCM Emmanuel Mlelwa.





Sheria mpya kuhusiana na maandamano dhidi ya Netanyahu Israel

Bunge la Israeli limepitisha rasimu ya sheria iliyoandaliwa kupunguza maandamano wakati wa karantini, ambayo imechukuliwa katika mfumo wa kupambana na janga la corona.

Pamoja na muswada uliopitishwa asubuhi na mapema, wakati wa karantini, umma utaweza kushiriki katika maandamano sio zaidi ya kilomita 1 kutoka nyumbani kwao.

Uamuzi huu umefungua njia ya kuzuia waandamanaji kutoka nje ya jiji na kutoka maeneo ya mbali ya jiji kushiriki katika maandamano ya kila wiki ya kumpinga Netanyahu mbele ya makazi ya Waziri Mkuu huko West Jerusalem kwa zaidi ya miezi minne.

Wapinzani wa Israeli wameitikia uamuzi huo, wakisema kwamba kuzuia maandamano hayo kumeumiza demokrasia ya nchi hiyo na kwamba sheria hiyo imetumikia masilahi ya kisiasa ya Netanyahu kwa kutumia Covid-19 kama kisingizio.

Serikali ya Netanyahu iliamua kuzuia maandamano hayo wiki iliyopita, lakini jaribio hili lilishindwa kwa sababu ya bunge kukataa.

Kwa zaidi ya miezi 4 maandamano yamekuwa yakifanyika nchini Israel  yakimtaka Netanyahu kujiuzulu kwa sababu ya usimamizi mbaya wa janga la Covid-19 na kesi ya ufisadi dhidi yake.

 

Ubabe, Matusi Vyatawala Mdahalo wa Trump, Biden



ZIKIWA zimesalia siku 35 kuelekea  uchaguzi mkuu wa urais nchini Marekani utakaofanyika Novemba 3 mwaka huu, wagombea urais,  Donald John Trump wa chama cha Republican na mpinzani wake Joe Biden wa Chama cha Democratic, wamekabana koo kwa mara ya kwanza kwenye mdahalo uliowakutanisha katika jiji la Cleveland, Ohio, nchini humo.

Mdahalo huo ulioongozwa na mtangazaji wa Fox News, Chris Wallace, ulichukua dakika 90 hadi kumalizika.


Wagombea walikabiliana kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo uchumi, uongozi, afya na janga la Corona huku kauli zisizo za kiungwana na za kibabe zikitawala wakati wa kujibu maswali

Aidha, kabla ya kuanza kwa mdahalo huo taarifa zilisambaa  zikieleza kuwa Rais Trump alipanga kutompa mwanya mpinzani wake kuzungumza na kumkatisha kila atakapokuwa anaongea jambo ambalo kweli amelifanya.


Katika suala la afya, Biden ambaye ni makamu wa rais mstaafu  wa Marekani amelaumu uongozi wa Trump kwa kudai idadi kubwa ya Wamarekani wanaugua magonjwa hatari kiafya

"Watu milioni 100 (Marekani) wanaugua magonjwa yanayowaweka katika hatari," alisema Biden.


Katika kujibu hoja hiyo Rais Trump alikanusha na kueleza idadi hiyo ilikuwa ni uongo huku akiwa hana jibu sahihi kuhusu idadi ya Wamarekani wenye matatizo ya afya.

Kwa mujibu wa idara ya afya nchini Marekani, kati ya watu milioni 50 na 129 ambao sio wazee tayari wamepata matatizo ya kiafya.


Mdahalo huo ulichukua sura mpya mara baada ya Trump anayesaka muhula wa pili kumwambia Biden "Watu wanaelewa kuwa miaka yako 47 ndani ya siasa hujafanya chochote wanaelewa," Trump alisema huku Biden akijibu na kusema " endelea kupiga kelele, utanyamaza tu" alisema mgombea huyo wa Democratic.


Katika kujadili suala la ugonjwa wa Corona ambao umesababisha vifo 205,942 nchini humo, Biden alimlaumu Trump kwa kusema "Watu wengi walikufa na wengine zaidi watakufa usipopata akili ya haraka kushughulikia," alisema Biden.

Trump aliyeongoza kwa kumkaripia mshindani wake pamoja na mwendeshaji wa mdahalo huo, Chris Wallace, alijibu na kusema, " watu wachache zaidi wanakufa sasa hivi, vilevile maambukizi yamepungua. Wewe kamwe usingeweza kufanya kazi ambayo sisi tumeifanya. Hicho kitu huna kwenye damu yako," hili lilikuwa jibu ya Trump kwa Biden.


Wagombea wote walionyesha kutofautiana takribani kwenye kila swali waliloulizwa na mwenyekiti wa mdahalo huo, kuanzia masuala ya afya, usalama, hadi ya kifamilia.


Sehemu kubwa ya mdahalo ilitawaliwa na Trump, ambaye wachambuzi wanasema alifanikiwa kuuendesha kwa njia yake mwenyewe, yaani badala ya kujadili masuala muhimu alikuwa anarusha maneno kama vile "Nyamaza kimya…hebu nyamaza wewe!!"


Kura za maoni zinamuonesha Biden akiongoza lakini Trump amesisitiza kauli yake ya kutokuwa na imani na mfumo wa upigaji kura kwa njia ya posta.


Pia amekataa kutamka kama atayakubali matokeo ya uchaguzi huo licha ya mshindani wake kusema yuko tayari kwa matokeo yoyote.

HESLB Yatoa Siku Tano (05) Kwa Wahitimu Mafunzo Jkt Kuomba Mikopo


Na Mwandishi Wetu, HESLB
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetoa muda wa siku 5 kuanzia Oktoba mosi hadi 5 mwaka huu ili kuwawezesha wanafunzi waliomaliza mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) hivi karibuni kuingia katika mfumo wa kuomba mkopo kwa njia ya mtandao na kukamilisha maombi yao.

Katika taarifa yake aliyotoa kwa vyombo vya habari leo Jumatano (Septemba 30, 2020) Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Abdul-Razaq Badru alisema uamuzi huo unatokana na maombi ya wanafunzi, wazazi na walezi ambao hawakuweza kuomba au kukamilisha maombi yao kutokana na sababu ya kujiunga na mafunzo hayo.

Kwa mujibu wa Badru alisema katika muda huo wa siku tano, mfumo pia utakuwa wazi ili kuwawezesha waombaji ambao maombi yao yana upungufu kurekebisha kwa kuweka nyaraka sahihi ili kuiwezesha HESLB kuendelea na hatua nyingine.

"Kwa wanaorekebisha taarifa, wanapaswa kuingia katika akaunti zao walizofungua kuombea mkopo na watapata ujumbe kuhusu maeneo ya kurekebisha. Tunawasihi watumie muda huu wa siku tano kurekebisha na kukamilisha maombi yao'' alisema Badru.

Katika mwaka wa masomo 2020/2021, Serikali imetenga TZS Bilioni 464 zitakazowanufaisha jumla ya wanafunzi 145,000. Kati yao, wanafunzi 54,000 watakuwa wa mwaka wa kwanza na wengine 91,000 ni wanafunzi wanufaika wanaoendelea na masomo. Mwaka 2019/2020 jumla ya TZS 450 bilioni zilitengwa na zimewanufaisha jumla ya wanafunzi 132,119.

MWISHO



Source

Watuhumiwa 4 wa mauaji ya kada wa CCM Njombe,waidhinishiwa mashtaka ya mauaji ya kukusudia


Na Amiri Kilagalila, Njombe.

Ofisi ya taifa ya Mashtaka imewaidhinishia mashtaka ya mauaji ya kukusudia watuhumiwa wanne wa mauaji ya kada wa Chama cha Mapinduzi na kiongozi wa wanafunzi wa vyuo na vyuo vikuu mkoa wa Iringa Emmanuel Mlelwa aliyeuawa mkoani Njombe.




 

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...