Wednesday, September 30, 2020

Barabara za juu kutoka Mwenge kwenda Buguruni katika makutano za barabara ya morogoro,Nelson Mandela na Sam Nujoma zaanza kutumika rasmi leo

Barabara za juu kutoka Mwenge kwenda Buguruni katika makutano za barabara ya morogoro,Nelson Mandela na Sam Nujoma zaanza kutumika rasmi leo( Picha- MAELEZO)


 


Shauri la Muungano latolewa ufafanuzi

 


Wakili Mkuu wa Serikali Gabriel Malata amesema kuwa Mahakama ya Afrika Mashariki haina mamlaka kisheria kusikiliza hoja za kupinga uwepo wa Taifa la Tanzania lililotokana na Muungano wa Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar. 


Wakili Malata amesema hayo leo wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu usikilizwaji na uamuzi wa shauri namba 09/2016 katika Mahakama ya Haki ya Afrika Mashariki baina ya Rashid Salum na wenzake 39,999 dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Katibu Mkuu Kiongozi wa Baraza la Mapinduzi la Zanzibar na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyosikilizwa jana Septemba 29, 2020.


Wakili Malata amesema kuwa Mahakama ilikubaliana na hoja hizo ambazo kwa mujibu wa mkataba wa uanzishwaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Tanganyika na Zanzibar sio nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki bali mwanachama wa jumuiya hiyo ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Mnamo Novemba 2, 2016 Rashid Suleiman Adily na wenzake 39,999 walikwenda Mahakama ya Haki ya Afrika Mashariki na kufungua shauri namba 09 ya mwaka 2016 dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Katibu Mkuu kiongozi wa Baraza la Mapinduzi la Zanzibar na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Huyu Hapa Director wa Video WCB Wasafi Kenny na Mkewe...Wapata Mtoto


Huyu Hapa Director wa Video WCB Wasafi Kenny na Mkewe...Wapata Mtoto

Director Kenny ndio anahusika na Video zote za Wasafi ..Mwaka Jana Alipata tuzo ya Muongozaji bora wa Video Afrimma

Marekani Yampa Shavu Mondi



HUJATAJWAhata na mkuu wa mkoa, msanii unavimba kichwa! Sikia hii: "Serikali ya Marekani yampa shavu msanii Diamond au muite Nasibu Abdul a.k.a Mondi.


Kapu la stori za sanaa mwishoni mwa wiki iliyopita, lilijaa ishu kubwa ambayo Risasi liliinyaka kwamba, baada ya Diamond kufanya kolabo ya heshima na msanii wa Marekani, Alicia Augello Cook 'Alicia Keys', ubalozi wa nchi hiyo Bongo, umetoa shavu kwa Mondi kwa kuandika katika ukurasa wake wa Twitter: "Great to see American artist @aliciakeyscollaborate w/Tanzanian artist @DiamondPlatnumz."



 

Ambapo kwa Kiswahili ubalozi huo uliandika: "Inafurahisha kuona msanii @aliciakeys akimshirikisha msanii wa Kitanzania, @diamondplatnumz."


Jicho la mwandishi limebaini kuwa 'Twiti' hiyo ya ubalozi wa Marekani nchini, unaoongozwa na balozi Donald Wright, ni ya kipekee kwa Mondi na kwamba inawasha taa ya kijani kwa msanii huyo kutamba kimataifa.


CHANZO CHA PONGEZI NI HIKI


Chanzo cha pongezi za Marekani kwa Mondi, ni baada ya msanii huyo wa Bongo kushirikishwa na staa huyo wa muziki wa Marekani katika wimbo wake wa Wasted Energy, ambao unapatikana katika Albam mpya ya Alicia Keys iitwayo Alicia, ambayo aliifyatua Ijumaa, Septemba 18, mwaka huu.


Katika wimbo huo wa Wasted Energy, mtoto wa Tandale alitupia mashairi yake kwa Lugha ya Kiswahili, jambo ambalo wengi wamempongeza kwa kusema ameijenga heshima ya Tanzania kimataifa.


Kionjo cha mistari ambayo Mondi alimuonjesha msanii huyo wa kike mwenye mvuto wa Marekani, ni:"Kwa nini penzi umelikata miguu,Unalibidua mara chini mara juu?Why? (Kwa nini?)Why? (Kwa nini?)Moyo unaumia, Moyo unaumia Moyo unaumia kwa nini unaugeuza nguo karaha?


Eti karaha, oh-oh," yaani kama hivyo tu mzee baba; huku Alicia Keys yeye akitiririka sehemu ya mashairi yake kama ifuatavyo:


"Too many times, you turned a blind eye to the way I feel Oh, you're the reason why I'm numb And when I try to give you my time, it's never, ever ideal Had to learn it the hard way, oh yeah," akimaanisha hivi kwa tafsiri isiyo rasmi ya Kiswahili:


"Mara nyingi sana, ulifumbia macho jinsi ninavyohisi Ah, wewe ndio sababu nimeshikwa na ganzi,Na ninapojaribu kukupa wakati wangu, sio bora kabisa, Ilibidi nijifunze kwa njia ngumu, oh ndio."


FAIDA KWA MONDI KWA KUTAJWA NA MAREKANI


Macho ya watazama mambo ya muziki kwa kina, yanaona kwamba kitendo cha Mondi kushirikishwa na Alicia Keys na kupewa heshima na ubalozi wa Marekani, kitamfanya msanii huyo kujulikana zaidi kimataifa, jambo ambalo lina faida kubwa kwake.


"Naona muziki wetu unakua sasa, kama wasanii wa Marekani wanaomba kolabo na sisi, hii ni hatua kubwa, hongera Diamond."


"Mzee jiandae kwa shoo za kufa mtu baada ya Corona kuisha.""Hii ni level nyingine kabisa ya Diamond, ila kuna wengine bado wanamchukulia poa, wakati dogo (Mondi) kapasua anga za Trump (Donald, rais wa Marekani).Hizo ni baadhi ya komenti ambazo zilitupia kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kusherehesha kile alichoki-skoo kibabe mtoto wa Tandale.


REKODI TATU ZA KIPEKEE


Uchunguzi unaonesha kuwa, tukio la Mondi kushirikishwa na staa huyo wa Marekani, kumemfanya msanii huyo kuweka rekodi tatu kibabe.


Rekodi ya kwanza aliyoweka Mondi ni kwamba, anakuwa msanii wa kwanza Bongo kuombwa, rudia tena "kuombwa", siyo kuomba kolabo kwa msanii huyo mkubwa; kama ambavyo wasanii wengine huwa wanafanya; usichanganye madawa.


Nyingine ya ajabu ambayo ameiweka Mondi ni ile ya msanii kutoka Bongo kufanya kolabo hiyo na msanii nyota wa Marekani na wimbo wake kuingizwa kwenye nyimbo zinazokamilisha Albam kwa Bongo haijapata kutokea.Rekodi ya tatu ni kitendo cha ubalozi wa nchi kubwa kama Marekani kupongeza ushirikiano wa msanii wa nchi yake kufanya kolabo na msanii wa Bongo.


ALICIA KEYS ALIVYOANZA KUMZIMIA MONDI


Mapema wiki hii, Keys alitupia orodha ya nyimbo anazopenda kuzisikiliza ukiwemoNana ambao Mondi amemshirikisha staa wa Nigeria, Mr Flavour.


Kama hiyo haitoshi, alisikiliza pia Wimbo wa African Beauty ambao Mondi amemshirikisha staa wa Marekani, Omarion, hiyo ni kuonesha kuwa msanii huyo wa Marekani alianza kumkubali Mondi kitambo.


Kama hilo alitoshi mapema mwaka huu, mume wa Alicia Keys, Beatz naye aliposti wimbo wa Gere wa Mondi alioshirikishwa na aliyekuwa mwandani wake, Tanasha Donna ambapo alisema anatamani kuufanyia remix wimbo huo.


ALICIA KEYS NI NANI?


Alicia Keys ni mrembo, staa wa muziki wa R&B kutoka pande za Marekani, ambaye ana umri wa miaka 39. Amesumbua na ngoma zake kali ikiwemo No One ambayo ilikamata namba moja katika chati za Hot 100.


Wimbo huo ulikuwa kwenye Albam yake iliyofahamika kwa jina la As I Am, ambayo iliitoa mwaka 2007 na kusimama namba moja kwenye Billboard 200 nchini humo na kuuza kopi 742,000 kwa wiki ya kwanza.Hii ina maana kwamba, Alicia Keys siyo msanii wa kispotispoti ukilinganisha na wasanii wa Bongo.


NI SOMO KWA HARMO, KIBA NA ZUCHU


Katika kitu ambacho kinaonesha kuwa Wabongo wamekuwa na kiu ya kuona vitu vyao vinapenya kimataifa, waliwatolea mwito wasanii wengine kama Ali Kiba, Zuhura Othman 'Zuchu' na Rajab Abdul Kahali 'Harmonize' nao kuzidi kukaza buti, ili nao wapenye zaidi kimataifa.


"Umefika muda wa kuelewana, Wabongo tuzidi kuongeza sauti kwenye vitu vyetu, iwe michezo, sanaa na mambo mengine, ili tutoke kimataifa."


"Kazi kwenu wasanii wengine Bongo, mkichukulia ishu ya Mondi kichawi mtaishia kununa, lakini mkiichukulia positive, mtakaza buti ili nanyi mpite njia anayotoboa Diamond."


Baadhi ya komenti zilizotupiwa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kuhusu ishu ya Mondi na pongezi za ubalozi wa Marekani.



Mambo muhimu mnayopaswa kufanya ili kuyafurahia mahusiano yenu


Mahusiano ya mwanaume na mwanamke hukutanisha watu kutoka koo mbalimbali. Kila mtu anakuwa amelelewa tofauti kwa wazazi wake.  Tabia haziwezi kufanana. Huyu anaweza kuwa na tabia fulani ambayo mwenzake anakuwa hana. Mnapokutana wawili, ili muweze kwenda sawa ni lazima muelewane tabia, mshibane na kila mmoja amvumilie mwenzake. Hakuna binadamu aliyekamilika. Inawezekana kuna vitu ambavyo mwenzako anavyo, na pengine si vizuri. Suala la msingi ni kupata muda sahihi wa kumbadilisha mwenzako ili naye aweze kukubaliana na mabadiliko unayotaka kumpa, na mwisho wa siku mtakwenda sawa.

Unapomuelekeza mwenzako juu ya tabia fulani, unapaswa kutumia lugha rafiki; lugha ya mtu na mpenzi wake! Ambayo itamfanya asijisikie vibaya, akubaliane na kile kitu unachomueleza bila hata ya kuweka kipingamizi. Ukitumia lugha ya ukali, yenye kuonesha dharau na kuona anachokifanya ni cha kijinga, basi jua unakaribisha ugomvi. Utamfanya akuone unamdharau na mtu akishaona anadharaulika, hata kama kitu unachomueleza ni kizuri, anaweza kukipinga tu.

Inahitaji busara, hekima ya hali ya juu ili uweze kumkosoa mwenzi wako. Yawezekana kwa mazingira aliyolelewa, anachokifanya huamini ni sahihi lakini sasa amekuja kwako, mnaanzisha ulimwengu wenu, hivyo inahitajika akili ya ziada kuweza kumbadilisha. Tengeni muda mzuri wa kuelezana mambo mbalimbali ya kudumisha uhusiano wenu. Mzungumze na kusikilizana. Kila mmoja amueleze mwenzake kile anachoamini kinaweza kusaidia kustawi wa penzi lao, kwa kutumia lugha nzuri isiyokuwa na kebehi.

Mnapokuwa kwenye uhusiao, kwanza kila mmoja ajifunze namna ya kujipenda mwenyewe. Unapojua kujipenda mwenyewe na ukajua unahitaji nini ili kuipata furaha yako, basi ni rahisi sana kumtafutia mwenzako pia furaha unayoipata wewe. Usiwe na ubinafsi, furaha unayoipata wewe mpe na mwenzako. Unavyojijali, basi mjali na mwenzako. Kujipenda unavyojipenda basi kwa kiasi hichohicho mpende na mwenzi wako. Ukifanya hivyo, mwenzi wako naye hatakuwa na namna ya kufanya zaidi ya kukurejeshea upendo.Related image

Jifunze kuwa na imani na mwenzako. Unapomjengea mwenzako imani, inamfanya wakati mwingine ashindwe kufanya maovu. Unapomuamini, unamfanya mwenzako ajiheshimu, maana anajua unamuamini na akifanya lolote la kijinga, lazima nafsi yake itamsuta. Muamini mwenzi wako. Mtengenezee mazingira ya kumuamini ili na yeye pia akuamini. Msiishi kwa kufuatiliana, maana maisha  hayapo hivyo. Binadamu hawezi kuchungwa kama kondoo au mbuzi. Kubwa linalohitajika ni kujua thamani ya kuaminiana.

Anayekuamini anakujali, anayekujali atakulindia heshima. Hivyo, mkigundua hilo na mkaelekezana kiutu uzima, hakika mtaaminiana. Kila moja awe mkweli na mwaminifu. Ni ukweli pekee utakaowafanya muwe na furaha muda wote. Mkiwa waongowaongo, hamtadumu. Uongo una madhara. Ujanja ujanja ni tatizo katika uhusiano. Kuwa mwaminifu kwa mwenzako, naye pia awe mkweli na mwaminifu.

Kuweni nyinyi, tengenezeni maisha yenu. Msijilinganishe na mtu mwingine. Wekeni mikakati yenu na namna mnavyotaka kuishi, ishini maisha yenu. Mkiyafanya hayo yote, hakika penzi lenu litastawi na mtafurahia maisha ya uhusiano, uchumba na hata ndoa!


ASKOFU SANGU AOMBA MSAADA KUKARABATI KANISA KATOLIKI NGOKOLO NA MITAMBO YA REDIO FARAJA ILIYOATHIRIWA NA MVUA YENYE UPEPO


Kushoto ni Askofu wa Jimbo Katoliki la Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu,kulia ni muonekano wa sehemu ya kanisa iliyoathirika kwa kuangukiwa na mnara wa Redio Faraja

Na Simeo Makoba - Shinyanga
Askofu wa Jimbo Katoliki la Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu amewaomba wadau,waamini na watu wote wenye mapenzi mema kuguswa na kutoa michango mbalimbali ili kusaidia ukarabati wa miundombinu ya kanisa kuu la jimbo na Redio Faraja ambayo imeathiriwa na mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali.

Askofu Sangu ametoa ombi hilo katika kikao cha dharura ambacho kiliwahusisha Mapadre wa Parokia zote zilizopo katika manispaa ya Shinyanga,Viongozi wa Halmashauri ya walei kutoka kanisa kuu la Ngokolo pamoja na uongozi wa Redio Faraja Fm Stereo.

Askofu Sangu amebainisha kuwa,mvua kubwa iliyonyesha mjini Shinyanga jioni ya jana tarehe 28.09.2020 ambayo iliambatana na upepo mkali ilisababisha mnara unaotumika kurushia matangazo ya Redio Faraja Fm Stereo kuangukia kanisa na kusababisha uharibifu mkubwa wa sehemu ya kanisa na miundombinu ya Redio inayotumika kurushia matangazo.

Shinyanga limeguswa ikizingatiwa kuwa,kanisa kuu la Mama mwenye Huruma la Ngokolo ndiyo lililobeba sura ya jimbo halikadhalika Redio Faraja ndiyo chombo kikuu cha mawasialiano na uinjilishaji katika jimbo ambayo nayo miundombinu yake imeathiriwa.

Askofu Sangu amewaomba wadau wa Redio na Kanisa,Waamini na watu wote wenye mapenzi mema kuguswa na kutoa michango mbalimbali ili hatua za kufanya ukarabati wa kanisa na mitambo ya Redio iliyoathiriwa ziweze kuanza mara moja.

Ameelekeza michango yote iwekwe kwenye Akaunti maalum ya jimbo la Shinyanga Benki ya CRDB yenye namba 01J1058390001 (DIOCESE OF SHINYANGA) na kwa njia ya M-PESA kwa namba 0762444746 yenye jina la Liberatus Sangu.

Wakati huo huo, Askofu Sangu ameunda kamati maalum ambayo itashughulika na mchakato wote wa tathmini pamoja na kusimamia hatua zote za ukarabati wa kanisa na miundombinu ya Redio iliyoharibiwa,ambayo itaongozwa na Paroko wa Parokia ya Ngokolo Padre Aldof Makandagu.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mkurugenzi wa Idara ya mawasiliano wa jimbo la Shinyanga Padre Anatoly Salawa amesema hivi sasa wanaendelea na mchakato wa kurejesha matangazo ya Redio katika eneo la Shinyanga kwa kufunga Antena katika sehemu ya mnara iliyobakia ili kuwawezesha wananchi wa Shinyanga kufuatilia Matangazo ya Redio wakati hatua nyingine za kufanyia matengenezo miundombinu iliyoharibiwa zikiendelea.
Mhashamu Baba Askofu Liberatus Sangu akiwa katika eneo la tukio wakati wa zoezi la kuondoa mnara juu ya paa la kanisa la Mama Mwenye Huruma Ngokolo. Picha na Samir Salum
Mhashamu Baba Askofu Liberatus Sangu akiwa katika eneo la tukio wakati wa zoezi la kuondoa mnara juu ya paa la kanisa la Mama Mwenye Huruma Ngokolo.

Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano Jimbo la Shinyanga, Padre Anatoly Salawa akionesha Mnara wa Matangazo ya Redio Faraja ulioangukia Kanisa la Mama Mwenye Huruma Ngokolo.

Muonekano wa mnara wa kurushia matangazo Redio Faraja Fm Stereo ukiwa umeangukia paa la Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga 
Muonekano wa mnara wa kurushia matangazo Redio Faraja Fm Stereo ukiwa umeangukia paa la Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga 
Muonekano wa sehemu ya ndani ya Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga baada ya kuangukiwa na Mnara wa Matangazo ya Radio Faraja Fm Stereo 
Muonekano wa sehemu ya ndani ya Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga baada ya kuangukiwa na Mnara wa Matangazo ya Radio Faraja Fm Stereo 
Muonekano wa sehemu ya ndani ya Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga baada ya kuangukiwa na Mnara wa Matangazo ya Radio Faraja Fm Stereo 
Muonekano wa sehemu ya ndani ya Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga baada ya kuangukiwa na Mnara wa Matangazo ya Radio Faraja Fm Stereo 
Muonekano wa mnara wa kurushia matangazo Redio Faraja Fm Stereo ukiwa umeangukia paa la Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga 
Muonekano wa mnara wa kurushia matangazo Redio Faraja Fm Stereo ukiwa umeangukia paa la Kanisa Katoliki la Mama Mwenye Huruma Parokia ya Ngokolo Mjini Shinyanga.

Tuesday, September 29, 2020

Mbaroni Kwa Kumbaka Mwanae Wa Kumzaa Shinyanga

SALVATORY NTANDU, SHINYANGA
Jeshi la Polisi mkoa wa Shinyanga linamshikilia mkazi wa Mtaa wa Kambarage Manspaa ya Shinyanga Petro Maro (43) kwa tuhuma ya Kumbaka mtoto wake wa kumzaa mwenye umri wa miaka 13 Mwanafunzi wa Darasa la Saba.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari Leo Septemba 29,2020 na Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba amesema kuwa Petro alitekeleza tukio hilo Septemba 27 majira ya usiku nyumbani kwake.

Alisema kuwa Mama Msamaria mwema anayeishi jirani na Petro aligundua  binti huyo kubakwa na baba yake Mzazi na kisha kutoa taarifa kwa jeshi la polisi ambao walifika na kisha kumkamata.

"Binti huyu alibakwa na baba yake usiku akiwa amelala na chanzo cha tukio hilo ni tamaa za kingono baada ya kutengana na Mke wake hali iyosababisha kuendelea kuishi na mwanae wa kike nyumba mmoja," alisema Magiligimba.

Kamanda Magiligimba alitoa wito wananchi mkoani humo kuendelea kutoa taarifa kwa jeshi la polisi ili kukomesha matukio na vitendo vya ukatili dhidi ya watoto mkoani humo.

Aliongeza kuwa hatua Kali za kisheria zitachukuliwa kwa mtuhumiwa huyo na upelelezi ukikamilika atafikishwa Mahakamani kujibu tuhuma inayomkabili.

Mwisho.



Source

Mke wa King Kiki awaonya wanaojidai wasemaji wa familia



COSTANSIA Kalanda ambaye ni mke wa msanii muziki wa dansi nchini Tanzania, King Kiki, amefunguka kuhusu kuumwa kwa mumewe huyo huku akiwaonya wanaochukuwa jukumu la kuzungumzia afya ya mumewe.


King Kiki ni mmiliki wa bendi ya La Capital, inayotesa na mtindo wake wa Kitambaa Cheupe.


Habari za kuumwa kwa King Kiki zilizagaa wiki iliyopita  zikimuonyesha akiwa katika picha na familia yake kitandani  wakimpa msaada wa kukaa.



 

Taarifa hizo zilisema "Anaumwa yuko kitandani mwanamuziki nguli  anahitaji msaada wa hali na mali. Alikuwa anaumwa mgongo na baadae kupooza alilazwa Muhimbili gharama zikawa kubwa sasa uanugulia nyumbani kwake,".


Akizungumzia jambo hilo, mke wa msanii huyo Costansia, amesema taarifa za kuwa mume wake anaumwa ni za kweli japokuwa amekanusha kuwa familia haijashindwa kumuhudumia kimatibabu.


"Ni kweli King Kiki anaumwa, lakini taarifa kuwa ametoka hospitali kwa kushindwa kumudu gharama za matibabu hazina ukweli wowote kwani familia tupo tunamuhudumia,"amesema.


Akizungumzia kuhusu ugonjwa unamsumbua, Costansia amesema alipata tatizo la uti wa mgongo kama mwezi mmoja uliopita na kufanyiwa upasuaji wa pingili za shingo wiki mbili zilizopita.


Amesema kutokana na upasuaji huo alijikuta akishindwa kunyanyuka na kukaa mwenyewe kutokana na madhara aliyopata wakati wa kuwekewa ganzi.


"Madaktari wametumbia kwa kuwa kutokana na King Kiki kuwa mtu mtu mzima ilibidi wampige ganzi ile ya kuuwa mwili mzima wakati wa kumfanyia upasuaji.


"Ni kutokana na hilo walisema ingemchukua takribani wiki mbili kurudi katika hali yake ya kawaida na mpaka tunafika leo wiki mbili hizo tayari zimefika, hapa tunafanya utaratibu kesho tumrudishe hospitali kwa uchunguzi zaidi," amesema Costansia.


Hata hivyo amewaonya watu wanajitwika usemaji wa familia kwa kumzungumzia msanii huyo  na kusema kwamba wanaopaswa kufanya hivyo ni yeye na mtoto wake mkubwa wa kiume.


Pia aliwaondoa hofu mashabiki wa msanii huyo na kueleza kuwa hayupo katika hali mbaya kihivyo kama inavyosemwa huku akiwaomba wamuombee  ili aweze kunyanyuka na kuendelea na kazi zake za sanaa.

Monday, September 28, 2020

KUTANA NA CHUCK FEENEY BILIONEA ALIYEGAWA MALI ZAKE ZOTE KWA WALIMWENGU


Chuck Feeney katikati amekuwa bilionea kwa muda wa miaka 40 iliyopita.
**
Charles "Chuck" Feeney ni bilionea ambaye alikuwa na ndoto za kumaliza mali yake yote akiwa hai, kwa kutoa fedha zake zote kwa mashirika ya hisani.

Mfanyabiashara huyo wa Marekani mwenye umri wa miaka 89 , hatimaye amefikia lengo lake siku chache ziliopita alipotoa dola ,milioni 8,000 kusimamia miradi ya hisani duniani.

Hivi sasa hana nyumba wala gari na ni maarufu kwa kuvalia saa iliyonunuliwa kwa dola 15 pekee.

''Nilikuwa na wazo ambalo halikuondoka katika fikra zangu , kwamba unapaswa kutumia mali yako kuwasaidia watu'', alisema mfanyabiashara huyo. Na kwa kipindi kirefu alichangisha fedha bila kujulikana.

Wakati mwandishi Gerardo Lissardy, kutoka BBC Mundo alipomuuliza 2017 kwanini alikuwa akifanya kuwa siri, alijibu, ''kwa sababu hakuna haja ya kuelezea watu kwanini unafanya hivyo''.

Kulingana na Conor O'Clery, aliyeandika kitabu kuhusu Feeney, anasema kwamba mtu huyo alipatiwa msukumo na kitabu cha 'Mali', kikijulikana, 'The Gospel of Wealth', kilichoandikwa na Andrew Carnegie.

Mishororo kama ''Kufa tajiri ni kufa kwa aibu'', iliwacha kovu katika fikra za Feeney. Alisafiri kote duniani kwa siri , akitafuta njia za kukamilisha kazi yake ndio maana aliitwa jina la Utani James Bond wa hisani.

Je Chuck Feeney ni nani? 

Charles F. Feeney alizaliwa mjini Elizabeth, New Jersey mwaka 1931. Mama yake alifanya kazi kama nesi katika hospitali huku baba yake akiwa wakala wa bima.

Akiwa kijana mdogo alionesha uwezo wake wa kufanya biashara.

Aliuza kadi za krisimamsi mlango hadi mlango akiwa na umri wa miaka 10. Akiwa kijana alisajiliwa katika jeshi na kushiriki katika vita vya Korea.
Chuck Feeney

Alitumia fursa ya mpango wa elimu wa Marekani kwa wakongwe na kuwa mtu wa kwanza wa familia yake kujiunga na chuo cha masomo.

Baada ya kuhitimu katika chuo kikuu cha Cornell University mjini New York , alianza biashara yake akiuza bidhaa kwa wanajeshi wa Marekani waliopo katika kambi barani Ulaya.

Biashara hiyo ilipiga hatua na kuwa maduka yasiotoza ushuru DFS kampuni ya mauzo isiotoza ushuru alioanzisha kwa pamoja na Robert Miller 1960.
Chuck Feeney alitoa fedha ya msaada Australia, Cuba na Ireland

''Mali inakuja na majukumu'' alikuwa akinukuliwa akisema.

''Sikufanya hivyo ili kuthibitisa chochote: Tajiri huyo aliyechangisha dola bilioni nane na kuwachwa na bila kitu.

''Watu wanapaswa kuchukua jukumu kutumia baadhi ya mali yao kuimarisha maisha ya wanadamu wenzao, la sivyo watajenga matatizo makubwa katika vizazi vya siku za baadaye''.

Kwa sasa anaishi katika nyumba ya vyumba viwili katika mji wa San Fransisco na mkewe Helga.

James Bond wa hisani
Mwaka 1982 alianzisha wakfu wa Atlantic Philanthropies Foundation , shirika la kimataifa kusambaza mali kwa miradi ya hisani duniani.

Katika kipindi cha miaka 15 ya kwanza, Feeney kisiri alichangisha fedha, na kumfanya kuitwa James Bond wa hisani, hadi alipojitokeza 1997.
Ufadhili umetajwa kubadili maisha ya wengi

Tangu alipoanzisha wakfu wa Atlatntic Phillanthropies, ametoa karibia dola bilioni nane kama misaada.

Wakfu huo umetangaza kwamba utasitisha operesheni zake siku ya mwisho ya mwaka wa 2020 baada ya lengo la Feeny kuafikiwa,

Filosofia yake ya kutoa wakati unapoishi imewapatia msukumo mabilionea wengi , ikiwemo mwanzilishi wa Microsoft Bill Gates na mwekezaji Warren Buffet.

Feeney hajulikana sana kama matajiri wengine kwasababu ya kutoa michango yake kisiri katika kipindi cha kwanza cha miaka 15 cha kazi yake.

CHANZO- BBC SWAHILI
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...