Wednesday, September 30, 2020
Barabara za juu kutoka Mwenge kwenda Buguruni katika makutano za barabara ya morogoro,Nelson Mandela na Sam Nujoma zaanza kutumika rasmi leo
Shauri la Muungano latolewa ufafanuzi
Wakili Mkuu wa Serikali Gabriel Malata amesema kuwa Mahakama ya Afrika Mashariki haina mamlaka kisheria kusikiliza hoja za kupinga uwepo wa Taifa la Tanzania lililotokana na Muungano wa Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.
Wakili Malata amesema hayo leo wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu usikilizwaji na uamuzi wa shauri namba 09/2016 katika Mahakama ya Haki ya Afrika Mashariki baina ya Rashid Salum na wenzake 39,999 dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Katibu Mkuu Kiongozi wa Baraza la Mapinduzi la Zanzibar na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyosikilizwa jana Septemba 29, 2020.
Wakili Malata amesema kuwa Mahakama ilikubaliana na hoja hizo ambazo kwa mujibu wa mkataba wa uanzishwaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Tanganyika na Zanzibar sio nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki bali mwanachama wa jumuiya hiyo ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mnamo Novemba 2, 2016 Rashid Suleiman Adily na wenzake 39,999 walikwenda Mahakama ya Haki ya Afrika Mashariki na kufungua shauri namba 09 ya mwaka 2016 dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Katibu Mkuu kiongozi wa Baraza la Mapinduzi la Zanzibar na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Huyu Hapa Director wa Video WCB Wasafi Kenny na Mkewe...Wapata Mtoto
Huyu Hapa Director wa Video WCB Wasafi Kenny na Mkewe...Wapata Mtoto
Director Kenny ndio anahusika na Video zote za Wasafi ..Mwaka Jana Alipata tuzo ya Muongozaji bora wa Video Afrimma
Marekani Yampa Shavu Mondi
HUJATAJWAhata na mkuu wa mkoa, msanii unavimba kichwa! Sikia hii: "Serikali ya Marekani yampa shavu msanii Diamond au muite Nasibu Abdul a.k.a Mondi.
Kapu la stori za sanaa mwishoni mwa wiki iliyopita, lilijaa ishu kubwa ambayo Risasi liliinyaka kwamba, baada ya Diamond kufanya kolabo ya heshima na msanii wa Marekani, Alicia Augello Cook 'Alicia Keys', ubalozi wa nchi hiyo Bongo, umetoa shavu kwa Mondi kwa kuandika katika ukurasa wake wa Twitter: "Great to see American artist @aliciakeyscollaborate w/Tanzanian artist @DiamondPlatnumz."
Ambapo kwa Kiswahili ubalozi huo uliandika: "Inafurahisha kuona msanii @aliciakeys akimshirikisha msanii wa Kitanzania, @diamondplatnumz."
Jicho la mwandishi limebaini kuwa 'Twiti' hiyo ya ubalozi wa Marekani nchini, unaoongozwa na balozi Donald Wright, ni ya kipekee kwa Mondi na kwamba inawasha taa ya kijani kwa msanii huyo kutamba kimataifa.
CHANZO CHA PONGEZI NI HIKI
Chanzo cha pongezi za Marekani kwa Mondi, ni baada ya msanii huyo wa Bongo kushirikishwa na staa huyo wa muziki wa Marekani katika wimbo wake wa Wasted Energy, ambao unapatikana katika Albam mpya ya Alicia Keys iitwayo Alicia, ambayo aliifyatua Ijumaa, Septemba 18, mwaka huu.
Katika wimbo huo wa Wasted Energy, mtoto wa Tandale alitupia mashairi yake kwa Lugha ya Kiswahili, jambo ambalo wengi wamempongeza kwa kusema ameijenga heshima ya Tanzania kimataifa.
Kionjo cha mistari ambayo Mondi alimuonjesha msanii huyo wa kike mwenye mvuto wa Marekani, ni:"Kwa nini penzi umelikata miguu,Unalibidua mara chini mara juu?Why? (Kwa nini?)Why? (Kwa nini?)Moyo unaumia, Moyo unaumia Moyo unaumia kwa nini unaugeuza nguo karaha?
Eti karaha, oh-oh," yaani kama hivyo tu mzee baba; huku Alicia Keys yeye akitiririka sehemu ya mashairi yake kama ifuatavyo:
"Too many times, you turned a blind eye to the way I feel Oh, you're the reason why I'm numb And when I try to give you my time, it's never, ever ideal Had to learn it the hard way, oh yeah," akimaanisha hivi kwa tafsiri isiyo rasmi ya Kiswahili:
"Mara nyingi sana, ulifumbia macho jinsi ninavyohisi Ah, wewe ndio sababu nimeshikwa na ganzi,Na ninapojaribu kukupa wakati wangu, sio bora kabisa, Ilibidi nijifunze kwa njia ngumu, oh ndio."
FAIDA KWA MONDI KWA KUTAJWA NA MAREKANI
Macho ya watazama mambo ya muziki kwa kina, yanaona kwamba kitendo cha Mondi kushirikishwa na Alicia Keys na kupewa heshima na ubalozi wa Marekani, kitamfanya msanii huyo kujulikana zaidi kimataifa, jambo ambalo lina faida kubwa kwake.
"Naona muziki wetu unakua sasa, kama wasanii wa Marekani wanaomba kolabo na sisi, hii ni hatua kubwa, hongera Diamond."
"Mzee jiandae kwa shoo za kufa mtu baada ya Corona kuisha.""Hii ni level nyingine kabisa ya Diamond, ila kuna wengine bado wanamchukulia poa, wakati dogo (Mondi) kapasua anga za Trump (Donald, rais wa Marekani).Hizo ni baadhi ya komenti ambazo zilitupia kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kusherehesha kile alichoki-skoo kibabe mtoto wa Tandale.
REKODI TATU ZA KIPEKEE
Uchunguzi unaonesha kuwa, tukio la Mondi kushirikishwa na staa huyo wa Marekani, kumemfanya msanii huyo kuweka rekodi tatu kibabe.
Rekodi ya kwanza aliyoweka Mondi ni kwamba, anakuwa msanii wa kwanza Bongo kuombwa, rudia tena "kuombwa", siyo kuomba kolabo kwa msanii huyo mkubwa; kama ambavyo wasanii wengine huwa wanafanya; usichanganye madawa.
Nyingine ya ajabu ambayo ameiweka Mondi ni ile ya msanii kutoka Bongo kufanya kolabo hiyo na msanii nyota wa Marekani na wimbo wake kuingizwa kwenye nyimbo zinazokamilisha Albam kwa Bongo haijapata kutokea.Rekodi ya tatu ni kitendo cha ubalozi wa nchi kubwa kama Marekani kupongeza ushirikiano wa msanii wa nchi yake kufanya kolabo na msanii wa Bongo.
ALICIA KEYS ALIVYOANZA KUMZIMIA MONDI
Mapema wiki hii, Keys alitupia orodha ya nyimbo anazopenda kuzisikiliza ukiwemoNana ambao Mondi amemshirikisha staa wa Nigeria, Mr Flavour.
Kama hiyo haitoshi, alisikiliza pia Wimbo wa African Beauty ambao Mondi amemshirikisha staa wa Marekani, Omarion, hiyo ni kuonesha kuwa msanii huyo wa Marekani alianza kumkubali Mondi kitambo.
Kama hilo alitoshi mapema mwaka huu, mume wa Alicia Keys, Beatz naye aliposti wimbo wa Gere wa Mondi alioshirikishwa na aliyekuwa mwandani wake, Tanasha Donna ambapo alisema anatamani kuufanyia remix wimbo huo.
ALICIA KEYS NI NANI?
Alicia Keys ni mrembo, staa wa muziki wa R&B kutoka pande za Marekani, ambaye ana umri wa miaka 39. Amesumbua na ngoma zake kali ikiwemo No One ambayo ilikamata namba moja katika chati za Hot 100.
Wimbo huo ulikuwa kwenye Albam yake iliyofahamika kwa jina la As I Am, ambayo iliitoa mwaka 2007 na kusimama namba moja kwenye Billboard 200 nchini humo na kuuza kopi 742,000 kwa wiki ya kwanza.Hii ina maana kwamba, Alicia Keys siyo msanii wa kispotispoti ukilinganisha na wasanii wa Bongo.
NI SOMO KWA HARMO, KIBA NA ZUCHU
Katika kitu ambacho kinaonesha kuwa Wabongo wamekuwa na kiu ya kuona vitu vyao vinapenya kimataifa, waliwatolea mwito wasanii wengine kama Ali Kiba, Zuhura Othman 'Zuchu' na Rajab Abdul Kahali 'Harmonize' nao kuzidi kukaza buti, ili nao wapenye zaidi kimataifa.
"Umefika muda wa kuelewana, Wabongo tuzidi kuongeza sauti kwenye vitu vyetu, iwe michezo, sanaa na mambo mengine, ili tutoke kimataifa."
"Kazi kwenu wasanii wengine Bongo, mkichukulia ishu ya Mondi kichawi mtaishia kununa, lakini mkiichukulia positive, mtakaza buti ili nanyi mpite njia anayotoboa Diamond."
Baadhi ya komenti zilizotupiwa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kuhusu ishu ya Mondi na pongezi za ubalozi wa Marekani.
Mambo muhimu mnayopaswa kufanya ili kuyafurahia mahusiano yenu
Mahusiano ya mwanaume na mwanamke hukutanisha watu kutoka koo mbalimbali. Kila mtu anakuwa amelelewa tofauti kwa wazazi wake. Tabia haziwezi kufanana. Huyu anaweza kuwa na tabia fulani ambayo mwenzake anakuwa hana. Mnapokutana wawili, ili muweze kwenda sawa ni lazima muelewane tabia, mshibane na kila mmoja amvumilie mwenzake. Hakuna binadamu aliyekamilika. Inawezekana kuna vitu ambavyo mwenzako anavyo, na pengine si vizuri. Suala la msingi ni kupata muda sahihi wa kumbadilisha mwenzako ili naye aweze kukubaliana na mabadiliko unayotaka kumpa, na mwisho wa siku mtakwenda sawa.
Unapomuelekeza mwenzako juu ya tabia fulani, unapaswa kutumia lugha rafiki; lugha ya mtu na mpenzi wake! Ambayo itamfanya asijisikie vibaya, akubaliane na kile kitu unachomueleza bila hata ya kuweka kipingamizi. Ukitumia lugha ya ukali, yenye kuonesha dharau na kuona anachokifanya ni cha kijinga, basi jua unakaribisha ugomvi. Utamfanya akuone unamdharau na mtu akishaona anadharaulika, hata kama kitu unachomueleza ni kizuri, anaweza kukipinga tu.
Inahitaji busara, hekima ya hali ya juu ili uweze kumkosoa mwenzi wako. Yawezekana kwa mazingira aliyolelewa, anachokifanya huamini ni sahihi lakini sasa amekuja kwako, mnaanzisha ulimwengu wenu, hivyo inahitajika akili ya ziada kuweza kumbadilisha. Tengeni muda mzuri wa kuelezana mambo mbalimbali ya kudumisha uhusiano wenu. Mzungumze na kusikilizana. Kila mmoja amueleze mwenzake kile anachoamini kinaweza kusaidia kustawi wa penzi lao, kwa kutumia lugha nzuri isiyokuwa na kebehi.
Mnapokuwa kwenye uhusiao, kwanza kila mmoja ajifunze namna ya kujipenda mwenyewe. Unapojua kujipenda mwenyewe na ukajua unahitaji nini ili kuipata furaha yako, basi ni rahisi sana kumtafutia mwenzako pia furaha unayoipata wewe. Usiwe na ubinafsi, furaha unayoipata wewe mpe na mwenzako. Unavyojijali, basi mjali na mwenzako. Kujipenda unavyojipenda basi kwa kiasi hichohicho mpende na mwenzi wako. Ukifanya hivyo, mwenzi wako naye hatakuwa na namna ya kufanya zaidi ya kukurejeshea upendo.Related image
Jifunze kuwa na imani na mwenzako. Unapomjengea mwenzako imani, inamfanya wakati mwingine ashindwe kufanya maovu. Unapomuamini, unamfanya mwenzako ajiheshimu, maana anajua unamuamini na akifanya lolote la kijinga, lazima nafsi yake itamsuta. Muamini mwenzi wako. Mtengenezee mazingira ya kumuamini ili na yeye pia akuamini. Msiishi kwa kufuatiliana, maana maisha hayapo hivyo. Binadamu hawezi kuchungwa kama kondoo au mbuzi. Kubwa linalohitajika ni kujua thamani ya kuaminiana.
Anayekuamini anakujali, anayekujali atakulindia heshima. Hivyo, mkigundua hilo na mkaelekezana kiutu uzima, hakika mtaaminiana. Kila moja awe mkweli na mwaminifu. Ni ukweli pekee utakaowafanya muwe na furaha muda wote. Mkiwa waongowaongo, hamtadumu. Uongo una madhara. Ujanja ujanja ni tatizo katika uhusiano. Kuwa mwaminifu kwa mwenzako, naye pia awe mkweli na mwaminifu.
Kuweni nyinyi, tengenezeni maisha yenu. Msijilinganishe na mtu mwingine. Wekeni mikakati yenu na namna mnavyotaka kuishi, ishini maisha yenu. Mkiyafanya hayo yote, hakika penzi lenu litastawi na mtafurahia maisha ya uhusiano, uchumba na hata ndoa!
ASKOFU SANGU AOMBA MSAADA KUKARABATI KANISA KATOLIKI NGOKOLO NA MITAMBO YA REDIO FARAJA ILIYOATHIRIWA NA MVUA YENYE UPEPO
Tuesday, September 29, 2020
Mbaroni Kwa Kumbaka Mwanae Wa Kumzaa Shinyanga
Jeshi la Polisi mkoa wa Shinyanga linamshikilia mkazi wa Mtaa wa Kambarage Manspaa ya Shinyanga Petro Maro (43) kwa tuhuma ya Kumbaka mtoto wake wa kumzaa mwenye umri wa miaka 13 Mwanafunzi wa Darasa la Saba.
Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari Leo Septemba 29,2020 na Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba amesema kuwa Petro alitekeleza tukio hilo Septemba 27 majira ya usiku nyumbani kwake.
Alisema kuwa Mama Msamaria mwema anayeishi jirani na Petro aligundua binti huyo kubakwa na baba yake Mzazi na kisha kutoa taarifa kwa jeshi la polisi ambao walifika na kisha kumkamata.
"Binti huyu alibakwa na baba yake usiku akiwa amelala na chanzo cha tukio hilo ni tamaa za kingono baada ya kutengana na Mke wake hali iyosababisha kuendelea kuishi na mwanae wa kike nyumba mmoja," alisema Magiligimba.
Kamanda Magiligimba alitoa wito wananchi mkoani humo kuendelea kutoa taarifa kwa jeshi la polisi ili kukomesha matukio na vitendo vya ukatili dhidi ya watoto mkoani humo.
Aliongeza kuwa hatua Kali za kisheria zitachukuliwa kwa mtuhumiwa huyo na upelelezi ukikamilika atafikishwa Mahakamani kujibu tuhuma inayomkabili.
Mwisho.
Source
Mke wa King Kiki awaonya wanaojidai wasemaji wa familia
COSTANSIA Kalanda ambaye ni mke wa msanii muziki wa dansi nchini Tanzania, King Kiki, amefunguka kuhusu kuumwa kwa mumewe huyo huku akiwaonya wanaochukuwa jukumu la kuzungumzia afya ya mumewe.
King Kiki ni mmiliki wa bendi ya La Capital, inayotesa na mtindo wake wa Kitambaa Cheupe.
Habari za kuumwa kwa King Kiki zilizagaa wiki iliyopita zikimuonyesha akiwa katika picha na familia yake kitandani wakimpa msaada wa kukaa.
Taarifa hizo zilisema "Anaumwa yuko kitandani mwanamuziki nguli anahitaji msaada wa hali na mali. Alikuwa anaumwa mgongo na baadae kupooza alilazwa Muhimbili gharama zikawa kubwa sasa uanugulia nyumbani kwake,".
Akizungumzia jambo hilo, mke wa msanii huyo Costansia, amesema taarifa za kuwa mume wake anaumwa ni za kweli japokuwa amekanusha kuwa familia haijashindwa kumuhudumia kimatibabu.
"Ni kweli King Kiki anaumwa, lakini taarifa kuwa ametoka hospitali kwa kushindwa kumudu gharama za matibabu hazina ukweli wowote kwani familia tupo tunamuhudumia,"amesema.
Akizungumzia kuhusu ugonjwa unamsumbua, Costansia amesema alipata tatizo la uti wa mgongo kama mwezi mmoja uliopita na kufanyiwa upasuaji wa pingili za shingo wiki mbili zilizopita.
Amesema kutokana na upasuaji huo alijikuta akishindwa kunyanyuka na kukaa mwenyewe kutokana na madhara aliyopata wakati wa kuwekewa ganzi.
"Madaktari wametumbia kwa kuwa kutokana na King Kiki kuwa mtu mtu mzima ilibidi wampige ganzi ile ya kuuwa mwili mzima wakati wa kumfanyia upasuaji.
"Ni kutokana na hilo walisema ingemchukua takribani wiki mbili kurudi katika hali yake ya kawaida na mpaka tunafika leo wiki mbili hizo tayari zimefika, hapa tunafanya utaratibu kesho tumrudishe hospitali kwa uchunguzi zaidi," amesema Costansia.
Hata hivyo amewaonya watu wanajitwika usemaji wa familia kwa kumzungumzia msanii huyo na kusema kwamba wanaopaswa kufanya hivyo ni yeye na mtoto wake mkubwa wa kiume.
Pia aliwaondoa hofu mashabiki wa msanii huyo na kueleza kuwa hayupo katika hali mbaya kihivyo kama inavyosemwa huku akiwaomba wamuombee ili aweze kunyanyuka na kuendelea na kazi zake za sanaa.
Monday, September 28, 2020
KUTANA NA CHUCK FEENEY BILIONEA ALIYEGAWA MALI ZAKE ZOTE KWA WALIMWENGU




-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Mara nyingi wanawake wamekuwa watu wa kukaa kimya bila kusema wanataka nini ili kuridhishwa katika mapenzi na mbaya zaidi katika swala zima ...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...










