SALVATORY NTANDU, SHINYANGA
Jeshi la Polisi mkoa wa Shinyanga linamshikilia mkazi wa Mtaa wa Kambarage Manspaa ya Shinyanga Petro Maro (43) kwa tuhuma ya Kumbaka mtoto wake wa kumzaa mwenye umri wa miaka 13 Mwanafunzi wa Darasa la Saba.
Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari Leo Septemba 29,2020 na Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba amesema kuwa Petro alitekeleza tukio hilo Septemba 27 majira ya usiku nyumbani kwake.
Alisema kuwa Mama Msamaria mwema anayeishi jirani na Petro aligundua binti huyo kubakwa na baba yake Mzazi na kisha kutoa taarifa kwa jeshi la polisi ambao walifika na kisha kumkamata.
"Binti huyu alibakwa na baba yake usiku akiwa amelala na chanzo cha tukio hilo ni tamaa za kingono baada ya kutengana na Mke wake hali iyosababisha kuendelea kuishi na mwanae wa kike nyumba mmoja," alisema Magiligimba.
Kamanda Magiligimba alitoa wito wananchi mkoani humo kuendelea kutoa taarifa kwa jeshi la polisi ili kukomesha matukio na vitendo vya ukatili dhidi ya watoto mkoani humo.
Aliongeza kuwa hatua Kali za kisheria zitachukuliwa kwa mtuhumiwa huyo na upelelezi ukikamilika atafikishwa Mahakamani kujibu tuhuma inayomkabili.
Mwisho.
Source
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala ndogo ya Dar es Salaam, imetupilia mbali shauri lililokuwa limefunguliwa na Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina...