Monday, September 28, 2020

KUTANA NA CHUCK FEENEY BILIONEA ALIYEGAWA MALI ZAKE ZOTE KWA WALIMWENGU


Chuck Feeney katikati amekuwa bilionea kwa muda wa miaka 40 iliyopita.
**
Charles "Chuck" Feeney ni bilionea ambaye alikuwa na ndoto za kumaliza mali yake yote akiwa hai, kwa kutoa fedha zake zote kwa mashirika ya hisani.

Mfanyabiashara huyo wa Marekani mwenye umri wa miaka 89 , hatimaye amefikia lengo lake siku chache ziliopita alipotoa dola ,milioni 8,000 kusimamia miradi ya hisani duniani.

Hivi sasa hana nyumba wala gari na ni maarufu kwa kuvalia saa iliyonunuliwa kwa dola 15 pekee.

''Nilikuwa na wazo ambalo halikuondoka katika fikra zangu , kwamba unapaswa kutumia mali yako kuwasaidia watu'', alisema mfanyabiashara huyo. Na kwa kipindi kirefu alichangisha fedha bila kujulikana.

Wakati mwandishi Gerardo Lissardy, kutoka BBC Mundo alipomuuliza 2017 kwanini alikuwa akifanya kuwa siri, alijibu, ''kwa sababu hakuna haja ya kuelezea watu kwanini unafanya hivyo''.

Kulingana na Conor O'Clery, aliyeandika kitabu kuhusu Feeney, anasema kwamba mtu huyo alipatiwa msukumo na kitabu cha 'Mali', kikijulikana, 'The Gospel of Wealth', kilichoandikwa na Andrew Carnegie.

Mishororo kama ''Kufa tajiri ni kufa kwa aibu'', iliwacha kovu katika fikra za Feeney. Alisafiri kote duniani kwa siri , akitafuta njia za kukamilisha kazi yake ndio maana aliitwa jina la Utani James Bond wa hisani.

Je Chuck Feeney ni nani? 

Charles F. Feeney alizaliwa mjini Elizabeth, New Jersey mwaka 1931. Mama yake alifanya kazi kama nesi katika hospitali huku baba yake akiwa wakala wa bima.

Akiwa kijana mdogo alionesha uwezo wake wa kufanya biashara.

Aliuza kadi za krisimamsi mlango hadi mlango akiwa na umri wa miaka 10. Akiwa kijana alisajiliwa katika jeshi na kushiriki katika vita vya Korea.
Chuck Feeney

Alitumia fursa ya mpango wa elimu wa Marekani kwa wakongwe na kuwa mtu wa kwanza wa familia yake kujiunga na chuo cha masomo.

Baada ya kuhitimu katika chuo kikuu cha Cornell University mjini New York , alianza biashara yake akiuza bidhaa kwa wanajeshi wa Marekani waliopo katika kambi barani Ulaya.

Biashara hiyo ilipiga hatua na kuwa maduka yasiotoza ushuru DFS kampuni ya mauzo isiotoza ushuru alioanzisha kwa pamoja na Robert Miller 1960.
Chuck Feeney alitoa fedha ya msaada Australia, Cuba na Ireland

''Mali inakuja na majukumu'' alikuwa akinukuliwa akisema.

''Sikufanya hivyo ili kuthibitisa chochote: Tajiri huyo aliyechangisha dola bilioni nane na kuwachwa na bila kitu.

''Watu wanapaswa kuchukua jukumu kutumia baadhi ya mali yao kuimarisha maisha ya wanadamu wenzao, la sivyo watajenga matatizo makubwa katika vizazi vya siku za baadaye''.

Kwa sasa anaishi katika nyumba ya vyumba viwili katika mji wa San Fransisco na mkewe Helga.

James Bond wa hisani
Mwaka 1982 alianzisha wakfu wa Atlantic Philanthropies Foundation , shirika la kimataifa kusambaza mali kwa miradi ya hisani duniani.

Katika kipindi cha miaka 15 ya kwanza, Feeney kisiri alichangisha fedha, na kumfanya kuitwa James Bond wa hisani, hadi alipojitokeza 1997.
Ufadhili umetajwa kubadili maisha ya wengi

Tangu alipoanzisha wakfu wa Atlatntic Phillanthropies, ametoa karibia dola bilioni nane kama misaada.

Wakfu huo umetangaza kwamba utasitisha operesheni zake siku ya mwisho ya mwaka wa 2020 baada ya lengo la Feeny kuafikiwa,

Filosofia yake ya kutoa wakati unapoishi imewapatia msukumo mabilionea wengi , ikiwemo mwanzilishi wa Microsoft Bill Gates na mwekezaji Warren Buffet.

Feeney hajulikana sana kama matajiri wengine kwasababu ya kutoa michango yake kisiri katika kipindi cha kwanza cha miaka 15 cha kazi yake.

CHANZO- BBC SWAHILI

Bodi ya ligi yaufungia uwanja wa Jamhuri Morogoro

 


Bodi ya ligi kuu Tanzania (TPLB) imeufungia uwanja wa mabatini unaotumiwa kwa michezo ya nyumbani na klabu ya Ruvu Shooting kwa kukosa sifa za kimashindano.



Wednesday, September 23, 2020

NITAKUWA KIUNGANISHI KATI NGO'S,BUNGE,SERIKALI NA WAFADHILI KULETA MAENDELEO ENDELEVU-NEEMA

Mbunge Mteule Viti Maalum Kundi la Asasi za kiraia Tanzania bara Neema Lugangira (kulia) akizungumza jambo na baadhi ya viongozi wa Mtandao wa Vikundi vya wakulima wadogo Tanzania (MVIWATA) alipotembelea ofisi hiyo.



MBUNGE Mteule Viti Maalum kundi la Asasi za kiraia Tanzania bara kwa tiketi ya CCM Neema Lugangira, amesema kuwa atakuwa kiunganishi kati ya Asasi za kiraia(NGO'S), bunge, serikali, wafadhili na chama ili kubadilishana mawazo katika kuleta maendeleo endelevu.

Neema ameyasema hayo wakati alipotembelea Mtandao wa Vikundi vya wakulima wadogo Tanzania (MVIWATA) mkoani Morogoro ili kujua changamoto zinazo wakabili na namna ya kuzitatua. 

Ameeleza kuwa kwa kuongea na wadau hao anapata fursa ya kupata mambo ya kujadili yaliyomo kwenye ilani ya CCM yanayohusiana na Asasi hizo na kuweza kubadilishana mawazo yatakayosaidia kwenye utekelezaji.

Akizungumzia maeneo yaliyoguswa na ilani ya CCM amesema lengo kubwa ni kuongeza tija katika kilimo ili kusaidia viwanda, kuimarisha miundo mbinu na uzalishaji, kumsaidia mkulima kuzalisha na kupata masoko, usimamizi wa mazao ya kimkakati, lishe na kuzijengea uwezo Asasi za ndani.

Naye Mkurugenzi wa MVIWATA Stephen Ruvuga akitoa shukrani zake kwa chama na serikali amesema kwa kitendo hicho cha kiongozi kuwatembelea na kujua changamoto zao wanatarajia kuwepo kwa maelewano mazuri kati ya serikali na Asasi hizo, hali itakayochochea maendeleo kwa haraka.

Mkongo Wa Taifa Wa Mawasiliano Waunganisha Visiwa Vya Pemba Na Unguja

Na Prisca Ulomi, WUUM, Zanzibar
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zimeweka saini ya mkataba wa makubaliano wa kuunganisha visiwa vya Pemba na Unguja na Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano na Mkongo wa Zanzibar

Utiaji saini huo umeshuhudiwa na katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Mawasiliano), Dkt. Zainabu Chaula wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Dkt. Mustafa Aboud Jumbe, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar

Utiaji saini huo umefanywa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Waziri Kindamba kwa upande wa Bara na Mhandisi Shukuru Awadh Slueiman, Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Miundombinu ya TEHAMA Zanzibar (ZICTIA) kwa upande wa Zanzibar

Kabla ya kushudia tukio hilo, Dkt. Zainabu Chaula alisema kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imejenga Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 700 na kuunganisha kwenye mikoa yote 26 ya Tanzania Bara na kwenye nchi jirani za Congo, Zambia, Rwanda, Burundi, Kenya, Uganda na Malawi ambapo maunganisho haya yanaenda kufungua fursa za wawekezaji na watumia wa huduma za mawasiliano wa ndani na nje ya nchi  kuunganishwa na Zanzibar kwa kuwa katika kipindi cha miaka mitano tumeshuhudia kuibuka kwa mifumo ya TEHAMA ambayo inawezesha utoaji wa huduma za mawasiliano kwa wananchi kwa kasi zaidi

Naye Dkt. Jumbe amesema kuwa haya ndio matunda ya mapinduzi, matunda ya mapinduzi sio maembe wala mapapai bali ni maendeleo yanayopatikana katika nchi yetu, na Serikali yetu ya SMZ imetumia zaidi ya shilingi bilioni 30 kuunganisha mikoa na wilaya zote za Unguja na Pemba bali kulikuwa na changamoto ya kuunganisha Unguja na Pemba ila sasa kwa kupitia makubaliano haya, tutatumia barabara ya Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano kuunganisha visiwa Pemba na Unguja na hivyo Zanzibar kuunganishwa na Tanzania Bara moja kwa moja na utawezesha kupunguza gharama za mawasiliano ili ziwe nafuu

Ndugu Kindamba amesema kuwa ufunguzi wa njia za mawasiliano ya Mkongo kati ya Tanzania Bara na Zanzibar utakuwa na manufaa makubwa sana kwa taifa hasa katika kuwezesha kuongezeka kwa matumizi ya data na intaneti na makubaliano hayo yanahusisha kutunza vifaa vya miundombinu ya TEHAMA vya ZICTIA kwenye majengo ya TTCL 

Mhandisi Suleimani ameongeza kuwa ZICTIA imekamilisha ujenzi wa Mkongo wa Zanzibar na sasa unaunganishwa na Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano ambapo itakuza na kuongeza huduma za mawasiliano; kuondoa changamoto iliyokuwepo Zanzibar ya kutumia njia ya mawasiliano ya mawimbi ya radio kutoa huduma za mawasiliano ambayo hayana kasi na ubora unaohitajika, kupunguza gharama za mawasiliano na kuingizia mapato kwa Serikali

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano


Bia iliyotengenezwa Kwa Kutumia Majitaka

Katika juhudi za kuongeza ufahamu juu ya uwezekano wa kuyabadilisha Majitaka kuwa maji salama kampuni moja inayozalisha bia jijini Stockholm nchini Swaeden imetengeneza bia iliyobatizwa jina la PU: REST kwa kutumia Majitaka yaliyotibiwa (recycled sewage water).

Kampuni hiyo ambayo katika uzalishaji wa bia hiyo wameshirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Mazingira nchini Sweden imedhamiria kupitia kinywaji hicho kuwashawishi wakazi wa nchi hiyo kuwa 'Maji taka yaliyotibiwa (recycled sewage water)' ni maji safi na salama kama yanayotoka kwenye mabomba.

Kwa mujibu wa Taasisi ya Utafiti wa Mazingira nchini Sweden wamesema kuwa changamoto ya watu kutoyaamini majitaka yaliyotibiwa sio ya kiufundi bali ni changamoto ya kisaikolojia na ndio maana wametengeneza bia ili kuwashawishi watu kuyatumia Majitaka yaliyotibiwa.

Kwa sasa PU:REST bia inapatikana pekee katika mgahawa wa New Camegie Brewery's jijini Stockholm na July 2 itauzwa kwenye migahawa na kwenye matamasha yote nchini Sweden.
Source

Kiongozi wa kijeshi wa Mali ashinikiza kuondolewa vikwazo


Kiongozi wa kijeshi nchini Mali, Kanali Assimi Goita ametaka taifa lake kuondolewa vikwazo vya kiuchumi, ambavyo vimewekwa baada ya mapinduzi ya mwezi uliopita katika taifa hilo masikini la Sahel.

 Akizungumza na waandishi wa habari katika maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru wa Mali hapo jana, Goita amesema uteuzi wa hivi karibuni wa rais wa mpito raia, unamaanisha kwamba viongozi wa mataifa ya Afrika Magharibi lazima wasitishe marufuku yao ya kufanya biashara na Mali. 

Jumuiya ya kiuchumi ya mataifa ya Afrika Magharibi yenye mataifa15 wanachama ECOWAS mpaka wakati huu haijasema lolote lakini Ufaransa, ambayo ina vikosi vyake kwa ajili ya kukabiliana na ugaidi nchini Mali, imeupokea vyema uteuzi wa waziri wa zamani wa ulinzi Bah Ndaw na viongozi wengine wa mpito kama hatua yenye kutia moyo. 

ECOWAS, iliifunga mipaka ya mataifa yake na Mali na kuweka vikwazo, baada ya jeshi la Mali Agosti 18, kumuondoa madarakani rais Boubacar Keita.

Majaliwa: Tarehe 28 Oktoba Siyo Siku Ya Mzaha

MJUMBE wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Kassim Majaliwa amemaliza ziara yake mkoa wa Mara na kuwaeleza wananchi kwamba tarehe 28 Oktoba, 2020 siyo siku ya mzaha.

"Tarehe 28 Oktoba, 2020 siyo siyo ya mzaha na wala siyo siku ya majaribio. Ni siku ya kuchagua Kiongozi atakayetufaa, na huyo si mwingine bali Dkt. John Pombe Magufuli, " amesema.

Ametoa kauli hiyo jana mchana (Jumanne, Septemba 22, 2020) wakati akizungumza na wakazi wa Kibara, wilayani Bunda, mkoani Mara kwenye mkutano wa kuwanadi wagombea wa CCM uliofanyika katika uwanja wa michezo wa Kibara.

Amesema kiongozi wa nchi anayefaa kuchaguliwa ni yule anayeweza kusimamia rasilmali za Taifa. "Ni yule anayeweza kusimamia tunu za Taifa... siyo mnapata kiongozi halafu akipewa nchi anabadilisha hadi wimbo wa Taifa."

"Tunahitaji kiongozi anayeweza kupambana na rushwa, awe mtu wa kutetea watu wake wapate haki bila kuombwa rushwa. Huyo si mwingine bali ni Dkt. John Pombe Magufuli," amesema. 

Mheshimiwa Majaliwa ambaye alikuwa mkoani Mara kumuombea kura mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dkt. John Pombe Magufuli alitumia fursa hiyo kuwaombea kura mgombea ubunge wa jimbo la kuwaombea kura Charles Kajege na diwani wa Kibara, Bw. Nyanguli Mtesigwa na madiwani wengine wa jimbo hilo. Jioni hii anaingia mkoa wa Mwanza.

Akielezea umuhimu wa chama kuwa na Ilani ya Uchaguzi, Mheshimiwa Majaliwa amesema Chama cha Mapinduzi kimeandaa ilani yake yenye kurasa 303 ikisimamia yale yaliyokuwemo kwenye ilani iliyopita ambayo ilikuwa na kurasa 236 na mengine mengi mapya. 

"Watekelezaji wa hayo yote yaliyoainishwa kwenye Ilani ni hawa watatu ambao nawaombea kura leo. Namwombea kura Dkt. Magufuli ili akamilishe aliyoyaanza na atekeleze yaliyomo kwenye Ilani ya sasa. Ni lazima tumpatie mbunge na diwani wa CCM ili waweze kuzungumza lugha moja."

Kuhusu uboreshaji kwenye sekta ya afya, Mheshimiwa Majaliwa alisema zilitumika sh. bilioni 1.8 za kujenga hospitali ya wilaya hiyo na bado kuna sh. milioni 152 zilitolewa ili kuisaidia Halmashauri kujenga zahanati.

Kuhusu sekta ya maji, Mheshimiwa Majaliwa amesema sh. bilioni 6.2 zimetumika kukarabati na ujenzi wa miradi mbalimbali kwenye Halmashauri ya wilayani Bunda, ikiwemo uchimbaji wa visima virefu na vifupi, utengenezaji wa matenki ya kuvuna maji na uchimbaji wa mabwawa. 
"Vijiji vilivyonufaika na miradi hii ni Nyatwali, Nyamuswa, Mgeta –Nyang'aranga, kinyabwiga, Bulamba na Kibara. Pia jumla ya shilingi milioni 90.1 zimetumika kwa ajili ya ukarabati na usafishaji wa pampu za mkono 67 na visima vitatu," amesema.

Mapema asubuhi, akiwa kata ya Kisorya, Mheshimiwa Majaliwa aliwaeleza wananchi hao kwamba Serikali ya CCM ina mpango wa kuboresha kituo chao cha afya kwa kuongeza wodi tatu za wanawake, wanaume na watoto.

Pia alisema zimetengwa sh. milioni 550 za kuimarisha kituo hicho kwa kuongeza majengo ya jiko, chumba cha kufulia na chumba cha kuhifadhia maiti.

Kuhusu barabara, amesema kiasi cha sh. bilioni 2.9 kimetumika kutengeneza barabara za kuunganisha vijiji kwa vijiji, kukarabati sehemu korofi zilizoharibiwa na mafuriko, madaraja, makalvati na matengenezo ya kawaida.

Kuhusu umeme, amesema vijiji 77 kati ya 78 vina umeme isipokuwa kijiji kimoja tu cha Nafubu kilichopo kisiwani, ambacho amesema watapelekewa huduma ya umeme wa jua kwa vile siyo rahisi kupitisha nyaya za umeme majini.

(mwisho) 


Tuesday, September 22, 2020

AKINA MAMA MKOANI MWANZA WAPEWA ELIMU YA MTOTO


Wanawake wakinyonyesha watoto wao wakati wa mafunzo ya unyonyeshaji na makuzi kwa watoto wenye umri chini ya miezi sita yaliyoandaliwa na mradi wa USAID Tulonge afya katika  halmashauri ya Nyamagana jijini Mwanza jana.

****
Iwapo mama ataanza kumpatia vyakula mtoto ambaye hajafikisha miezi sita anaweza kumsababishia magonjwa mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuharibu mfumo mzima wa makuzi yake hivyo ni vyema kuzingatia maelekezo na makuzi ya mtoto.

Pia, watoto wanapoumwa au kuonyesha dalili za kuumwa wazazi wanapaswa kuwakimbiza hospitalini badala ya kwenda kwa waganga wa kienyeji ambao huweza kuharibu mfumo wa makuzi yao.

Hayo yamebainishwa na wataalaamu wakati wa kongamano la afya ya mama na mtoto lilioandaliwa na Mradi wa Usaid Tulonge Afya kwa ajili ya kuwapatia elimu makuzi ya watoto wanawake wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza jana.

Mratibu wa Afya ya Uzazi na Mtoto wa Halmashauri ya jiji la Mwanza, Bertha Yohana alisema kumekuwapo na changamoto ya afya ya makuzi ya watoto kutokana na mila, tabia na desturi za jamii kushindwa kuzingatia maelekezo ya wataalamu.

"Tumekuwa na tabia kwenye jamii wanafundishana wao kwa wao, wapo wanaoamini kwamba mtoto akinyonya maziwa ya amma pekee hashibi, jambo hili sio kweli, mtoto anaweza kunyonya maziwa ya mama akashiba bila kula chakula kingine mpaka afikishe miezi sita," alisema

Alisema wakati mwanamke anapokuwa ananyonyesha mtoto mchanga anatakiwa asiwe na msongo wa mawazo, ale ashibe ili aweze kuzalisha maziwa ya kutosha.

Naye mhudumu ngazi ya jamii kata ya Mhandu, Rachael Mahulu alisema hakuna budi jamii ikaondokana na mila potofu za kuataka kuwalisha watoto wadogo vyakula na dawa kwa misingi ya kuwakuza kumbe kufanya hivyo wanawaharibu.

"mtoto akiota meno haya yanaitwa ya plstikli, wengi wnawakimbiza kwa waganaga na kuwapaka dawa kienyeji, kufanmya hivi ni kosa nenda hospitali utapewa mwongozo," alisema

Alisema iwapo mama akimnyonyesha mtoto wake mara kwa mara anamjengea uhusiano mzuri kati yake na yeye katika makuzi.

Naye Ofisa Uwanda (field officer), kutoka mradi wa USAID Tulonge afya wilaya ya Nyamgana, Esuphvat Lewis, alisema katika kongamano hilo wamefundisha tabia nne za kiafya katika makuzi ya mtoto ambayo ni pamoja na unyonyeshaji wa maziwa kwa kipindi cha miezi sita.

Zingine ni kuhakikisha mama analala na mtoto kwenye chandarua kimoja angalau mpaka afikishe miezi tisa, mama akiona dalili zozote hatarishi ampeleke mtoto hospitalini na njia za uzazi wa mpango baada ya mtoto kufikisha miezi 24.

Alisema katika mafunzo hayo jumla ya wanawke 50 wameshiriki kutoka kata za wilaya ya Nyamagana.

Nao baadhi ya wanawake walioshiriki mafunzo hayo, Tatu Ramadhani na Ester Suleiman kwa nyakati tofauti walisema mafunzo hayo yameweza kuwafungua na kutambua mambo muhimu katika makuzi ya mtoto ambayo walikuwa hawayajui awali..

"Nimejifunza unyonyeshaji wa mtoto na jinsi ya kumlinda na malaria, kiukweli kuna changmoto kubwa wanawake wengi wnashauriana kuwapa watoto uji hasa wa udaga kumbe unaweza kumsbaishia matatizo makubwa," alisema Tatu mkazi wa Igoma.

Mradi huu ambao unafahamika kama Mothers Meets Up events unafanyika kati ya wilaya 27 za Tanzania ambapo kupitia majukwaa ya watu wazima ya Naweza chini ya mradi wa Tulonge afya Tanzania kwa lengo la kuhamasisha huduma bora za afya kwa ngazi ya familia na jamii kwa kuondoa Mila pitiful na kuwapata mbinu za kiafya kujikinga na maradhi kama ukimwi , malaria, uzazi wa mpango na afya ya uzazi pamoja na ugonjwa wa kifua kikuu.
 Wanawake wakibeba watoto wao wakati wa mafunzo ya unyonyeshaji na makuzi kwa watoto wenye umri chini ya miezi sita yaliyoandaliwa na mradi wa USAID Tulonge afya katika  halmashauri ya Nyamagana jijini Mwanza jana.

 Wanawake wakicheza wakati wa mafunzo ya unyonyeshaji na makuzi kwa watoto wenye umri chini ya miezi sita yaliyoandaliwa na mradi wa USAID Tulonge afya katika  halmashauri ya Nyamagana jijini Mwanza jana. 


Friday, September 18, 2020

RC KUNENGE AMTAKA MKANDARASI WA UJENZI WA BARABARA YA TEGETA NYUKI KUKAMILISHA UJEZI IFIKAPO MWEZI OKTOBA, "AKIKAIDI PATACHIMBIKA"


Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh. Aboubakar Kunenge
Na Azmala Said - Dar es salaam 
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh. Aboubakar Kunenge ametoa mwezi mmoja kwa mkandarasi anayetekeleza mradi wa Ujenzi wa barabaara ya Tegeta Nyuki yenye urefu wa Kilometa 1.06 kuhakikisha anakamilisha kwa wakati  na kueleza kuwa endapo atashindwa kutekeleza agizo hilo atachukuliwa hatua za kisheria.

RC Kunenge ametoa maagizo hayo wakati Wa ziara ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo ambapo amesema mkandarasi huyo wa Kampuni ya CMG Construction amekuwa akisuasua kumaliza mradi licha ya kuongezewa muda ambapo amewaelekeza TARURA kumsimamia ipasavyo Mkandarasi huyo.

Aidha RC Kunenge pia ametembelea na kukagua Mradi wa ujenzi wa Stand Mpya ya kisasa Mbezi Louis ambayo ujenzi wake umefika 80% na inagharimu Kiasi cha Shilingi Bilioni 56 ambapo ameonyesha kuridhishwa na hatua ya ujenzi ilipofikia.

Akiwa kwenye ukaguzi wa Barabara ya Madale - Wazo yenye urefu wa Km 6 inayogharimu kiasi cha Shilingi Bilioni 9.9, Kunenge amefurahishwa na juhudi za mkandarasi huyo huku akieleza kuwa barabara hiyo ikikamilika itakuwa "shortcut" nzuri ya kutoka Mbezi kupitia Madale hadi Wazo.

Katika ziara hiyo Kunenge pia ametembelea ujenzi wa Daraja la Ulongoni A lililopo Kata ya Gongolamboto ambalo ujenzi wake unagharimu Shilingi Bilioni 4.3 na Ujenzi wa Daraja la Ulongoni B ambapo amewahimiza wakandarasi kuongeza juhudi ili ujenzi ukamilike ndani ya Muda uliopangwa ili kupunguza kero walizokuwa wakizipata wananchi.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...