







MBUNGE Mteule Viti Maalum kundi la Asasi za kiraia Tanzania bara kwa tiketi ya CCM Neema Lugangira, amesema kuwa atakuwa kiunganishi kati ya Asasi za kiraia(NGO'S), bunge, serikali, wafadhili na chama ili kubadilishana mawazo katika kuleta maendeleo endelevu.
Neema ameyasema hayo wakati alipotembelea Mtandao wa Vikundi vya wakulima wadogo Tanzania (MVIWATA) mkoani Morogoro ili kujua changamoto zinazo wakabili na namna ya kuzitatua.
Ameeleza kuwa kwa kuongea na wadau hao anapata fursa ya kupata mambo ya kujadili yaliyomo kwenye ilani ya CCM yanayohusiana na Asasi hizo na kuweza kubadilishana mawazo yatakayosaidia kwenye utekelezaji.
Akizungumzia maeneo yaliyoguswa na ilani ya CCM amesema lengo kubwa ni kuongeza tija katika kilimo ili kusaidia viwanda, kuimarisha miundo mbinu na uzalishaji, kumsaidia mkulima kuzalisha na kupata masoko, usimamizi wa mazao ya kimkakati, lishe na kuzijengea uwezo Asasi za ndani.
Naye Mkurugenzi wa MVIWATA Stephen Ruvuga akitoa shukrani zake kwa chama na serikali amesema kwa kitendo hicho cha kiongozi kuwatembelea na kujua changamoto zao wanatarajia kuwepo kwa maelewano mazuri kati ya serikali na Asasi hizo, hali itakayochochea maendeleo kwa haraka.
Akizungumza na waandishi wa habari katika maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru wa Mali hapo jana, Goita amesema uteuzi wa hivi karibuni wa rais wa mpito raia, unamaanisha kwamba viongozi wa mataifa ya Afrika Magharibi lazima wasitishe marufuku yao ya kufanya biashara na Mali.
Jumuiya ya kiuchumi ya mataifa ya Afrika Magharibi yenye mataifa15 wanachama ECOWAS mpaka wakati huu haijasema lolote lakini Ufaransa, ambayo ina vikosi vyake kwa ajili ya kukabiliana na ugaidi nchini Mali, imeupokea vyema uteuzi wa waziri wa zamani wa ulinzi Bah Ndaw na viongozi wengine wa mpito kama hatua yenye kutia moyo.
ECOWAS, iliifunga mipaka ya mataifa yake na Mali na kuweka vikwazo, baada ya jeshi la Mali Agosti 18, kumuondoa madarakani rais Boubacar Keita.