Wednesday, April 30, 2025

WAKULIMA CHEKETU WALALAMIKIA UVAMIZI WA MIFUGO, WAILILIA SERIKALI KUTENGA MAENEO


Mwenyekiti wa Kijiji cha Cheketu Kata ya Somanga Hashimu Changajua akizungumza na Wananchi wa Kijiji hicho cha Cheketu kuhusu Sheria walizoziweka kati ya Wakulima na Wafugaji
Baadhi ya wananchi waliojitokeza katika Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Cheketu Kata ya Somanga Wilayani Kilwa

Na Regina Ndumbaro Kilwa-Lindi.

Wakulima wa kitongoji cha Cheketu, kata ya Somanga wilayani Kilwa, wameonesha kutoridhishwa na vitendo vya wafugaji wanaoingiza mifugo yao kiholela kwenye maeneo ya wakulima, hali inayosababisha migogoro ya mara kwa mara. 

Wakizungumza katika mkutano wa hadhara uliolenga kutoa elimu kuhusu sheria ndogo za halmashauri ya Kilwa kuhusu mahusiano ya wakulima na wafugaji, wakulima hao wameitaka serikali kuchukua hatua madhubuti kudhibiti hali hiyo.

Ali Mzungu, mkulima kutoka kitongoji hicho, amesema kata ya Somanga haijatenga maeneo rasmi kwa ajili ya wafugaji, jambo linalowafanya wafugaji kununua mashamba na kuingiza mifugo kwa idadi kubwa, bila kuzingatia matumizi ya ardhi yaliyopo. 

Ametoa wito kwa serikali kuu kuielekeza serikali ya kijiji cha Somanga kutenga maeneo rasmi na kuweka mipaka kwa alama maalum zitakazoonesha utengano kati ya maeneo ya wakulima na wafugaji.

Kwa upande wake, Mwenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kata ya Somanga, Saidi Japhet, ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa kwa kutunga sheria ndogo zinazolenga kutatua changamoto za muda mrefu kati ya wakulima na wafugaji. 

Hata hivyo, amesisitiza haja ya serikali kuwa wazi kuhusu uhalali wa matumizi ya ardhi na kuhakikisha kuwa kila kundi linatambua mipaka ya maeneo yao ili kulinda amani ya jamii.

Awali, Mwenyekiti wa kitongoji cha Cheketu, Hashimu Changajua, amewaeleza wakulima kuhusu sheria hizo ndogo, akisisitiza umuhimu wa kila mwananchi kuzifahamu ili kutambua haki na wajibu wao. 

Ameeleza kuwa elimu hiyo itasaidia kuimarisha uelewa wa pamoja na kuondoa migogoro isiyo ya lazima baina ya wakulima na wafugaji.

John Mrema Avuliwa Uanachama Chadema....



Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kupitia Tawi lake la Bonyokwa mkoani Dar es Salaam, kimemvua rasmi uanachama, John Mrema, kwa kile kilichoelezwa kuwa ni utovu wa nidhamu, dharau kwa mamlaka halali za chama, na kukaidi misingi na maadili ya chama.

Kwa mujibu wa barua rasmi iliyoandikwa na kusainiwa Aprili 30, 2025 na Katibu wa Tawi, Solomini Kagaruki, ambayo Jambo TV tumepata kuiona, na ambayo ilitolewa na tawi hilo, Kamati Tendaji ya tawi hilo ilikutana Aprili 29, 2025 na kupitia tuhuma dhidi ya Mrema, kisha kufikia uamuzi wa pamoja wa kumvua uanachama wake kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA @ChademaTz ya mwaka 2006, toleo la 2019, ibara ya 5.4.3.



Miongoni mwa tuhuma zilizomkabili Mrema @JonMrema , aliyekuwa Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa chama hicho, ni pamoja na dharau dhidi ya mamlaka za chama ambapo imeelezwa kuwa alisambaza barua ya wito ya kufika mbele ya kamati ya nidhamu kwenye mitandao ya kijamii badala ya kuitikia kwa utaratibu wa chama, jambo lililotafsiriwa kuwa ni dharau kwa mamlaka husika.

Tuhuma nyingine ni kukaidi maadili na misingi ya chama, ikielezwa kuwa akiwa bado katika mchakato wa kujieleza, alifanya mkutano na waandishi wa habari Aprili 22, 2025 na kutoa tuhuma hadharani dhidi ya chama chake, akibeza misimamo na programu za CHADEMA kinyume cha utaratibu wa ndani wa chama.

Barua hiyo imeeleza kuwa, kutokana na mienendo hiyo, Mrema amepoteza sifa za kuendelea kuwa mwanachama wa CHADEMA kuanzia tarehe 30 Aprili, 2025. Hata hivyo, amepewa haki ya kukata rufaa kwa ngazi ya juu endapo hataridhika na uamuzi huo.


SHINCHEONJI KANISA LA YESU ; KANISA PEKEE ULIMWENGUNI AMBALO WASHIRIKI WOTE HUMILIKI KITABU CHA UFUNUO


"Kuongeza au kupunguza kutoka katika Kitabu cha Ufunuo ina maana huwezi kuingia mbinguni (Ufu 22:18-19)"

***
Kuna kanisa ambalo hufanya Mtihani wa Biblia kila Wiki na washiriki wote wanajua Kitabu cha Ufunuo. Sasa Hivi Kanisa la Shincheonji la Yesu, Hekalu la Hema la Ushuhuda(Hukumbi wa Makao makuu )Mwenyekiti Man -hee Lee, ambaye baadaye anajulikana kama Kanisa la Shincheonji ).

 Ni wale tu ambao wamemaliza kozi zote (za msingi, za kati na za juu) katika Kituo cha Misheni cha Zion Christian na kufaulu mtihani wa kuhitimu (takriban maswali 100) ndio wanaoruhusiwa kuingia katika kanisa hili, ambalo ni maarufu ulimwenguni pote kwa kuwa na sherehe nne mfululizo za kuhitimu zenye wahitimu zaidi ya 100,000 kila Sherehe.

Hivi Karibuni, Mwenyekiti Man-hee Lee wa Kanisa la Shincheonji amekuwa akitembelea Makanisa ya Shincheonji kote nchini, wakati wowote anapohubiri kwenye Jukwaa, amekuwa akihubiri, "Kitabu cha Ufunuo Lazima kisiongezwe wala kupunguza; wale wanaofanya hivyo hawataingia mbinguni," akinukuu Ufunuo 22:18-19, na kusisitiza kwamba Kitabu cha Ufunuo Kinapaswa Kuandikwa kwenye Akili ya Mtu na  moyo.
Kufuatia mtiririko huu, Idara ya Elimu ya Shincheonji ya Baraza kuu inaendesha "Mtihani wa Uthibitishaji wa Kutiwa Muhuri" kwa waumini wote wa Shincheonji ulimwenguni kote, kulingana na nia ya Mwenyekiti Man -hee Lee ya kuwafanya waumini wote kukidhi na  kuingia mbinguni kwa kuwatia muhuri.

 Mtihani huo, ambalo ulianza kwa njia ya mtandao wakati wa janga la kimataifa la UVIKO-19, sasa Unafanywa ana kwa ana kwenye mahekalu na kusimamiwa kila wiki ili kuhakikisha kwamba washiriki wote wa Kanisa la Shincheonji duniani kote wanakuwa Biblia zinazotembea.

Kanisa la Shincheonji limesema rasmi , "Njia pekee ya kujua maana ya kweli na uhalisia wa Ufunuo ni kupokea ushuhuda kutoka kwa shahidi ambaye ameona moja kwa moja na kusikia utimilifu wa kitabu kizima cha Ufunuo mahali kilipotimizwa. 

Ukristo wa leo wa ulimwengu haujawahi kuona au kusikia uhalisia wa utimilifu wa Ufunuo, kwa hivyo kutoka kwa wachungaji hadi waumini, kila mtu ameongeza au kupunguza kutoka kwenye Ufunuo. 

Isipokuwa kwa washiriki wa Shincheonji, hakuna mtu hata mmoja kati ya Wakristo ulimwenguni kote ambaye hajaongeza au kupunguza kutoka Humo. Ufunuo 22: 18-19 inasema kwamba wale wanaoongeza au kupunguza kutoka katika Kitabu cha Ufunuo hawataingia mbinguni, lakini wachungaji na Waumini wao hawana hata wasiwasi hata juu ya kuongeza au kupunguza kutoka humo. 
Hii inawezaje kuchukuliwa kuwa imani ya kweli?"

Aliendelea, " Kanisa la Shincheonji la Yesu, lililopewa jina la uzushi na Ukatoliki na Uprotestanti, Je, waumini  wao wote wamebobea Kitabu cha Ufunuo. Hata hivyo, Ukatoliki na Uprotestanti, kuanzia wachungaji wao hadi waumini  wao, wote wameongeza au kupunguza kutoka kwenye Ufunuo. Kwa hiyo, amua ni nani ni Halisi  na  nani ni Mzushi  kulingana na Biblia," alisisitiza.
Mtihani wa Biblia unaofanywa kila wiki na washiriki wote wa Kanisa la Shincheonji unazingatia unabii katika Injili nne na Kitabu chote cha Ufunuo. Kanisa la Shincheonji linaeleza kwamba mtihani huu ni mafunzo ya kutia muhuri neno la Mungu moyoni mwa mtu na kushika Ufunuo wa agano jipya.

Kulingana na Idara ya Elimu ya Baraza kuu la Shincheonji, alama ya wastani ya jumla ya mtihani wa uthibitisho wa kutiwa muhuri wa watakatifu wote uliofanyika kuanzia Januari hadi Aprili mwaka huu ulikuwa pointi 99, na kiwango cha washiriki cha 97%, na 99.9% ya washiriki walipata pointi 90 au zaidi. Takwimu hii inaonyesha kuzamishwa kwa kina kwa waumini katika neno na kiwango chao cha juu cha imani.

Shincheonji Kanisa la Yesu lilisema rasmi, "Wakristo wa leo hawajui wala hawajali unabii katika Injili nne za Agano Jipya na maneno ya Ufunuo. Ingawa waitaja Shincheonji kama wazushi, hawawezi kujibu kwa maandiko wanapoulizwa kwa nini. Hii ni hali sawa na wakati wa ujio wa kwanza wa Yesu."

 Waliongeza, "Ikiwa mafundisho ya Kanisa la Shincheonji la Yesu si sahihi, tafadhali uonyeshe kupitia maandiko. Si sawa kutesa Kanisa la Yesu  Shincheonji kwa sababu tu mshiriki wa kanisa hufuata neno la ukweli na kwenda Shincheonji.
Je, Yesu alifundisha kuwatesa majirani katika Agano Jipya?"

Licha ya utata huu wa Uzushi, wachungaji wa zamani ambao wamejiunga na Shincheonji Kanisa la Yesu wanashuhudia kwa kauli moja kwamba " Shincheonji Kanisa la Yesu linafundisha na kutendea kazi neno kulingana na maandiko." 

Ni sauti kwamba Kanisa la Shincheonji linapaswa kutathiminiwa kulingana na Biblia badala ya kukosoa tu kirahisi.
Mchungaji Kim, ambaye alikuja kukubali mafundisho ya Shincheonji Kanisa la Yesu, alisema, "Ukristo unaita Shincheonji Wazushi, lakini nilipokuja hapa, sikupata kanisa lolote linalofuata Biblia kama hili."

 Aliendelea, "Katika Shincheonji, wanasaidia Waumini kuelewa Biblia nzima, kutoka Mwanzo hadi Ufunuo, kwa hivyo maarifa ya kibiblia ya washiriki yanazidi yangu kama mchungaji. Nimetupilia mbali kila kitu nilichojua hapo awali na ninaanza imani yangu upya."

Mchungaji Choi Kwang-sun pia alisema, "Ingawa nilifundisha neno kama mchungaji, baada ya kuja katika Shincheonji Kanisa la Yesu, niligundua jinsi nilivyokuwa mjinga. Badala ya kukashifu tu Shincheonji, Makanisa yanapaswa kuwapa waumini fursa ya kusikiliza na kujihukumu wenyewe." 

Alikata rufaa, "Ni uzembe wa wajibu kwa makanisa kutofundisha vizuri neno la Biblia. Viongozi wa Kikristo wanapaswa kusikiliza neno kwanza ili watu wote duniani waweze kujua kazi ya mwisho ya Mungu."

Kanisa la Yesu Shincheonji  lilisisitiza, "Kama mtu mwenye kiu anayetafuta maji, waumini wanaotafuta ukweli wanakusanyika mahali ambapo neno la ukweli lipo. Kile ambacho waumini wa ulimwengu wanapaswa kuzingatia sasa ni kutofautisha ukweli na uwongo kupitia neno la Mungu, Biblia, ambaye ameumbwa kulingana na Agano Jipya na Ufunuo, ambaye anajua Ufunuo."

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA MAKANDARASI WA BARABARA WANAOJENGA CHINI YA KIWANGO

OR- TAMISEMI

Serikali kupitia Ofisi ya Rais – TAMISEMI inataendelea kuwachukulia hatua wakandarasi wanaotekeleza miradi ya ujenzi wa Barabara chini ya kiwango.

Hayo yamesemwa  leo Aprili 30, 2025 Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri Ofisi ya Rais – TAMISEMI Mhe. Zainab Katimba kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa wakati akijibu swali la nyongeza la Mhe. Aleksia Kamguna,mbunge wa Viti maalum aliyetaka kujua serikali inawachukulia hatua gani wakandarasi wanojenga Barabara chini ya kiwango.

"Serikali inapotoa nafasi ya ujenzi wa barabara hizi kwa wakandarasi inatarajia wakandarasi waweze kuzingatia mkataba wanapokuwa wanatekeleza ujenzi wa barabara hizi za wilaya na serikali inakuwa makini kusimamia viwango"  amesema Mhe.Katimba

Katika swali la msingi la Mhe. Kamguna ameuliza lini Serikali itajenga barabara za Wilaya ya Malinyi kwa kiwango cha Lami

Akijibu Swali hilo Mhe. Katimba amesema "Serikali inakusudia kujenga kwa tabaka la lami barabara za makao makuu ya wilaya zote hapa nchini ikiwemo wilaya ya Malinyi na katika mwaka 2024/25"

"Serikali inaendelea na ujenzi wa barabara ya Mnadani-Bomani inayoelekea Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi kwa tabaka la lami (kilomita 0.85) kwa thamani ya shilingi 759,000,000.00 Mpaka sasa ujenzi bado unaendelea na umefikia 30%". Mhe. Zainab Katimba

JWTZ YATANGAZA NAFASI ZA VIJANA KUANDIKISHWA JESHINI



Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ ) Kanali Gaudentius Ilonda,akisisitiza jambo Kwa waandishi wa habari leo Aprili 30,2025 Jijini Dodoma kuhusu nafasi za kuandikishwa Jeshini kwa vijana wa Kitanzania wenye elimu kuanzia elimu ya Sekondari hadi elimu ya juu.

Na Kulwa Meleka_Dodoma

JESHI la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) limetangaza nafasi za kuandikishwa Jeshini kwa vijana wa Kitanzania wenye elimu kuanzia elimu ya Sekondari hadi elimu ya juu.

Hayo yameelezwa leo April 30,2025 na Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano (JWTZ) Kanali Gaudentius Ilonda wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma.

Kanali Ilonda amesema sifa za mwombaji ni lazima awe raia wa Tanzania mwenye kitambulisho cha Taifa,awe na afya nzuri na timamu,mwenye tabia na nidhamu nzuri,hajapatikana na hatia ya makosa ya jinai mahakamani na kufungwa, Cheti halisi Cha kuzaliwa(Original Birth Certificate)Vyeti vya Shule na taaluma.

Vilevile awe hajatumikia Jeshi la Polisi, Magereza,Chuo Cha Mafunzo au kikosi Cha kuzuia Magendo,awe amehitimu Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT kwa mkataba wa kujitolea au mujibu wa sheria na kutunukiwa Cheti.

Amesema kwa vijana wenye elimu ya kidato cha Nne na kidato cha Sita wawe na umri usiozidi miaka 24,Vijana wenye Elimu ya Stashahada umri usiozidi miaka 26, Vijana wenye elimu ya juu umri usiozidi miaka 27,na Madaktari Bingwa wa binadamu umri usiozidi miaka 35 ya kuzaliwa

Aidha Taaluma adimu zinazohitajika ni Generall Surgeon,Orthopaedic Surgeon,Urologist Radiologist,ENT Specialist,Anaesthesiologist,Physician, Ophthalmologist, Paediatrician, Obstetrician & Gynaecologist,Ocologis, Pathologist, Psychiatrist, Emergency Medicine Specialist na Haematologist.

Pamoja na Medical Doctor, Dental Doctor, Veterinary Medicine,Bio Medical Engineer,Dental Laboratory Technician, Anaesthetic, Radiographer,Optometry, Physiotherapy na Aviation Doctor.

Aidha Taaluma za Uhandisi(Engineer) ni pamoja na Bachelor of Electronic Engineering, Bachelor of Mechanical Engineering, Bachelor in Marine Engineering, Bachelor in Marine transportation & Nautical Science, Bachelor in Mechanic in Marine Diesel Engine, Bachelor in Aviation Management, Bachelor in Aircraft Accident & Incident Investigation, Bachelor in Meteorology, Air Traffic Management & Aeronautic Engineering bila kusahau Fundi Mchundo Aluminum Welding na Welding & Metal Fabrication.

Sanjari na hayo utaratibu wa kutuma maombi kwa makundi yote mawili ni maombi yote yaandikwe Kwa mkono na yawasilishwe Makao Makuu ya Jeshi Dodoma kuanzia Mei 1 2025 hadi tarehe 14 Mei,2025 yakiwa na Nakala ya kitambulisho cha Taifa au nambari ya NIDA,Nakala ya Cheti Cha kuzaliwa,vyeti vya Shule na chuo, Nakala ya Cheti Cha JKT kwa waombaji waliomaliza mkataba wa kujitolea pamoja na nambari ya simu ya mkononi ya Mwombaji.

Kuhusu miaka isiyozidi 35 kwa madaktari bingwa wa binadamu kuwa mdogo,Kanali Ilonda amesema wamefanya hivyo kutokana na kuwapa kipaumbele vijana na wamepima Kisayansi na kuona umri huo ni sahihi.

"Kule pia kuna mafunzo magumu ndio maana tuwepa Nafasi zaidi vijana lakini ukifuata mtiririko wa kuanzia shule ya msingi mpaka Chuo Kikuu bado miaka 35 ni michache kwani tuna madaktari bingwa wengi ambao wapo chini ya miaka 30,"amesema Kanali Ilonda.

Kuhusu kutoa nafasi zaidi katika kada ya afya kuliko kada zingine,Kaimu Mkurugenzi huyo wa Habari na Uhusiano JWTZ,amesema mahitaji yamekuwa makubwa kutokana na ongezeko la Hospitali za Jeshi.

"Tuna Lugalo,tuna Hospitali mpya Msalato ambayo itahudumia Askari na wananchi mahitaji ni makubwa ndio maana tumeipa msukumo mkubwa fani hiyo,"amesema Kanali Ilonda.

Hata hivyo ametoa angalizo kwa wananchi kutokubali kurubuniwa na matapeli kwa kudai hatua kali zitachukuliwa kwao ikiwemo kupelekwa Polisi.

"Naomba niwakumbushe hakuna nafasi ya kujiunga Jeshini kwa kutoa fedha atakae toa na kupokea Sheria ipo pale pale hatua Kali kwao zitachukuliwa,"amesema Kanali Ilonda

Hatimaye Hersi Said Aipongeza Timu Hii Kwa Ushindi......




Rais wa klabu ya Yanga SC na mwenyekiti wa Shirikisho la Vilabu barani Afrika ACA, Engineer Hersi Said ametoa salamu za pongezi kwa timu ya taifa ya vijana chini ya miaka kumi na tano kwa kuchukua ubingwa wa mashindano ya mpira wa miguu kwa shule za Afrika (CAF Africa Schools Football Championship).


Kulingana na taarifa tulizozipata hivi sasa, timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 15 wameshinda ubingwa wa mashindano hayo kwa mara ya pili mfululizo. Jambo ambalo huenda likainua vipaji katika soka nchini Tanzania.

Mechi hiyo iliandaliwa na kuchezwa nchini Ghana. Rais Hersi Said alitoa ahadi ya zawadi kwa vijana hawa. Kulingana na taarifa tulizozipata hivi sasa, zawadi hiyo itakabidhiwa na Mtendaji mkuu wa klabu ya Yanga SC baada ya timu hiyo kutendeka nchini Tanzania.



Asante kwa kusoma taarifa hii, unaweza kutoa maoni yako ili kuboresha uandishi wetu, maoni yatolewe kwenye nafasi ya kutoa maoni iliyopo hapo chini.

GASCO YANG’ARA, YATWAA TUZO NNE- WIKI YA USALAMA NA AFYA MAHALA PA KAZI, SINGIDA

Watumishi wa TPDC na GASCO katika picha ya pamoja wakati wa kupokea tuzo

Kampuni ya GASCO, ambayo ni kampuni tanzu ya TPDC, imepokea tuzo nne (4) kwa niaba ya viwanda vya kuchakata gesi asilia vya Madimba na Songosongo, pamoja na Kituo cha Kupokea Gesi Asilia cha Kinyerezi, sambamba na tuzo ya heshima kwa udhamini.

Tuzo hizi zilitolewa mbele ya Mgeni Rasmi, Mheshimiwa Ridhiwani Jakaya Kikwete, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), ikiwa ni kutambua mafanikio ya GASCO katika kuzingatia viwango bora vya afya na usalama kazini.

Tuzo hizo zimetolewa na Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) katika maonesho yaliyofanyika kitaifa na kushirikisha makampuni kutoka sekta mbalimbali. Ushindi huu umeweka alama ya kipekee kwa GASCO kama kinara katika utekelezaji wa sera na taratibu bora za usalama kazini.
Mwakilishi wa Meneja Mkuu wa GASCO, Ndg. Msaada Elson akipokea tuzo

Akizungumza mara baada ya kupokea tuzo hiyo kwa niaba ya Meneja Mkuu wa GASCO, Ndg. Msaada Elson alieleza kuwa ushindi huo ni matokeo ya mshikamano, uwajibikaji na juhudi za pamoja kati ya menejimenti na wafanyakazi wote wa kampuni hiyo.

"Ushindi huu ni matokeo ya juhudi za pamoja kati ya menejimenti na wafanyakazi wote katika kuzingatia viwango bora vya afya na usalama kazini. Kampuni itaendelea kuboresha mifumo ya usalama na kutoa kipaumbele matumizi ya akili mnemba kwa ustawi wa wafanyakazi wake," alisema Ndg. Msaada Elson.

Aidha, alitumia fursa hiyo kuwashukuru OSHA kwa kuandaa maonesho hayo ambayo yanatoa jukwaa muhimu kwa makampuni kubadilishana uzoefu na kujifunza mbinu bora za usimamizi wa usalama kazini.

Tuzo hizo zinaonesha dhamira ya dhati ya GASCO katika kuhakikisha mazingira salama kwa wafanyakazi, kuongeza tija kazini na kuchangia maendeleo endelevu ya sekta ya nishati nchini.

#TPDCTUNAWEZESHA

PICHA A: Mwakilishi wa Meneja Mkuu wa GASCO, Ndg. Msaada Elson akipokea tuzo

PICHA B: Watumishi wa TPDC na GASCO katika picha ya pamoja wakati wa kupokea tuzo


MAJAJI WAANZA KUCHAMBUA KAZI ZA WAANDISHI NA KUKAGUA VYOMBO VYA HABARI KWA AJILI YA TUZO ZA UWIANO WA KIJINSIA 2025



Kilio cha wakazi Igomba kufika mwisho,TASAF wataka Zahanati ikamikike wapate huduma

 

Mwenyekiti wa kamati ya uongozi ya Taifa ya TASAF Peter Ilomo ameipa mwezi mmoja kamati ya usimamizi miradi ya jamii TASAF kijiji cha Igomba kuhakikisha majengo ya zahanati ya kijiji hicho yanakamilika ili iweze kuanza kutoa huduma na kuwapunguzia adha wakazi wa Igomba kufuata huduma ya afya umbali mrefu.

Ilomo ametoa agizo hilo mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa majengo ya zahanati hiyo iliyopo katika kijiji cha Igomba wilaya ya Wanging'ombe mkoani Njombe ambapo amesema uwepo wa Zahanati ni muhimu katika kijiji hicho kwa kuwa wamekuwa wakifuata huduma ya afya kijiji jirani cha Isimike pamoja na kituo cha afya Saja vinavyopatikana umbali wa KM 6 kutoka kijijini hapo. 

"Tujitahidi usiku na mchana,nimeambiwa mpango ni kumaliza mwezi wa tano lakini na mimi naongeza kidogo mpaka mwezi wa sita kwa kazi nilizoziona ili ikiwezekana mwezi wa saba huduma zianze kutolewa hapa"ameagiza Ilomo

Joyce Mdemwa ni Mratibu wa TASAF wilaya ya Wanging'ombe ameeleza kupokea maelekezo ya kukamilisha mradi huo huku wakazi wa Igomba wakishukuru kukamilishiwa zahanati yao ili kupunguza changamoto ya kufuata huduma ya afya umbali mrefu.

"Tunatarajia kukamilisha mradi huu tarehe theleathini mwezi wa tano na agizo la Mwenyekiti sisi tunamuahidi tutakamilisha na mwezi wa saba tutaanza kutoa huduma"amesema Joyce Mdemwa

Kijiji cha Igomba ni miongini mwa vijiji vya wilaya ya Wanging'ombe  ambavyo vinanufaika na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) ambapo licha ya kusaidia kaya maskini lakini pia kijiji hicho kilipokea Milioni 200.2 kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya Zahanati pamoja na nyumba ya mganga.








Source

Raisi Samia Afanya Uteuzi Mpya....



Dodoma. Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameendelea kuimarisha taasisi za umma kwa kufanya uteuzi wa viongozi wanne wa mashirika ya Serikali.

Tarifa iliyotolewa leo Jumanne, Aprili 29, 2025 na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu ikimnukuu Katibu Mkuu Kiongozi, Dk Moses Kusiluka imebainisha walioteuliwa ni wenyeviti wa bodi.

Rais Samia amemteuwa Dk Fatma Kassim Mohamed kuendelea na wadhifa wake kama Mwenyekiti wa Bodi ya Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) kwa kipindi cha pili mfululizo.

Pili, Dk Jilly Maleko ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), akichukua nafasi ya Balozi Begum Karim Taj ambaye amemaliza muda wake wa uongozi.

Pia, Rais Samia amemteua Profesa Eliakimu Zahabu kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Kituo cha Taifa cha Ufuatiliaji wa Kaboni (National Carbon Monitoring Center - NCMC), taasisi inayohusika na masuala ya mabadiliko ya tabianchi.

Aidha, Lucas Mwino, ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA), akichukua nafasi ya Dk John Mduma aliyemaliza muda wake," taarifa hiyo inaeleza.


Tuesday, April 29, 2025

FIKIRIA UNATEMBEA UTUPU HUKU NYUKI WAKIWA KWENYE MWILI WAKO

Jina langu ni Abeli Waihiga, mkazi wa Langata nchini Kenya kwa miaka zaidi ya 10 sasa, nimekuwa nikiishi maisha yangu bila wasiwasi wowote, najua hakuna ambacho kitaweza kuvamia nyumba au familia yangu.

Ngoja leo nikupe siri hii bure, unajua hakuna kinachomtisha mwizi kama kukuta hakuna kitu cha usalama kwenye mlango wa mbele, hakuna mbwa au kamera za CCTV zilizowekwa.

SOMA ZAIDI <HAPA>

WATENDAJI UBORESHAJI WA DAFTARI AWAMU YA PILI WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA

Mwemyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza na watendaji wa uboreshaji ngazi ya Kata na Waandishi Wasaidizi na Waendesha vifaa vya Biometriki kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Iringa mkoani Iringa leo Aprili 29,2025 wakati alipotembelea mafunzo hayo ikiwa ni maandalizi ya awamu ya pili mzunguko wa kwanza wa uboreshaji Daftari la Kudumu la Wapiga Kura unaoanza Mei Mosi hadi Mei 07, 2025 katika mikoa 15.
Sehemu ya Washiriki wa Mafunzo hayo wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume.


Sehemu ya Washiriki wa Mafunzo hayo wakimsikiliza Mwenyekiti wa Tume.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akikagua mafunzo ya watendaji wa Uboreshaji ngazi ya Kata kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Iringa leo Aprili 29,2025 ikiwa ni maandalizi kuelekea awamu ya pili ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na uwekaji wazi wa Daftari la awali la wapiga Kura.


Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akikagua mafunzo ya watendaji wa Uboreshaji ngazi ya Kata kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Iringa leo Aprili 29,2025 ikiwa ni maandalizi kuelekea awamu ya pili ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na uwekaji wazi wa Daftari la awali la wapiga Kura.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Daftari na TEHAMA wa Tume.
*******
Na. Mwandishi wetu, Iringa
TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi imewataka watendaji wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kufanya kazi kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na taratibu za Uchaguzi wakati wa utekelezaji wa awamu ya pili ya zoezi hilo litakalofanyika sambamba na uwekaji wazi wa Daftari la Awali la Wapiga Kura ambapo mzunguko wa kwanza utahusisha mikoa 15 kuanzia mei mosi hadi saba mwaka huu.

Hayo yamesemwa leo Aprili 29,2025 na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele wakati akizungumza na washiriki wa mafunzo ya siku moja ya watendaji hao ngazi ya Kata kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Iringa mkoani Iringa.
"Nawakumbusha tena kama nilivyowakumbusha katika zoezi lililopita, kwamba katika utekelezaji wa zoezi hili mzingatie sheria, kanuni na taratibu za uchaguzi, muwe wanyenyekevu kwa wateja mtakao kuwa mnawahudumia,"alisema Jaji Mwambegele.

Jaji Mwambegele amewaeleza watendaji hao kuwa wateja wengi watakaowahudumia ni wananchi wa kawaida hivyo hawana budi kuwahudumia vyema kwa lugha nzuri naikitokea kuna ulazima wa kuwarekebisha pale wanapokosea basi wafanye hivyo kwa staha.

"Zoezi hilo linafanyika kwa mujibu wa masharti ya kifungu cha 16(5) cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 1 ya mwaka 2024 kinachoipa Tume jukumu la kuboresha Daftari la Kudumu la Wapiga Kura mara mbili mara baada ya uchaguzi mkuu na kabla ya uteuzi wa wagombea kwa uchaguzi mkuu unaofuata," alisema.

Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya pili utafanyika sambamba na uwekaji wazi wa Daftari la Awali la Wapiga Kura kuanzia tarehe 01 Mei, 2025 na kukamilika tarehe 04 Julai, 2025.

Uboreshaji wa Daftari unataraji kufanyika kwa mizunguko mitatu ambapo mzunguko wa kwanza utajumuisha mikoa 15, mzunguko wa pili mikao 16 na mzunguko wa tatu utajumuisha vituo vya magereza na vyuo vya mafunzo.

Mikoa itakayohusika kwenye mzunguko wa kwanza wa uboreshaji ni pamoja na Iringa, Geita, Kagera, Mara, Shinyanga, Mwanza, Simiyu, Rukwa, Tabora, Katavi, Kigoma, Ruvuma, Mbeya, Njombe na Songwe ambapo zoezi hilo litafanyika kuanzia Mei 1 hadi 7 mwaka huu.

Aidha, mzunguko wa pili utahusisha mikoa ya Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Tanga, Morogoro, Pwani, Singida, Dodoma, Dar es Salaam, Lindi, Mtwara, Mjini Magharibi, Kaskazini Unguja, Kusini Unguja, Kaskazini Pemba na Kusini Pemba ambapo zoezi hilo litafanyika kuanzia Mei 16 hadi 22, 2025.

Mzunguko wa tatu wa zoezi la uboreshaji wa Daftari utahusisha vituo 130 vilivyopo kwenye magereza ya Tanzania Bara na vituo 10 vilivyopo katika Vyuo vya Mafunzo Tanzania Zanzibar kwa wakati mmoja na utafanyika kwa muda wa siku saba kuanzia Juni 28 hadi Julai 04, 2025.

Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa awamu ya pili, utafanyika ngazi ya kata kwa Tanzania Bara na ngazi ya jimbo kwa Tanzania Zanzibar, ambapo jumla ya vituo 7,869 vitahusika, vituo 7,659 vipo Tanzania Bara na vituo 210 vipo Tanzania Zanzibar.

Katika awamu ya pili ya uboreshaji, wapiga kura wapya 1,396,609 wataandikishwa, wapiga kura 1,092,383 wataboresha taarifa zao na wapiga kura 148,624 watafutwa kwenye Daftari kwa kukosa sifa za kuendelea kuwepo kwenye Daftari," amesema Jaji Mwambegele.

Mambo mengine ni kuhamisha taarifa za wapiga kura waliohama kutoka kata au jimbo walipoandikishwa awali na kuondoa taarifa za wapiga kura waliopoteza sifa za kuwemo kwenye Daftari kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kifo.

Aidha, kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 11(1) na (2) cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 1 ya Mwaka 2024, Tume pia ina jukumu la kuandaa Daftari la Awali la Wapiga Kura na kuliweka wazi kwa umma.

Lengo la uwekaji wazi wa Daftari hilo ni kutoa fursa kwa wananchi kukagua, kufanya marekebisho ya taarifa za wapiga kura na uwekaji wa pingamizi dhidi ya wapiga kura waliomo kwenye daftari ambao hawana sifa na litabandikwa katika vituo vyote vilivyotumika wakati wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya kwanza.

Tume iliboresha Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya kwanza kuanzia tarehe 20 Julai, 2024 na kukamilisha tarehe 25 Machi, 2025.

Timu Zinazoongoza Kufunga Magoli Eneo la Hatari Ligi Kuu Tanzania



Katika takwimu mpya za Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara msimu wa 2024/25, klabu ya Young Africans (Yanga SC) imeendelea kudhihirisha ubabe wake kwa kuongoza kwa mabao mengi yaliyofungwa ndani ya eneo la hatari (boxi), ikiwa na jumla ya mabao 55.

Yanga SC imewazidi watani wao wa jadi Simba SC ambao wamefunga mabao 48 ndani ya boxi, huku Azam FC ikishika nafasi ya tatu kwa mabao 38. Singida Big Stars nao wameonyesha uwezo wao kwa kufunga mabao 37.

Timu nyingine zilizopo kwenye orodha ya juu ni Tabora United na Dodoma Jiji ambazo zote zina mabao 23, zikifuatiwa kwa karibu na Namungo FC yenye mabao 22 na Fountain Gate yenye mabao 20.

Hii ni dalili kuwa timu hizo zimekuwa na uwezo mkubwa wa kupenya ngome za wapinzani na kutumia nafasi zao vizuri ndani ya eneo la hatari. Kwa upande wa Yanga, mafanikio haya yanaonesha uimara wa safu yao ya ushambuliaji ambayo imekuwa moto wa kuotea mbali msimu huu.

Mashabiki na wadau wa soka wanaendelea kushuhudia ushindani mkali huku timu zikisaka pointi muhimu na nafasi bora kwenye msimamo wa ligi.


WAZIRI MKUU : SERIKALI ITAENDELEA KULINDA UHURU WA HABARI KWA VITENDO, WAANDISHI TUMIEMI AKILI MNEMBA KWA UWAJIBIKAJI


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, akizungumza jijini Arusha leo Aprili 29, 2025 wakati akifungua rasmi maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani- Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, akizungumza jijini Arusha leo Aprili 29, 2025 wakati akifungua rasmi maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, akizungumza jijini Arusha leo Aprili 29, 2025 wakati akifungua rasmi maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani

**

🔹Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Asisitiza Akili Mnemba Isaidie, Isiwe Kikwazo kwa Uhuru wa Habari

🔹 Serikali Yaanza Mchakato wa Kuandaa Sera ya Akili Mnemba kwa Uhuru wa Habari

🔹 Sera ya Habari na Utangazaji ya 2003 Kupitiwa Upya

Na Kadama Malunde - Malunde 1 Blog

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, amesema Serikali itaendelea kulinda uhuru wa vyombo vya habari kwa vitendo na si kwa maneno, akisisitiza matumizi sahihi ya akili mnemba (Artificial Intelligence) kama chachu ya uwajibikaji na si kikwazo kwa waandishi wa habari.

Akizungumza jijini Arusha leo Aprili 29, 2025, wakati akifungua rasmi maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani (World Press Freedom Day 2025) yenye kaulimbiu ya mwaka huu isemayo "Uhabarishaji katika Dunia Mpya: Mchango wa Akili Mnemba kwenye Uhuru wa Vyombo vya Habari", Mhe. Majaliwa ametoa wito kwa wanahabari kutumia akili mnemba kwa weledi na kuzingatia ukweli wa taarifa wanazotoa.

Waziri Mkuu ameeleza kuwa teknolojia ya Akili Mnemba inaweza kuwa msaada mkubwa katika kuboresha kazi za uandishi wa habari, lakini pia inaweza kuwa chanzo cha changamoto iwapo haitatumika kwa busara na uangalifu. 

"Akili Mnemba itumike kama nyenzo kwa waandishi wa habari na siyo kikwazo. Mjitahidi kuitumia vizuri kwa uwajibikaji, kutoa taarifa sahihi na zenye kuzingatia maadili ya taaluma. Serikali kwa kushirikiana na wadau tunaendelea na mchakato wa kutengeneza sera kuhusu Akili Mnemba," amesema  Mhe. Majaliwa.

Mhe. Kassim Majaliwa

Ameeleza kuwa Serikali imeanzisha mchakato wa kuandaa Sera ya Akili Mnemba, ili kuhakikisha teknolojia hiyo inaendana na misingi ya uhuru wa vyombo vya habari, uwazi na uadilifu katika taaluma ya uandishi wa habari. 

Aidha, sambamba na mchakato huo, Serikali inaendelea kupitia upya Sera ya Habari na Utangazaji ya mwaka 2003 ili kuhakikisha inaimarisha na kulinda taaluma ya uandishi wa habari nchini.

"Hivyo, kupitia mijadala yenu katika maadhimisho haya, toeni maoni yenu kuhusu namna sera hiyo ya Akili Mnemba inavyopaswa kuwa, ili iendane na misingi ya uhuru wa vyombo vya habari," amesema Mhe. Majaliwa.

Katika kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, Mhe. Majaliwa ametaka vyombo vya habari kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha uchaguzi unakuwa huru, haki na wa uwazi, akihimiza utoaji wa taarifa sahihi, zinazojenga amani na mshikamano.

"2025 huu ni mwaka wa uchaguzi. Sisi kama Serikali, kama wadau wa uchaguzi, pindi Tume Huru ya Uchaguzi watakapotoa ratiba, tunatarajia nyie ndiyo mtalieleza taifa. Na sisi ushiriki wetu ni kuhakikisha kwamba yale yaliyo muhimu ya kuufanya uchaguzi huu kuwa wa usalama, na kila mmoja atakwenda kushiriki kwa usalama wake... Na watu wa Tume Huru ya  Taifa ya Uchaguzi wametuambia kwamba uchaguzi huu watausimamia kwa uhuru na haki na uwazi. Na sisi Serikali kama wadau wa uchaguzi tunataka tuwahakikishie kuwa uchaguzi huu utakuwa ni wa amani na utulivu," amesema Waziri Mkuu.

"Uchaguzi huu utakuwa wa amani na utulivu. Ninyi waandishi wa habari mtakuwa sehemu ya walinzi wa amani. Toeni taarifa zinazohamasisha kulinda tunu zetu za kitaifa," amesisitiza.

Waziri Mkuu pia amesema Serikali itaendelea kulinda uhuru wa habari kwa vitendo kwa kushirikiana na waandishi wa habari, ambapo tayari imeunda kamati ya kutathmini hali ya tasnia hiyo na kutatua changamoto zake. 

Amesisitiza umuhimu wa vyombo vya habari kuelimisha na kuhabarisha jamii kuhusu maendeleo ya taifa kwa kuzingatia ukweli na uadilifu.

Profesa Paramagamba Kabudi

Kwa upande wake, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Profesa Paramagamba Kabudi, amewataka waandishi wa habari kutoitegemea tu teknolojia ya Akili Mnemba, bali waendelee kutumia uwezo wao wa kiakili kuchakata na kuandaa maudhui ya habari.

"Akili Mnemba isiwafanye mfubae, Waandishi wa habari tumieni akili yenu pia",amesema Profesa Kabudi.

Gerson Msigwa

Naye Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Gerson Msigwa, amewapongeza waandishi wa habari kwa kutekeleza majukumu yao licha ya changamoto mbalimbali, huku akiwaasa wasikate tamaa kwani wao ni nguzo ya matumaini kwa wananchi.

Mhe. Paul Makonda

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Paul Makonda, amesema waandishi wa habari wanalo jukumu kubwa la kulinda uchumi wa Taifa, na hivyo kuwataka wazipe kipaumbele habari zinazohamasisha wananchi kujikita katika shughuli za kiuchumi.

"Waandishi wa habari andikeni kuhusu uchumi, habari mnazoandika ziguse masuala ya kuchagiza uchumi",amesema Makonda.

Awali, Mwenyekiti wa Maadhimisho hayo ya uhuru wa vyombo vya habari mwaka huu 2025, Maxence Melo, ambaye pia ni Mkurugenzi wa JamiiAfrica, akiwasilisha baadhi ya maazimio ya mijadala ya wadau wa habari, amesema wamependekeza kufanyike mapitio ya Sera ya Habari na Utangazaji ya mwaka 2003 ili iendane na maendeleo ya teknolojia ya Akili Mnemba.Maxence Melo

Maazimio mengine ni pamoja na kuboreshwa kwa kanuni za maadili ya habari na kuhakikisha usalama na ulinzi wa waandishi wa habari, hususan kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.



Soma pia :

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...