Wednesday, April 9, 2025

EVANCE KAMENGE ATANGAZA NIA YA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA NKENGE UCHAGUZI MKUU 2025

Na Lydia Lugakila - Kagera

Evance Kamenge, Mkulima na mchumi kutoka Wilaya ya Missenyi, Mkoani Kagera, ametangaza rasmi nia yake ya kugombea nafasi ya ubunge katika Jimbo la Nkenge katika uchaguzi wa mwaka 2025. 

Hii ni hatua ya tatu kwake baada ya kushiriki katika uchaguzi wa mwaka 2015 na 2020 bila ya kufanikiwa.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Manispaa ya Bukoba, Kamenge amethibitisha kwamba yuko tayari kuwasilisha ombi lake la ridhaa kwa wananchi wa Nkenge.

 "Niliwahi kugombea na sasa nataraji kugombea tena mwaka huu 2025," alisema Kamenge.

Kamenge ameeleza kuwa yeye ni sehemu ya mabadiliko na kwamba kuna umuhimu wa kuweka mikakati thabiti ya kuboresha hali ya maisha ya wananchi.

 "Mimi ni mkulima na ninaajiri watu, haya ninayoyasema yanatokana na hali halisi ya maisha ya familia yangu," amesema Kamenge.

Mwanasiasa huyo pia amesisitiza kwamba anapokusudia kugombea, anataka kuwa sehemu ya mapinduzi siyo mageuzi.

 Amesema kuwa ameona mambo mengi yanapaswa kubadilishwa ili kufikia maendeleo halisi huku akidai kutoridhishwa na hali ya maendeleo katika eneo hilo.

Aidha, Kamenge ameonesha kuwa ana imani kwamba viongozi wa sasa wanapaswa kutekeleza ahadi zao huku akiongeza kuwa anatazamia kuwaambia wananchi ukweli huo wakati atakapokuwa na afya njema.

Kamenge pia amegusia umuhimu wa viongizi kuwa waaminifu katika siasa, akitaja msemo ulioko kwenye kadi yake ya chama chake isemayo "Nitasema kweli daima, fitina kwangu ni mwiko." kauli ambayo imeonesh ya kukazia dhamira yake na kueleza haja ya kuwa na viongozi waaminifu na wanaojali maslahi ya wananchi.

KIKOSI Cha Simba Vs Al Masry Leo Tarehe 09 April 2024

KIKOSI Cha Simba Vs Al Masry Leo Tarehe 09 April 2024


Simba itamenyana na Al Masry Port Said katika mchujo wa kuwania kufuzu kwa Kombe la Shirikisho Aprili 9. Mchezo utaanza saa 16:00 kwa saa za kwenu.

Huku Simba na Al Masry Port Said zikiendelea kwa mara nyingine, kumbukumbu ya ushindi wa mabao 2-0 wa Simba katika mechi ya Mchujo ya Kombe la Shirikisho siku 6 zilizopita bado ingalipo. Baada ya kipigo dhidi ya Al Masry Port Said Jumatano iliyopita, Simba wanatamani kurejea kwenye mtanange huu.

Al Masry Port Said wanaingia kwenye kinyang'anyiro hiki kufuatia sare dhidi ya Ceramica Cleopatra Jumamosi iliyopita, na kuweka hai msururu wao wa kutoshindwa katika mechi tano.

Udaku Special inaangazia Simba dhidi ya Al Masry Port Said katika muda halisi, ikitoa mtiririko wa moja kwa moja na matokeo ya moja kwa moja ya mechi, safu za timu, takwimu kamili za mechi, maoni ya mechi ya moja kwa moja na muhtasari wa video rasmi. Tunashughulikia mechi zote za Mechi za Mchujo za Kombe la Shirikisho kwa wakati halisi na kutoa utiririshaji wa moja kwa moja inapowezekana.


KIKOSI Simba Vs Al Masry Port Said

  1. Camara
  2. Chamou
  3. Ngoma
  4. Ahoua
  5. Kapombe
  6. Ateba
  7. Hamza
  8. Hussein
  9. Kagoma
  10. Mpanzu
  11. Kibu

Tuesday, April 8, 2025

Mhagama aongoza msafara wa Tanzania mkutano wa 150 mabunge ya duniani Uzbekistan


Mbunge wa Jimbo la Madaba Joseph Kizito Mhagama, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Wabunge Wawakilishi wa umoja wa Mabunge Duniani kutoka Tanzania, ameongoza msafara wa Wabunge wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika Mkutano wa 150 wa Mabunge Duniani (IPU) unaoendelea mjini Kashkenti, Uzbekistan, kuanzia Aprili 5 mpaka 9, 2025.

Katika mkutano huu, Mhagama ameonyesha juhudi za Bunge la Tanzania katika kuisimamia serikali na kuhakikisha kwamba inatekeleza majukumu yake kikamilifu, hasa katika nyanja za maendeleo na haki za binadamu.

Mkutano huo unazungumzia nafasi ya Mabunge katika kupigania maendeleo na haki za jamii (Social Development and Justice), ambapo Bunge la Tanzania limekuwa na nafasi muhimu katika kuhamasisha na kutunga sheria zinazolenga kuboresha hali ya maisha ya wananchi.

Mhagama ameelezea hatua muhimu ambazo Tanzania imechukua katika kuimarisha maendeleo ya kijamii na haki za binadamu, akisisitiza umuhimu wa Mabunge duniani kushirikiana ili kufikia malengo ya pamoja ya maendeleo endelevu.

Huu ni mkutano wa kihistoria ambao umeipa Tanzania fursa ya kuonyesha mchango wake katika masuala haya ya kimsingi, huku ikiendelea kujenga mifumo bora ya utawala inayozingatia haki na maendeleo ya wananchi wake.



 


Source

AUCHO.....Moja kati ya viungo bora kuwahi kucheza kwenye ligi yetu

 

AUCHO.....Moja kati ya viungo bora kuwahi kucheza kwenye ligi yetu


Moja kati ya viungo bora kuwahi kucheza kwenye ligi yetu,ukitaka kuona tempo ya Yanga basi unatakiwa kutazama miguu ya Aucho.


Aucho anau-care mpira na kuachia kwa pasi fupi fupi,Aucho ni "controller" ambaye ana-control kila kitu kati kati ya uwanja.


Ila kusema ukweli kila lenye mwanzo lina mwisho,akili ya Aucho bado inautaka mpira ila mwili umeanza kukataa.


Aucho ametumika sana,mwili umechoka,mwishoni mwa msimu Yanga watafute namba 6 wa maana ambaye atakuja kumpunguzia Aucho majukumu na matumizi makubwa.


Kwa sasa Aucho anahitaji mechi 10-15 kwa msimu.

Kuwalaumu Azam FC kwa nini walipoteza Mchezo ni Kuwakosea Heshima Singida Black Stars

 

Kuwalaumu Azam FC kwa nini walipoteza Mchezo ni Kuwakosea Heshima Singida Black Stars

Kuwalaumu Azam FC kwa nini walipoteza Mchezo ni Kuwakosea Heshima Singida Black Stars

Baada ya Azam FC kupoteza mchezo jana kwa kufungwa goli 1-0 na Singida Black Stars pale uwanja wa Liti, Singida, nimeona maandiko na mijadala mingi kupitia vyombo mbalimbali vya habari wakilaumu imekuaje Azam imefungwa na Singida Black Stars!

Wengine wakafika mbali zaidi na kusema pengine huenda wachezaji hawakujituma wakitunza nguvu kuusubiri mchezo wao ujao dhidi ya Yanga [April 10, 2025] pale Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

Kwanza kuwalaumu Azam FC kwa nini walipoteza ule mchezo ni kuwakosea heshima Singida Black Stars, kwamba hawakustahili kushinda mbele ya Azam FC kitu ambacho si sawa. Singida Black Stars imesheheni wachezaji wengi wenye madaraja ya juu hata nafasi waliyopo kwenye msimamo wa ligi [4] hawapo kwa bahati mbaya.

Tukirejea kwa Azam FC, kufungwa 1-0 na Singida Black Star inawezekana kuna sababu nyingi za kiufundi na kimbinu ndani ya uwanja. Mimi naangazia sababu moja kubwa ya nje ya uwanja ambayo huenda imepelekea kwa kiasi kikubwa Azam kupoteza siku ya jana.

Aprili 3, 2025 Azam FC ilicheza mchezo wa Ligi jijini Mbeya [KenGold 0-2 Azam FC] baada ya mchezo wa Mbeya, wakalazimika kusafiri kwenda Mkoani Singida kucheza na Singida Black Stars Aprili 6, 2025.

No muda wa kupumzika wachezaji wanatakiwa kusafari [Mbeya-Singida], kumbuka hakuna safari ya ndege ya Mbeya-Singida! Uwanja wa ndege wa karibu na Singida ni Dodoma, kwa bahati mbaya hakuna safari ya ndege ya Mbeya-Dodoma!


Kwa hiyo wachezaji wa Azam FC walisafiri umbali mrefu kwa njia ya barabara na kuzalisha uchovu, hivi vitu lazima pia tuviangalie kwa sababu wanaocheza pia ni binadamu na sayansi inawataka kupumzika walau saa 72 baada ya mchezo mmoja hadi mwingine.


Kabla ya kuwahukumu Azam FC kwa kupoteza mchezo sai uliopita dhidi ya Singida Black Stars tuangalie na kujiridhisha kila kitu kilikuwa sawa?


Source

TEA YAANZA UTEKELEZAJI MIRADI YA AMALI ZANZIBAR

Naibu katibu Mkuu – Utawala, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Bw, Khalid Waziri akizungumza katika kikao kazi kati ya TEA na wizara hiyo kuhusu ujenzi wa shule za amali visiwani Unguja na Pemba.

***********

Unguja

Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) imeanza rasmi utekelezaji wa miradi ya amali kwa upande wa Zanzibar, ambapo shilingi bilioni 3.2 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa shule mbili za mafunzo ya amali. 

Huu ni muendelezo wa jitihada za Serikali za kuboresha sekta ya elimu, na ni sehemu ya mkakati wa kuunga mkono Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2025 na Mpango wa Maendeleo wa Muda Mrefu wa Taifa 2011/12 hadi 2024/25. 

Miradi hii inalenga kutoa elimu ya vitendo inayokidhi mahitaji ya soko la ajira na kukuza ujuzi wa vijana ili kuchangia kwa ufanisi katika maendeleo ya Taifa.

Katika kikao kazi kilichofanyika tarehe 8 Aprili 2025 kwenye ukumbi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali (WEMA) kisiwani Unguja, Mkurugenzi Mkuu wa TEA, Dkt. Erasmus Kipesha amesema kuwa, utekelezaji wa miradi hiyo ni sehemu ya mkakati wa mamlaka ya kuhakikisha mafanikio ya uboreshaji wa Sera ya Elimu na mtaala mpya unaolenga elimu jumuishi na ya vitendo. 
Dkt. Kipesha ameeleza kuwa miradi hiyo itajumuisha ujenzi wa madarasa na karakana zitakazotumika kwa ajili ya mafunzo ya vitendo, ambapo wanafunzi watapata ujuzi wa kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi baada ya kuhitimu masomo yao.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu – Utawala Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Bw. Khalid Waziri, ameshukuru na kuipongeza TEA kwa utekelezaji wa miradi hiyo kwani asilimia kubwa ya shule zilizopo visiwani Zanzibar hazina miundombinu ya amali. 

Aliendelea kusema kuwa miradi hiyo itakuwa na manufaa makubwa kwa jamii, kwani itawezesha vijana kupata ujuzi wa vitendo utakaowasaidia kujikwamua kiuchumi na kuchangia katika maendeleo ya Taifa.

Aidha, Bw. Waziri alifafanua kuwa Wizara ya Elimu imetenga maeneo kwa ajili ya ujenzi wa shule hizo, moja ikiwa Unguja na nyingine Pemba ili kuhakikisha kuwa watoto wa Zanzibar wanapata fursa sawa ya elimu. 

Alisema kuwa utekelezaji wa miradi hiyo utasimamiwa kikamilifu na Wizara ili kuhakikisha kuwa unakamilika kwa wakati na ubora unaotakiwa na kwamba shule hizi zitakuwa na madarasa kwa ajili ya masomo ya nadharia na karakana kwa ajili ya mafunzo ya vitendo.

Kazi ya ujenzi wa shule hizo inatarajiwa kuanza mara moja, huku hatua za awali za usanifu wa michoro, upatikanaji wa vifaa vya ujenzi na maandalizi ya maeneo zikiendelea. Miradi hii itahusisha ujenzi wa shule mbili, ambapo kila shule itakuwa na wastani wa amali tatu zinazotolewa kwa wanafunzi. 

Hii itawawezesha vijana kupata ujuzi katika nyanja mbalimbali za kiufundi na kimaisha, na hivyo kuwa na uwezo wa kufanya kazi na kujiingizia kipato baada ya kuhitimu masomo yao.

Ujenzi wa shule hizi unatarajiwa kuleta mabadiliko makubwa katika sekta ya elimu visiwani Zanzibar kwani itatoa fursa kwa vijana wengi kujiendeleza katika fani mbalimbali za amali.

 Miradi hii ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar za kuhakikisha kuwa Watoto wote wanapata elimu bora na yenye tija inayozingatia mahitaji ya soko la ajira na kukuza uchumi wa Taifa.

Kupitia miradi hii, Zanzibar itakuwa na fursa ya kuwa na vijana wenye ujuzi wa vitendo watakaoweza kushiriki kikamilifu katika shughuli za uchumi, na hivyo kuchangia katika maendeleo ya Taifa kwa ujumla.
Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) Dkt. Erasmus Kipesha akifafanua jambo kwenye kikao kazi kati ya TEA na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kuhusu utekelezaji miradi ya amali.
Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) Dkt. Erasmus Kipesha (kulia) akiwa na baadhi ya watendaji wa mamlaka hiyo katika kikao kazi cha kujadili utekelezaji wa miradi ya amali upande wa Zanzibar.
Mkurugenzi Elimu ya Sekondari Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Bi. Asya Issa akifafanua jambo wakati wa kikao kazi cha kujadili utekelezaji wa miradi ya amali kati ya TEA na Wizara hiyo.

Walisema Kuna Wazee Wafupi na Mbuzi, Sasa Kama Mechi Haikuhusu Baki Nyumbani - CEO wa Simba

Walisema Kuna Wazee Wafupi na Mbuzi, Sasa Kama Mechi Haikuhusu Baki Nyumbani - CEO wa Simba

 "Nafahamu wote kwa pamoja tuna hamu ya kupata matokeo katika mechi hii lakini matokeo haya kuyapata kwa kushinda na kufuzu. Sisi tumeweka mazingira mazuri ambayo yataiwezesha timu yetu kufuzu."

"Nipo hapa kuwataka Watanzania kujitokeza kwa wingi Uwanja wa Mkapa alkini ningependa kutoa taarifa muhimu kwamba tunaendelea kushirikiana na serikali kuimarisha usalama wa siku hiyo. Tunawataka wapenzi wetu kuhakikisha kwamba wanazingatia mazingatio yote ambayo yatawekwa ya usalama. Hatutaruhusu mtu yeyote ambaye sio Mwanasimba kutuharibia shughuli yetu."

"Katika mchezo uliopita walisema maneno mengi kwamba kuna wazee wafupi, mbuzi lakini tuwatumie ujumbe kwamba kama mechi haikuhusu wabaki nyumbani na sisi tumejiandaa kuthibiti hilo kama klabu."- CEO wa Simba, Zubeda Sakuru akiongea kwenye mkutano na wanahabari

RC Tanga awaita wananchi wenye migogoro katika kampeni ya msaada ya sheria


Na Rebeca Duwe Tanga

MKuu wa mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batilda Buriani  amewataka wananchi wa wa mkoa wa Tanga wenye Migogoro mbalimbali ikiwemo ndoa ,ukatili wa kijinsia vitendo vya ulawiti kwa watoto wa kike na wa kiume katika jamii ,wanawake na makundi maalumu na wale wenye migogoro ya ardhi kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Kampeni ya msaada ya sheria ya Mama Samia itakayoanza rasmi kesho April 8

Hayo aliyasema  wakati akifungua mafunzo ya siku moja yaliyofanyika katika ukumbi wa mkoa Tanga ya wataalamu  mbalimbali  wakiwemo  wanasheria wa kujitegemea,wanasheria wa serikali, polisi Dawati,na maafisa maendeleo kutoka halmashauri zote 11 ili kuweza kuwafikia wananchi wa mkoa huo katika siku tisa za kampeni hiyo ambapo itahitimishwa April 17 .

Aidha Batlida alieleza kuwa kamapeni hiyo katika mkoa wa Tanga itazinduliwa rasmi kesho tarehe 8 April katika viwanja wa vya Tangamano jijini Tanga ambapo tarehe 9 wataalamu watatawanyika kuendelea kutoa huduma hizo katika kata zote na vijiji na mitaa yote katika halmashauri zote za mkoa huo.
 
Samabamba na hayo alitoa wito kwa wataalam wote kuwafikia wananchi wote kama ambavyo wamekusudia  kuwafikia na kuweza kusaidia wale wenye changamoto ya migororo ya muda mrefu.

Kwa upande wake MKurugenzi wa Huduma za msaada wa Sheria  Esta Msambazi  alisema kuwa  lengo kampeni hiyo nikuweza  kuwafikia wananchi kwenye ngazi ya vijiji wenye changamoto mbalimbali ikiwemo migogoro  ya ardhi  ili kuweza kuwapunguzia idadi kuwaya watu wanaofikia katika ofisi ya mkoa ili watatuliwe migogoro yao.

Alisema kwamba kampeni imekuwa na mafanikio makubwa kwani wametatua migogoro ya aina mbalimbali  na kuweza kuwafikia mtu mmoja mmoja  zaidi ya milioni 2.2 katika mikoa 22 ambapo Jana wamekamilisha mkoa wa Arusha na kesho mkoa wa Tanga ambao ndio wa 24.

 

Monday, April 7, 2025

BALOZI NCHIMBI AFUNGA KAZI RUVUMA


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, amehitimisha ziara yake ya siku tano mkoani Ruvuma, akisisitiza kuwa CCM itaendelea kuwa chama cha wanachama, kwa ajili ya kuwatumikia wananchi wote na kuwa mtetezi wa wanyonge.

Balozi Nchimbi amesema kwamba katika kuendeleza nafasi yake kama taasisi imara inayohusika na uongozi wa nchi, CCM hakina budi kuendeleza misingi ya sera zake zinazolenga kubadilisha hali za maisha ya watu, kuendana na mahitaji ya nyakati, na kuzingatia maslahi ya taifa.

Dkt. Nchimbi aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na wanaCCM na wananchi wa mji wa Songea, waliokusanyika kumpokea alipofika kufungua mradi wa kitega uchumi wa Tawi la CCM la Mshangano mjini Songea, Jumapili tarehe 6 Aprili 2025, ikiwa ni siku ya tano tangu alipoanza ziara hiyo tarehe 2 Aprili 2025.

Katika ziara hiyo aliyoanzia katika Wilaya ya Tunduru, Namtumbo, Nyasa, na hatimaye Songea mjini, Balozi Nchimbi alitoa pongezi kwa Serikali ya CCM, inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM, kwa jinsi inavyotafsiri kwa vitendo na ufanisi, Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020-2025, kupitia miradi ya maendeleo na huduma kwa wananchi.

Balozi Nchimbi alitoa maelekezo kwa Serikali kuendelea kusimamia na kubuni mipango inayolenga kuongeza matokeo chanya kwenye shughuli za uzalishaji mali, ikiwemo kilimo na madini, ili wakulima na wachimbaji madini waendelee kuzalisha kwa tija itakayoongeza pato la taifa na kuboresha maisha ya wananchi.

Aidha, Balozi Nchimbi alitembelea na kutoa maelekezo mahsusi katika miradi kadhaa ya maendeleo na ya kimkakati inayotekelezwa na Serikali kupitia wizara na taasisi zake, ikiwemo mradi wa uzalishaji mbegu chini ya Mamlaka ya Mbegu Nchini (ASA) na ujenzi wa Bandari ya Nyasa, kwa lengo la kuendelea kutafsiri utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM.

Katika mikutano ya hadhara katika wilaya mbalimbali, pamoja na kusalimia wananchi katika maeneo ya Songea Vijijini, Mbinga na Songea mjini, Balozi Nchimbi alipokea taarifa za utendaji wa kazi kutoka kwa viongozi wa Chama na Serikali, na pia alipokea maoni ya wananchi kuhusu changamoto zinazowakabili, kupitia kwa wabunge na wananchi moja kwa moja, kisha kutoa maelekezo ya kutatuliwa kwa kero hizo.

Balozi Nchimbi, ambaye amehitimisha rasmi ziara yake kwa kuondoka mkoani humo Jumatatu tarehe 7 Aprili 2025, alitumia nafasi hiyo kuwashukuru wanaCCM na Watanzania wote kwa ujumla kwa ushirikiano wao na Serikali ya CCM katika kulinda tunu za taifa, ikiwemo amani na utulivu. Alitoa wito wa kuendeleza hali hiyæo wakati nchi inapoelekea kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu.


Source

Diva awachana waandaji wa tuzo za EAEA za Kenya! Adai wanaotoa hela ndio wanaoshinda

 Diva awachana waandaji wa tuzo za EAEA za Kenya! Adai wanaotoa hela ndio wanaoshinda



Source

Maria Sarungi Hana Mamlaka ya Kutoa Maamuzi ya Ndani Chadema - John Mrema

Maria Sarungi Hana Mamlaka ya Kutoa Maamuzi ya Ndani Chadema - John Mrema


 "Hivi karibuni, Mwanaharakati, Maria Sarungi, aliandika katika ukurasa wake wa "X" akikitaka Chama kiyaweke hadharani majina ya wote wanaotaka ubunge kwa udi na ubani bila reforms, na akatuhumu kuwa watu hao wanataka kufanya "blackmail" (kutishia) eti watahama chama. Pia, Maria Sarungi, bila kujali mamlaka ya Ofisi yako, ametaka ajulishwe ni nani amewaita watiania kwenye mkutano huo maalum maana uongozi mzima upo field. Na akataka Chama kisiwahusishe watiania ("do not engage them"), bali waachwe waende CCM. Kauli hizi za Maria Sarungi (ambaye si mwanaChadema), zinafanana na kauli za Mhe. Lissu na Mhe. Lema. Aidha, kauli hizi zinaingilia mamlaka ya ndani ya Chama, na Ofisi yako imezinyamazia kimya, huku kukiwa na taarifa kuwa Mwanaharakati huyo ana mgongano wa kimaslahi wa kutaka Chama kisishiriki uchaguzi wa mwaka huu kwa maslahi yake binafsi. Kauli za Maria ambaye ni swahiba wa karibu wa baadhi ya viongozi wetu wakuu zinazidi kuongeza vitisho na kufinya uhuru wa maoni kuelekea katika kikao maalum"- Mrema.


John Mrema, mmoja wa wanaounda kundi la G-55 ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) akisoma waraka wao kwa Katibu Mkuu wa CHADEMA wakati akizungumza na wanahabari kwa niaba ya wenzake ambao baadhi walikuwapo eneo hilo mkoani Dar es Salaam siku ya Jumapili Aprili 6, 2025.

Heche: Hatuogopi Uchaguzi, Tunataka Mabadiliko Kwanza

 

Heche: Hatuogopi Uchaguzi, Tunataka Mabadiliko Kwanza


Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo @chadematzofficial, John Heche, leo Aprili 6, 2025, akizungumza na wakazi wa Wilaya ya Tandahimba mkoani Mtwara amewaambia CHADEMA haiogopi uchaguzi ila wanataka mabadiko ya kimsingi ili uchaguzi uwe huru na wa haki.

"Mimi Heche niogope uchaguzi kweli? Dkt. Slaa anajua nimeanza kugombe nikiwa mwaka wa pili Chuo Kikuu, pale kwetu Tarime ni CHADEMA ni kama dini kila uchaguzi tulikuwa tunawapiga mpaka walipoanza kutuibia, ndio maana tunasema (No Reform no Election)"


Source

“SALAMA” , WIMBO WA NYASANI UNAOPONYA MIOYO, UKILETA AMANI KATIKA KILA NAFSI!

 

Je, umewahi kusikia wimbo unaokugusa hadi kwenye nafsi yako? Basi usikose kutazama video ya Salama kutoka kwa msanii huyu mwenye kipaji kikubwa – Nyasani.

Katika video hii inayopatikana YouTube, Nyasani ametuletea ujumbe mzito wa matumaini, upendo na amani, akitumia sauti ya kuvutia na mashairi yenye nguvu. 

Mandhari ya video ni ya kupendeza, yenye ubunifu mkubwa na uhalisia unaoendana na maudhui ya wimbo.

Wimbo huu hauishii tu kuwa burudani  bali ni tiba ya moyo kwa yeyote anayepitia changamoto au anayetafuta utulivu wa ndani. 

"Salama" ni wimbo wa kutazama zaidi ya mara moja, utakuacha ukitafakari na kutamani kuusikiliza tena na tena.

Utakubaliana nasi – hii ni moja ya kazi bora kabisa kutoka kwa wasanii wa kizazi kipya. Usiwe wa mwisho kuiona. Shiriki na rafiki, tusambaze ujumbe wa amani! ✨

🎧 Bonyeza hapa kutazama sasa hivi 👉 Salama - Nyasani (YouTube)

Pentagon FC yakubali mziki wa Utalingolo FC

 


Timu ya Pentagon FC ya Jijini Mbeya inayoshiriki ligi daraja la tatu  imekubali kichapo cha goli moja kwa sifuri dhidi ya timu ya kata ya Utalingolo FC ya mkoani Njombe katika mchezo wa kirafiki uliopigwa kwenye uwanja wa Iyunga Sekondari jijini humo.

Wakizungumza mara baada ya kuibuka na ushindi huo baadhi ya viongozi wa kata ya Utalingolo akiwemo Elia Chilatu afisa Mtendaji wa kijiji cha Utalingolo pamoja na Renatus Mgani ambaye ni Afisa Mtendaji wa kata hiyo wanasema ushindi huo umekuwa ni chachu kubwa kwao kuelekea kwenye mashindano mengine mkoani Njombe.

"Kuja huku ni moja ya maandalizi ya  mashindano ya Mwanyika Cup yanayoenda kuanza tarehe tisa ambapo sisi ni mabingwa watetezi na tumedhamiria kwenda kutetea ubingwa wetu ndio maana tumekuja huku ili kufanya maandalizi ya kutosha"amesema Chilatu

Delbet Ngole ni Kamptain wa Utalingolo FC Mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo amesema maandalizi yao kwa sasa yamekamilika kuingia kwenye mashindano.

"Tumemaliza mchezo wetu hapa salama lakini tunamshukuru Diwani wetu Erasto Mpete kwa kutuwezesha ziara yetu kwa ajili ya maandalizi ya ligi ya Mbunge, kwa kuwa hapa tumekutana na kipimo kizuri"amesema Ngole

Yohana Homba ni mwalimu wa Pentagon FC amefurahishwa na mchezo huo uliozidi kuimarisha ushirikiano baina ya timu hizo zinazotoka mikoa tofauti.

"Jambo lililofanyika hapa ni zuri na sisi tumetamani kufika halmashauri ya mji wa Njombe kwasababu ya hii changamoto waliotuonyesha"amesema Homba

Baadhi ya mashabiki waliosafiri na timu wamefurahishwa na kiwango cha timu yao huku wakimpongeza diwani kwa kuwaandalia ziara hiyo ambayo imekuwa kubwa kwao.

Kufika kwa Timu hiyo jijini Mbeya ni ahadi ya diwani wa kata ya Utalingolo ambaye pia ni mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa Njombe Erasto Mpete,kutoka nje ya mkoa na kutembelea sehemu mbalimbali ikiwemo Uwanja wa Sokoine unaotumika kwenye michezo ya ligi kuu na hii ni baada ya timu hiyo kufanya vizuri kwenye mashindano ya msimu wa mwaka wa 2024 ya ligi ya Mbunge wa Njombe mjini Mwanyika CUP ambapo timu hiyo iliibuka mabingwa. 

Msaada wa kisheria wawafikia wakazi wa Tanga (Mama Samia leagal Aid)


NA REBECA DUWE TANGA

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi  wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi  kujitokeza kwa  katika kampeni ya msaada wa kisheria  ya Mama Samia ambayo itafanyika kwa siku tisa katika kata zaidi ya 100  zilipo katika Halmshauri  zote 11 za mkoani hapa.

Kampeni hiyo, ambayo tayari imeshafanyika katika mikoa 22 ya Tanzania Bara, imeweza kuwafikia wananchi zaidi ya milioni 2.2 na kushughulikia jumla ya migogoro elfu 20,000, ambapo migogoro zaidi ya 4000 imeweza kutatuliwa na kumalizika kabisa.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini  kwake Mkuu wa mkoa huyo amesema kuwa kampeni hiyo si yalele  mama hivyo amewataka wananchi watoe taarifa za ukweli na za uhakika ili waweze kupatiwa msaada wa kisheria.

Kwa upande wake Laurent Burilo ambaye ni Afisa Uchunguzi Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria na Mratibu wa kampeni hiyo  alisema kuwa   changamoto zote  walizokutana nazo katika mikoa hiyo 22 ambayo tayari wamepita kuzitatua kisheria.

Alisema miongoni mwa Migogoro ya Ardhi, Mirathi na  ndoa ambayo  inahatarisha amani na usalama wa familia na jamii, na wakati mwingine husababisha mivutano isiyokwisha, ambayo inazuia maendeleo na ushirikiano.

Burilo aliongeza kusema kuwa  ni muhimu kwa jamii kuhamasika kutatua migogoro hii kwa njia ya amani ili kudumisha umoja na ushirikiano.

Sunday, April 6, 2025

WAZIRI MAVUNDE ATOA SIKU 30 MGODI WA MAGAMBAZI KUTHIBITISHA UWEZO WA KUUENDELEZA


📍 Handeni, Tanga

Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, ametoa muda wa siku 30 kwa Kampuni PMM Tanzania Limited inayoendesha na kumiliki Mgodi wa Kati wa Dhahabu wa Magambazi, uliopo katika Wilaya ya Handeni, Mkoani Tanga, kuwasilisha taarifa za kifedha na kiufundi ili kuthibitisha uwezo wake wa kuendesha mgodi huo kwa viwango vinavyohitajika kisheria.

Waziri Mavunde ametoa agizo hilo leo Aprili 6, 2025, wakati akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Nyasa, Kata ya Kang'ata, Wilaya ya Handeni, ambapo alizungumza na wananchi wanaozunguka mradi huo.

Amesema kuwa baada ya kusikiliza pande zote za Kampuni ya PMM ma CANACO zinazohusika katika mgodi huo, ameona ni muhimu kuchukua hatua ili kuhakikisha rasilimali hiyo inaleta manufaa kwa wananchi wa Nyasa, Handeni na taifa kwa ujumla.

"Nimeagiza kuwa ndani ya siku 30, kampuni inayoliki huu mgodi, inatakiwa kuwasilisha taarifa za kifedha na kiufundi zinazoonesha uwezo wa kuendesha mgodi wa leseni ya kati, ikiwa ni pamoja na kuwa na mtaji usiopungua Shilingi Bilioni 30 kwa mujibu taarifa ya upembuzi yakinifu ya mradi na zoezi hili litaanza Aprili 8 hadi Mei 7, 2025." Amesema Mavunde.

Sambamba na taarifa hiyo, Mhe. Mavunde amewaelekeza wamiliki hao kuhakikisha katika kipindi hicho cha siku 30, kama Kampuni haitakuwa na uwezo wa kuendesha mgodi iwe imempata mwekezaji mwenye uwezo wa kiufundi na kifedha kuendesha mgodi huo kwa tija na kwamba kinyume na hivyo, Serikali itachukua hatua za kutangaza mgodi huo kwa wawekezaji wengine wenye sifa.

Aidha, amemuelekeza Mkuu wa Wilaya ya Handeni kuandaa utaratibu maalum wa kuhesabu fedha za asilimia mbili kutoka mauzo ya awali ya dhahabu, na kuhakikisha zinawekwa kwenye akaunti ya maalum kwa ajili ya wachimbaji wadogo waliopisha maeneo hayo ya uchimbaji kama walivyokubaliana awali.

Amesisitiza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ina dhamira ya dhati kuhakikisha wananchi wananufaika moja kwa moja na rasilimali za madini zinazopatikana katika maeneo yao.

Vilevile, Waziri Mavunde ameahidi kuwa wananchi wa Nyasa wataanza kuona uzalishaji wa dhahabu ndani ya mwaka huu 2025.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Wakili Albert Msando, amesema kuwa hatua hiyo itakuwa na tija kwa wananchi wa Nyasa na Wilaya nzima ya Handeni kuona matokeo chanya ya uwepo wa madini katika maeneo yao.

Naye, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Handeni, Mhe. Amiri Changogo, amesema hatua ya Waziri Mavunde ni utekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi na maagizo ya chama kwa Serikali.

Akizungumza katika Mkutano huo, Mbunge  wa Handeni Vijijini, Mhe. John Sallu, amemshukuru Waziri Mavunde kwa kusikiliza na kufanyia kazi kilio cha wananchi wa Nyasa, na kueleza kuwa hatua hiyo inaleta matumaini kwa maendeleo ya eneo hilo.

Coastal Union Yamtimua Kocha Mwambusi, Kuikabili Yanga Kesho Bila Kocha




Coastal Union imemfuta kazi kocha Juma Mwambusi kutokana na mwenendo mbaya wa timu na kutoelewana na baadhi ya wachezaji

Aliondoka kambini jana usiku na amedumu kwa miezi 5 na nusu ndani ya timu hiyo

Kesho Jumatatu Coastal wataikabili Yanga pale KMC Complex

VIONGOZI WA MIKOA NA WILAYA WAAGIZWA KUHAMASISHA WANANCHI KUSHIRIKI MBIO ZA MWENGE


OR-TAMISEMI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa, amewataka Wakuu wa Mikoa na Wilaya kote nchini kuhamasisha ushiriki wa wananchi katika Mbio za Mwenge wa Uhuru za mwaka 2025, ambazo zinalenga kuchochea utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika halmashauri ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi na kuleta maendeleo nchini.

Ametoa agizo hilo akiwa katika Shule ya Msingi Ukombozi, Ikwiriri, kabla ya kumkaribisha Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Taifa, Ismail Ussi, kuzungumza na wananchi waliokusanyika kushuhudia uraghabishaji wa falsafa ya Mwenge wa Uhuru uliofanywa na wanafunzi wa shule hiyo.

Mhe. Mchengerwa amesisitiza kuwa atahakikisha wananchi wanashiriki kikamilifu kwenye maeneo yote ambayo Mwenge wa Uhuru utapita kukagua miradi ya maendeleo na kuwaelekeza Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha wanahamasisha wananchi kwa nguvu zote kushiriki shughuli hizo muhimu.

"Mbio za Mwenge zinahamasisha maendeleo, na ndio maana zinaambatana na uzinduzi wa miradi ya kimkakati ya maendeleo. Ushiriki wa wananchi ni fursa muhimu ya kuwajengea uelewa katika usimamizi na utekelezaji wa miradi hiyo," amesema Waziri Mchengerwa.

Aidha, Waziri Mchengerwa amemweleza Kiongozi wa Mbio za Mwenge Taifa, kuwa Wilaya ya Rufiji imepiga hatua kubwa katika miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa shule, barabara, masoko, vituo vya afya na zahanati, miradi ambayo baadhi yake itakaguliwa na Mwenge wa Uhuru mwaka huu.

Kwa upande wake, Ismail Ussi amesema kila Mtanzania anapaswa kuienzi falsafa ya Baba wa Taifa, akisisitiza kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendeleza falsafa hiyo kwa kumkabidhi jukumu la kuongoza Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025, ambapo miradi ya maendeleo itakaguliwa na kuzinduliwa pale itakapobainika kutekelezwa kwa viwango stahiki.

Source

UTEUZI MPYA: Rais Samia afanya uteuzi, yumo Balozi Sirro, Prof Kondoro

UTEUZI MPYA: Rais Samia afanya uteuzi, yumo Balozi Sirro, Prof Kondoro


Rais Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali huku akimteua IGP mstaafu Balozi Simon Sirro kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO).


Balozi Sirro anachukua nafasi ya Meja Jenerali mstaafu, Michael Isamuhyo ambaye amemaliza muda wake.


Taarifa iliyotolewa leo Aprili 5, 2025 na Katibu Mkuu Kiongozi Dk. Moses Kusiluka, imesema Rais amemteua Profesa John Kondoro kuwa Mwenyekiti wa Kamisheni ya Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech), akichukua nafasi ya Profesa Makenya Maboko ambaye amemaliza muda wake.


Profesa Emanuel Mjema ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) kwa kipindi cha pili.


Taarifa hiyo iliyosainiwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Sharifa Nyanga imesema Mhandisi Mwanasha Tumbo ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), akichukua nafasi ya Profesa Esnat Chaggu aliyemaliza muda wake.


Rosemary Silaa ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Bohari ya Dawa (MSD) kwa kipindi cha pili.

Saturday, April 5, 2025

Wimbo Mpya : NG'WANA KANG'WA - SUMU KALI

Ng'wana Kang'wa ameachia Album Mpya inaitwa MBINA... Ngoma zote zipo https://www.youtube.com/@ngwanakangwa .. Hii hapa ngoma inaitwa SUMU Kali

SIGARA, POMBE ZACHANGIA ONGEZEKO LA WAGONJWA WA MACHO


Na Hadija Bagasha - Tanga

Matumizi ya sigara na pombe yametajwa kuwa ni moja ya sababu zinazopelekea ongezeko la wagonjwa wa macho siku hadi siku.  

Ugonjwa wa macho umetajwa kuwa ni changamoto ambayo imekuwa ikiongezeka ikihusishwa na sababu kadhaa ikiwemo matumizi hayo ya sigara,  pombe na wagonjwa kutumia dawa za macho bila kupata ushauri wa kitaalamu. 

Katika kambi ya siku mbili ya macho ambayo inaendelea katika shule ya sekondari Usagara inayoratibiwa na taasisi ya Bilal Muslim Mission of Tanzania kwa kushirikiana na Mbunge wa jimbo la Tanga Ummy Mwalimu ambapo idadi ya watu wameonekana kumiminika kwenye huduma hiyo wakihitaji huduma za matibabu. 

Mbunge wa jimbo la Tanga Ummy Mwalimu ametoa wito kwa wananchi kuacha kutumia dawa za macho kiholela bila kupata ushauri wa kidaktari kutokana na sababu za kitaalamu zinazoonyesha sababu hiyo kama ugonjwa wa macho. 

"Ummy amesema kwamba kutokana na uwepo wa changamoto ya macho hasa kwa baadhi ya wananchi katika jimbo hilo ameona ni vyema kuwepo na kambi hiyo ambayo itakuwa mkombozi kwa wananchi ambao wanashindwa kuoata huduma za matibabu kutokana na sababu za kiuchumi. 

"Nitumie fursa hii kutoa wito kwa wananchi kutumia nafasi hiyo kujitokeza kwa wingi ili kufanyiwa uchunguzi na hatimaye kuweza kupata matibabu ya changamoti zitakazobainika, "alisisitiza Mbunge Ummy. 

Kwa upande wake Mratibu wa kambi za macho wa Bilal Muslim Mission of Tanzania Ally Sharif amemshukuru Mbunge huyo kwa kuishawishi kambi hiyo kuja kwa mara ya pili katika Jiji la Tanga kutokana na kuwepo kwa wananchi wenye uhitaji wa huduma za macho.

Mratibu huyo amesema kwamba wanatarajia kuwaona wagonjwa zaidi ya 5000 kwa kuwapatia miwani,  dawa,  na kufanya upasuaji kwa wagonjwa watakaogundulika kuwa na tatizo la mtoto wa jicho. 

"Awali tulipokuja wagonjwa walikuwa ni wengi mno tulitoa matibabu tukaondoka lakini Mbunge wa jimbo la Tanga Ummy Mwalimu alituomba turudi tena na hivyo tukakaona tuje tena kwenye kambi hii na kutoa huduma kwa wananchi hivyo tumpongeze sana kwa namna anavyowajali wananchi wake hasa katika sekta ya afya, "alisema 

Naye Mratibu wa kambi ya macho Mkoa Tanga ambaye ni Daktari Bingwa wa macho katika Hosoitali ya Rufaa ya Mkoa Tanga Bombo Dkt Hussein Tayebji amesema sababu zinazochangia watu kuwa na matatizo ya macho ni kwamba watu hawana utamaduni wa kwenda kupima macho hospitalini mara kwa mara wakati mwingine kutokana na sababu za kiuchumi.

"Lazima watu waje hospitali wapime afya ya macho wajue tatizo lao kama ni dawa matibabu yake ni miwani au ni dawa au kubadilisha mfumo wa maisha lakini tabia ya kuvuta sigara,  unywaji wa Pombe pia huchangia tatizo la macho, "alisema Dkt huyo. 

Baadhi ya wagonjwa waliopatiwa matibabu ya macho katika kambi hiyo wamempongeza Mbunge Ummy kwa kuwajali wanyonge ambao kama sio uwepo wa kambi hiyo wangelazimika kulipia huduma za matibabu katika hospitali mbalimbali. 













Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...