Tuesday, September 24, 2019

Picha : TAMASHA LA 14 LA JINSIA LAFUNGULIWA JIJINI DAR ES SALAAM..ANGALIA MATUKIO YOTE YALIYOJIRI HAPA


Balozi Getrude Mongella ambaye ni Rais wa Kwanza wa Bunge la Afrika (PAP) na Katibu Mkuu wa Mkutano wa Nne wa wanawake duniani uliofanyika mwaka 1995 Beijing China amefungua Tamasha la 14 la Jinsia 2019 leo Jumanne Septemba 24,2019 katika viwanja vya TGNP Mtandao Mabibo Jijini Dar es salaam.



Akizungumza wakati wa kufungua Tamasha hilo litakalodumu kwa muda wa siku nne (Septemba 24 hadi 27,2019),Balozi Mongella maarufu 'Mama Beijing' amesema ili kujenga Tanzania ya Viwanda ni lazima wanawake na wanaume washiriki.

Balozi Mongella pia amehamasisha umuhimu wa wanawake kushirikishwa katika utengezaji wa Ilani za uchaguzi za vyama vya siasa ili kuhakikisha masuala ya wanawake yanaingizwa kufikia usawa wa kijinsia.

"Huu msemo wa Wanawake wakiwezeshwa wanaweza mimi nasema hii ni dhambi...hatupaswi kuwa omba omba...Sisi wanawake tunaweza tunachotaka ni vikwazo vinavyotukwamisha viondolewe njiani,tunataka wanawake washiriki kwenye utengenezaji wa ilani za uchaguzi ili Rais atakayegombea apewe na kubeba ajenda zinazohusu wanawake",alisema Balozi Mongella.

"Tuone masuala yanayotuhusu wanawake ni sehemu ya ajenda na uchaguzi utakapopita iwe rahisi kwa tutakayemchagua kuwa Rais kumuomba akimbizane na ajenda za wanawake na asipofanya hivyo atakuwa hajatekeleza Ilani",aliongeza Mama Mongella.

Hata hivyo aliipongeza serikali kwa kutekeleza ajenda za Mkutano wa Beijing mfano Sera ya elimu bure hali inayosababisha ongezeko la watoto wa kike kwenda shule na imeondoa kikwazo cha watoto kukosa elimu.

Aidha Balozi Mongella aliwataka wanasiasa kuepuka Rushwa huku akieleza kuwa Wanasiasa wanaohonga 'rushwa' ili wapate uongozi wanabaka siasa.

Naye Mgeni Maalumu kutoka serikalini,Naibu Waziri - Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile alisema Ukatili wa Kijinsia ni janga jipya linaloitia doa nchi ya Tanzania hivyo kuwaomba wadau wote kuungana kutokomeza hali hiyo.

"Hatuwezi kufikia usawa wa kijinsia katika taifa kama tunaendelea kuwa na matukio ya ukatili ya kijinsia ambayo nyuma yake yana sura ya mila,desturi,umaskini na ukosefu wa elimu.Naomba tuvunje ukimya na tuepuke kumaliza kesi zinazohusu masuala ya ukatili kwa kuyamaliza kienyeje",alisema Dkt. Ndugulile.

Dkt. Ndugulile alitumia fursa hiyo kuwahamasisha wanawake kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi za uongozi kwenye Uchaguzi Mkuu mwaka 2020 na uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 24,2019.

Akielezea kuhusu Tamasha la 14 la Jinsia 2019,Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao,Lilian Liundi alisema linahudhuriwa na wadau mbalimbali wa haki za wanawake kutoka ndani na nje ya Tanzania likiongozwa na mada kuu 'Wanaharakati wa jinsia mbioni kubadili dunia'.

"Tamasha hili lina umuhimu wa kipekee kwani tunaendelea kusherehekea maadhimisho ya miaka 25 ya TGNP tangu ianzishwe mwaka 1993 na kidunia tumeanza kusherehekea maadhimisho ya miaka 25 ya Azimio na Mpangokazi wa Beijing ambapo kilele chake ni mwaka 2020",alisema Liundi.

ANGALIA HAPA CHINI PICHA ZA MATUKIO YALIYOJIRI
Balozi Getrude Mongella akifungua Tamasha la 14 la Jinsia 2019 katika viwanja vya TGNP Mtandao Mabibo Jijini Dar es salaam leo Jumanne Septemba 24,2019. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Balozi Getrude Mongella akifungua Tamasha la 14 la Jinsia 2019 katika viwanja vya TGNP Mtandao Mabibo Jijini Dar es salaam leo Jumanne Septemba 24,2019.
Balozi Getrude Mongella akisalimiana na Naibu Waziri - Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati wa kufungua Tamasha la 14 la Jinsia 2019 katika viwanja vya TGNP Mtandao Mabibo Jijini Dar es salaam leo Jumanne Septemba 24,2019. 
Naibu Waziri - Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akizungumza wakati wa ufunguzi wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019.
Awali Balozi Getrude Mongella (kulia) na Mwenyekiti wa Bodi ya TGNP Mtandao,Asseny Muro wakifurahia jambo wakati akiwasili katika viwanja vya TGNP Mtandao kwa ajili ya kufungua Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019.
Meza kuu wakiwa wamesimama baada ya Balozi Getrude Mongella kuwasili katika viwanja vya TGNP Mtandao jijini Dar es salaam.
Washiriki wa Tamasha la 14 la Jinsia 2019 wakiendelea na burudani wakati Balozi Getrude Mongella akiwasili katika viwanja vya TGNP Mtandao kwa ajili ya kufungua tamasha hilo.
Mwenyekiti wa Bodi ya TGNP Mtandao,Asseny Muro akizungumza wakati wa ufunguzi wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019.
Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao,Lilian Liundi akizungumza wakati wa ufunguzi wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019.
MC wakati wa ufunguzi wa Tamasha la 14 la Jinsia 2019 ambaye ni Mwanachama wa TGNP Mtandao Ulu Mallya akitoa maelekezo mbalimbali wakati wa sherehe hizo za ufunguzi wa tamasha.
Sehemu ya wageni waalikwa wakati wa tamasha hilo.
Spika Mstaafu wa Bunge la Tanzania,Anne Makinda akizungumza wakati wa ufunguzi wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019.
Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Anders Sjoberg akizungumza wakati wa ufunguzi wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019.
Waziri Mkuu Mstaafu Tanzania,Joseph Sinde Warioba akizungumza wakati wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakicheza muziki.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 likiendelea.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo.
Mwakilishi wa balozi wa Ireland nchini akizunguza kwenye tamasha la 14 la jinsia 2019
Mwakilishi Mkazi Un Women nchini Tanzania akizunguza kwenye tamasha la 14 la jinsia 2019

Utoaji Tuzo maalum kwa viongozi wa serikali ambao wamechangia mabadiliko ya kisera kuwezesha masuala ya kijinsia kufanikiwa ikiwemo utekelezaji wa maazimio ya Beijing mwaka 1995.Kushoto ni Afisa Programu Mwandamizi TGNP Mtandao,Deogratius Temba akishikana mkono na Balozi Getrude Mongella baada ya kupokea cheti kwa niaba ya Rais Mstaafu wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Benjamin Mkapa ambaye wakati wa uongozi wake aliweka mazingira wezeshi kupokea na kusaidia utekelezaji wa maazimio ya Beijing 1996.
Balozi Getrude Mongella akikabidhi tuzo kwa Mhe. Joseph Sinde Warioba ambaye ametunukiwa tuzo ya heshima kwa sababu kwa muda mrefu amekuwa mstari wa mbele kusimamia ajenda ya haki za wanawake na usawa wa kijinsia kila mahali anapokuwa.
Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya TGNP Mtandao,Asseny Muro akimkabidhi Balozi Getrude Mongella tuzo ya heshima kwa kumtambua kuwa mwanamke shupavu anayesimamia haki za wanawake na usawa wa kijinsia bila kutetereka.
Bhoke Wankyo Nyerere akipokea Tuzo ya Heshima iliyotolewa kwa hayati Baba wa taifa kama sehemu ya kuendeleza kuuenzi mchango wake katika kutetea,kulinda na kupigania haki za watu wote zikiwemo za wanawake na usawa wa kijinsia.
Tuzo ya heshima kwa Hayati marehemu Sophia Kawawa ikitolewa ikiwa ni tuzo ya heshima kuuenzi mchango wake katika kupigania haki za wanawake hasa waajiriwa.
Agripina Mosha akipokea kwa niaba ya Dr. Inj. Strato Mosha tuzo ya heshima kwake kwa kujitoa tangu awali kabisa wakati shirika la TGNP linaanza.
Mwakilishi wa Prof. Simon Mbilinyi akipokea tuzo ya heshima kwa kujitoa kwake kwa rasilimali na wakati mwingine ushauri
Utoaji tuzo kwa watu binafsi ambao walitumia rasilimali zao,muda,ushauri,kuwezesha TGNP Mtandao kusimama na kufika hapo ilipo sasa.
Mwakilishi,akipokea tuzo ya heshima kwa Marehemu Prof. Seth Chachage
Dkt. Hellen Kijo Bisimb akionesha tuzo ya heshima aliyopewa kutokana na kuendeleza agenda ya ukombozi wanawake kimapinduzi ndani ya shirika la LHRC.
Vicky Tetema kutoka Under the Same Sun akipokea tuzo kutokana na kuendeleza agenda ya ukombozi wanawake kimapinduzi ndani ya shirika hilo.
Mary Lusindi akipokea tuzo kutokana na kuendeleza agenda ya ukombozi wanawake kimapinduzi ndani ya TGNP.
Usu Mallya akioesha tuzo ya heshima aliyopewa kutokana na kuendeleza agenda ya ukombozi wanawake kimapinduzi ndani ya TGNP
Usu Mallya akipiga picha na Mkurugenzi wa TGNP Mtandao,Lilian Liundi baada ya kupewa tuzo ya heshima.
Perpetua Magoka akipokea tuzo ya heshima kwa niaba ya WLC
Utoaji tuzo ukiendelea
Mwakilishi wa halmashauri ya Kishapu akipokea tuzo kutokana na halmashauri hiyo kutenga fedha kwenye bajeti zake mwaka wa fedha 2019/2020 kwa mrengo wa kijinsia baada ya kujengewa uwezo na TGNP Mtandao.Halmashauri hiyo pia imetenga bajeti kuwezesha wasishana waliopo shuleni kupata taulo za kike bure wanapozihitaji.
Mwakilishi wa halmashauri ya Kisarawe akipokea tuzo kutokana na halmashauri hiyo kutenga fedha kwenye bajeti zake mwaka wa fedha 2019/2020 kwa mrengo wa kijinsia baada ya kujengewa uwezo na TGNP Mtandao.Halmashauri hiyo pia imetenga bajeti kuwezesha wasishana waliopo shuleni kupata taulo za kike bure wanapozihitaji.
Mwakilishi wa halmashauri ya Morogoro akipokea tuzo kutokana na halmashauri hiyo kutenga fedha kwenye bajeti zake mwaka wa fedha 2019/2020 kwa mrengo wa kijinsia baada ya kujengewa uwezo na TGNP Mtandao.Halmashauri hiyo pia imetenga bajeti kuwezesha wasishana waliopo shuleni kupata taulo za kike bure wanapozihitaji.
Mwakilishi wa UN Women nchini Tanzania akipokea tuzo ya heshima
Mwakilishi wa Sweden nchini Tanzania,Anders Sjoberg akipokea tuzo ya heshima
Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao akipokea tuzo ya heshima kwa kupigania masuala yanayohusu wanawake.
Wafanyakazi wa TGNP Mtandao wakipiga picha ya pamoja baada ya mkurugenzi wa TGNP Mtandao kupokea tuzo.
Wafanyakazi wa TGNP Mtandao wakipiga picha ya pamoja baada ya mkurugenzi wa TGNP Mtandao kupokea tuzo.
Naibu Waziri - Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikata utepe kufungua maonesho kwenye Tamasha la 14 la Jinsia 2019 katika viwanja vya TGNP Mtandao Mabibo Jijini Dar es salaam leo Jumanne Septemba 24,2019. 
Picha ya pamoja baada ya ufunguzi wa Tamasha la 14 la Jinsia 2019 katika viwanja vya TGNP Mtandao Mabibo Jijini Dar es salaam leo Jumanne Septemba 24,2019. 
Picha ya pamoja baada ya ufunguzi wa Tamasha la 14 la Jinsia 2019 katika viwanja vya TGNP Mtandao Mabibo Jijini Dar es salaam leo Jumanne Septemba 24,2019. 
Picha ya pamoja baada ya ufunguzi wa Tamasha la 14 la Jinsia 2019 katika viwanja vya TGNP Mtandao Mabibo Jijini Dar es salaam leo Jumanne Septemba 24,2019. 
Picha ya pamoja baada ya ufunguzi wa Tamasha la 14 la Jinsia 2019 katika viwanja vya TGNP Mtandao Mabibo Jijini Dar es salaam leo Jumanne Septemba 24,2019. 
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

Waziri Jafo awataka Watanzania kujitokeza Tamasha la JAMAFEST


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Suleiman Jaffo, amewataka watanzania
kujitokeza kwa wingi katika tamasha la JAMAFEST linaloendelea katika Uwanja wa
Taifa jijini Dar es Salaam ili kujifunza Utamaduni wa nchi zinazoshiriki tamasha hilo.

Waziri Jaffo ameyasema hayo mapema hii leo alipotembelea maonesho ya Utamaduni wa Nchi za Afrika Mashariki yanayoendelea katika uwanja wa Taifa jijini Dar es
Salaam.

"Naomba nitumie nafasi hii kuwaomba watanzania kujitokeza kwa wingi katika
tamasha hili la Utamaduni ili kujifunza Utamaduni wa nchi mbalimbali zinazoshiriki
tamasha hili na hii ndio fursa pekee ya kukuza lugha ya Kiswahili ili kuunga mkono
juhudi za Mheshimiwa Rais," Waziri Jaffo.

Aidha Waziri Jaffo amewakumbusha amesema kuwa tamasha hili ni la kihistoria hapa nchini kwani limekutanisha zenye Utamaduni tofautitofauti kwa wakati mmoja hivyo ni fursa kwa watanzania kujifunza mambo mbalimbali kama ususi, ushonaji, ngoma za asili na michezo mbalimbali.

Tamasha la JAMAFEST linashirikisha jumla ya nchi tano ambazo ni Kenya, Uganda,
Burundi, Rwanda na wenyeji Tanzania tamasha hilo linarajiwa kumalizika siku ya
tarehe 28 Septemba 2019

Saturday, September 21, 2019

Kilimo bora cha maboga


Boga ni zao ambalo mmea wake unakuwa kwa kutambaa na ni la mviringo, ngozi yake ni nyororo na rangi yake ni ya njano inayoelekea kwenye rangi ya chungwa au rangi ya kijani. Katikati ya boga kuna mbegu na massa, Boga lipo katika jamii ya Cucurbita pepo.

Asili yake
Asili ya boga ni Amerika kaskazini, maboga yamekuwa yakipandwa kwaajili ya biashara na kwaajili ya chakula. Kwa sasa maboga yamekuwa yakilimwa maeneo mbalimbali duniani, Antarctika pekee ndiko maboga hayawezi kustawi. Mataifa yanayozalisha maboga kwa wingi ni Marekani (USA), Canada, Mexico, India, and China.

Hali ya hewa & udongo 
Maboga yanahitaji joto la wastani kutoka kwenye jua, pia eneo ambalo halituamishi maji udongo wake uwe na pH kati ya 6.0 – 6.8. Pia udongo uwe na joto inchi tatu (sm 7.6) kushuka chini angalau nyuzi 60 °F (15.5 °C), maboga yatadhoofika kama maji yatakosekana.

Utayarishaji wa shamba
Shamba litayalishwe kwa umakini bila kuwa na sehemu ya kutuamisha maji maana mmea wa maboga na maboga yenyewe hutambaa chini, tumia jembe la ng'ombe, trekta, jembe la mkono au pawatila, changanyia mbolea za asili (samadi au mboji) na udongo ili kurutubisha shamba.

Utayarishaji wa mbegu
Mbegu za maboga zinatoka ndani ya maboga, kuna mbegu zilizoboreshwa (za kisasa) na za asili, andaa mbegu mapema wiki moja au mbili kabla ya kupanda.

Upandaji
Maboga hupandwa kwa kufukia mbegu sentimita 1 au 2 chini ya udongo , panda mbegu 2 kila shimo. Pia panda umbali wa sentimeta 30 kutoka shina hadi shina na mita 1.5 – 2 kutoka mstari hadi mstari.

Matandazo (mulches )
Kwasababu ni zao linalotambaa basi lazima tuangalie namna ya kutandaza, weka nyasi na mabaki ya mimea mingne kufunika ardhi. Baada ya miche kutambaaa kwa kiasi unaweza kuweka matandazo (mulches) ambayo yaweza kuwa nyasi kavu kwenye udongo ili kuzuia upotevu wa unyevu vile vile kupunguza uotaji wa magugu shambani kwako. Vile vile matandazo yakioza yanaongeza rutuba kwenye udongo na hulinda udongo dhidi ya mmomonyoko wa udongo.

Mbolea
Katika matumizi ya mbolea yanatofautiana kutokana na mbegu, Lakini tumia mbolea za asili (samadi au mboji) ili kuongeza rutuba kwenye udongo, ukihitaji kutumia mbolea za viwandani weka kiasi sana, labda eneo hilo kama hakuna rutuba, mbolea ya NPK inaweza tumia.

Upaliliaji & unyevu
Palilia shamba nyasi zinapoanza kuota, pia safisha shamba ili kuondoa wadudu. Shamba la maboga linatakiwa liwe na unyevunyevu kila mara ili maboga yaweze kustawi vizuri yasidumae.

Uvunaji
Maboga hukomaa baada ya siku 95 mpaka 120, ili kujua kuwa boga lako limekomaa unaangalia kikonyo, kikonyo cha boga kinapoteza maji na kinaanza kuwa kikavu.

Thursday, September 19, 2019

MAMBO Manne (4) Ya Kimafanikio Ya Kumfundisha Mtoto Wako Mapema...!!!


Msingi mkubwa wa mafanikio ya mtu yeyote kitabia unatokana na malezi bora aliyopata hasa akiwa mtoto kuanzia mwaka mmoja hadi miaka kumi na mbili. Katika kipindi cha mwaka 1 hadi 12 ndio kipindi muhimu sana cha malezi.

Tabia nyingi ambazo zinatengenezwa au kufundishwa katika kipindi hiki, huwa kuna uwezekano mkubwa wa kudumu maishani mwako kote. Hapa hii inatokea bila kujali tabia hiyo ni nzuri kwako au mbaya.

Kwa mfano, kama ulikuwa unaendekeza uvivu au kama ulikuwa mtu wa kuchapa kazi sana na kujiona huo ndio kama utamaduni katika kipindi cha mwaka 1 hadi 12, ni rahisi tu tabia hizo kuendelea hadi ukubwani.

Kwa mantiki hiyo ndiyo maana ni muhimu sana kumfundisha mtoto wako mambo ya kimafanikio yatakayomsaidia  kwa baadae kwenye maisha yake. Mambo hayo ni yepi? Karibu na twende pamoja tujifunze.   

1. Mfundishe, njia bora ya kufikiri.

Ikiwa hupendi sana maisha yako yalivyokuwa mwanzoni yaendelee kwa kizazi chako, sasa ni wakati wa kumfundisha mtoto wako namna bora ya kufikiri. Hapa ni lazima umfanye mtoto wako aweze kufikiri chanya.

Unaweza kumfanya moto wako afikiri chanya kwa kumpa vitabu vizuri chanya kama uwezo wa kusoma anao au kwa maneno maneno unayomwambia. Hiyo haitoshi pia unaweza ukamtafutia marafiki wazuri wenye mtazamo chanya.

Kama mtoto wako unamlea kwa mtazamo chanya, kufikiri kwa njia bora itakuwa kwake ni jambo ambalo halikwepeki. Anza leo kuweka mikakati yakumjengea mwanao njia bora ya kufikiri itakayomsaidia hata kumjengea mtazamo chanya pia.

2. Mfundishe, kujitegemee mapema.

Kati ya kitu kitakachofanya ujenge msingi imara kwa watoto wako kwa baadae ni kule kufanya wajitegemee mapema. Hapa inatakiwa umfundishe mtoto wako kufanya baadhi ya mambo mwenyewe.

Kwa mfano, anapokuwa mkubwa kidogo kama ni kufua mwache afue mwenyewe. Kama ni kusaidia kazi fulani acha aifanye. Njia hii inakuwa bora kwa kujua kwamba kuna vitu fulani anatakiwa awajibike.

Lakini kama utakuwa ni mtu wa kumlea mtoto wako kwa kutaka kila kitu  afanyiwe basi wewe ndiye utakuwa mtu wa kwanza kumharibu mtoto wako. Mfanye mtoto wako ajitegemee mapema, 
itamsaidia sana kwa baadae katika makuzi yake.

3. Mfundishe, ajifunze kuchukua hatua mapema.

Siku zote vitendo ni bora sana kuliko kusema. Kwa kuwa unajua umuhimu wa hili anza kumfundisha mtoto wako juu ya umuhimu wa kuchukua hatua mapema katika maisha yake hata kwa vitu vidogo ambavyo anavyofanya.

Kwa kumfundisha hivi unakuwa unajenga utamaduni imara ambao utamfanya mtoto wako hata atakapokuwa mkubwa atakuwa anajua na kutambua umuhimu wa kuchukua hatua mapema pia kwenye maisha yake.

Ili hili lifanikiwe, mfundishe kitu fulani halafu anza kufatilia utekelezaji. Unaweza ukamwacha hata maswali kama kazi ya nyumbani, halafu uone atamaliza baada ya muda gani? Utakuwa unafanya hivyo mara kwa mara ili kumfanya achukue hatua mapema zaidi.

4. Mfundishe ajue mambo yote huwa hayaendi kama yalivyopangwa.

Katika kumfundisha atambue kwamba mambo kuna wakati hayaendi kama yanavyopangwa, subiri kipindi ambapo anataka kitu fulani tena kwa hamu kubwa. Inapofika katika hicho kipindi kwa makusudi mnyime.

Najua kama ilivyo kwa watoto walio wengi tabia zao atalia. Mwache alie halafu tafuta siku ama muda akitulia, kama kile kitu kilikuwa cjha kununua, mnunulie na mpe somo mapema atambue kuna wakati mambo hayaendi moja kwa moja kama uliyopanga.

Fanya hivi kwa mtoto ambae ameshaanza kujitambua ikiwezekana kuanzia angalau darasa la tano. Rudia tena na tena zoezi hili, mpaka ifike mahali ajue kwamba mategemeo na uhalisia ni vitu viwili tofauti.

Yapo mambo mengi unayoweza kumfundisha mwanao ya kumweka juu kimafanikio kwa baadae. Unaweza kumfundisha mwanao pia jinsi ya kuishi na watu sahihi, uaminifu katika maisha, misingi bora ya kuishi maisha ya kiroho napengine hata faida ya kujiamini.

Fanyia kazi haya machache kwa leo na chukua hatua katika kuweza kufikia mafanikio yako makubwa.

Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
0713 04 80 35,

DC NYIMBI AZINDUA MBIO NDEFU ZA ROCK CITY MARATHON 2019 MWANZA

Na Fabian Fanuel - Malunde 1 blog
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mkoa wa Mwanza Dkt. Phillis Nyimbi leo amezindua mbio ndefu za Rock City Marathon 2019 katika Uwanja wa Rock City Mall Mwanza.

Uzinduzi huo umefanyika leo Alhamis Septemba 19,2019 ukishirikisha wadau mbalimbali wa mbio hizo, viongozi kutoka Serikalini, Viongozi kutoka Taasisi mbalimbali, Wadhamini wa mbio pamoja na waandishi wa habari.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongela, Mkuu wa wilaya ya Nyamagana  Dkt. Phillis Nyimbi amewashukuru waandaji wa mbio hizo 'Capital Plus International' kwa kazi kubwa wanayoifanya na kuomba washiriki wengi kujiandisha kwa mwaka huu kushiriki mbio hizo zitakazofanyika Mkoani Mwanza 20 Oktoba mwaka huu.

Huu ni msimu wa kumi wa mbio hizi ambazo zimekuwa na mwitikio mkubwa kutokana na washiriki wengi kuongezeka kila mwaka na mwaka huu inatarajiwa washiriki zaidi ya elfu tatu watashiriki huku waandaji wakiweka bayana zawadi zaidi ya Milioni 30 zitashindaniwa kwa mbio za Aina mbalimbali Kama kilomita 42, 21, 5 na 2.5.

Miongoni mwa wadhamini wa mbio ndefu za Rock City Marathon 2019 ni Tigo Rock City Mall,Tiper, Global Guard,Mwanza Water,Pigeon Hotel,Bodi ya Utalii na Pepsi.
Mkuu wa Mkoa wa Nyamagana Dr Phillis Nyimbi akisaini namba yake ya ushiriki wa mbio za Rock City Marathon huku Mratibu wa mbio hizo Magdalena Laizer na Katibu wa chama cha mbio Mkoa wa Mwanza Peter Mugaya wakishuhudia.


Msimamizi wa Mbio za Rock City Marathon John Bayo akimvisha Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Dkt. Phillis Nyimbi medali.
Msimamizi wa Mbio za Rock City Marathon John Bayo akimvisha Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Dkt. Phillis Nyimbi medali.
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Dkt. Phillis Nyimbi akionesha medali.
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Dkt. Phillis Nyimbi akionesha medali.

Mkuu w Wilaya ya Nyamagana Dkt. Phillis Nyimbi akikata utepe wa Uzinduzi wa mbio za Rock City Marathon 2019 uliofanyia Viwanja vya Rock City Mall Mwanza.

Tuesday, September 17, 2019

Tatizo La Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

Dalili:mwili kuchoka,maumivu ya mgongo na kiuno,kutopata choo vizuri hata ukipata choo kinakuwa kigumu

Misuli  kulegea na kusinyaa hata kushindwa kufika kileleni miguu kuuma na kuwaka moto:

TIBA YAKE:

TULLO4 MIX.Ni dawa pekee inayoweza kutibu matatizi hayo, inarudisha nguvu za kiume mara dufu na kukufanya urudie tendo la ndoa zaidi mara tatu bila kuchoka au kukinai.

NTINJE3 PUMP.Ni dawa inayoongeza maumbile na kukupa umbile la kudumu.Itumie tiba hii kuokoa ndoa yako na kuokoa kukimbiwa na umpendae.
GASELA: Ni dawa mvuto kumvuta umpendae na kumrudisha alie mbali .

NTOBO: Inatibu KISUKARI:siku7 na kuzalisha insulin kwa wingi na kumfanya mwenyetatizo hili kupona kabisa ugonjwa wa kisukari.

mpigie DR LIZENGO .OFISI IPO MBAGALA SABASABA.SIMU 0655283534/0621737576


Tuesday, September 10, 2019

Nyumba Inauzwa Ipo Dodoma Uzunguni Bei Chee Kabisa...



BEST DALALI anakutangazia kuna Nyumba inauzwa ipo Dodoma maeneo ya Uzunguni, Nyumba inaukubwa wa mita 51 kwa 28 sawa na Sq.m 1,428, Nyumba haina mgogoro ipo Full Document, Bei Milion 200, wasiliana nasi kwa maelezo zaidi. 0657 16 82 72 / 0689 95 33 35

Pia kama una Nyumba ya kupangisha au kuuza au Kiwanja au Shamba unataka kuuza au kununua usipate tabu BEST DALALI tupo kwa ajili yako.  piga simu kwa mawasiliano zaidi 0657 16 82 72 / 0689 95 33 35

Mikoa tunayo ihudumia ni Dar es salaam, Dodoma, Arusha na Mwanza


Friday, September 6, 2019

Kambi Ya Kitaaluma Kwa Wanafunzi Wa Kidato Cha Nne Wenye Ufaulu Hafifu Yazinduliwa Simiyu

Na Stella Kalinga, Simiyu RS
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amezindua rasmi kambi ya kitaaluma ya siku 60 kwa wanafunzi wa kidato cha nne waliopata ufaulu hafifu (daraja sifuri) katika mtihani wa 'Mock', lengo likiwa ni kuwasaidia waweze kuongeza ufaulu wao katika mtihani wa Taifa utakaofanyika mwezi Novemba 2019.

Akizindua kambi hiyo Septemba 05, 2019 Mtaka amesema wanafunzi hao watafundishwa masomo manne tu ambayo ni Kiswahili, Kiingereza ,Uraia(Civics) na Historia, hivyo akatoa wito kwa walimu mahiri waliochaguliwa kuwafundisha wanafunzi hao kwa moyo na upendo ili wanafunzi hao waweze kupata alama D na kuendelea katika mtihani wa Taifa.

"Hawa watoto wafundisheni masomo manne, Kiswahili, Kiingereza, Historia na Civics; wafundisheni kwa moyo, wapeni mazoezi ya mara kwa mara katika siku hizi 60 watakazokuwa kambini, muwasaidie watoke kwenye F wapate angalau D nao wapate vyeti, kwa sababu hata ajira siku hizi kigezo ni angalau mtu awe na cheti cha kidato cha nne" alisema Mtaka.

Katika hatua nyingine Mtaka ametoa wito kwa jamii ya Simiyu kuendelea kuwekeza kwenye elimu ili kuuwezesha mkoa kushindana kiuchumi kwa kuwa maendeleo ya kiuchumi yanategemea maendeleo ya elimu katika eneo husika.

Afisa Elimu mkoa wa Simiyu, Mwl.Ernest Hinju amesema kati ya Wanafunzi 9956 waliofanya mtihani wa  Utimilifu (Mock), 1300 hawakupata alama D hata moja, hivyo waliopata matokeo hafifu (daraja sifuri) wamewekwa pamoja wafundishwe masomo manne ili waweze kuongeza ufaulu katika mtihani wa Taifa, huku waliopata daraja la kwanza hadi la nne wakiendelea na kambi kufundishwa masomo yote.

Aidha, Hinju ameongeza kuwa  kambi za kitaaluma zimechangia kuongeza ufaulu kwenye Mtihani ya Taifa wa darasa la saba, kidato cha nne na kidato cha sita, ambapo katika matokeo ya kidato cha nne mwaka 2016 ufaulu ulikuwa asilimia 74 mkoa ukiwa nafasi ya 14 kati ya mikoa 26, mwaka  2017 ufaulu asilimia 79.8 nafasi ya 11 na mwaka 2018 ufaulu asilimia 82.5  ukashika nafasi ya 9 kati ya mikoa 26.

Kwa upande wao wanafunzi wa kidato cha nne waliopo kambini  wameshukuru kuwekewa kambi hiyo na wakaeleza imani yao juu ya uwepo wa kambi hiyo ambapo wameomba kambi za kitaaluma Simiyu ziwe endelevu ili ziwasaidie kujifunza na kujiandaa vema na mitihani ya Taifa hatimaye mkoa uweze kufanya vizuri.

"Tunawashukuru viongozi wetu na wazazi wetu kwa kukubali kutuwekea kambi ya kitaaluma, ninashauri kambi hizi zisiishie kwetu ziendelee na kwa wadogo zetu ili mkoa wetu uweze kuongeza ufaulu" alisema Esther Nashoni mwanafunzi shule ya sekondari Bariadi(Bariadi)

Mkuu wa Shule ya Sekondari Simiyu, Mwl.Paul Susu amesema walimu wamejiandaa vema katika kuwafundisha wanafunzi na kuwapa mitihani ya mara kwa mara ili waweze kufanya vizuri, huku akitoa wito kwa wadau mbalimbali wa elimu kujitolea katika ujenzi wa miundombinu ya elimu ili kuwe na miundombinu ya kutosha itakayoongeza nafasi kwa kambi za kitaaluma kufanyika  vizuri.

Kambi ya kitaaluma kwa wanafunzi wa Kidato cha nne iliyozinduliwa Septemba 05, 2019 ilianza rasmi Septemba Mosi na inatarajiwa kufanyika ndani ya siku 60 kabla ya kufanya Mtihani wa Taifa mwezi Novemba.

MWISHO



Source
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...