Sunday, August 31, 2025

HIFADHI YA MPANGA-KIPENGERE YAKONGA NYOYO ZA WALIMBWENDE MISS UNIVERSE 2025


Na Beatus Maganja, Mbeya

Walimbwende wa Miss Universe Tanzania 2025 wametoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kutokana na maono yake ya kukuza sekta ya utalii nchini kupitia maboresho ya miundombinu ya Hifadhi ya Mpanga Kipengere jambo linaloifanya Hifadhi hiyo kuwa kivutio kikubwa cha watalii nyanda za juu kusini.

Kauli hiyo imetolewa Agosti 29, 2025 na walimbwende hao mara baada ya kufanya ziara maalum katika hifadhi hiyo iliyopo Wilaya ya Mbarali, Mkoa wa Mbeya ambayo inasimamiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA ambapo walibaini fursa kubwa ya kuitangaza Tanzania kimataifa kupitia urithi wa asili wa eneo hilo.

"Tumeona historia ya Chifu Mkwawa, maji ya baraka na maajabu ya asili ya kipekee. Mpanga-Kipengere ni hazina ya Taifa letu. Sasa ni jukumu letu kama mabalozi kuutangaza urithi huu Kwa dunia nzima " alisema Nais Sayona ambaye ni mshindi wa Miss Universe Tanzania 2025.

Mbali na kukiri kujifunza mengi katika ziara hiyo, Mkurugenzi wa Mashindano hao nchini, Millen Happiness Magesa alisema mshindi wa shindano hilo atabeba kipande cha makala ya ziara hiyo na kukipeleka katika mashindano ya dunia yanayotarajiwa kufanyika Thailand huku akisisitiza kuwa hiyo ni nafasi ya kipekee ya kuitangaza Tanzania kupitia hifadhi hiyo.

Kwa upande wake, Afisa Utalii Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Ananias Lugendo alisema Serikali imewekeza katika maboresho ya miundombinu ya hifadhi hiyo ili kuifanya iweze kufikika kwa urahisi zaidi. Aliongeza kuwa uwepo wa mazao mengi ya kiutalii unachangia kuifanya kuwa na mvuto wa kudumu mwaka mzima.

"Hifadhi hii inajivunia kuwa na zaidi ya maporomoko 53 yakiwemo aina 13 kati ya 14 zinazopatikana duniani ambapo maporomoko ya Kimani yamekuwa kivutio kikuu na sasa kupitia walimbwende hawa itapata hadhi ya kimataifa " alisema Lugendo.

Naye Afisa Utalii wa Hifadhi hiyo, Pendo Kimaro alisema ujio wa walimbwende hao ni hatua kubwa ya kuitangaza hifadhi hiyo Kimataifa kupitia majukwaa yao ya Kitaifa na Kimataifa.

"Tunataka ulimwengu ujue kuwa Tanzania ina maajabu, sio tu wanyamapori bali ina hazina ya kipekee yenye mvuto wa kiasili" alisema Kimaro.

Ziara hiyo ilifanyika kuanzia Agosti 27, 2025 ikihusisha walimbwende kumi bora wa Mashindano ya Miss Universe Tanzania 2025 wakiongozwa na mshindi wa taji hilo Bi. Nais Sayona.

Washiriki hao walipata fursa ya kujionea vivutio mbalimbali vya hifadhi hiyo ikiwemo historia ya Chifu Mkwawa, bustani ya dunia, eneo la "massage" ya asili, tafakuri ya kina, matembezi ya mwituni, kuoga mvuke na maporomoko makubwa ya Kimani yenye urefu za zaidi ya mita 250.


Tuesday, August 26, 2025

DOTTO BAHEMU AMEWAOMBA WANA - CCM KUVUNJA MAKUNDI NA KUSHIRIKIANA KWA PAMOJA KUTAFUTA USHINDI WA KISHINDO

 

Dotto Bahemu baada ya kukabidhiwa na msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Ngara 
Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Ngara Bwana Constatino Msemwa ( aliyeko upande  wa Kulia )  akimkabidhi Fomu Dotto Bahemu fomu ya Uteuzi wa kugombea Ubunge Jimbo la Ngara kupitia chama cha Mapinduzi 
Dotto Bahemu akisaini kwenye kitabu cha Wageni baada ya kufika ofisi za Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Ngara


Na Mariam Kagenda _Kagera

Mgombea Ubunge Jimbo la Ngara kupitia Chama cha Mapinduzi Dotto Bahemu amewaomba wanachama wa Chama Cha Mapinduzi ( CCM) kuvunja makundi na kuungana kwa Pamoja ili kukiwezesha   chama hicho kupata ushindi wa Kishindo  kwa Rais, Mbunge na Madiwani 

Bahemu amesema hayo leo Agosti 26,2025  baada ya kuchukua fomu ya Uteuzi wa kugombea Ubunge Jimbo la Ngara katika ofisi ya msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Ngara .

''Uchaguzi wa kura za maoni umeisha na kila mmoja alikuwa na kundi lake hivyo sasa  ni jukumu letu sote kuungana kwa pamoja kutafuta kura za kishindo kwa Rais wetu, Mbunge na madiwani wote wanaotokana na chama cha mapinduzi",amesema Dotto Bahemu.

Ameongeza kuwa atashirikiana na kila mtu hata ambao walikuwa hawamuungi mkono wakati wa uchaguzi wa kura za maoni   na kati ya watu atakaoanza kuwatafuta na kuzungumza nao  ni wale ambao walikuwa hawamuungi mkono  na hawakuwa upande wake ili kujua tatizo liko wap  huku akiwaomba wananchi wa Jimbo la Ngara kudumisha amani katika kipindi chote cha Uchaguzi.

Kwa upande wake Msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Ngara Constantino Msemwa amesema kuwa Dotto Bahemu amekabidhiwa fomu hiyo baada ya kutimiza  Vigezo na masharti yote.

Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo Bwana Ndaisaba Ruholo amesema atampatia ushirikiano wa Kutosha Dotto Bahemu katika kipindi chote cha Uchaguzi na kuwaomba wananchi na wanachama wa chama cha mapinduzi Jimbo la Ngara kumpa ushirikiano Mgombea aliyeteuliwa na CCM.


Wananchi waiomba Serikali kutengeneza mfumo mmoja ili wafanyabiashara walipe Kodi kulingana na uwezo wa biashara zao


Wananchi wameiomba Serikali  Kupitia Mamlaka ya mapato Tanzania TRA kuhakikisha unatengeneza mfumo mmoja ambao utasaidia kwa kila mtanzania anayefanyabiashara kulipa kodi kwa kiwango cha uwezo wa biashara yake.

Hayo aliyasema katibu w Jumuiya ya wa wafanyabiashara Mkoa wa Tanga  Ismail Masuod wakati akizungumza katika semina ya wafanyabiashara ya Elimu kwa mlipa kodi  mkoa wa Tanga  iliyofanyika katika ukumbi wa YDCP jijini Tanga

ambapo alisema kuwa elimu inasaidia wafanyabiashara kujua umuhimu wa kulipa kodi na sheria ya kodi.

Aidha alisema kuwa hiyo itasaidia mambo makubwa matatu kwanza ni kutengenza walipa kodi wapya,kwani kuwa na mpango maalum wa kutengeneza walipa kodi katika nchi kutakuwa walipo kodi wacheche.

Akizungumzia Daniel Ramadhani ambaye ni Kaimu meneja wa mkoa wa Tanga  alisema lengo la Mafunzo hayo kwa wafanyabiashara ni kuwawezesha kujua sheria ya fedha kutokana mabadiliko ya sheria kwaajili ya maborehsoya kodi yanayotokea kila baada ya bunge la bajet ambapo Mamlaka ya mapato Tanzania TRA imepanga kuwafikia makundi yote ambayo inatakiwa kulipa kodi.

Aliongeza kusema kuwa  sheria iliuofanyiwa marekebisho ni pamoja na sheria ya ongezeko la kodi ya samani ambayo kutakuwa  zuio la kodi ya samani ni mauzo ya biadhaa kwa maana ya asilimia tatu ya mauzo ya bidhaa na mauzo ya ya huduma kwa mfano banki na mitandao mengine.

Kwa upande Chama Siliwa Afisa Masidizi wa elimu na mawasiliano wa Mamlaka ya mapato Tanzania TRA  kutoka makao makuu alisema wametoa elimu kwa mlipa kodi kutokana mabadiliko ya sheria mpya ya ulipaji wa kodi hivyo tumeamua kuwapa elimu hiyo wazijue wanapoendelea kulipa kodi changamoto kuwa ya watu kutokulipa kodi ni pamoja na uelewa mdogo wa sheria.

Monday, August 25, 2025

WALICHOKIFANYA WANANCHI WA WILAYA YA MULEBA KWA WALIOTEULIWA KUGOMBEA NAFASI YA UBUNGE JIMBO LA MULEBA KASKAZINI NA KUSINI

Wananchi wa Jimbo la Muleba Kasikazini baada ya kumpokea ndugu Adonis Bitegeko mteuliwa nafasi ya Ubunge Jimbo la Muleba Kaskazini
Bwana Adonis Bitegeko aliyeteuliwa kugombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Muleba Kasikazini akizungumza baada ya kufika ofisi za chama cha Mapinduzi (CCM)

Na Mariam Kagenda _Kagera

Wananchi wa wilaya ya Muleba mkoani Kagera wamejitokeza kwa wingi uwanja wa Ndege Bukoba kuwapokea walioteuliwa na Chama Cha Mapinduzi kugombea nafasi ya Ubunge katika Jimbo la Muleba Kusini na Muleba Kaskazini wilaya ya Muleba mkoani Kagera .

Wananchi hao baada ya kuwapokea wateuliwa wa nafasi hiyo ambao ni Adonis Bitegeko aliyeteuliwa kugombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Muleba Kaskazini na Dkt. Oscar Kikoyo Jimbo la Muleba Kusini waliwasindikiza kwa msafara wa magari na pikipiki mpaka kwenye ofisi za chama cha mapinduzi .


Baada ya Wagombea hao kufika ofisi za Chama hicho wameishukuru halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi kwa imani yao kubwa ya kuwateuwa kugombea nafasi ya Ubunge katika uchaguzi mkuu ambao unatarajiwa kufanyika October 2025 na Wananchi ambao waliwachagua kwa kura nyingi katika uchaguzi wa Kura za maoni .


Leo Agosti 25 watachukua fomu za kugombea nafasi ya Ubunge kupitia Chama cha Mapinduzi katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika October 2025 .

Ikumbukwe kuwa Adonis Bitegeko ndiye aliyeongoza katika Uchaguzi wa kura za maoni kwa Jimbo la Muleba Kasikazini kwa kupata kura 4392 na Dkt Oscar Kikoyo aliongoza kwa kupata kura 4710 .

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Muleba Athumani Kahara amewahimiza wanachama wa chama hicho kuvunja makundi kwani kwa sasa kilichobaki ni kuwanadi Wagombea walioteuliwa na Chama Cha Mapinduzi na kuhakikisha wanatafuta ushindi wa kishindo wa Chama hicho.

Aidha amesema kuwa watafanya Kampeini za kistaarabu za kuhakikisha wanailinda amani na kujiepusha na vitendo vyote vinavyoweza kupelekea uvunjifu wa amani katika kipindi cha Uchaguzi mkuu .
Dkt. Oscar Kikoyo aliyeteuliwa kugombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Muleba Kusini akizungumza na wananchi baada ya kufika ofisi za Chama Cha Mapinduzi.
Adonis Bitegeko akisaini kitabu cha Wageni katika ofisi za Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Muleba
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Athumani Kahara( Aliyevaa Kanzu ) akiwa na wateuliwa wa nafasi ya Ubunge baada ya kufika ofisi za chama hicho.
Wananchi wa wilaya ya Muleba wakiwa uwanja wa Ndege kuwasubiri wateuliwa
Wananchi wakimpokea Adonis Bitegeko aliyeteuliwa kugombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Muleba Kaskazini

Thursday, August 14, 2025

KATAVI WAMPA HEKO RAIS SAMIA UMEME VIJIJINI


Wananchi wa Kijiji cha Mapili Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwawezesha kubadili maisha yao kupitia mradi wa umeme uliotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Wametoa shukrani hizo kwa nyakati tofauti kijijini hapo Agosti 11, 2025 wakati wa kampeni maalum ya uhamasishaji wa matumizi ya umeme kwa ajili ya shughuli za kiuchumi inayotekelezwa na REA katika maeneo mbalimbali kote nchini.

"Tunaishukuru Serikali inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kabla ya kupata nishati hii ya umeme mazingira hayakuwa mazuri, usiku hatukuwa na mwanga sasa hivi tunaishi kwa amani na hata baadhi ya shughuli za kimaendeleo zinafanyika hadi muda wa usiku lakini pia tunapata habari kwa kutazama luninga muda wowote tunaotaka pia baadhi ya vijana wamepata ajira kupitia umeme," alisema Mwalimu Mstaafu, Mkazi wa Kijiji cha Mapili, Amos Katawa.

Mrisho Mussa Fundi Uchomeleaji katika Kijiji cha Mapili alisema kabla ya umeme kufika kijijini hapo walikuwa wakilazimika kufanya shughuli zao maeneo ya mjini ambapo ni mbali na kijijini hapo na hivyo kusababisha kupanda kwa gharama ya bidhaa walizokuwa wakizalisha pamoja na kutumia muda mrefu kukamilisha kazi.

"Tulikuwa tunalazimika kutengenezea mageti huko Inyonga na kisha tunasafirisha, hali hii ilikuwa ni usumbufu kwetu hadi kwa wateja wetu, lakini sasa mambo yote tunafanya hapa, hakuna haja tena ya kurudi mjini, nawasihi mafundi na wengine wenye fani zao wasipende kukimbilia mijini; Rais Samia ametuona, kila kitu hapa kijijini sasa hivi kinapatikana," alisema fundi Mussa.

Kwa upande wake Scholastica Kitwewe, Mkazi wa Kijiji cha Mapili alisema umeme umerahisisha maisha ya wanawake kijijini hapo kwani hapo awali walikuwa wakitumia muda mwingi kuandaa mahindi ya unga kwa kutwanga katika kinu lakini sasa mashine za kusaga na kukoboa nafaka zimefunguliwa kijijini hapo jambo ambalo linarahisisha shughuli zao za mapishi ya kila siku na kuwaokolea muda.

Kwa upande wake, Elasto Mwampaya maarufu kama Fundi Lam ambaye ni Fundi Seremala kijijini hapo alisema kuwa umeme umewezesha kukua kwa karakana yake ya useremala na kwamba hivi sasa anatengeneza fenicha zenye ubora na kuuza katika mikoa mbalimbali kote nchini jambo ambalo halikuwezekana hapo awali kabla ya kufikishiwa umeme.

Alisema umeme umemuwezesha kupanua wigo wa ajira na kwamba katika karakana yake ameajiri vijana wengi na pia anatoa mafunzo kwa vijana namna ya kutengeneza bidhaa kwa kutumia vifaa vya kisasa vinavyotumia umeme.

Akizungumza kuhusiana na umeme kijijini hapo, Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Mapili Anthony Mwijuma, aliipongeza REA kwa kutekeleza mradi huo ambao alisema umekuwa ni neema kwa wananchi wake ikilinganishwa na hali ilivyokuwa kabla ya kufikiwa na umeme.

"Wananchi wa Mapili tunasema asante kwa Rais Samia kwani kupitia umeme vijana wamepata ajira, wengine wamebuni miradi na biashara ndogondogo za vinywaji, vifaa vya simu na wengine sasa hivi na mafundi wa kuchomelea hapahapa kijijini," alisema Mwijuma.

Akizungumza hali ya usambazaji umeme mkoani Katavi, Msimamizi wa miradi ya REA Mkoani humo, Mha. Gilbert Furia, alisema vijiji vyote vina umeme na kazi inayoendelea sasa ni kusambaza umeme katika vitongoji ambavyo havikufikiwa.

"Tunamshukuru Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha ambayo imewezesha kufikisha umeme katika vijiji vyote 49 ndani ya Halmashauri za Mlele na Mpimbwe na sasa tunatekeleza mradi wa kusambaza umeme vitongojini; hadi sasa katika Hamashauri hizi vitongoji 176 kati ya vitongoji 251 vimefikiwa na mradi unaendelea wa kufikisha umeme kwenye vitongoji vilivyobaki," alisema Mha. Furia

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Wilaya ya Mlele, Yahaya Mbulu aliipongeza REA kwa kukamilisha mradi wa kufikisha umeme vijijini na alisema kuwa amejionea namna ambavyo kazi ya kufikisha umeme vitongojini ikiendelea kutekelezwa kwa kasi.

"Tunaishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kupitia REA; vijiji vyote vimefikiwa; wananchi wa Mlele tunasema asante kwa Serikali maana umeme umeleta fursa, Mlele ya jana sio ya leo, hatua imepigwa," alisisitiza Mbulu.





 

Sunday, August 10, 2025

Mama Manyara adaiwa kumuua mtoto wake kikatili kwa shoka.


Na John Walter Babati, Manyara

Wakazi wa Kitongoji cha Vituwey, Kijiji cha Ngoley, Kata ya Mwada wilayani Babati mkoani Manyara wameshtushwa na tukio la kikatili lililofanywa na mwanamke anayejulikana kwa jina la Mariam Mohamed, anayedaiwa kumuuua mtoto wake wa kumzaa wa kiume mwenye umri wa miaka 2.5 kwa kumtenganisha viungo vya mwili wake kwa kutumia shoka.

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Vituwey, Jackson Mombo, amesema tukio hilo lililotokea majira ya saa nne asubuhi Agosti 8, 2025, limewaacha wananchi midomo wazi na kushindwa kuamini kilichotokea. 

Ameongeza kuwa ni muhimu jamii kuwa karibu na mtu yeyote anayeonyesha dalili za mawazo mazito au matatizo ya afya ya akili ili kuepusha madhila kama hayo.

Mashuhuda wamesema kuwa baada ya mauaji hayo, Mariam alipiga yowe akisema "jamani nisaidieni, nimemuua mwanangu", hali iliyowafanya majirani kukimbilia nyumbani kwake ambapo walipofika, walimkuta akiwa hajakimbia, huku mwili wa mtoto ukiwa juu ya godoro wanalolalia.

Baadhi ya majirani wamesema hawaamini kuwa mama huyo amefanya kitendo hicho kwa akili timamu, wakidhani huenda alikuwa na tatizo la afya ya akili.

Baba mkwe wa Mariam, Kimweri Juru, ameeleza kuwa aliwahi kumpa onyo mara kadhaa kuhusiana na tabia ya unywaji wa pombe, lakini hakutaka kusikia, na kwamba matokeo haya yanaweza kuwa ni sehemu ya madhara ya tabia hiyo.

Wakati tukio linatokea, mume wa Mariam hakuwepo nyumbani kwani usiku alikuwa akilinda mazao shambani dhidi ya wanyama waharibifu.

Jeshi la Polisi limefika eneo la tukio, kuchukua mwili wa marehemu na kumkamata Mariam kwa uchunguzi zaidi.

Tukio hili limeongeza hofu kwa wakazi wa Tarafa ya Mbugwe, kwani ni la pili ndani ya wiki moja, baada ya lile la kitongoji cha Mbugani, Kata ya Magugu, ambapo mwanaume alimuua jirani yake mbele ya watoto wake wawili wadogo kwa kumkatakata kwa panga.

Wakazi wanasema matukio haya ya mauaji miongoni mwa watu waliokuwa wakiheshimika na kuonekana wema, yanahitaji uchunguzi wa kina ili kubaini chanzo chake na kuchukua hatua za kudhibiti hali hiyo.

Thursday, August 7, 2025

Vasco Mgimba aibuka mshindi kwenye kura za maoni Ludende

 



Aliyekuwa Diwani wa kata ya Ludende wilaya ya Ludewa mkoani Njombe Ndugu Vasco Weston Mgimba ameibuka mshindi wa kura za maoni za wajumbe wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kata hiyo kwa ajiri ya kupata ridhaa ya kuwa diwani.

Mgimba aliyekuwa akitetea nafasi hiyo ameibuka kidedea kwa kupata kura 382 akimshinda mpinzani wake Stephano Weston Luoga aliyepata kura 11 za wajumbe ikiwa katika kata hiyo ni wajumbe wawili pekee waliokuwa wakishindania nafasi hiyo.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...