Wananchi wameiomba Serikali Kupitia Mamlaka ya mapato Tanzania TRA kuhakikisha unatengeneza mfumo mmoja ambao utasaidia kwa kila mtanzania anayefanyabiashara kulipa kodi kwa kiwango cha uwezo wa biashara yake.
Hayo aliyasema katibu w Jumuiya ya wa wafanyabiashara Mkoa wa Tanga Ismail Masuod wakati akizungumza katika semina ya wafanyabiashara ya Elimu kwa mlipa kodi mkoa wa Tanga iliyofanyika katika ukumbi wa YDCP jijini Tanga
ambapo alisema kuwa elimu inasaidia wafanyabiashara kujua umuhimu wa kulipa kodi na sheria ya kodi.
Aidha alisema kuwa hiyo itasaidia mambo makubwa matatu kwanza ni kutengenza walipa kodi wapya,kwani kuwa na mpango maalum wa kutengeneza walipa kodi katika nchi kutakuwa walipo kodi wacheche.
Akizungumzia Daniel Ramadhani ambaye ni Kaimu meneja wa mkoa wa Tanga alisema lengo la Mafunzo hayo kwa wafanyabiashara ni kuwawezesha kujua sheria ya fedha kutokana mabadiliko ya sheria kwaajili ya maborehsoya kodi yanayotokea kila baada ya bunge la bajet ambapo Mamlaka ya mapato Tanzania TRA imepanga kuwafikia makundi yote ambayo inatakiwa kulipa kodi.
Aliongeza kusema kuwa sheria iliuofanyiwa marekebisho ni pamoja na sheria ya ongezeko la kodi ya samani ambayo kutakuwa zuio la kodi ya samani ni mauzo ya biadhaa kwa maana ya asilimia tatu ya mauzo ya bidhaa na mauzo ya ya huduma kwa mfano banki na mitandao mengine.
Kwa upande Chama Siliwa Afisa Masidizi wa elimu na mawasiliano wa Mamlaka ya mapato Tanzania TRA kutoka makao makuu alisema wametoa elimu kwa mlipa kodi kutokana mabadiliko ya sheria mpya ya ulipaji wa kodi hivyo tumeamua kuwapa elimu hiyo wazijue wanapoendelea kulipa kodi changamoto kuwa ya watu kutokulipa kodi ni pamoja na uelewa mdogo wa sheria.
