Tuesday, August 26, 2025

Wananchi waiomba Serikali kutengeneza mfumo mmoja ili wafanyabiashara walipe Kodi kulingana na uwezo wa biashara zao


Wananchi wameiomba Serikali  Kupitia Mamlaka ya mapato Tanzania TRA kuhakikisha unatengeneza mfumo mmoja ambao utasaidia kwa kila mtanzania anayefanyabiashara kulipa kodi kwa kiwango cha uwezo wa biashara yake.

Hayo aliyasema katibu w Jumuiya ya wa wafanyabiashara Mkoa wa Tanga  Ismail Masuod wakati akizungumza katika semina ya wafanyabiashara ya Elimu kwa mlipa kodi  mkoa wa Tanga  iliyofanyika katika ukumbi wa YDCP jijini Tanga

ambapo alisema kuwa elimu inasaidia wafanyabiashara kujua umuhimu wa kulipa kodi na sheria ya kodi.

Aidha alisema kuwa hiyo itasaidia mambo makubwa matatu kwanza ni kutengenza walipa kodi wapya,kwani kuwa na mpango maalum wa kutengeneza walipa kodi katika nchi kutakuwa walipo kodi wacheche.

Akizungumzia Daniel Ramadhani ambaye ni Kaimu meneja wa mkoa wa Tanga  alisema lengo la Mafunzo hayo kwa wafanyabiashara ni kuwawezesha kujua sheria ya fedha kutokana mabadiliko ya sheria kwaajili ya maborehsoya kodi yanayotokea kila baada ya bunge la bajet ambapo Mamlaka ya mapato Tanzania TRA imepanga kuwafikia makundi yote ambayo inatakiwa kulipa kodi.

Aliongeza kusema kuwa  sheria iliuofanyiwa marekebisho ni pamoja na sheria ya ongezeko la kodi ya samani ambayo kutakuwa  zuio la kodi ya samani ni mauzo ya biadhaa kwa maana ya asilimia tatu ya mauzo ya bidhaa na mauzo ya ya huduma kwa mfano banki na mitandao mengine.

Kwa upande Chama Siliwa Afisa Masidizi wa elimu na mawasiliano wa Mamlaka ya mapato Tanzania TRA  kutoka makao makuu alisema wametoa elimu kwa mlipa kodi kutokana mabadiliko ya sheria mpya ya ulipaji wa kodi hivyo tumeamua kuwapa elimu hiyo wazijue wanapoendelea kulipa kodi changamoto kuwa ya watu kutokulipa kodi ni pamoja na uelewa mdogo wa sheria.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...