Monday, July 14, 2025

‎Mwenge wa Uhuru Waweka Jiwe la Msingi Ujenzi wa Ghala la Kuhifadhi Mazao Kiteto. ‎


Na John Walter -Kiteto 

Mwenge wa Uhuru umeweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa ghala la kuhifadhi mazao katika Wilaya ya Kiteto, mkoani Manyara.

‎Taatifa ya mkuu wa wilaya ya Kiteto Remidius Mwema kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2025, Ismail Ussi, imesema lengo la mradi huo ni kutoa huduma za kiutawala kupitia mfumo wa stakabadhi za ghala, kuinua uchumi wa wananchi na kutoa hifadhi salama ya mazao.

‎Mradi huo unagharimu shilingi milioni 149,680,000 ambazo ni mapato ya ndani ya Halmashauri.

‎Hadi sasa mradi umefikia asilimia 70 ya utekelezaji na unatarajiwa kuwa na uwezo wa kuhifadhi mahitaji ya tani kati ya 437.6 hadi 600 za mazao.

‎Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru na timu yake wameridhishwa na mradi huo na hatimaye wameweka jiwe la msingi kama ishara ya kuunga mkono jitihada hizo za maendeleo.

‎Kiongozi huyo wa Mwenge ameupongeza uongozi wa Wilaya kwa kuchukua hatua hiyo muhimu ya kuwakumbuka wakulima, akieleza kuwa kupitia ghala hilo wakulima watanufaika kwa kuhifadhi mazao yao kwa usalama na kupata fursa ya kuuza kwa bei bora kupitia mfumo wa stakabadhi za ghala.

‎Kauli mbiu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2025 ni:

‎"Jitokeze kushiriki uchaguzi mkuu wa 2025 kwa amani na utulivu."

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...