Tuesday, July 15, 2025

Mo Dewji : Toka Mwaka 2018 Hadi Leo Nimetumia Bilioni 87 Kwa Ajili ya Simba



"Kuanzia mwaka 2018 hadi leo nimewekeza shilingi Bilioni 45 kwa ajili ya mishahara, usajili, maandalizi ya Timu na mahitaji mengine ya uendeshaji, pia nimechangia shilingi Bilioni 20 kama sehemu ya ununuzi wa hisa asilimia 49 ndani ya Simba Sports Club na mara nyingi nimekuwa nikitoa msaada nje ya mfumo rasmi, kila palipojitokeza uhitaji wa dharura kuanzia mwaka 2017 hadi 2024 nimetumia takribani Bilioni 22 katika misaada ya dharura hivyo kufanya jumla ya mchango wangu kwa Simba kufikia shilingi Bilioni 87 hivyo kusema Mo hatoe hela ni kauli ya kupotosha yenye mwelekeo wa chuki, tuachane na fitna zisizo na msingi, tujenge palipotoboka, tuzibe ufa panapovuja na tusonge mbele bila kuonyeshana vidole" 

——— 
Mohammed Dewji, Mwekezaji na Rais wa heshima wa Simba Sports Club.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...