
Source
Semina hiyo imefanyika leo Juni 25, 2025 katika Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) Shinyanga kilichopo manispaa ya Shinyanga.
Akizungumza wakati wa semina hiyo, Afisa wa kodi kutoka TRA Shinyanga Semeni Mbeshi, amesema lengo ni kuwajengea msingi mzuri wa kizalendo vijana wanaotarajia kuingia kwenye soko la ajira na kujiajiri baada ya kuhitimu masomo yao.
Ameongeza kuwa elimu hiyo ni endelevu na inalenga kujenga taifa la watu waaminifu katika ulipaji wa kodi, huku akisisitiza matumizi ya IFD kwa wafanyabiashara na kutoa na kudai risiti pindi wanaponunua bidhaa.
"Haki ya mlipa kodi ni kuaminiwa pindi anapofika kwenye ofisi za TRA kwa ajili ya kufanyiwa makadilio yanayoendana na biashara yake, ni wajibu wa kila mfanyabiashara kutoa taarifa ya ufanyaji wa biashara kwa mamlaka ya mapato TRA, utoaji wa risiti za IFD zinasaidia kuweka rekodi sahihi ya kumbukumbu ya biashara kwa muda wa miaka 5, lakini kodi hiyo inakwenda moja kwa moja kwenye mfuko wa serikali na kuwezesha maendeleo kwenye taifa letu", amesema Semeni Mbeshi.
Kwa upande wake, Mkufunzi katika Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) Shinyanga, Emili Shirima amesema vitendo vya baadhi ya watu kutumia vishoka kujipatia huduma za kikodi si sahihi na ni hatari kwa uchumi wa taifa, alisema na kuwataka wanachuo kujiepusha na tabia hizo mara watakapoingia kwenye shughuli za uzalishaji mali.
Baadhi ya wanachuo walioshiriki mafunzo hayo wameishukuru TRA kwa kuwapa elimu hiyo muhimu, wakisema itawasaidia mara baada ya kuhitimu na kuanzisha biashara au shughuli za kujitegemea na kuo ngeza kuwa sasa anaelewa kwamba ulipaji wa kodi unasaidia huduma za jamii kama afya, elimu na miundombinu.
Afisa wa kodi kutoka TRA Shinyanga Semeni Mbeshi akizungumza wakati wa mafunzo hayo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, chama hicho kinaendelea na maandalizi ya mchakato wa ndani wa uteuzi wa wanachama watakaowania nafasi mbalimbali katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 kupitia CCM.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa mchakato huo utafanyika kwa hatua, ikiwemo uchukuaji na urejeshaji wa fomu, vikao vya awali na hatimaye kura za maoni. Hivyo, chama kimeagiza kusitishwa kwa shughuli zozote zinazohusiana na vikao vya uteuzi kabla ya hatua ya kura za maoni.
"Ni kwa kuzingatia hilo, CCM inasisitiza marufuku ya ZIARA, MIKUTANO, SEMINA na MAKONGAMANO yanayohusisha wajumbe wa vikao vinavyopiga kura za maoni kuhusiana na wagombea wa ngazi zote hadi kura za maoni zitakapopigwa," imesisitizwa kwenye taarifa hiyo.
Aidha, CCM imeonya wanachama wote wanaotarajia kugombea au wawakilishi wao dhidi ya kufanya vitendo vyovyote vinavyoweza kuashiria ukiukwaji wa Katiba, kanuni au miongozo ya chama hicho.
Chama hicho pia kimewataka viongozi, watendaji na wanachama wake kusimamia nidhamu, maadili na mshikamano katika kipindi hiki muhimu cha maandalizi ya uchaguzi. Viongozi wote wametakiwa kuhakikisha kuwa michakato yote inaendeshwa kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa.
Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, amehitimisha taarifa hiyo kwa kuwataka wanachama wote kutimiza wajibu wao katika kuimarisha umoja ndani ya chama na kudumisha imani ya wananchi waliyopewa na CCM.
Kidumu Chama Cha Mapinduzi!