Friday, September 13, 2024

Msanii Profesa Jay Ajitokeza Kwa Mara ya Kwanza Baada ya Kuzushiwa Kifo...Asema Haya

Msanii Profesa Jay Ajitokeza Kwa Mara ya Kwanza Baada ya Kuzushiwa Kifo...Asema Haya


Mbunge wa zamani wa Mikumi na msanii mkongwe wa muziki wa hip hop nchini Tanzania, Profesor Jay, amejitokeza kwa mara ya kwanza kupitia akaunti yake ya Instagram baada ya kuzushiwa taarifa za kifo. Kwenye posti hiyo, Professor Jay alimshukuru Mungu kwa zawadi ya uzima na kusema kuwa yupo tayari kwa mapambano ya maisha, akithibitisha kuwa hali yake ni nzuri.

Kwenye ujumbe wake, aliandika: "Asante sana Mungu kwa zawadi ya uzima, na kunilinda siku zote za maisha yangu, nipo kamiligado tayari kwa mapambano." Alimalizia posti hiyo kwa alama za ushindi na hashtag ya #KataaUtekaji, akijiunga na Watanzania wengine kulaani matukio ya utekaji na mauaji yanayoendelea kutokea nchini.


Mashabiki wake wengi wamejitokeza kumpongeza na kumpa maneno ya faraja, wakifurahia kuona kuwa msanii wao bado yupo salama na mwenye nguvu za kuendelea na mapambano.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...