Saturday, July 31, 2021

Meneja TTCL Atumbuliwa Kwa Kukwepa Ziara za Viongozi na Kupika Taarifa

 


Meneja wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) wa Mkoa wa Kagera, Irene Shayo ametenguliwa kuanzia Julai 30, 2021 kwa tuhuma za utumishi wake kusuasua na kukwepa ziara za viongozi katika eneo lake


Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Kundo Mathew amesema pia Meneja huyo amekuwa akipika Taarifa za Mapato na Matumizi


Naibu Waziri amesema Meneja huyo apangiwe majukumu mengine kulingana na wasifu wake kitaaluma ili aweze kufanya kazi vizuri kwasababu majukumu ya sasa hana uwezo nayo


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...