Friday, April 23, 2021
Baraza La Mawaziri La Kisekta La Afya La Ahidi Kuendelea Kushirikiana Katika Kukabiliana Na Changamoto Za Afya
Mkutano wa Kawaida wa 20 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Afya ngazi ya Mawaziri uliofanyika leo katika Makao Makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha, Tanzania; umekubaliana na kuahidi kuendelea kushirikiana katika kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya afya katika Jumuiya.
Mkutano huu uliotimishwa leo tarehe 23 Aprili 2021, umefanyika kwa siku tano kuanzia tarehe 19 hadi 23 Aprili 2021, ulikuwa na lengo la kufanya mapitio ya hatua ya maendeleo iliyofikiwa katika utekelezaji wa maamuzi na maagizo yaliyotolewa na Mkutano uliopita wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na la Kisekta, sambamba na kuibua maeneo mapya yanayohitajika kupewa kipaumbele kulingana na mapendekezo yaliyotolewa na Kamati za Wataalamu.
Mkutano huu uliokuwa ukiongozwa na Mhe. Mutahi Kagwe Waziri wa Afya wa Kenya ambale pia ni Mwenyekiti wa Baraza hilo, pamoja na masuala mengine umepitia kujadili na kutoa maelekezo katika kutatua changamoto mbalimbali, zinazokwamisha utekelezaji wa mikakati ya pamoja ya kukabiliana na Ugonjwa wa Homa kali ya Mapafu unaosababishwa na Virusi vya Korona (UVIKO-19), na usalama wa dawa na chakula katika Jumuiya.
Kila Nchi mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa nyakati tofauti katika mkutano huo imeeleza utayari wake wa kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wa mikakati na mipango mbalimbali waliyokubaliana kuitumia katika kutatua changamoto za sekta ya afya.
Mkutano huu umehudhuriwa na Mawaziri kutoka Nchi zote Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wanaosimamia masuala ya Afya. Tanzania imewakilishwa na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Mhe. Dkt. Dorothy O. Gwajima (Mb)
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
