Monday, March 29, 2021

Mjue Frank Lentini, Aliyezaliwa Akiwa na Miguu Mitatu

 


Frank Lentini alizaliwa Mei 1889 Nchini #Italia na alifariki Septemba 1966 akiwa Marekani. Aliishi maisha yake kama Mwanamaonesho akitumia umbo lake kama sehemu ya kazi hiyo


Frank ni moja kati ya Watoto waliotakiwa kuzaliwa pacha lakini pacha wake aliunganika naye kwa kile ambacho kisayansi kinaitwa 'Parasitic twin' ambapo alijikuta ameungana uti wa mgongo na pacha wake


Hali hiyo ilimfanya awe na miguu mitatu na sehemu mbili za siri, hali iliyoonesha kuwa pacha wake alikuwa Mwanaume. Alipozaliwa Wazazi wake walimuona ni laana na walimgawa kwa wengine waweze kumlea


Mbali na hali hiyo ambayo haikuwa kawaida, aliweza kuoa na kupata Watoto wanne

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...