Saturday, February 13, 2021
Bunge laahirishwa hadi Machi 30 mwaka huu
Mkutano wa pili wa Bunge la 12 ulioanza Februari 2, 2021 jijini Dodoma umeahirishwa leo Februari 13, 2021 na waziri Mkuu Kassima Majaliwa hadi Machi 30 mwaka huu.
Awali ilitarajiwa kuwa vikao hivyo vingemalizika jana, lakini ilishindikana baada ya shughuli za bunge kuahirishwa kufuatia kifo cha Mbunge wa Muhambwe, Atashasta Nditiye, aliyefariki kwa ajali ya gari.
Katika mkutano huo, shughuli mbalimbali zimefanyika ambapo ulianza kwa kuwatambulisha wabunge watano walioteuliwa na Rais ambao hawakuwepo kwenye mkutano wa kwanza. Wabunge wanne kutoka ACT Wazalendo na wabunge 19 wa Viti Maalum wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Aidha, wastani wa maswali 125 ya kawaida na maswali 16 ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa yameulizwa.
Wabunge pia walipata fursa ya kujadili Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Ufunguzi Rasmi wa Bunge la 12.
Katika hatua nyingine, bunge lilikaa kama Kamati ya Mipango ili kujadili na kushauri kuhusu 'Mapendekezo ya Mpango wa Taifa' unaokusudiwa kutekelezwa katika mwaka wa fedha 2021/2022.
Katika hotuba yake ya kuahirisha bunge, Waziri Mkuuu ameeleza mambo mbalimbali ambayo serikali imefanya na inaendelea kufanya ikiwemo utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo. Pia, ametumia nafasi hiyo kuzipongeza timu za taifa na vilabu vya Tanzania kwa mafanikio zilizopata kwenye mashindano mbalimbali ya kimataifa.
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
