Saturday, February 13, 2021
Bunge laahirishwa hadi Machi 30 mwaka huu
Mkutano wa pili wa Bunge la 12 ulioanza Februari 2, 2021 jijini Dodoma umeahirishwa leo Februari 13, 2021 na waziri Mkuu Kassima Majaliwa hadi Machi 30 mwaka huu.
Awali ilitarajiwa kuwa vikao hivyo vingemalizika jana, lakini ilishindikana baada ya shughuli za bunge kuahirishwa kufuatia kifo cha Mbunge wa Muhambwe, Atashasta Nditiye, aliyefariki kwa ajali ya gari.
Katika mkutano huo, shughuli mbalimbali zimefanyika ambapo ulianza kwa kuwatambulisha wabunge watano walioteuliwa na Rais ambao hawakuwepo kwenye mkutano wa kwanza. Wabunge wanne kutoka ACT Wazalendo na wabunge 19 wa Viti Maalum wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Aidha, wastani wa maswali 125 ya kawaida na maswali 16 ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa yameulizwa.
Wabunge pia walipata fursa ya kujadili Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Ufunguzi Rasmi wa Bunge la 12.
Katika hatua nyingine, bunge lilikaa kama Kamati ya Mipango ili kujadili na kushauri kuhusu 'Mapendekezo ya Mpango wa Taifa' unaokusudiwa kutekelezwa katika mwaka wa fedha 2021/2022.
Katika hotuba yake ya kuahirisha bunge, Waziri Mkuuu ameeleza mambo mbalimbali ambayo serikali imefanya na inaendelea kufanya ikiwemo utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo. Pia, ametumia nafasi hiyo kuzipongeza timu za taifa na vilabu vya Tanzania kwa mafanikio zilizopata kwenye mashindano mbalimbali ya kimataifa.
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Bongo Deco wauzai wa vifaa mbalimbali vya umeme kama TV, Subwoofer, Hometheator, Majiko madogo na makubwa ya Gesi, Friji, Generator nk leo w...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia)akimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii wa Jamhuri ya ...
-
Balozi mpya wa Kenya nchini Tanzania, Dan Kazungu akitoa hotuba yake kwa wageni mbalimbali waliohudhulia dhifa iliyoandaliwa maalum kwa kumk...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Wanajeshi wawili wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa wamejeruhiwa baada ya kifaru cha Israel kufyatua risasi kuelekea mnara wa Umoja wa M...
-
Katika kila makabiliano ya kijeshi kati ya Israel na Lebanon, bila kujali ni upande gani unaopigana huko Lebanon, Mto Litani, moja ya mito...
-
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema kuanzia kesho Jumatano Juni 23, 2021 itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kuingia eneo la hospita...