Tuesday, April 14, 2020

Korea kaskazini yafyatua makombora kadhaa

Korea kaskazini imefyatua makombora kadhaa ya masafa mafupi katika bahari ya mashariki leo, shirika la habari la Korea kusini Yonhap limeripoti, likinukuu jopo la wakuu wa majeshi ya nchi hiyo.

Makombora hayo, ambayo yanaaminika kuwa ni kutoka ardhini kwenda katika meli, yaliruka kwa karibu kilometa 150. Yalifyatuliwa kutoka mji wa pwani wa mashariki wa Munchon katika mwelekeo wa kaskazini magharibi.

Ufyatuaji huo unakuja katika mkesha wa uchaguzi wa bunge la Korea kusini. Mwezi Machi, Korea kaskazini ilifanya majaribio ya ufyatuaji wa makombora kadhaa katika muda wa mwezi mmoja baada ya kutofanya hivyo kwa muda wa miezi mitatu.

Nchi hiyo yenye silaha za nyuklia imepigwa marufuku kufanya majaribio ya makombora na Umoja wa mataifa, na imewekewa vikwazo vikali na jumuiya ya kimataifa kukabiliana nayo dhidi ya kuendelea kuunda makombora hayo.
Source
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...