Monday, September 3, 2018
Serikali yapanga kuigomea Kenya kutumia Mto Mara
Serikali ya Tanzania imesema itapinga mipango ya serikali ya Kenya kujenga mabwawa ya kuzalisha umeme na kilimo cha umwagiliaji kwenye Mto Mara.
Kwa mujibu wa waziri wa mazingira wa Tanzania, January Makamba iwapo mipango hiyo ya Kenya itatekelezwa, itapunguza mtiririko wa maji na kutishia ustawi wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Mto Mara unaanzia nchini Kenya kwenye milima ya Mau na kutiririka mpaka Tanzania ambako unatengeneza sehemu ya mpaka wa nchi hizo mbili. Mto Mara pia unatenganisha Hifadhi za Taifa za Masai Mara ya Kenya na Serengeti ya Tanzania.
Ni katika Mto Mara pia ambapo Nyumbu huvuka kwa wingi kutoka upande wa Tanzania kwenda Kenya na kuvutia maelfu ya watalii kwenye mbuga za Serengeti na Masai Mara kushuhudia tukio hilo ambalo linatajwa kama moja ya kivutio cha asili cha dunia.
"…Mto Mara, unaoanzia Kenya, ni mhimili wa Hifadhi ya Serengeti. Kulikuwa na taarifa za mipango ya Kenya kujenga mabwawa. Tulituma timu ya wataalam kufuatilia. Tuna Protocol ya Mto Mara, pia Lake Victoria Basin. Nitaenda Kenya na wenzangu kuongea na ndugu zetu," ameandika Makamba kwenye mtandao wake wa Twitter.
Ujumbe huo wa Twitter pia umeambatana na video ambayo inamwonesha Makamba akizuru kando ya Mto Mara ambapo amesema, "... Hii rasilimali (Mto Mara) ni ya kwetu sote, na sisi kama nchi hatuwezi kuruhusu jambo ambalo linaweza kuhujumu uchumi. Serengeti ni moja ya mali kubwa sana ya nchi yetu, na uti wa mgongo ni huu mto na ukiuvuruga huu mto kama nchi hatuwezi kukubali."
"Hairuhusiwi wewe mto unatoka nchi moja kwenda nyengine basi wewe (wa nchi ya) kule juu kufanya chochote maji yasifike huku chini. Kuna mikataba ya kimataifa tuliyosaini na tutasimama katika hiyo," amesema Makamba.
Sakata la Mto Mara linakuja siku chache baada ya vyombo vya habari nchini Kenya kuripoti kuwa mamlaka za hifadhi ya Serengeti nchini Tanzania zimefanya hujuma kwa kuchoma moto eneo la hifadhi ili kuzuia nyumbu kuvuka kuelekea nchini Kenya. Serikali ya Tanzania ilikanusha tuhuma hizo.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...


