Monday, September 3, 2018

Diamond Ataja Kilichomsibu Mpaka Kusuka Rasta

Staa wa muziki wa Bongo fleva Naseeb Abdul maarufu kama Diamond Platnumz amefunguka kuhusu staili yake ya kichwani inayoendelea kutengeneza headlines. Siku ya leo Diamond amezua gumzo baada ya kuanika staili yake baada ya kutupia picha iliyomuonyesha akiwa amesuka Rasta katika staili ya kipekee. Mara moja Diamond alianza kutrend huku watu wengi wakimponda na kudai amesuka Rasta kama mwanamke huku mashabiki wengine wakimpongeza kwa ubunifu. Kwenye mahojiano na Bongo 5, Diamond aliulizwa maswali ya Nini hasa kilichomsukuma mpaka kufikia uamuzi wa kusuka nywele kwa staili na akafunguka kuwa ameamua kubadilisha staili ya nywele zake: Nimeamua kubadilisha muonekano lakini baadae nitabadilisha Tena". Hii sio mara ya kwanza kwa Diamond kutengeneza nywele na kuzua gumzo mara kwa mara amekuwa akija staili mpya ambayo inazua gumzo na kutrend sana.

The post Diamond Ataja Kilichomsibu Mpaka Kusuka Rasta appeared first on Ghafla!Tanzania.


Source
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...