Monday, September 3, 2018

Dalili za awali za mtu mwenye ujauzito


Zipo dalili mbalimbali ambazo huwapata wanawake wakati wa ujauzito, Kila mwanamke hupata dalili tofauti na si wanawake wote  wataona dalili hizi ambazo nitazitabainisha hapa.

Dalili za awali za mtu mwenye mimba ni;

1. Kuhisi kuumwa
Baadhi ya wanawake hujihisi kuwa wanaumwa. Wengi huhisi kichefuchefu na kutapika hasa nyakati za asubuhi.

2. Kuhisi uchovu
wanawake wengi hujihisi uchovu na mwili kulegea. Hii hufanya wanawake wapende kulala. Mabadiliko ya homoni yanayotokea wakati huu ndio kiini ya matatizo haya.

3. Kuumwa maziwa-baadhi ya wanawake hujaa na kuumwa maziwa.

4. Kujisikia kichefuchefu.
Mara nyingi mwanamke anapokuwa amepata ujauzito hujisikia kichefufu, hii ni kutokana na mabadiliko na ukuaji wa kijusi.

5. Kupenda na kutopenda baadhi ya vyakula.

6. Kuwa na hasira zisikuwa na chanzo cha kuelewaka.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...