Monday, August 27, 2018

Mh.Makonda Awatoa Wananchi Hofu Kuhusu Hali ya Ommy Dimpoz

Mkuu wa mkoa wa Dar Es salam Paul Makonda amefunguka na kuwatoa hofu wananchi na mashabiki wa Ommy Dimpoz kwa muda mrefu baada ya kusambaa kwa taarifa kuwa msanii huyo yuko mahutiuti hospitali nje ya nchi akiwa katika chumba cha watu wasiojiweza. Katika ukurasa wake wa instagram Paul Makonda amsema kuwa ameongea na msanii huyo na kwamba amemwambia anaendelea vizuri na hivi karibuni atarudi kuendelea nae na mazoezi. Jana saa 8 usiku nilipata nafasi ya kuongea narafiki yangu Ommy Dimpoz,nilifurahi sana na kupiga stori na ndugu yangu  hsa baadaya kujua kuwa anendelea vizuri na soon tutarudi GYM. Kumekuwa na post nyingi sana za wasanii na watu wa karibu walioguswa na habari za Ommy Dimpoz kusambaa kuwa yuko katika chumba  cha ICU kwa muda sasa kutokna na hali yake kubadilika. Hata hivyo meneja wake alikanusha na kusema kuwa msanii huyo alikwenda hospitalini hapo kwa ajili ya kufanya chck-up inayotakiwa kufanya kila baada ya muda, hii inaweza kutokana na picha ya hospiali aliyokuwa ameweka ommy katika mtandao wa snapchat.  

The post Mh.Makonda Awatoa Wananchi Hofu Kuhusu Hali ya Ommy Dimpoz appeared first on Ghafla!Tanzania.


Source
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...