Monday, August 27, 2018

Thamani ya Taji la Miss Tanzania ni Milioni 6


Kamati ya Miss Tanzania imeweka wazi taji atakalovaa Miss Tanzania mwaka huu linathamani ya Sh6 milioni.


Mkurugenzi wa kampuni ya Look inayoendesha mashindano hayo Basila Mwanukuzi ameonyesha taji hilo litakalovaliwa na mshindi atakayepatikana Septemba 8.


Amesema sanjari na taji hilo mrembo atakayeibuka kidedea katika shindano hilo atapewa zawadi ya gari.


Mwanukuzi ameeleza kuwa kamati yake imeendelea kusimamia na kuhakikisha mrembo anapata zawadi bora na yenye viwango.


Amesema kulingana na maandalizi ya kamati hiyo mshindi atapewa gari zuri ambalo hata hivyo hakuweka wazi ni aina gani.


Kando na hilo alielezea utaratibu wa kupata tiketi ambazo mwaka huu zitauzwa kwa mfumo wa kielektroniki.


Meneja Masoko wa kampuni ya Otapp inayohusikan na uuzaji wa tiketi hizo Joachim Ferdinand amesema tayari tiketi timeshaanza kuuzwa.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...