Saturday, March 22, 2025

Manara: Huu ni Mwaka wa Uchaguzi Msigombanishe Serikali na Wananchi Kwa Maswala ya Simba na Yanga




Serikali yaijia juu bodi ya ligi baada ya bodi ya ligi kutaka msaada kutoa serikalini na hii ni baada ya klabu ya yanga kudai alama tatu dhidi ya mpinzani wake simba lakini bodi ya ligi wameitupilia mbali hoja hiyo na hivyo imewataka wakae kikao na klabu ya yanga lakini klabu ya yanga awajataka kukaa kikao chochote kile na bodi ya ligi.

Aliyekua Msemaji wa Yanga amesema kuna uzushi unaendelea kuwa Serikali itaingia suala la Derby ya Kariakoo ambapo amesisitiza hata wao wameshabaini wenye mamlaka ya mpira wamekosea hivyo nao wamekaa pembeni hawataki kuchonganishwa na wananchi ikizingatiwa huu ni mwaka wa uchaguzi.

Kwamba Serikali haitaki kubeba mzigo wa mtu ,acha wahangaike nao wenyewe kwani serikali inajiandaa na msimu wa kampeni hivyo serikali haitaki kuingilia maswala kama hayo kwani ni jambo zito sana serikali kuingilia kati maswala ya kimchezo kwani sheria ya mpira aitaki serikali ijiusishe na maswala ya mpira kwani mpira utaongozwa na sheria na taratibu zake

Mpira wa Tanznia umekuwa na mpira wenye maendeleo makubwa sana hivyo basi chochote kinachofanyika ni kutia doa katika mpira huu kwani endapo serikali itaingilia kati maswala ya mpira litakuwa ni kosa kubwa na uenda ikasabisha ata Shirikisho la mpira duniani kuingilia kati

Bodi ya ligi wanatakiwa wajitathmini kwa hiki wanachokifanya kwani siyo kujenga mpira bali ni kubomoa na chanzo ya hayo yote ni baada y raisi wa mpira wa miguu Tanzania wallace karia kuongea maneno ambayo yalileta mijadala mingi sana mtandaoni kwani aikuwa sahihi kwa mtu kama yeye kuzungumza maneno kama yale siyo jambo zuri na alikustahili kuzungumzwa.


KLABU YA COASTAL UNION YAPOKEA BASI JIPYA KUTOKA BENKI YA NBC

Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu wa Ligi Kuu ya NBC imekabidhi basi jipya kwa Klabu ya soka ya Coastal Union FC ya jijini Tanga inayoshiriki ligi hiyo ikiwa ni mwendelezo wa dhamira ya dhati ya benki hiyo katika kuboresha ligi hiyo.

Coastal Union FC inakuwa klabu ya nne inayoshiriki ligi hiyo kunufaika na mpango huo unaohusisha mkopo nafuu kutoka benki ya NBC baada ya klabu za KMC ya Kinondoni, Singida Big Stars na Namungo FC kunufaika na mpango kama huo hapo awali. Mkopo wa basi la Coastal Union FC unaifanya benki ya NBC kuwa imetoa jumla ya mikopo yenye thamani ya sh bil 1.2 kwenye usafiri wa vilabu hivyo vinne vilivyonufaika na mpango huo.

Hafla ya makabidhiano ya basi hilo iliyohusisha paredi maalum la basi hilo katika maeneo mbalimbali ya jiji la Tanga, imefanyika leo kwenye tawi la benki ya NBC jijini Tanga ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Lushoto Bw. Zephania Stephan Sumaye aliemuwakilisha Mkuu wa Mkoa huo Balozi Dkt Batilda Burian.

Pia hafla hiyo ilihusisha uwepo wa Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga, Al-Hajj Abdulrahman Shiloow, viongozi waaandamizi wa benki ya NBC wakiongozwa na Mkurugenzi wa Biashara wa Benki ya NBC, Elvis Ndunguru, Mwenyekiti wa Klabu ya Coastal Union FC, Bw Muhsin Ramadhan Hassan, mdhamini wa klabu hiyo kampuni ya RATCO Express, benchi la ufundi pamoja na wachezaji.

Akizungumza kwa niaba ya Balozi Dkt Burian, DC Sumaye pamoja na kuipongeza benki hiyo kwa hatua hiyo muhimu, alisema hatua hiyo imekuja kipindi ambacho uongozi wa mkoa huo upo kwenye utekelezaji wa wito wa Rais Samia wa kuchochea kasi ya maendeleo mkoani humo ikiwemo sekta ya michezo kupitia uboreshaji wa miundombinu ya michezo.

"Kilichofanywa na NBC leo ni kama kuunga mkono muitikio wa wito huu wa Rais Samia. Nimevutiwa zaidi kuona NBC wanagusa hadi masuala ya bima kwa wanamichezo hilo ni jambo zuri zaidi. Ombi Langu kwa wachezaji na viongozi wa klabu ni kuhakikisha kwamba jitihada hizi zinatoa majibu kwenye matokeo ya uwanjani,'' alisema.

Awali akizungumza kwenye hafla hiyo iliyoambatana na msafara maalum kutoka kwenye tawi la NBC hadi Makao makuu ya klabu hiyo, Ndunguru alisema basi hilo ni sehemu ya mpango wa utoaji wa mikopo yenye masharti nafuu kwa vilabu vinavyoshiriki ligi hiyo.

"Ukosefu wa vyombo vya usafiri maalum kwa ajili ya timu zinazoshiriki ligi Kuu ya NBC imekua ni moja ya chanzo cha vikwazo vingi katika gharama za uendeshaji na utendaji wa timu husika.Jitihada zetu kama wadhamini haziishii hapa tu kwenye mikopo ya usafiri bali tunagusa maboresho ya baadhi ya viwanja vinavyotumia kwenye ligi hii, tunatoa bima za afya kwa wachezaji na mabenchi ya ufundi na zaidi tunatoa huduma za kifedha ikiwemo elimu ya kifedha kwa wadau wa michezo wakiwemo wachezaji,'' alisema.

Wakizungumza kwenye hafla hiyo Mwenyekiti wa Klabu ya Coastal Union FC Bw Muhsin Ramadhan Hassan na Mstahiki Meya Al-Hajj Shiloow pamoja kuishukuru benki hiyo kwa jitihada zake za kuiboresha ligi hiyo walikiri kuwa klabu hiyo ilikuwa ikikabiliwa na changamoto ya usafiri bora hapo awali hali ambayo iliongeza changamoto katika ubora wat imu hiyo.

"Tanga sasa tumeweka alama kupitia benki ya NBC. Kupitia usafiri huu sasa tuna uhakika wa kusafirisha wachezaji wetu kwenda popote, wakati wowote tena wakiwa na utulivu zaidi.Ni wazi sasa tunakwenda kuongeza ushindani zaidi kwenye ligi kupitia hatua hii ya leo,'' alisema Mwenyekiti Muhsin.
Mkuu wa Wilaya ya Lushoto Bw. Zephania Stephan Sumaye (wa pili kulia) akikabidhi mfano wa ufunguo kwa Mwenyekiti wa Klabu ya Coastal Union FC ya jijini Tanga Bw Muhsin Ramadhan Hassan (wa pili kushoto) ikiwa ni ishara ya kumkabidhi basi lilotolewa na Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambaye ni Mdhamini Mkuu wa Ligi Kuu ya NBC.
Mkurugenzi wa Biashara wa Benki ya NBC, Elvis Ndunguru (katikati) akizungumza na viongozi, wanachama na mashabiki wa Klabu ya Coastal Union FC ya jijini Tanga alipotembelea makao makuu ya klabu hiyo jijini humo wakati wa hafla ya makabidhiano ya basi lililotolewa na benki ya NBC kwa klabu hiyo kama mkopo.
Baadhi ya wakazi wa jiji la Tanga wakifuatilia hafla fupi ya makabidhiano ya basi lililotolewa na benki ya NBC kama mkopo kwenda Klabu ya Coastal Union FC ya jijini Tanga. Hafla hiyo imefanyika leo kwenye tawi la NBC jijini Tanga.
Mkuu wa Wilaya ya Lushoto Bw. Zephania Stephan Sumaye akizungumza na wageni waalikwa kwenye hafla hiyo.
Mkuu wa Mahusiano ya Idara ya Mahusiano ya Umma na Mawasiliano wa NBC, Godwin Semunyu akizungumza na wageni waalikwa kwenye hafla hiyo.
Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga, Al-Hajj Abdulrahman Shiloow akizungumza na wageni waalikwa kwenye hafla hiyo.
Mwenyekiti wa Klabu ya Coastal Union FC Bw Muhsin Ramadhan Hassan akizungumza na wageni waalikwa kwenye hafla hiyo.
Meneja wa NBC Tawi la Tanga Bw Japhary Hassan akizungumza na wageni waalikwa kwenye hafla hiyo.
Baadhi ya wachezaji wa Klabu ya Coastal Union FC wakiwa kwenye hafla hiyo.

Maajabu! MTI ULIOANGUSHWA NA UPEPO, UKAKATWA ,WASIMAMA TENA GEITA

 

Zaidi ya wakazi 1,000 wa Mtaa wa Mpomvu, Kata ya Mtakuja, katika Manispaa ya Geita wamekusanyika kushuhudia tukio la kushangaza baada ya mti ulioangushwa na upepo mkali uliombatana na mvua kubwa, ukakatwa, kusimama tena asubuhi iliyofuata.

 Tukio hilo limezua gumzo kubwa na hisia tofauti miongoni mwa wakazi wa eneo hilo.

Mti huo, unaomilikiwa na Kanisa la Golan Gospel Center lililopo mtaani hapo, umeibua mijadala kuhusu uwezekano wa tukio hilo kuwa la miujiza.

 Baadhi ya viongozi wa kanisa na wananchi wameeleza kushangazwa na hali hiyo.

Katibu wa Kanisa la GGC, Yohana Mathias, amesema tukio hilo limewashangaza waumini wa kanisa na wakazi wa Mpomvu, huku wengine wakilihusisha na nguvu za kiimani.

Mkazi wa Mpomvu, Emmanuel Lameck, amesema hajawahi kushuhudia jambo kama hilo maishani mwake na kwamba bado linafikirisha.

Naye Stella Saimon, mkazi wa Mpomvu, amekiri kuwa tukio hilo limeleta mshtuko kwa wengi, huku wengine wakitafsiri kuwa ni tukio la kiimani au la kishirikina.

Mchungaji wa Kanisa la Golan Gospel Center, Jefta Lameck, amesema mti huo ulikuwa wa muda mrefu, na baada ya kuangushwa na upepo, waliamua kuukata kwa kuwa ulikuwa umezuia njia. Hata hivyo, walipofika asubuhi iliyofuata, walikuta mti huo umesimama tena hali iliyozua mshangao mkubwa.

Amesema tukio hilo lisihusishwe na imani za kishirikina na amewataka wananchi kuwa watulivu huku wakilitafakari kwa mtazamo wa kawaida wa kimaumbile badala ya kuingiza hofu au imani potofu.


Chanzo - Maduka Online Blog

Wamarekani Hawautaki Ushirikiano wa TRUMP na Elon Mask, Washambulia Magari ya Tesla

 

Wamarekani Hawautaki Ushirikiano wa TRUMP na Elon Mask, Washambulia Magari ya Tesla

Mashambulizi dhidi ya vituo vya Tesla yameongezeka baada ya #ElonMusk kushirikiana na utawala wa #Trump kwenye Idara ya Ufanisi wa Serikali (#DOGE), ambayo imepunguza matumizi makubwa ya serikali.


Miji kama Portland na Seattle imeathirika zaidi, huku magari ya Tesla, vituo vya kuchaji, na stoo za magari vikilengwa. Kwenye shambulio moja #LasVegas, magari kadhaa yaliwashwa moto na neno "#resist" likaandikwa kwenye jengo.


Mwanasheria Mkuu wa Marekani, Pam Bondi, alisema watu watatu waliokamatwa kwa mashambulizi hayo wanakabiliwa na kifungo cha hadi miaka 20 kwa ugaidi wa ndani.


Trump alitumia #TruthSocial kutangaza kuwa wahusika wanapaswa kufungwa kwa miaka 20 na kupendekeza wafungwe katika magereza ya #ElSalvador, akiyataja mashambulizi hayo kama ugaidi wa ndani. Alisisitiza kuwa Tesla ni "kampuni kubwa ya Marekani" na hata kununua gari lake la #Tesla kuonyesha uungaji mkono.

Friday, March 21, 2025

DR. MPANGO AWAFARIJI WAFIWA MSIBA WA HAWASSI



Na Mwandishi wetu,Dodoma

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango na Mwenza wake Mama Mbonimpaye Mpango wameshiriki msiba wa Bi. Damaris Hawassi ambaye ni Mke wa Katibu wa NEC (Uchumi na Fedha) wa Chama Cha Mapinduzi Dkt. Frank Hawassi katika makazi ya familia hiyo mtaa wa Miyuji Jijini Dodoma.

Akiwafariji waombolezaji katika msiba huo, Makamu wa Rais ametoa salamu za rambirambi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye ametoa salamu za pole kwa familia na waombolezaji wote kufuatia msiba huo.

Makamu wa Rais amewaombea faraja wanafamilia pamoja na wote walioguswa na msiba huo. Amewashukuru wananchi waliojitokeza kuifariji familia katika kipindi hiki kigumu kwao.

Makamu wa Rais amesema ni vema Watanzania kuendelea kushirikiana katika changamoto mbalimbali zinapotokea katika jamii ikiwemo magonjwa na vifo kwa kudumisha undugu, amani na kupendana ili kuwa na Taifa zuri na lenye ustawi.

Halikadhalika Makamu wa Rais amesema Bi.Damaris Hawassi alikua mchapakazi hodari aliyetimiza vema wajibu wake katika umri aliyojaaliwa duniani. Ameongeza kwamba ni vema kujifunza juu ya kila mmoja kutimiza wajibu wake pamoja na kuishi vema na wanadamu wengine.





Ripoti Ya Ufuatiliaji wa Uwajibikaji wa Jamii Katika Malezi na Makuzi ya Awali ya Mtoto Yaonesha Changamoto Kadhaa Babati

Na John Walter -Babati 

Marafiki wa Elimu wilaya ya Babati wamewasilisha ripoti ya ufuatiliaji wa uwajibikaji wa jamii katika malezi na makuzi ya awali ya mtoto.

Ripoti hiyo, iliyowasilishwa na Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Mji wa Babati, Benjamin Richard, inaonesha changamoto mbalimbali zinazowakabili watoto katika malezi, usalama, na mazingira ya kujifunzia.

Utafiti huu ulifanyika katika kata nne za Babati ,Bagara, Maisaka na Nangara kwenye shule za Msingi 16, ambapo wadau mbalimbali walihojiwa, wakiwemo watendaji wa kata, wamiliki wa vituo vya kulelea watoto (day care), walimu, wawakilishi wa asasi za kiraia, viongozi wa serikali za mitaa na vijiji, pamoja na wazazi wenye watoto katika shule za awali.

Matokeo Muhimu ya Ripoti

  1. Usalama wa Watoto Shuleni

    • Kati ya shule 16 zilizotembelewa, hakuna hata moja yenye uzio, hali inayohatarisha usalama wa watoto.
    • Shule nyingi zipo karibu na barabara, hivyo kuongeza hatari kwa watoto.
  2. Adhabu kwa Watoto

    • Asilimia 11.2 ya waliohojiwa walithibitisha kuwepo kwa adhabu za kuumiza katika baadhi ya shule.
    • Hata hivyo, asilimia 60 ya wazazi na walimu walikiri kuwa shule ni salama na wanatambua umuhimu wa ulinzi na usalama wa watoto.
  3. Afya na Mazingira ya Shule

    • Asilimia 68 ya vyoo vya shule si salama kwa watoto, hali inayohatarisha afya zao.
    • Ni shule tano pekee ndizo zenye vyoo maalum kwa wanafunzi wa awali.
  4. Malezi na Muda wa Wazazi na Watoto

    • Asilimia 93.7 ya watu 168 waliohojiwa walikiri kuwa wazazi wengi hawana muda wa kukaa au kucheza na watoto wao.
    • Wazazi wengi wamekuwa wakiacha majukumu yao kwa wafanyakazi wa ndani, ambao mara nyingi huonekana kama mama na baba wa watoto hao.

Hatua Zinazochukuliwa

Baada ya uwasilishaji wa ripoti hii, Mwenyekiti wa Kikosi Kazi cha Marafiki wa Elimu Babati, Gaudencia Igoshalimo, amesema kuwa watarejea kwa wananchi kwa ajili ya kuhamasisha marekebisho ya changamoto zilizobainika.

Marafiki wa Elimu Babati, chini ya mwavuli wa HakiElimu, wanatekeleza miradi mbalimbali ya kuboresha mazingira ya watoto, ikiwa ni pamoja na:

  • Ujenzi wa vyoo katika shule tano ili kuboresha usafi na usalama wa wanafunzi.
  • Ujenzi wa bweni katika Shule ya Sekondari Nakwa, ambapo wazazi watachangia ujenzi wa msingi na HakiElimu itakamilisha mradi huo.

Wito kwa Wazazi

Wazazi wametakiwa kutenga muda wa kukaa na watoto wao badala ya kuwaachia malezi kwa wafanyakazi wa ndani pekee.

 "Wazazi waache tabia ya kuwa bize na maisha huku wakitelekeza watoto wao, ni jukumu la mzazi kuhakikisha mtoto anapata malezi bora na muda wa kufundwa katika misingi sahihi ya maisha," ilisisitizwa katika ripoti hiyo.

Kwa hatua hii, Marafiki wa Elimu Babati wanaendelea kushirikiana na jamii kuhakikisha kuwa watoto wanalelewa katika mazingira salama, yenye afya, na yanayochochea maendeleo yao ya elimu na maisha kwa ujumla.

Picha mbalimbali wakati wa Uwasilishaji ripoti.








Bosi Hakujua Kama Nimemfunga Mke wangu

Bosi Hakujua Kama Nimemfunga Mke wangu


Jina langu Abdallah, unajua wahenga hawakukosea waliposema ukistaajabu ya musa utayaoana ya firauni, huu ni msemo ambao hadi sasa unaishi katika maisha ya watu na jamii kwa ujumla kutokana na matukio na visa mbalimbali vinavyowakumba.

Singependa kutaja jina langu kutokana sababu za kiusalama ila naishi nchini Kenya, nimeamua kuandika ujumbe huu baada ya Bosi wangu kuleta mambo ya ajabu sana, nayo ni kung'ang'ania kuzaa mtoto na mke wangu wa ndoa.

Hata hivyo, mke wangu hakujua kama nimemfunga, wala Bosi wangu hakujua hilo, hivyo nilipokuwa napata safari za kikazi nilikuwa na amani tele na furaha zaidi hasa kutokana na kuongezeka kwa fedha ambayo nilikuwa napatiwa kama posho ya kujikimu na safari.

Baada ya muda wa miezi kadhaa mke wangu aliniita chumbani na kuniambia Bosi wangu alikuwa akimtongoza na kumwambia anataka kuzaa naye kutokana anaona watoto wetu ni wazuri sana na wanavutia.

Mke wangu aliniambia kwa muda mrefu alifanya jambo hilo kuwa siri lakini anaona kadiri anavyofanya siri moyo wake unakosa amani kabisa kutokana na jinsi anavyosumbuliwa.

Alilia sana na kuniomba msamaha kwa kutunza siri hiyo ya ajabu ambayo ingeweza kumfanya akazaa nje ya ndoa yetu ambayo imedumu kwa miaka mingi sasa, huku ikiwa na amani na upendo.

Hadi kufika hapo nikajua kabisa dawa ya Kiwanga Doctors kweli inafanya kazi yake ipasavyo, kilichokuja kunishangaza ni yule Bosi wangu alikuja kufukuzwa kazi katika mazingira ambayo sikuwahi kuyaelewa hadi sasa na hapo ndoa yangu ikazidi kuwa na usalama zaidi.

Unajua tulifikaje hapo?. kwa uwezo wa Kiwanga Doctors kutoka Migori, Kenya ndipo nilipobaini mbinu hiyo chafu ya Bosi wangu, nakumbuka nafiki yangu mmoja alinipa namba ya mtaalamu huyo na kuniambia anaweza kumfunga mke wangu asiweze kutoka nje ya ndoa.

Nilifika ofisini kwake na alinipatia dawa na kuanza kuzitumia, niliendelea na shughuli zangu, wakati huo Bosi wangu alikuwa kila mara ananipa safari nyingi za kikazi ili apate muda wa kuendelea kumshawishi mke wangu bila kujua tayari nilishamfunga.

Kwa hakika ni watu wengi wamepata uponyaji, mafanikio, furaha kupitia huduma za Kiwanga Doctors ambao unaweza kuwasiliana na kwa namba +254 116469840 au tembelea tovuti yao, www.kiwangadoctors.co.tz kwa maelezo zaidi kuhusu huduma zao.

Ommy Dimpoz Amefukuzwa na GSM na kuachishwa Kazi? Aandika haya baada ya tetesi kusambaa

 Ommy Dimpoz amefukuzwa na GSM na kuachishwa kazi? Aandika haya baada ya tetesi kusambaa


Thursday, March 20, 2025

JUHIBU Yaja na Mbinu Mpya Kukabiliana na Wanyamapori Waharibifu

Na John Walter -Babati

Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori Burunge (JUHIBU) imeendelea kubuni mbinu mbalimbali za kuzuia wanyamapori waharibifu kuvamia mashamba na kula mazao ya wakulima.

Katika juhudi hizo, JUHIBU imeanzisha matumizi ya baruti, pilipili na mchanga vilivyowekwa kwenye mipira ya kondomu kama moja ya njia za kuwazuia wanyama hao kuingia kwenye mashamba ya wananchi.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Wilaya ya Babati, Emmanuela Kaganda, amekabidhi vifaa mbalimbali vyenye thamani ya shilingi milioni 76 vya kuimarisha ulinzi wa mashamba kwa vijiji 10 vya kata ya Mwada, Nkaiti na Magara vinavyohudumiwa na JUHIBU.

Kwa mujibu wa Katibu wa JUHIBU Benson Mwaise, Vifaa hivyo ni pamoja na vilipuzi na honi, ambavyo vinalenga kusaidia wakulima kuwatisha wanyama waharibifu na hivyo kuwaepusha na hasara ya mazao yao.

Amesema kuwa hatua hiyo inalenga kupunguza migogoro kati ya binadamu na wanyamapori, hasa katika maeneo yanayopakana na hifadhi za wanyama.

"Tunapenda kuona wakulima wakiendelea kufanya shughuli zao bila hofu ya wanyama waharibifu, huku tukihakikisha kuwa wanyama hawa wanahifadhiwa kwa njia endelevu," alisema Kaganda.

JUHIBU imekuwa mstari wa mbele katika kutafuta suluhisho endelevu kwa changamoto hiyo, kwa kushirikiana na serikali na wananchi kuhakikisha wanyama na binadamu wanaishi kwa amani bila kuathiri ustawi wa pande zote mbili.


“Hadi Akaanza Kunipapasa Pale Sebleni,” Jamaa Asimulia


Unajua huku duniani kuna matukio ya ajabu sana, unaweza kushangaa na kujiuliza yote haya yanafanyika kwa sababu gani, kwa faida ya nani, na huyu mtu anayefanyiwa hivyo ananufaika na kipi hasa sasa na hapo baadaye.

Jina langu ni Ally kutokea Mombasa ila nyumbani kwa wazazi wangu ni Lamu, mwaka 2021 nilikuja Mombasa kutafuta kazi yoyote ya kufanya maana nilikuwa sijasoma na sina ujuzi wowote ule maishani.


Nilifikia kwa rafiki yangu ambaye miaka ya nyuma tulisoma wote shule ya upili, nilikaa kwake kwa muda wa miezi mitatu hadi nilipopata kazi kwa Baba moja ambaye ni mtu aliyefanikiwa sana kimaisha.


Kusema kweli Bosi huyu alinipenda sana kama mtoto wake maana nilimsaidia sana vitu vingi, umri wake ulikuwa umekwenda ila mke wake alionekana bado ni kijana mbichi, bado alikuwa anatamanisha sana tu.

Walikuwa wanaishi wenyewe tu katika nyumba yao kubwa, hivyo mimi nikawa ni mtu watatu katika familia ile ambayo fedha kwao hazikuwa tatizo kwani watoto wao wanaoishi nje ya nchi walikuwa wanawatumia fedha nyingi za matumizi.

Nilikuwa nafanya kazi yangu ya kutunza bustani nje, kufanya usafi ndani kisha kupika, baada ya hapo nilikaa tu na kutazama tamthilia mbalimbali. Cha ajabu mke wa Bosi wangu wakati mume wake anakuwa hayupo alipenda kuja kukaa wenye sofa ambalo nimekaa na kujikuta tumebanana.

Aliendelea na mtindo huo hadi kuna siku akaanza kunipapasa pale sebleni, hadi akanitamkia kuwa ananipenda sana na analihitaji penzi langu. Nilimwambia siwezi kufanya kitendo kama hicho, basi baada ya siku hiyo akaanza kunichukia na kunileta visa vingi mule ndani.

Asubuhi moja ambayo siwezi kuisahau, nilikamatwa na Polisi na kufikishwa kituo cha Polisi na kuambia usiku wa jana yake nilitaka kumbaka Bosi wangu huyo!. Nilifikishwa mahakamani na kusomewa kesi ya ubakaji, baada ya miezi kadhaa nilipewa dhamana na kuwa nje kwa masharti maalumu.

Nilirejea nyumbani kwa yule rafiki yangu, akaniambia tuwasiliana na mtu anayeitwa Kiwanga Doctors kutokea Migori atatusaidia kwani amewasaidia watu wengi kushinda kesi mbalimbali hasa zile za kusingiziwa.

Basi tulimpigia simu Kiwanga Doctors na kumueleza shida yangu, alinisikiliza kwa makini sana na kunifanyia tiba yake, alinihakikishia baada ya muda sio mrefu nitashinda kesi hiyo, hivyo hakuna sababu ya kuwa na wasiwasi.

Niliendelea kwenda mahakamani kila tarehe ambaye kesi ile ingetajwa, nashukuru kweli niliweza kushinda kesi ile kwa kuonekana sikuwa na hatia yoyote. Sikuweza kuamini daima maana Bosi wangu alikuwa mtu mwenye fedha nyingi, hivyo ingekuwa ni vigumu sana kumshinda katika kesi ile ila nikashinda.

Kwa hakika ni watu wengi wamepata uponyaji, mafanikio, furaha kupitia huduma za Kiwanga Doctors ambao unaweza kuwasiliana na kwa namba +254 116469840 au tembelea tovuti yao, www.kiwangadoctors.co.tz kwa maelezo zaidi kuhusu huduma zao.


Source

Wednesday, March 19, 2025

DC Babati ataka elimu itolewe kwa wananchi kilimo kisichowavutia Wanyama.

Na John Walter -Babati 

Mkuu wa Wilaya ya Babati, Emmanuela Kaganda, amewataka watendaji wa maeneo yanayozungukwa na hifadhi kuwapa wananchi elimu juu ya kulima mazao yasiyowavutia wanyama waharibifu ili kuepuka migogoro kati ya binadamu na wanyamapori.

Kaganda ameyasema hayo wakati wa hafla ya kukabidhi magunia 309 ya mahindi kwa vijiji 10 vinavyopakana na hifadhi, mahindi ambayo yamenunuliwa na Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori Burunge (JUHIBU).

Katibu wa JUHIBU, Benson Mwaise, amesema kuwa mahindi hayo yamenunuliwa kwa ajili ya wanachama wa jumuiya hiyo katika vijiji 10 vilivyokubali kuacha kilimo na badala yake kushiriki kwenye uhifadhi. 

Mahindi hayo yamegawiwa kwa shule mbalimbali za msingi zilizopo katika kata za Mwada, Nkaiti, na Magara, ili kusaidia chakula cha mchana kwa wanafunzi.

Mkuu wa wilaya ameagiza wanafunzi waelimishwe kuhusu namna chakula hicho kilivyopatikana, ili wapate uelewa wa umuhimu wa uhifadhi wa wanyamapori na mazingira.

Aidha, Kaganda ameagiza kuandaliwa mpango bora wa matumizi ya ardhi kwa vijiji vinavyopakana na hifadhi ili kuweka mipaka bayana kati ya shughuli za kilimo na maeneo ya uhifadhi. 

Ameeleza kuwa utalii unalipa na wananchi wanapaswa kulima mazao kama tumbaku, ufuta, na aina maalum ya alizeti ambayo hayawavutii wanyama waharibifu.

Pia, amesisitiza umuhimu wa kuweka alama katika maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya utalii ili kuepusha migogoro, pamoja na kuhakikisha mifugo kama ng'ombe haiingii katika maeneo ya hifadhi.

Mkuu wa wilaya amepongeza JUHIBU, wananchi, na viongozi kwa kazi nzuri ya kusimamia uhifadhi na kuhakikisha jamii inanufaika na rasilimali za wanyamapori kwa njia endelevu.

Diwani wa Nkaiti, Steven Saruni Mollel, amepongeza juhudi za JUHIBU akisema kuwa jumuiya hiyo imeleta manufaa makubwa kwa wananchi, ambao sasa wanaelewa thamani ya uhifadhi.

Amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwezesha jamii kunufaika kupitia rasilimali za wanyamapori.

Hatua ya kugawa mahindi hayo inasaidia wazazi na walezi katika kugharamia chakula cha mchana kwa wanafunzi, hasa kutokana na kupungua kwa shughuli za kilimo kwenye vijiji hivyo kutokana na uwekezaji katika uhifadhi.

Endapo Suala ya Yanga na Simba Litashindikana, Basi Tutawahusisha Serikali...



Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Kuu, Steven Mguto katika mahojiano yake na Kituo cha Habari cha Mwananchi Digital amesema iwapo wao Kama mamlaka za kimpira watashindwa kutatua sakata la Simba na Yanga kuhusiana na mechi Yao iliyoshindikana kupigwa Machi 8, 2025 basi wataishirikisha Serikali.

Hayo yamejiri baada ya bodi kuahirisha mchezo huo wa Derby ya Kariakoo na Yanga kuandika barua ya kubainisha kuwa hawataucheza tena mchezo huo na kudai alama tatu.

"Jambo hili likitushinda kabisa lazima tuihusishe Serikali iweze kusaidia, kwasababu kuhakikisha amani inakuwepo sio suala letu sisi peke yetu kila mtu anatakiwa kuhakikisha kuna kuwa na amani," amesema Mguto.

Source

𝐎𝐅𝐅𝐈𝐂𝐈𝐀𝐋: Kifungo cha Paul Pogba Kimeisha na Maisha Yanaendelea Japo Kwa Ugumu

𝐎𝐅𝐅𝐈𝐂𝐈𝐀𝐋: Kifungo cha Paul Pogba Kimeisha na Maisha Yanaendelea Japo Kwa Ugumu


🗣️Paul Pogba: "Pesa hubadilisha watu. Inaweza kuvunja familia. Inaweza kuunda vita. Wakati fulani nilikuwa peke yangu na nilihisi kama sitaki kuwa na pesa tena wala sitaki kucheza tena.

Nilitaka kuwa na watu wa kawaida, kwa hivyo marafiki na familia yangu wananipenda kwa ajili yangu, sio kwa umaarufu, sio kwa pesa."

Paul Pogba Brothers wakiwa na magenge mengine kweli walienda kumuibia, kwa bahati mbaya wezi hao Paul Pogba aliweza kumtambua kaka yake kati yao licha ya yeye kuvaa barakoa (mask) 🎭.

Kwa nini ndugu waligeuka dhidi yake? Sababu ni hii; walihisi Paul hakuwa akiwapa pesa za kutosha licha ya kuwa mmoja wa wanasoka tajiri zaidi duniani, hivyo wakaanza kufanya kila kitu ili kumuangusha Paul Pogba, hata wakatoa siri ya jinsi Paul Pogba alivyoenda Afrika kufanya Voodoo 💔

Baadhi ya wanafamilia ni adui yako mkubwa, kuwa mwangalifu. Mtu anatakiwa kuwa makini sana siku hizi

𝐎𝐅𝐅𝐈𝐂𝐈𝐀𝐋: Kifungo cha Paul Pogba sasa ni kimeisha na anapatikana kucheza soka kuanzia leo ✨

Pogba, bado yuko sokoni kama mchezaji huru na yuko wazi kwa ukurasa mpya baada ya mazoezi ya mara kwa mara huko Miami…


Unahisi ni klabu gani inapaswa kwenda kumchukua Paul?

Jinsi ya Kununua Tiketi za Mpira Mtandao wa Vodacom M-Pesa

 

Jinsi ya Kununua Tiketi za Mpira Mtandao wa Vodacom M-Pesa

Jinsi ya Kununua Tiketi za Mpira Mtandao wa Vodacom M-PesaJinsi Ya


Vodacom M-Pesa inatoa urahisi wa kununua tiketi za mpira bila usumbufu wa foleni ndefu. Ukiwa na simu yako tu, unaweza kupata tiketi yako ndani ya dakika chache. Zaidi ya hayo, huduma hii ni salama, ikilinda taarifa zako za kifedha.


Jinsi ya Kununua Tiketi za Mpira Vodacom M-Pesa

Piga *150*00#

Chagua 4 (Lipa kwa M-Pesa)

Chagua 9 (Zaidi)

Chagua 1 (E-payment)

Chagua 1 (Tiketi za Michezo)

Chagua 1 (Tiketi za Mpira)

Chagua mechi unayotaka kulipia

Chagua kiingilio

Weka namba ya kadi ya N-Card

Ingiza namba ya siri

Thibitisha

Exclusive: Mwakinyo Aongea Baada ya Polisi Kumuschia 'Niweke Wazi Hakuna wa Kunihamisha Mtaani Kwangu'

Exclusive: Mwakinyo Aongea Baada ya Polisi Kumuschia, Niweke Wazi Hakuna wa Kunihamisha Mtaani Kwangu 


Tuesday, March 18, 2025

Wananchi 7000 Kilosa kunufaika na mnara wa mawasiliano wa Airtel Tanzania


Morogoro, Machi 2025 - Kampuni ya Airtel Tanzania imejenga mnara wa mawasiliano wa 4G Kijiji cha Idete, wilayani Kilosa, Morogoro, ambao unatarajiwa kuwanufaisha wakazi wapatao 7000, hatua ambayo itawafungulia fursa wananchi hao kunufaika kiuchumi na kijamii. 

Akizungumza wakati wa ziara maalumu ya kukagua maendeleo ya ujenzi mnara huo katika Kijiji hicho, Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Jerry Silaa, amesema kuwa ujenzi wa minara hiyo iko sambamba na dhamira ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan ya kuona Tanzania ya kidjitali na kuona maeneo yote yanafikishiwa mawasiliano. 

"Kama alivyosema Mkuu wa Wilaya, kilimo chao wanachokifanya na shughuli zao za kuchunga wanazozifanya wasisumbuke tena kuhangaika kwenda Kilosa mjini. Basi na wenyewe wakae ndani ya mawasiliano waweze kuwasiliana na wateja wao, wauza pembejeo, na waweze kuwasiliana na ndugu zao. Lakini cha muhimu waweze kuwasiliana kama watanzania wengine," alisema Waziri Silaa.

Aliongeza "Lengo hili sisi wasaidizi wa Rais lazima tuhakikishe hili linatimia. Tunataka tarehe moja mwezi wa nne mnara huu uwashwe na tunataka tarehe 15 mnara huu uzinduliwe rasmi na mnara huu uzinduliwe rasmi na mawasiliano yapatikane hapa idete."

Waziri Silaa alisisitiza kuwa mnara huo wa mawasiliano sio tu kwa ajili ya wananchi wa Kijiji cha idete bali ni kwa wananchi milioni 8.5 ndani ya nchi ya Tanzania, akiongeza kuwa kabla ya minara hiyo kujengwa wananchi walikosa mawasiliano, lakini Mheshimiwa Rais alitoa fedha ili wananchi hao waweze kupata mawasiliano.

Kwa upande wake, Meneja Uhusiano kwa Umma wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando, alisema kuwa wahandisi wanaojenga mnara huo wameeleza kuwa ujenzi huo unatarajia kukamilika mapema na kuwashwa tarehe moja mwezi Aprili mwaka huu.

"Jambo kubwa ambalo timu yetu ya mauzo imefanya tayari mpaka leo wameshapata mawakala wakubwa watatu ambao ni wakazi wa hapa hapa. Kwa hiyo ni ajira ambayo tumeitoa. Lakini bado pia tumepata mawakala wadogo wadogo ambao wanakuwa wanatoa huduma za Airtel money na Airtel Money branch 10 ambaoi tayari tumeshawasajili na tayari wanangojea mnara ule uwashwe waanze kufanya kazi," alisema Mmbando.

Mmbando aliwataka wananchi kuchangamkia fursa zinazotokana na mnara huo ambao unajengwa kwa kushirikiana na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF).

Monday, March 17, 2025

Asake akubali kuwasaidia Baba pamoja na Mtoto wake baada ya shutuma za kuwatelekeza, Baba ambariki

 Asake akubali kuwasaidia Baba pamoja na Mtoto wake baada ya shutuma za kuwatelekeza, Baba ambariki


Tuna Wachezaji Wazawa Wazuri Lakini Tunakosa Mwendelezo wa Ubora, Shida Ipo Wapi?



Kwanye hii miaka ya hivi karibuni ukimuondoa Aishi Manula aliyechukua tuzo ya mlinda lango bora back to back ana tuzo 6+ za ligi, ameivusha Simba bora kwenye michuano ya Caf, Afcon timu ya Taifa.

Feisal Salumu mchezaji mwingine mwenye mwendelezo wa ubora wake kwa miaka 4+ mfululizo bila kushuka Alicheza akiwa Yanga akachukua tuzo binafsi za kutosha ubingwa wa Yanga,

Feisal akajiunga Azam timu iliyopo kwenya kivuko cha kuingia kwenye timu kubwa kimafanikio Feisal anaibeba timu mabegani, kama kiungo kuingia kwenye orodha wa washambuliaji wawili bora sio kawaida, Kiungo bora kitakwimu na uwezo hakubahatisha ndiyo maana namba zinaendelea mpaka msimu huu.

Mtazame kwa sasa Clement Mzize alicheza mbele ya Mayele, anacheza mbele ya Msonda, Dube, Pacome na Chama, Guede kamkimbia.

Kila mwalimu anaekuja Yanga anamtumia anafunga anachezesha timu na anasaidia ulinzi anacheza kama mshambuliaji winga na kuna muda anashuka chini kama beki namba zake zinaongezeka kila msimu,

Warejee Simba na mbavu zao zote mbeli Kapombe + Hussen ukiulizwa nani aondoke pale Simba kati ya hawa wawili kila mtu atakuuliza kuna mafanikio yeyote ya Simba kwa zaidi ya miaka 10 utayataja bila kuzihusianisha hizi mbavu mbili za ulizi ?

Pale England waandishi wa habari wanatajwa kuwa sehemu kubwa ya kuwalinda wachezaji wao, kuna nyakati kwetu mchezaji bora ndiye anasimangwa zaidi kisa utani wa jadi na mambo mengine yasiyo ya muhimu.

unajiuliza kukosa muendelezo kwa wachezaji wazawa shida ipo wapi ????

@cheyolutenganotz
@bongotzfm

Sunday, March 16, 2025

ASKOFU MTEULE WA KKKT DAYOSISI YA MWANGA DKT. MONO APOKELEWA KWA SHANGWE KUBWA SHINYANGA


Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry

Na Isaac Masengwa
*******************
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga mkoani Kilimanjaro Daktari Daniel Henry Mono amepewa mapokezi makubwa na waumini wa KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria inayofanya kazi katika mikoa ya Shinyanga na Simiyu.

Mapokezi hayo makubwa yakiongozwa na Askofu wa dayosisi hiyo Mchungaji Daktari Yohana Ernest Nzelu, yamekuwa mapokezi ya kwanza tangu ateuliwe kuwa askofu wa dayosisi ya Mwanga na yamefanyika leo Machi 15, 2025.

Akizungumza katika sala fupi ya mapokezi hayo iliyofanyika katika usharika wa Ebenezer Kanisa Kuu Shinyanga, Askofu mteule Daktari Daniel Henry Mono amesema kuwa hakutegemea kukutana na mapokezi makubwa kama haya.


"Kwa kweli leo nimetekewa kwa sababu ukweli kabisa sikujua kama kuna jambo la namna hii. Nimekutana na jambo ambalo sikulitegemea kabisa, nimeona magari, watu na tarumbeta ambapo nilijikuta nikitekewa"

"Jambo la kwanza ninamshukuru Mungu kwa yote aliyotenda, ninamshukuru kwa jinsi alivyonipitisha katika utumishi wake na mpaka sasa ameniita tena kutumika katika nafasi hii kubwa."

"Pia nikushukuru sana baba Askofu Yohana Ernest Nzelu, umekuwa rafiki yangu kwa muda mrefu, nimeishi na wewe kama rafiki na kama ndugu. Hata ulipofika wakati wa kufanya kazi na wewe nimefurahi sana kufanya kazi na mimi. Pia nikushukuru hata kwa jinsi umenishauri katika kuliendea jambo hili."

"Lakini pia nikushukuru sana baba Askofu mstaafu Makala, umekuwa mwalimu wetu mwema katika utumishi huu. Umenipa malezi mazuri ya kiutumishi, umetuntengeneza hadi kuwa hivi nilivyo. Kupata nafasi kama hii wewe umekuwa sehemu ya kufikia hatua hii."

Naye Askofu wa Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria Daktari Yohana Ernest Nzelu, amemshukuru Mungu kwa ajili ya nafasi hii ya utumishi aliyoipata askofu mteule Daktari Mono.

"Ni haki yetu kama dayosisi kumshukuru Mungu kwa ajili ya nafasi hii aliyoipata

"Nimshukuru sana Baba Askofu mstaafu Daktari Emmanuel Makala kwa kuwa yeye ndio amekuwa lango la wengine kupata nafasi kama hizi. Katika utumishi wako umekuwa chanzo cha sisi wengine kupata nafasi hizi."

"Nimepokea barua kutoka dayosisi ya Mwanga wakiniomba Daktari Mono uende ukatumike katika dayosisi ya Mwanga".

"Nami nimewajibu majibu ya awali kuwa Daktari Mono atakuja kutumika katika dayosisi ya Mwanga tukiwa tunasubiri maamuzi ya mwajiri wake"

Naye kwa upande wake askofu mstaafu wa Dayosisi hiyo Askofu Makala amempongeza Askofu mteule Daniel Mono na kumtaka kuwa kiongozi atakayeandaa viongozi wajao.

"Ukipewa nafasi ya kuongoza andaa wengine ili kanisa liweze kusonga mbele. Baba askofu mteule hongera sana, wewe nenda kafanye kazi ya Mungu kwa kadri Mungu atakavyokutumia."

Daktari Daniel Henry Mono ni msaidizi wa Askofu wa dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria. Na alichaguliwa na mkutano mkuu wa dayosisi ya Mwanga iliyopo mkoani Kilimanjaro kuwa askofu wa pili wa dayosisi hiyo yeye akiwa katika majukumu yake Nchini Burundi.

Hii inakuja baada ya aliyekuwa Askofu wa kwanza wa dayosisi hiyo Chediel Sendoro kufariki dunia mwaka jana Septemba 9, 2024 kwa ajali ya gari

Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Mono akitoa neno la shukrani kwa waumini wa KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria wakati wa mapokezi

Askofu Daktari Yohana Ernest Nzelu akiongoza mapokezi ya Askofu mteule wa Dayosisi ya Mwanga Mchungaji Daktari Daniel Henry Mono

Askofu Daktari Yohana Ernest Nzelu akiongoza mapokezi ya Askofu mteule wa Dayosisi ya Mwanga Mchungaji Daktari Daniel Henry Mono
Katibu Mkuu wa KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria Bi. Happiness Geffi akitoa maelekezo wakati wa mapokezi yaAskofu mteule wa Dayosisi ya Mwanga Mchungaji Daktari Daniel Henry Mono


Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Mono akiwasili usharika wa Ebenezer Kanisa Kuu Shinyanga wakati wa mapokezi hayo
Mama Askofu mteule Heavenlight Daniel Mono akifuatilia kwa makini kinachoendelea wakati wa mapokezi hayo

Askofu mstaafu wa KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria Mchungaji Daktari Emmanuel Joseph Makala akizungumza machache wakati wa mapokezi ya Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Mchungaji Daktari Daniel Henry Mono

Askofu mstaafu wa KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria Mchungaji Daktari Emmanuel Joseph Makala akizungumza machache wakati wa mapokezi ya Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Mchungaji Daktari Daniel Henry Mono.
Askofu mstaafu Daktari Emmanuel Makala (katikati), Mama Askofu mstaafu Mdiakonia Lilian Makala (kushoto) na Chaplain wa Kanisa Kuu Mchungaji Zinyangwa Silas Mkiramweni wakifuatili kwa makini tukio la kumpokea Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Mchungaji Daktari Henry Mono

Akofu wa KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria Mchungaji Daktari Yohana Ernest Nzelu (kulia) na Katibu Mkuu wa KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria Bi. Happiness Geffi (kushoto) wakati wa mapokezi ya Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Mchungaji Daktari Daniel Henry Mono
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Mono (kushoto) akiwa na mwenyeji wake Askofu wa KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria Mchungaji Daktari Yohana Ernest Nzelu wakati wa mapokezi hayo


Askofu Daktari Yohana Ernest Nzelu akifuatilia kwa makini kinachoendelea wakati wa mapokezi ya Askofu mteule wa Dayosisi ya Mwanga Mchungaji Daktari Daniel Henry Mono




Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Mono akifauatilia kwa makini kinachoendelea wakati wa mapokezi yake mkoani Shinyanga
Katibu Mkuu wa KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria Bi. Happiness Geffi akifuatilia kwa umakini kinachoendelea wakati wa mapokezi ya Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Mchungaji Daktari Daniel Mono (kulia), Askofu wa KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria Mchungaji Daktari Yohana Ernest Nzelu (katikati) Mama Askofu Lilian Yohana Ernest Nzelu (katikati) na Mama Askofu mteule Heavenlight Daniel Mono (kulia) wakiwa wanafuatilia kinachoendelea wakati wa mapokezi hayo

Wachungaji wa KKKT Dayosisi Kusini mashariki wakifuatilia kwa makini kinachoendelea wakati wa mapokezi ya Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga
Wachungaji wa KKKT Dayosisi Kusini mashariki wakifuatilia kwa makini kinachoendelea wakati wa mapokezi ya Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga
Kwaya ya Muungano ya watumishi wa KKKT Dayosisi Kusini Mashariki Ofisi kuu za Dayosisi pamoja na watumishi wa Usharika wa Ebenezer Kanisa Kuu Shinyanga wakiimba wakati wa mapokezi ya Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga

Kwaya ya Muungano ya watumishi wa KKKT Dayosisi Kusini Mashariki Ofisi kuu za Dayosisi pamoja na watumishi wa Usharika wa Ebenezer Kanisa Kuu Shinyanga wakiimba wakati wa mapokezi ya Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga
Kwaya ya Muungano ya watumishi wa KKKT Dayosisi Kusini Mashariki Ofisi kuu za Dayosisi pamoja na watumishi wa Usharika wa Ebenezer Kanisa Kuu Shinyanga wakiimba wakati wa mapokezi ya Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga
Waumini na Wachungaji wa KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria wakimlaki kwa shangwe na kumpongeza Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga wakati wa mapokezi
Waumini na Wachungaji wa KKKT Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria wakimlaki kwa shangwe na kumpongeza Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga wakati wa mapokezi
Msafara wa magari wakati wa mapokezi ya Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Mchungaji Daktari Daniel Mono

Msafara wa magari wakati wa mapokezi ya Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Mchungaji Daktari Daniel Mono
Msafara wa magari wakati wa mapokezi ya Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Mchungaji Daktari Daniel Mono
Msafara wa magari wakati wa mapokezi ya Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Mchungaji Daktari Daniel Mono
Msafara wa magari wakati wa mapokezi ya Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Mchungaji Daktari Daniel Mono
Msafara wa magari wakati wa mapokezi ya Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Mchungaji Daktari Daniel Mono
Msafara wa magari wakati wa mapokezi ya Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Mchungaji Daktari Daniel Mono
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...