Aliyekuwa kocha wa Yanga Sc, Sead Ramovic ameshinda mchezo wake wa kwanza kwenye Ligi Kuu Nchini Algeria kufuatia ushindi wa 3-0 dhidi ya klabu ya USM Khenchela.
Kwa ushindi huo CR Belouizdad imekwea kileleni mwa msimamo wa Ligi ikifikisha pointi 29 baada mechi 16, wakiwa alama moja mbele ya MC Alger waliopo nafasi ya pili huku wakiwa na mchezo mmoja mkononi.
FT: CR Belouizdad 3-0 Khenchela
⚽ 27' Mayo
⚽ 51' Hamroune
⚽ 86' Boukerchaoui