Wednesday, June 2, 2021
RC Kafulila aanza kwa kuzichimbua fedha za madini ya ujenzi.
Samirah Yusuph
Simiyu. Mkuu wa mkoa wa Simiyu David Kafulila ameagiza uhakiki wa kiasi cha madini ya ujenzi yanayotoka katika kila halmashauri za wilaya ya mkoa huo kwenda katika ujenzi wa barabara na miradi mingine.
Agizo hilo amelitoa Juni 1,2021 alipo kuwa katika ukaguzi wamradi wa ujenzi wa Barabara ya Bariadi, Mwigumbi yenye urefu wa kilometa 50.3 kufuatia uwepo wa halmashauri za wilaya ambazo hazifahamu thamani ya malipo ya madini hayo.
Kafulila ameagiza kuwa kila halmashauri kufanya uhakiki wa kiasi cha madini ambayo yamechimbwa kwa kipindi cha miaka mitano na kupata thamani yake ili mkandarasi aliyehusika na uchimbaji huo afanye malipo.
"Halmashauri zote ndizo zenye mamlaka ya kutenga maeneo ya kuchimba madini ya ujenzi na walipwe ushuru wao, ili pesa ya Mrahaba na asilimia moja ya ukaguzi iende tume ya madini...Ile dhana ya mtu kuendelea kuvuna kokoto kwa leseni ya Tanroad baada ya kuwa mradi umekamilika iwe ni mwisho".
Aidha ameongeza kuwa hadi sasa Tume ya madini mkoa wa Simiyu inadai tsh670 milioni za mirahaba ya madini kwa mkandarasi wa barabara hiyo huku pesa iliyolipwa kwa kipindi chote hicho ikiwa ni tsh 20 milioni pekee huku halmashauri ya wilaya ya Maswa yalipo machimbo ya kokoto hizo haifahamu ni kiasi gani inatakiwa kulipwa.
Jambo ambalo mkurugenzi wa wilaya hiyo Dkt Fredrick Sagamiko ameelezea kuwa licha ya halmashauri kufuatilia kwa ukaribu zoezi la uchimbaji wa madini hayo kwa kipindi chote hawakuweza kupewa ushirikiano na wakala wa barabara (tanroads) ambaye ndiye mwenye mkataba na mkandarasi.
Katika hatua nyingine Kafulila amewatahadharisha wakandarasi wanaofanya kazi chini ya kiwango katika mkoa huo kuwa hakuna nafasi ya kuwavumilia tena huku akimtaka mkandarasi anayejenga kipande hicho cha barabara kufanya kazi kwa weredi baada ya kazi ya awali kulazimika kuirudia kutokana na kuwa ilijengwa chini ya kiwango ujenzi ambao umeanza tangu 2015 hadi sasa haujakamilika.
Mwisho.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
