Wednesday, June 2, 2021
RC Kafulila aanza kwa kuzichimbua fedha za madini ya ujenzi.
Samirah Yusuph
Simiyu. Mkuu wa mkoa wa Simiyu David Kafulila ameagiza uhakiki wa kiasi cha madini ya ujenzi yanayotoka katika kila halmashauri za wilaya ya mkoa huo kwenda katika ujenzi wa barabara na miradi mingine.
Agizo hilo amelitoa Juni 1,2021 alipo kuwa katika ukaguzi wamradi wa ujenzi wa Barabara ya Bariadi, Mwigumbi yenye urefu wa kilometa 50.3 kufuatia uwepo wa halmashauri za wilaya ambazo hazifahamu thamani ya malipo ya madini hayo.
Kafulila ameagiza kuwa kila halmashauri kufanya uhakiki wa kiasi cha madini ambayo yamechimbwa kwa kipindi cha miaka mitano na kupata thamani yake ili mkandarasi aliyehusika na uchimbaji huo afanye malipo.
"Halmashauri zote ndizo zenye mamlaka ya kutenga maeneo ya kuchimba madini ya ujenzi na walipwe ushuru wao, ili pesa ya Mrahaba na asilimia moja ya ukaguzi iende tume ya madini...Ile dhana ya mtu kuendelea kuvuna kokoto kwa leseni ya Tanroad baada ya kuwa mradi umekamilika iwe ni mwisho".
Aidha ameongeza kuwa hadi sasa Tume ya madini mkoa wa Simiyu inadai tsh670 milioni za mirahaba ya madini kwa mkandarasi wa barabara hiyo huku pesa iliyolipwa kwa kipindi chote hicho ikiwa ni tsh 20 milioni pekee huku halmashauri ya wilaya ya Maswa yalipo machimbo ya kokoto hizo haifahamu ni kiasi gani inatakiwa kulipwa.
Jambo ambalo mkurugenzi wa wilaya hiyo Dkt Fredrick Sagamiko ameelezea kuwa licha ya halmashauri kufuatilia kwa ukaribu zoezi la uchimbaji wa madini hayo kwa kipindi chote hawakuweza kupewa ushirikiano na wakala wa barabara (tanroads) ambaye ndiye mwenye mkataba na mkandarasi.
Katika hatua nyingine Kafulila amewatahadharisha wakandarasi wanaofanya kazi chini ya kiwango katika mkoa huo kuwa hakuna nafasi ya kuwavumilia tena huku akimtaka mkandarasi anayejenga kipande hicho cha barabara kufanya kazi kwa weredi baada ya kazi ya awali kulazimika kuirudia kutokana na kuwa ilijengwa chini ya kiwango ujenzi ambao umeanza tangu 2015 hadi sasa haujakamilika.
Mwisho.
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mjini Richard Kasesela Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mjini Richard Kasesela amelishauri Kanisa la Kiinjili la Kilutheri ...
