Thursday, April 29, 2021
Waziri Kalemani Atoa Maagizo Shirika la Viwango Tanzania (TBS)
Na Teresia Mhagama, Dar es Salaam
Waziri wa Nishati, Dkt.Medard Kalemani ameliagiza Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kuhakikisha kuwa uwekaji wa vinasaba kwenye mafuta kama vile petroli na dizeli unafanyika kuanzia kwenye matenki yanayohifadhi mafuta hayo badala ya magari ili kuhakikisha kuwa mafuta yote yanayosambazwa nchini yanakuwa na ubora na Serikali inapata kodi stahiki.
Dkt.Kalemani alitoa agizo hilo tarehe 28 Aprili, 2021 mara baada ya kufanya ziara kwenye maghala ya mafuta ya kampuni za Camel Oil na Oil Com, Kurasini mkoani Dar es Salaam na kukuta wataalam kutoka TBS wakifanya kazi ya uwekaji wa vinasaba kwenye magari ya kusafirisha mafuta ya kampuni tajwa.
"Nataka muanze kupima mafuta kuanzia kwenye matenki yenyewe, hadi kwenye vituo, siyo tu kusubiri pale wanapopakia kwenye magari, Je ikitokea wamepakia wakati hampo, mtajuaje kuwa mafuta husika yana ubora?"Alisema Dkt.Kalemani
Dkt.Kalemani alieleza kuwa, amefanya ukaguzi wa kazi ya uwekaji wa vinasaba kwenye mafuta ili kujiridhisha kama TBS wanafanya kazi husika kwa ufanisi baada ya kukabidhiwa kutekeleza jukumu hilo ambalo awali lilikuwa likifanywa na mkandarasi binafsi ambaye alikuwa akilipwa takriban shilingi Bilioni Tano kwa mwezi.
Aliongeza kuwa, Serikali imekuwa ikipoteza fedha nyingi kumlipa mkandarasi binafsi kuweka vinasaba kwenye mafuta badala ya TBS ambayo ndiyo yenye dhamana ya kuhakikisha kuwa mafuta yanayouzwa nchini yanakuwa na ubora stahiki.
"Lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa, mafuta yanakuwa na ubora, kodi zinapatikana na pia tunajenga uwezo wa watu wetu kufanya kazi husika na Taasisi zetu zisimamie kazi hii badala ya kutegemea watu kutoka nje ya nchi." Alisisitiza Dkt.Kalemani
Katika ukaguzi huo, Dkt.Kalemani aliiagiza Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), kuhakikisha kuwa, wanasimamia kikamilifu kazi ya uwekaji wa vinasaba kwenye mafuta nchini kwani TBS ina jukumu la kupima mafuta hayo na EWURA ndiye mwenye jukumu la kumsimamia mpimaji.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dkt. Athuman Ngenya alimhakikishia Waziri wa Nishati kuwa, TBS ina uwezo wa kufanya kazi ya uwekaji vinasaba kwenye magari na kwamba mafuta yote yanayosambazwa nchini yanakuwa na vinasaba.
Katika ziara yake kwenye maghala hayo ya mafuta mkoani Dar es Salaam, Waziri wa Nishati aliambatana na Kaimu Kamishna wa Petroli na Gesi, Sebastian Shana, na Wakuu wa Taasisi za Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA), TBS na EWURA.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Baadhi ya raia walioyatoroka makaazi yao baada ya mlipuko wa volkano uliotokea usiku wa kuamkia huko mjini Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kid...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...