Monday, March 29, 2021

CAF yatupilia mbali malalamiko ya Corona ya Al Merreikh dhidi ya Simba




Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF) limetupilia mbali malalamiko ya klabu ya Al Merreikh kuhusu kufanyiwa hujuma na Simba SC juu ya vipimo vya Covid-19 kwa wachezaji wake wakati wa mchezo wa kundi A, uliopigwa Machi 16, 2021 kwenye uwanja wa Mkapa.



Kabla ya mchezo huo wa Ligi ya Mabingwa Afrika uliyopigwa uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam wachezaji nane (8) wa Al Merrikh waligundulika na kuwa na viashiria vya Virusi vya Corona hali iliyopelekea kukkosa kucheza kwenye mechi hiyo dhidi ya wenyeji Simba SC.


Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...