Samirah Yusuph.
Maswa. Kukamilika kwa ujenzi wa matundu ya vyoo katika shule za msingi wilayani Maswa imetajwa kuwa ni moja ya sababu za kutokomeza magonjwa ya mlipuko wilayani hapo.
Ujenzi uliogharim kiasi cha shilingi milioni 178.7 kukamilisha matundu 125 katika shule saba za msingi itakuwa ni msaada kwa wanafunzi na jamii katika kujilinda na magonjwa hayo kwa matumizi sahihi ya vyoo.
Ambapo mkurugenzi mtendaji wa wilaya hiyo Fedrick Sagamiko alisema ujenzi umekamilika kwa asilimia 95, mradi uliotekelezwa kupitia programu ya Afya na Elimu shuleni (SWASH) katika awamu ya kwanza, alisema:
"Ni mradi wa benki ya dunia lakini upo chini ya usimamizi wa ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI) mradi huo unatekelezwa katika shule ambazo zilikuwa na changamoto ya vyoo kwa wanafunzi pamoja na walimu".
Sagamiko Alizitaja shule hizo kuwa ni Jija A matundu (20), Malampaka(33), Mandang'ombe(7), Maswa(30), Mwabulimbu(15), Mwashegeshi(9) na Sangamwalugesha(11).
Katika ujenzi huo kuna mambo ya msingi ambayo yamezingatiwa ambayo ni elimu,afya na maji kwa lengo la kutunza mazingira na kuwa msafi ili kujiepusha na magonjwa ya mlipuko yanayotokana na uchafu.
Alisema kuwa wamehakikisha vyoo hivyo vinakuwa na mfumo wa maji ili mtumiaji mara baada ya kutumia ananawa mikono na kuwa msafi na hivyo kujiepusha na aina yoyote ya magonjwa yanayotokana na uchafu na kuongeza kuwa:
"Ujenzi wa vyoo hivyo umechangiwa na wananchi wa maeneo husika huku akiwashukuru kwa kujitoa katika kushiriki na kuhakikisha vyoo hivyo vinakamilika".
Awali Afisa Elimu Msingi wilaya ya Maswa Saimon Bujimu, alihakikisha kuwa kwa ushirikiano na wakala wa maji wilayani hapo wataweza kutatua changamoto ya maji katika shule hizo ili kuhakikisha wanafunzi wanasoma katika mazingira safi na salama".
MWISHO.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
