Shirika la haki za binadamu la Amnesty International limeishutumu polisi nchini Marekani kwa uvunjaji wa haki za binadamu za waandamanaji wakati wa maandamano ya kupinga ubaguzi wa rangi nchini humo.
Katika ripoti yake iliyochapishwa hii leo, shirika hilo linasema polisi ilitumia vurugu za kimwili mara kwa mara, kemikali kama vile gesi ya kutoa machozi na pilipili, pamoja na vitupo vingine visivyo na madhara makubwa kama risasi za mpira kuwatawanya waandamanaji wa amani.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, matukio ya hivi karibuni yamezusha wasiwasi kuhusiana na haki za kuishi, usalama wa mtu, ulinzi sawa wa sheria, uhuru wa kutobaguliwa na uhuru wa kujieleza na kukusanyika kwa amani.
Shirika hilo la haki za binadamu limeorodhesha matukio huru 125 ya matumizi ya nguvu isivyo laazima katika majimbo 40 pamoja na mji mkuu Washington.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...