Friday, May 1, 2020
Ugonjwa Uliomuondoa Jaji Mkuu Mstaafu Ramadhani Huu Hapa, Leo Kuagwa Kitaifa Karimjee
Jaji Mkuu Mstaafu, Augustino Ramadhani ataagwa leo kitaifa katika viwanja vya vya Karimjee na mazishi yatafanyika kesho Kimara jijini Dar es Salaam.
Kiongozi huyo ataagwa kitaifa kwa mujibu wa sheria ya mazishi ya viongozi wa kitaifa ya mwaka 2006.
Taarifa iliyotolewa na msajili wa Mahakama ya Rufani, Kelvin Mhina jana ilieleza kuwa taratibu za mazishi na maandalizi zinafanywa na kusimamiwa na kamati ya mazishi ya viongozi wa kitaifa inayoongozwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.
'Siku ya Ijumaa (leo) kutakuwa na mazishi ya kitaifa viwanja vya Karimjee kuanzia saa 6:00 hadi saa 8:00 mchana," ilieleza taarifa hiyo.
Aidha, Mhina alisema Jaji Ramadhani atazikwa kesho Jumamosi katika eneo la Makaburi ya familia yaliyopo Kimara King'ongo jijini Dar es Salaam.
Mazishi yatafanyika saa tisa alasiri na kutanguliwa na ibada itakayofanyika katika kanisa la Anglikana la Mtakatifu Albano kuanzia saa 6:00 mchana jijini.
Jaji Ramadhani alifariki dunia Aprili 28, 2020 majra ya saa 2:05 asubuhi katika hospitali ya AgaKhan jijini Dar es Salaam baada ya kuugua kwa muda mrefu maradhi ya saratani na mwishoni kupata mshtuko wa moyo (Heart Attack).
Marehemu Jaji Ramadhani alianza kuugua mwaka 2011 na kugundulika kuwa na ugonjwa wa saratani ambao alipatiwa matibabu katika hospitali mbalimbali nje na ndani ya nchi. Hospitali alizotibiwa ni Apolo na Banglow nchini India, Afrika Kusini, Nairobi na Dar es Salaam.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
NA REBECA DUWE TANGA Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batlida Burian amewataka wananchi wenye migogoro mbalimbali ikiwemo ya ndoa na ardhi ...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
