Friday, May 1, 2020
Maandamano ya Mei Mosi ulimwenguni yaathiriwa na corona
Wafanyakazi mjini Hong Kong waliojaribu kuandamana kama ilivyo desturi ya siku ya kimataifa ya wafanyakazi, Mei Mosi, wamezuiliwa kuandamana kufuatia maambukizo ya virusi vya corona.
Hata hivyo baadhi yao waliovalia barakoa walielekea mitaani huku wengine wakielezea hisia zao kupitia mitandao ya kijamii.
Kwa kawaida mamilioni ya wafanyakazi hujitokeza mitaani kuandamana siku hii ya kimataifa ya wafanyakazi.
Lakini kufuatia masharti ya watu kukaa mbalimbali, utamaduni huo uliozoleka haujashuhudiwa leo katika miji mingi.
Nchini Ufaransa, ambayo bado iko chini ya amri ya kutosafiri, wafanyakazi wanaiadhimisha siku yao kupitia mitandao ya kijamii au kwenye mabaraza ya nyumba zao.
Mjini Berlin Ujerumani, takriban maafisa 5,000 watakuwa wakifanya doria mitaani kukabiliana na watakaokiuka maagizo ya watu kukaa mbalimbali endapo wafanyakazi wataandamana.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
