Chama Cha Walimu Tanzania (CWT), kimeahidi kufanya mapinduzi katika soka, kwa kuwa na timu imara itayoshiriki Ligi za ndani na nje ya nchi.
Hatua hiyo inatokana na mikakati kabambe inayotarajia kuwekwa na Walimu kupitia uongozi wa Makao Mkuu, mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi Mkuu wa chama hicho unaotarajia kufanyika Mei 28 mwaka huu.
Hayo yalielezwa na Mwalimu Abubakari Alawi akizungumza na Waandishi wa Habari mjini Kibaha,ambaye ni mgombea wa nafasi ya Mhazi kwenye uchaguzi huo ndani ya chama hicho, alipojibu swali kuhusiana na mikakati ndani ya soka.
Alawi ambaye ni Katibu wa Chama Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani COREFA, aliyasema hayo akizungumza na Waandishi wa habari mjini Kibaha ambapo alibainisha ,Walimu wamedhamiria kuikomboa nchi kwenye medani hiyo hususani michuano ya Kimataifa.
"Nakumbuka Rais wetu dkt.John Magufuli alishawahi kunukuliwa na vyombo vya habari akisema kuwa ana hamu ya kuiona timu itayoipeperusha nchi kwenye michuano ya Kimataifa kwa mafanikio, tunasema kuwa Walimu tutakata kiu hiyo ya wa-Tanzania," alisema Alawi.
Alawi ambaye ni mgombea wa nafasi ya Mhazini ndani ya chama hicho cha Walimu Taifa akitetea nafasi hiyo, aliongeza kuwa tayari wameshaweka mikakati madhubuti itayokwenda kutekelezwa baada ya uchaguzi huo.
Alieleza, vilabu vingi vinavyoshiriki ligi mbalimbali zina wachezaji ambao ni walimu.
Aliongeza kwamba kwa sasa kuna baadhi ya wilaya zina timu na kushiriki Ligi ngazi zilizopo, lakini moja ya mikakati iliyopo ni kwamba baada ya kufanyika kwa uchaguzi watakaa kuhakikisha hilo wanaliwekea mikakati madhubuti.
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
