Tuesday, April 14, 2020
Ujerumani yahofia idadi ya maambukizi inayorekodiwa
Mkuu wa taasisi ya afya ya Robert Koch amesema idadi ndogo ya visa vya maambukizi Ujerumani huenda imetokana na upimaji mdogo katika kipindi cha likizo ya Pasaka
Kwa mujibu wa taasisi ya afya ya Robert Koch, ni kuwa huenda visa vichache vya maambukizi ya virusi vya Corona vimetokana na vipimo vichache vilivyofanywa wakati wa likizo ya Pasaka kinyume na inavyodhaniwa kuwa maambukizi hayo yamepungua.
Mkuu wa taasisi hiyo Lothar Wieler amewaambia waandishi wa habari kuwa hawawezi kutoa tathmini ya moja kwa moja kuwa visa vya maambukizi ya virusi vya Corona vinapungua. Amewataka watu kuendelea kuchukua tahadhari na kufuata maelekezo ya kutokaribiana ili kuzuia kuenea kwa virusi vya Corona.
Na nchini Uingereza, idadi ya vifo vinavyotokana na ugonjwa wa COVID-19 iliyoripotiwa huenda ikawa chini tofauti na idadi halisi ya vifo. Kwa mujibu wa takwimu zilizochapishwa leo Jumanne, idadi kamili ya vifo huenda ikazidi asilimia 15 ya ile inayoripotiwa kila siku.
Ofisi ya takwimu za kitaifa imesema kuwa mnamo Aprili 3, watu 6235 walifariki dunia nchini England na Wales kutokana na ugonjwa wa COVID 19 lakini huenda idadi hiyo iliotajwa ikawa chini tofauti na hali ilivyo.
Mtaalamu wa takwimu katika ofisi hiyo Nick Stripe amesema kuwa idadi ya watu waliokufa kwa ugonjwa wa COVID-19 ni kubwa zaidi ya iliyotajwa kwani ripoti za serikali zimenakili vifo vilivyotokea hospitali pekee bila ya kujumuisha vifo vilivyotokea majumbani na hata kliniki za kijamii.
India yaongeza muda wa watu kutotoka nje hadi Mei, 3.
Na nchini India, Waziri Mkuu Narendra Modi ameongeza muda wa watu kutotoka nje hadi Mei 3. Hata hivyo, amesema kuwa huenda akaondoa vikwazo hivyo katika baadhi ya miji kutokana na changamoto wanazopitia maskini.
Na katika tangazo tofauti, safari zote za ndege za ndani na kimataifa pia zimesimamishwa hadi Mei 3.
Hatua ya kusitisha shughuli katika miji iliyoanza kutekelezwa mnamo mwezi Machi 25 kwa siku 21, imeathiri mamilioni ya watu wenye kipato cha chini hasa wakati huu ambapo uchumi wa India unayumbayumba.
Modi amesema kuwa India imelipa gharama kubwa kutokana na agizo hilo japo amesema limesaidia kupunguza kasi ya maambukizi ya virusi vya Corona.
Nchi hiyo imerekodi zaidi ya visa 10,000 vya maambukizi ya Corona huku watu 339 wakifariki dunia.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
