KIMENUKA! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya aliyekua Kaimu Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo, Yeremia Maganja kutangaza kukihama chama hicho kwa kile alichoeleza kutoridhishwa na mwenendo wa chama hicho.
Maganja ambaye pia amewahi kuwa mshauri wa ACT amesema sababu kuu zilizomfanya ajiondoe kwenye chama hicho ni namna ambavyo uchaguzi mkuu uliofanyika Machi mwaka huu ulivyoendeshwa pamoja na ujio wa Maalim Seif Sharif Hamad kutokea Chama cha Wananchi (CUF).
Amesema mwanzoni walivyoanzisha ACT ilikua ni kukitengeneza kuwa chama kinachofanya maamuzi yake kupitia vikao halali lakini matokeo yake kimekua chama cha mtu binafsi.
Akizungumzia uchaguzi mkuu uliofanyika katikati ya mwezi Machi, Maganja amesema haihitaji uchunguzi kujua kuwa uongozi wote uliochaguliwa ulikwishachaguliwa kabla ya mkutano mkuu uliowachagua.
" Uongozi wote mnaouona ulishachaguliwa kabla ya uchaguzi. Niwatapa mfano. Wapo watu waliochukua fomu za uongozi mbalimbali lakini wakajitoa siku ya uchaguzi na baadae wote wakateuliwa katika nafasi nyeti za Ujumbe wa Kamati Kuu.
Kuna wagombea walipigwa vita hadharani akiwemo mgombea wa Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana ndugu Winston pamoja na ndugu Kaila. Walisakamwa hadharani kwamba hawafai kuwa viongozi.
Lakini hata Makamu Mwenyekiti aliechaguliwa bara, Ndugu Dorothy yeye alishinikizwa achukue fomu kugombea nafasi hiyo kwa kuwa ni Mwanamke na Mkristo. Sasa mtaweza kuona tupo kwenye chama cha namna gani," Amesema Maganja.
Amesema ujio wa Mwenyekiti wa ACT Taifa, Maalim Seif Sharif Hamad akitokea Chama cha Wananchi CUF kumesababisha mgawanyo ndani ya chama hicho kutokana na Maalim na watu wake kutaka kituo cha chama kiuongozi, kiuchumi na rasilimali watu kuwa Zanzibar.
Amesema Maalim Seif na watu wake wana ajenda yao na ACT ina ajenda yao na ajenda ya Maalim ni kuhakikisha chama hicho kinakua na nguvu Zanzibar kuliko bara.
" Siku moja Zitto aliweka picha yake akiwa Ubelgiji na Lissu na kusema wao ndo wanafaa kuwa marais wa Tanzania, nilicheka sana, Zitto anasukumwa na vitu viwili tu, maslahi binafsi na umaarufu. Hakuna kingine.
Niwaambie tu na nacheka moyoni, Zitto hafai kuwa kiongozi, atauza mpaka watu achilia mbali rasimali vitu, chama chetu kina matatizo na matatizo yetu ni Zitto Kabwe, huyu ndie huwa anapanga watu kwa wakati kwa maslahi yake binafsi na umaarufu wake," Amesema Maganja.
Akizungumzia muelekeo wake baada ya kuondoka ACT amesema amejipa siku kadhaa za kujitafakari ili kujua wanaenda chama gani ili waendelee kufanya siasa.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
