Serikali ya wilaya ya Iringa imepiga marufuku sherehe zote harusi ambazo hazina kibali maalumu kutoka kwa Mganga mkuu wa wilaya (DMO) kutokana na kuwepo kwa tishio la maambukizi ya virusi vya Corona nchini.
Akizungumza kwenye kikao cha wadau wa sekta ya afya,mkuu wa wilaya ya iringa Richard kasesela alisema kuwa sherehe zote za harusi haziruhusiwi kufanyika bila kupata kibari maalumu kwa lengo la kulinda afya za wananchi wanaokuwa wanasherekea harusi kutokana na kuwepo kwa tishio la maambukizi ya virusi vya corona.
Ni lazima kila sherehe katika wilaya ya Iringa kuwepo mfumo wa kusafishia mikono kwa lengo la kukwepa maambukizi ya virusi vya corona ambavyo vimekuwa tishio hapa nchini na duniani kwa ujumla.
Kasesela alisema kuwa kwenye harusi huwa kuna kuwa na mkusanyiko wa watu wengi hivyo ni lazima kuweka king a mapema ili yasitokee maambukizi makubwa kama ambayo yametokea nchi nyingine.
Aisha kasesela aliwataka wananchi wa wilaya ya Iringa kuwa makini na mikusanyiko ya watu ili kuepuka kupata maambukizi ya virusi vya corona ambavyo vimekuwa vinatishia uhai wa wananchi.
"Misiba,kusalimia,vituo vya usafiri,makanisani na misikitini ni lazima kuondokana na Mira na tamaduni zetu ambazo tumekuwa tumezizoea ili kuepukana na maambukizi ya virusi vya corona" alisema kasesela
Kasesela alitaka halmashauri zote za wilaya ya Iringa kuhakikisha kwenye vituo vya afya,vituo vya mabasi,maduka makubwa,kampuni mbalimbali zote lazima kuwe na sehemu za kunawia mikono ili kuepuka na maambukizi ya virusi vya corona.
"Iringa hakuna hata mgonjwa mmoja wa maambukizi ya virusi vya corona na taarifa zinazoenea sio za kweli wananchi wa iringa wanatakiwa kuzipuuza na mwenye jukumu la kutangaza uwepo virusi hivyo ni waziri husika au viongozi wa ngazi za juu"alisema kasesela
Kwa upande wake mdau wa sekta ya afya mkoani Iringa Ahmed Asas alisema kuwa wamekuwa wakitoa elimu juu ya maambukizi ya virusi vya corona kwa waandishi wa habari,wafanyakazi wa kampuni ya Asas na taasisi binafsi kwa lengo la kuepuka kuambukizwa virusi vya corona.
Ahmed alisema kuwa kwenye kampuni ya Asas wamefanikiwa na kuwa na chumba maalumu kwa ajiri ya wafanyakazi watao kuwa na dalili za maambukizi ya virusi vya corona na wameganikiwa kutoa elimu kwa baadhi ya wafanyakazi kwa lengo la kuwa msaada kwa wafanyakazi wengine.
"Sisi tupo tayari kutoa elimu juu ya maambukizi ya virusi vya corona sehemu yeyeyo ile kwa kushirikiana na serikali ya wilaya ya Iringa kama ambavyo yumeanza na mkuu wa mkoa wa Iringa Richard kasesela" alisema Ahmed
Naye mganga mkuu wa wilaya ya Iringa Dr Samwel Marwa alisema kuwa wamejipanga kila idara kuhakisha wanatoa elimu na kudhibiti maambukizi ya virusi vya corona.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
Kulia ni Mkurugenzi wa Stedom House of Beauty Bi. Stella Mhondo akigonga Cheers na wadau wa masuala ya Urembo na Vipodozi waliohudhuria uzin...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
