Waziri wa Mambo ya Nchi za Kigeni wa Iran Mohammed Javad Zarif amesema kuwa Iran imezidisha ukomo wa viwango vya madini yake ya urani katika hifadhi zake, uliowekwa chini ya mkataba wa 2015 wa nyuklia.
Shirika la habari la Iran - ISNA limeripoti kuwa Iran ilipitisha kiwango cha ukomo wa kilo 300 kwenye mpango wake.
Marekani ilijiondoa kwenye mpango huo wa nyuklia mwaka jana na ikaiwekea Iran vikwazo vikali kama sehemu ya kampeni ya kuiongezea mbinyo mkali.
Kwa kulipiza kisasi, mnamo Mei 8, Iran ikatangaza kuwa haitaheshimu tena viwango vya mwisho vilivyowekwa vya hifadhi zake za madini ya urani yaliyorutubishwa.
Ilitishia pia kwenda mbali zaidi na kuachana na ahadi zake za nyuklia kama washirika waliobaki katika mkataba huo, ambao ni pamoja na Uingereza, China, Ufaransa, Ujerumani na Urusi, hawataisaidia nchi hiyo kutokana na vikwazo ilivyowekewa na hasa vya kuuza mafuta yake.
Muda mfupi baada ya tangazo hilo la Iran kutolewa, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kudhibiti matumizi ya nishati ya nyuklia - IAEA limethibitisha kuwa Iran ilipindukia ukomo wa viwango vyake vya madini ya urani.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
