Sunday, June 23, 2019
Waziri Lugola azidi kukomalia suala la Polisi na Bodaboda
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amesema serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wa Rais Dkt. John Magufuli kupitia ilani ya Chama Cha Mapinduzi iliyodhamiria kupambana na umaskini na changamoto ya ajira, Serikali ipo makini na wanahakikisha wananchi wanapambana na umaskini na tatizo la ajira.
Amesema hayo alipofanya ziara ya kushtukiza katika Kituo cha Polisi Gogoni kilichopo Wilaya ya Kipolisi Kimara, Wilayani Ubungo, jijini Dar es Salaam, leo kwa lengo la kuangalia utendaji wa Polisi kituoni hapo.
Aidha, amesema vijana wengi wameamua kupambana na umaskini kwa kujiajili kupitia pikipiki maarufu bodaboda lakini kumekuwa na malalamiko mengi ambayo yalifika hadi bungeni kwa vijana hao kuonewa, kupigwa na kunyang'anywa pikipiki zao.
"Nilitoa maagizo kwa Jeshi la Polisi juu ya bodaboda ambazo zinaweza kukamatwa na kuwekwa katika vituo vya polisi; bodaboda zinazostahili kukamatwa ni zile zilizohusika na uharifu, zilizohusika na ajali, zilizopotea na kuonekana na zile zilizookotwa," alisema Lugola.
Aliongeza kuwa, bodaboda nyingine zinazokamatwa na makosa mengine ya usalama barabarani kwa kupakia abiria zaidi ya mmoja maarufu kama mshikaki na kutovaa kofia ngumu na mshtakiwa anaweza kutozwa faini ambayo italipwa ndani ya siku saba.
Hata hivyo, Waziri Lugola baada ya ziara yake hiyo ambapo alizikagua bodaboda mbalimbali kituoni hapo, alisema amejiridhisha kwa kukuta bodaboda zote zipo kwenye makundi aliyoyaainisha na amelipongeza na amempongeza Mkuu wa Jeshi hilo, Simon Sirro kwa maelekezo yake aliyoyatoa kwa Jeshi hilo kufanyiwa kazi.
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
WATU saba wamefariki dunia baada ya bajaji waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori eneo la Mpemba, Tunduma wilayani Momba, mk...
-
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine nchini Kenya wametuma salamu zao za rambi rambi kwa familia ya marehemu Yusuf Haji. Rais Uhuru Kenya...
-
MWANA-mfalme wa Uingereza,. Prince Charles, ambaye ni mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza, na mrithi wa kwanza katika ...
-
Mfanyabiashara raia wa Kenya, Raphael Ongangi anayedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay, Dar es Salaam nchini Tanzania am...
-
Zikiwa zimesalia siku chache tu Hoteli Mpya ya Kisasa yenye Ubora wa hali ya juu 'SHY PARK HOTEL' ifunguliwe Rasmi mwezi Agosti 202...
-
Vijana wametakiwa kuwa wazalendo katika nchi yao kwa kukemea vitendo viovu katika jamii na kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha Sil...
-
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko amefunga rasmi mafunzo ya sheria za usalama barabarani kwa maaskofu na wachungaji wa makanisa ya...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi, yenye nia ya kuleta ch...
