Sunday, June 23, 2019
Waziri Lugola azidi kukomalia suala la Polisi na Bodaboda
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amesema serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wa Rais Dkt. John Magufuli kupitia ilani ya Chama Cha Mapinduzi iliyodhamiria kupambana na umaskini na changamoto ya ajira, Serikali ipo makini na wanahakikisha wananchi wanapambana na umaskini na tatizo la ajira.
Amesema hayo alipofanya ziara ya kushtukiza katika Kituo cha Polisi Gogoni kilichopo Wilaya ya Kipolisi Kimara, Wilayani Ubungo, jijini Dar es Salaam, leo kwa lengo la kuangalia utendaji wa Polisi kituoni hapo.
Aidha, amesema vijana wengi wameamua kupambana na umaskini kwa kujiajili kupitia pikipiki maarufu bodaboda lakini kumekuwa na malalamiko mengi ambayo yalifika hadi bungeni kwa vijana hao kuonewa, kupigwa na kunyang'anywa pikipiki zao.
"Nilitoa maagizo kwa Jeshi la Polisi juu ya bodaboda ambazo zinaweza kukamatwa na kuwekwa katika vituo vya polisi; bodaboda zinazostahili kukamatwa ni zile zilizohusika na uharifu, zilizohusika na ajali, zilizopotea na kuonekana na zile zilizookotwa," alisema Lugola.
Aliongeza kuwa, bodaboda nyingine zinazokamatwa na makosa mengine ya usalama barabarani kwa kupakia abiria zaidi ya mmoja maarufu kama mshikaki na kutovaa kofia ngumu na mshtakiwa anaweza kutozwa faini ambayo italipwa ndani ya siku saba.
Hata hivyo, Waziri Lugola baada ya ziara yake hiyo ambapo alizikagua bodaboda mbalimbali kituoni hapo, alisema amejiridhisha kwa kukuta bodaboda zote zipo kwenye makundi aliyoyaainisha na amelipongeza na amempongeza Mkuu wa Jeshi hilo, Simon Sirro kwa maelekezo yake aliyoyatoa kwa Jeshi hilo kufanyiwa kazi.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
