Siku chache baada ya picha zake kusambaa akionekana na wabunge tofauti kwenye Viwanja vya Bunge jijini Dodoma, huku kukiwa na madai kuwa ameenda kudanga, mrembo anayetikisa na umbo matata katika mitandao ya kijamii, Jacqueline Obeid 'Poshy Queen' amevunja ukimya juu ya safari yake hiyo.
Poshy amesema kuwa anawashangaa sana watu wote wanaomjadili na kumsemea maneno mabaya na kuuliza kuwa yeye kwenda bungeni ni makosa.
"Mbona watu wana matatizo sana, yaani mimi kwenda bungeni ni matatizo jamani au sistahili? Kule kila mtu anakaribishwa kama mgeni wakati mimi kuna jambo lilinipeleka kule na nimejifunza vingi", amesema Poshy.
Poshy ameongeza kuwa asingependa kabisa watu waendelee kumjadili kuhusu yeye kwenda bungeni kwa sababu kila mtu anaruhusiwa kwenda, lakini alivyokwenda yeye ilikuwa kwa sababu maalum ya kipindi cha Bunge la Bajeti ambapo amesomea mambo ya usimamizi wa fedha katika Chuo cha IFM jijini Dar es salaam.
"Kule nilikwenda na mimi kuwasilisha mawazo yangu katika kipindi hiki cha Bunge la Bajeti, licha ya kuhudhuria hata nilivyokutana na baadhi ya wabunge niliwaambia mawazo yangu na wamesema watayafikisha huko", ameongeza Poshy.
Katika habari zilizoenea, Poshy alidaiwa kuwa alikwenda jijini humo kudanga baada ya kupata mualiko na mbunge mmoja ambaye ana uhusiano naye. Poshy ametokea kujizolea umaarufu mitandaoni kutokana na umbo lake matata la namba nane ambalo inasemekana kuwa amelipata ghafla au ni la kutengeneza.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Msanii maarufu Ntemi O Mabala ' Ng'wana Kang'wa kutoka Kahama Mkoani Shinyanga anakualika kusikiliza wimbo wake mpya unaitwa M...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Hii hapa ngoma mpya ya Msanii wa Nyimbo za asili Mama Ushauri ameshirikiana na Ng'wana Ng'washi inaitwa Merimela ,imetengenezwa Lw...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...