Mtafiti wa Chuo kikuu cha Makerere nchini Uganda Dkt. Stella Nyanzi ameagizwa kujitetea katika kesi ambapo anatuhumiwa kumtukana rais Yoweri Museveni.
Ikitoa uamuzi wake mahakama iliopo katika barabara ya Baganda ilisema kuwa alikuwa na kesi ya kujibu.
Kwa mujibu wa gazeti la The Monitor nchini Uganda, baada ya kusikiza ushahidi kutoka kwa mashahidi watatu wa serikali, hakimu bi Gladys Kamasanyu aliamuru siku ya ijumaa kwamba Dkt Nyanzi, ambaye anazuiliwa katika gereza la Luzira ana kesi ya kujibu.
Baada ya uamuzi huo Dkt Nyanzi alisema kuwa atawasilisha kati ya mashahidi watano hadi saba kumtetea.
Hakimu huyo amesema kuwa mshukiwa huyo anamiliki akaunti ya ukurusa wa facebook ambao ulichapisha 'matusi' hayo.
Dkt Nyanzi anashtakiwa kwa kutekeleza unyanyasaji wa mtandaoni pamoja na kutoa matamshi machafu swala ambalo linakiuka sheria nchini Uganda.
Mnamo tarehe 9 mwezi Novemba , Dkt Nyanzi alikataa kuomba dhamana.
Hatahivyo bwana Isaac Ssemakade, wakati huo alisema kwamba mteja wake alitaka serikali kuharakisha uchunguzi ili kumwezesha kuendelea na kesi.
Upande wa mashtaka unasema kuwa mnamo mwezi Septemba tarehe 16 2018, Dkt Stella Nyanzi alichapisha katika ukurasa wake wa facebook madai yaliodaiwa kuwa machafu kwa rais Museveni na marehemu mamake.
Imedaiwa kwamba pia alichapisha ujumbe wa kuvuruga amani, utulivu na kuingilia faragha ya rais Museveni.
Hii ni mara ya pili maafisa wa polisi wanamtuhumu Dkt Nyanzi kwa madai ya kumtusi Museveni na familia yake.
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na...
-
Na Mbuke Shilagi Kagera. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema kuwa mradi wa umeme wa maji ya maporomoko wa Rusumo...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania November 23, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za ny...
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Dar es salaam October 9, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na ...
-
Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga Daktari Daniel Henry Na Isaac Masengwa ******************* Askofu mteule wa KKKT Dayosisi ya Mwanga...
-
Mhamasishaji maarufu wa mitandaoni, Mwijaku, ameandika ujumbe unaotoa ushauri kwa Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Said Hersi, kupitia ukuras...
-
Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025 Msimamo Ligi Kuu Bara 2024/2025, NBC Premier League Tanzania Msimamo Ligi Kuu NBC 2024/2025 Tanzania Premier...
-
Zaidi ya ghorofa 100 jijini Dar es Salaam zilibainika kujengwa kinyume cha taratibu za ujenzi, Bunge lilielezwa. Kwa mujibu wa ripoti iliy...
-
Msanii wa nyimbo za asili Nyanda Madirisha Obhado 'Maliganya' maarufu Shikomba Bhulolo anakualika kusikiliza wimbo wake mpya 2021 un...
-
Ninakualika kutazama Video Mpya kabisa mwaka 2021 kutoka kwa Msanii Yobat amemshirikisha Bhudagala Ng'wana Malonja na Shija Kadoke wim...
